Friday, 29 October 2021 08:40

Kiswahili Questions and Answers - Class 7 End of Term 2 2021 Set 1 with Marking Schemes

Share via Whatsapp

SEHEMU YA KWANZA:LUGHA
SOMA MAAGIZO HAYA KWA MAKINI 

  1. Umepewa kijikaratasi hiki cha maswali na karatasi ya majibu. Kijikatatasi hiki kina naswali 50. 
  2. Katika karatasi ya majibu hakikisha umeandika:
    1. Jina lako
    2. Jina la shule yako


MASWALI

Kamilisha kifungu hiki kw akujaza nafasi kwa kuchagua kiteuzi kifaacho.
Hati nadhifu ni hati safi. Ni mwandiko _1__ na matatizo_2_. Herufi___3_ hutakiwa kuwa sawa, kuna herufi za kuweka vitone; ni__4_vitone hivyo viwepo. Kama ni herufi_5____kukunjwa chini au jau ya msitari_6__kukunjwa. Baadhi ya herufi huwa na vistari juu, kwa__7_ vistari hivyo hupaswa kuwekwa. Mwandiko unatakiwa uwe__8_wastani __9__ mkubwa sana _10_mdogo sana, usomeke vilivyo. Haifai kuka__11___ au kufutafuta kazi iliyoandikwa. Mwandiko12_unavutia na_13__machoni hata kabla ya mtu kukisoma
__14__kilichoandikwa. Jifunze kuandika_ 15_ 

  1.                    
    1. isiyo
    2. yasiyo 
    3. usio
    4. usiwo
  2.                      
    1. lolote
    2. zozote
    3. yoyote
    4. yeyote
  3.                            
    1. yote
    2. zote
    3. wote
    4. lote
  4.                          
    1. nzuri
    2. vizuri
    3. uzuri
    4. zuri 
  5.                          
    1. za
    2. ya
    3. kwa
    4. kunafaa
  6.                        
    1. linafaa
    2. zinafaa
    3. tunafaa
    4. hilo
  7.                            
    1. hapo 
    2. hiyo
    3. hivyo
    4. kwa
  8.                          
    1. ya
    2. wa
    3. na
    4. isiwe
  9.                        
    1. kusiwe
    2. zisiwe
    3. usiwe 
    4. tena
  10.                        
    1. pengine 
    2. zaidi
    3. au
    4. katakata
  11.                    
    1. takata
    2. kutakasa
    3. takataka
    4. nzuri
  12.                      
    1. zuri
    2. mizuri
    3. mzuri 
    4. kupendeza
  13.                            
    1. kupendwa
    2. kupendesa
    3. kupendea
    4. hiki
  14.                      
    1. hilo 
    2. kile
    3. hiyo
    4. mzuri
  15.                    
    1. bora
    2. viema
    3. vyema
    4. ta

Tegua kitendawili hii:.

  1. Ndege wengi baharini
    1. jua
    2. nyota
    3. gari
    4. meza 
  2. Umbo hili utaliitaje?
    17 ujggu
    1. tufe
    2. maraba
    3. mche
    4. mstatili
  3. Tunasema biwi la simanzi, pia tunasema .................... la moshi. 
    1. wingu
    2. mtungo 
    3. mvuke
    4.  mkuroro
  4. Katika kamusi, neno la tatu litakuwa lipi?
    1. landa
    2. lafudhi
    3. lahani
    4. laiki
  5. Mchele, mawele na wimbi ni nafaka ilhali ng'ombe, mbuzi, kondoo na nguruwe ni
    1. hombwe
    2. ombwe
    3. hongwe
    4. howa
  6. Shuka ni teremka. Shuka pia ni:
    1. kifaa cha kukatia hasa miti 
    2. kitambaa kinachotandikwa kitandani
    3. ndege mkubwa mwenye mbawa za kahawia
    4. mnazi mchanga unaochomoza
  7. Katika uwakifishaji, sauti (') huitwaje? 
    1. kituo
    2. kipumuo
    3. king'ongo 
    4. hisi 
  8. Majina haya ni ya ngeli gani? Maji, mafuta, maisha, manukato
    1. YA-YA
    2. U-ZI
    3. U-YA
    4. MA-MA
  9. Gari la majangili liliegeshwa....................njia.
    1. kando mwa 
    2. kando ya
    3. kando kwa
    4. kando na
  10. Nahau, piga mafarba haina maana ya
    1. kumzandiki mtu
    2. kumlaghai mtu
    3. kumghilibu mtu
    4. kumsema mtu
  11. Mshororo wa tatu katika shairi la tarbia huitwa
    1. mloto
    2. mleo
    3. tathlitha
    4. utao
  12. Wachezaji wanane kwa tisa ndio huitwa
    1. thumuni tisa
    2. tusui nane
    3. thumuni nane
    4. themanini na tisa .
  13. Kanusha sentensi hii
    Akinipiga nitalia
    1. kama hatanipiga sitalia
    2. asiponipiga nitalia
    3. akinipiga sitalia
    4. asiponipiga sitalia 
  14. Ni nomino ipi isiyostahiki katika orodha ifuatayo? 
    1. mtu
    2. mvulana 
    3. daktari
    4. juma 
  15. Kutokana na kitenzi "andika" hatupati nomino
    1. mwandishi
    2. kuandikika 
    3. uandishi
    4. mwandiko

Soma kifungu kifuqtacho kisha ujibu maswali kutoka 31 hadi 40.
Dalili za mvua ni mawingu. Baada ya kiangazi cha miezi tandatu, hatimaye mawingu yalitana angani. Wakulima walijawa na furaha kwa tumaini la kupata afueni ya mazao. Kila mtu alionekana shambani akiwa na jembe mkononi kwa kwamini kuwa achanikaye kwenye mpini hafi njaa.
Hatimaye jioni moja, kiza kiligubika nchi ikawa kama chumba kilichozimwa taa. Kwa ghafla mimweko na mingurumo ya radi ilisikika na kufuatwa na matone mazito yaliyosikika kwenye mapaa ya nyumba kijijini. Watu waliimba nyimbo za kumshukuru. Jalali kwa kuwajaalia mvua pamoja na kutoa dua za kushukuru.
Usiku ule mvua ilinyesha kwa makeke na upepo uliangusha miti na hata kubomoa nyumba zilizokuwa hafifu. Vifijo, hoi na nderemo viligeuka kuwa kwikwi za vilio kwa kupoteza mali na makao.
Mvua iliendelea kunyesha kidindia, siku zikaunda majuma ambayo hayakuchelewa kukomaa na a miezi. Kama kwamba Mungu alifungulia biluli akasahau, mvua ilinyesha kwa miezi takribani
la kupungua. Si wahenga walisema kuwa hakuna kapa isiyokuwa na usubi? Mito ilifurika, barabara zikaharibika, mashamba yakageuka kuwa vinamasoi huku watu wengi wakikosa makao.
Hewaa! Baada ya kisa mkasa. Ati hakuna msiba usiokuwa na mwenziwe. Katika hali ya sitaifahamu, mvua ilisababisha mlipuko wa maradhi mbalimbali. Wenye kipindupindu walitibiwa huku waliokuwa na homa ya matumbo wakipewa ushauri na walioumwa na mbu wakishughulikiwa kunako zahanati za muda. Hali hii haikukoma hata baada ya miezi minane mvua ilipopusa.
Si wenye ndimi za kihenga waliamba kuwa aisifuye mvua imemnyea?

  1. Kiangazi cha miezi tandatu ndicho kipi?
    1. Miezi ya kutanda kwa mawingu 
    2. Miezi sita 
    3. Miezi ya kutanda mvua
    4. Miezi saba 
  2. Mvua inayozungumziwa iliwapa nini wakulima?
    1. ukosefu wa sehemu za kujisetiri 
    2. wasiwasi wa kupoteza makao yao 
    3. wahaka kuhusu mafuriko
    4.  tumaini na afueni ya mazao
  3. Mbona mwandishi anamithilisha dunia na chumba kilichozimwa taa? 
    1. ilivyokuwa anga baada ya mawingu kutanda 
    2. ilivyokuwa hali baada ya umeme kupotea
    3. baada ya upepo mkali kuzizima taa vyumbani
    4.  baada ya vyumba kukosa mwangaza 
  4. Kwa mujibu wa aya ya pili, ni kipi kilichokuwa cha mwisho?
    1. Matone ya mvua 
    2. mingurumo ya radi
    3. mimweko ya umeme
    4. giza kufunika nchi 
  5. Iliponyesha mvua usiku wa kwanza, watu walifanya yote ila
    1. kushukuru 
    2. kukashifu
    3. kupiga dua 
    4. kushangilia
  6. Mvua inayonyesha kidindia ndiyo inayonyesha vipi?
    1. kwa wingi 
    2. bila kukoma 
    3. bila baridi
    4. na upepo mkali 
  7. Mvua inayosemwa ilinyesha kwa muda gani?
    1. Thuluthi mbili za mwaka 
    2. Thumni mbili za mwaka
    3. Robo tatu za maka
    4. Sudusi tatu za mwaka 
  8. Kwa mujibu wa aya ya nne, ni mambo mangapi ambayo yalitokea? 
    1. Matatu
    2. Manne 
    3. Matano
    4.  Mengi
  9.  Kulingana na kifungu maradhi yaliyozuka hayakuwa pamoja na? 
    1. Malaria . 
    2. Kichocho 
    3. Waba
    4. Homa ya matumbo 
  10. Kipe kifungu hiki kichwa mwafaka
    1. Maji ni uhai 
    2. Na ije baa iondoke baa 
    3. Hakuna kapa isiyokuwa na usubi
    4. Aisifuye mvua imemnyea

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali kutoka 41 hadi 50.
Kungutu aliugud maradhi mabaya kwa muda mrefu. Alikonda sana. Hakuwa na nguvu za kutafuta chakula. Njaa ilimuuma si haba. Hakujua jinsi ya kutafuta chakula kwani ubongo wake haungefikiria vizuri.
Nyumbani kwake kulikuwa na nyasi nyingi sana ndefu. Huko kulijaa panzi lakini kunguru nangeweza kuwadona kwa sababu walitoroka. Panzi walimcheka kunguru mnyonge kwalkwa!kwa! kunguru alipokuwa akitembea siku moja aliwaona panzi wawili wakipigana kufa na kupona. Baadaye waliaga dunia, baada ya kuumizana na kupata majeraha mabaya sana.
Kunguru alitoka pahali alikuwa na kuwadona. Aliwala, walikuwa watamu ajabu. Alijaribu kutafuta panzi wengine waliokuwa wamekufa kwa sababu hakushiba. Hakufanikiwa hata kidogo.
Aliamua kuwachochea panzi, alitumia panzi moja mlafi kwa kumdanganya ati alikulia nyasi mbovu ilk Ji wengine walikuwa nyasi nzuri. Panzi mlafi alienda na akaanza kutoa fujo kwa panzi wengine. Vita vilizuka baina ya panzi. Kunguru alikuwa mbali akicheka na kusema, "Wajinga ndio waliwao."
Panzi wengi walikufa sana kutokana na vita vile, karibu wamalizane. Kunguru alizidi kuchochea panzi kuuana aijifanya rafiki aliyekuwa na hofu zaidi. Baada ya panzi wengi kufa, waliamua kumaliza vita ili wasimalizane. Baada ya vita, kunguru alionekana akiwala mizogo wa panzi waliokufa kwa furaha sana. Panzi walipoona hivyo walijua kunguru ni mwongo.

  1. Kunguru alikonda kwa nini .
    1. aliugua muda mrefu 
    2. hakutaka kula 
    3. hakuwa na hamu ya kula
    4. hakukuwa na panzi 
  2. Kwa nini kunguru hakujua jinsi ya kupata chakula? 
    1. Aliatafuta panzi 
    2. Alikuwa peke yake
    3. Ubongo wake haungefikiria vizuri
    4.  Panzi hawakufa
  3. Kwa nini kunguru alitamani kuwala panzi wengine
    1. Panzi walikufa zaidi 
    2. Ni watamu sana
    3. Hakushiba
    4. Ili awe na nguvu 
  4. Kunguru alipowatafuta panzi wengine
    1. hakuwapata 
    2. aliwapata 
    3. alichoka
    4. walitoroka
  5. Kisawe cha neno maradhi ni 
    1. ugonjwa
    2. afya 
    3. njaa
    4. unyonge
  6. Kusema vita vilizuka ni kusema kwamba
    1. vita viliendelea 
    2. vita vilianza
    3. vita vilikoma
    4. vita vilimalizwa 
  7. Mnyama akiaga huitwa mzoga, je binadamu akiaga huitwa? 
    1. Mzoga
    2. Mtu 
    3. Maiti
    4. Jeneza 
  8. Kunguru alitumia mbinu gani kupata chakula? 
    1. Kutafuta panzi waliokufa
    2. Alichochea vita kwa panzi 
    3. Alienda hospitalini
    4. Aliwinda panzi na akala nyasi
  9. Panzi waliamua kumaliza vita wakati gani?
    1. Walipochoka kupiga 
    2. kunguru alipowacheka 
    3. walipouana sana .
    4. walipojua ulikuwa uwongo wa kunguru
  10. Kichwa kifaacho habari hii ni
    1. vita vya panzi furaha ya kunguru 
    2. Uongo wa kunguru 
    3. panzi watamu 
    4. kunguru mgonjwa


MEALEKEZO YA KUSAHISHA

swa ms



INSHA

Endeleza insha hii:
Asubuhi hiyo siku ya jumatatu tulipokuwa gwarideni, mwalimu mkuu.....................................................



INSHA MEALEKEZO YA KUSAHISHA

MARKING CRITERION
The composition will be assessed according to the following general guidelines.

  • The maximuin mark will be 40 and the minimum mark 01.
  • Does the script show that the candidate can communicate accurately, fluently and imaginatively in English?

Accurency (16 marks)

  1. Correct tenses and agreement of verbs (4 marks)
  2. Accurate use of vocabulary (4 marks) 
  3. Following a sequence (4 marks)
  4. Correct punctuation (4 marks)

Fluency (16 marks)

  1. Words in correct order (4 marks)
  2. Sentence connection and paragraphs (4 marks)
  3. Correct spellings (4 marks)
  4. Ideas developed in logic sequence (4 marks)

Imagination (8 marks)

  1. Unusual but appropriate use of words and phrases (4 marks) 
  2. Variety of structure (4 marks)
    NB: Please, teachers are requested to scrutinize this marking scheme before use, its worthy.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Class 7 End of Term 2 2021 Set 1 with Marking Schemes.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students