Wednesday, 15 September 2021 13:03

Sarufi na Matumizi ya Lugha - Class 7 Kiswahili Revision Notes

Share via Whatsapp


Mnyambuliko wa Vitenzi

Huku ni kuvibadili vitenzi kwa kurefusha viambishi tamati ili kuleta kauli mbalimbali Kauli hizi ni.

  • Tendana: uma - umana
  • Tendesha: lala – laza
  • Tendeka: Lima – limika

Huu ni upachikaji wa viambishi kwenye mzizi wa kitenzi ili kuunda vitenzi vipya

Kauli ya Kutendeshwa/Fanyisha

Huonyesha kuwa kitendo kimesababishwa na kitu Fulani

Vitenzi hivi hutambulishwa na vitenzi vya, za, sha, fya, na ,sa

Kauli ya Kutendata

Kauli hii huonyesha dhana ya kurudia rudia tendo
Mfano
Kata – katakata
Imba – imbaimba
Tia – tiatia
Ruka – rukaruka

Sifa Kutokana na Vitenzi

Ni kuunda maneno yenye kivumishi au kusifu nomino kutoka kwenye viarafa

Sifa hizi huwa ni herufi kama f, v, mw
Mfano
Amini – mwaminifu
Sikia- sikivu
Tii – tiifu
Dhulumu – dhalimu



Tanakali za Sauti

Ni maneno yanayoonyesha au kuiga milio ya sauti, hali Fulani, sura au vitendo mbalimbali. Hutumia kusisitiza namna vitendo vilivyo, vinavyotendeka au kitakavyotendeka

Mfano:

  • Funika gubigubi!
  • Papatika papatupapatu!
  • Kula fyu!
  • Kuregea regerege!


Matumizi ya Vihusishi ‘katika’ na Kiambishi Tamati –ni’

Katika na –ni ni vihusishi vinavyotumiwa kumaanisha ndani ya au kwenye

Vihusishi hivi havitumiwi pamoja katika sentensi

Mfano

  • Ingia katika darasani ni kosa
  • Ingia darasani au ingia katika darasa ni sahihi

-ni huambishwa kwenye nomino za kawaida kisha nomino hiyo huorodheshwa katika ngeli ya PAKUMU
Pia hutumika kuonyesha ndani ya au mahali ndani
Mfano
Vijiko vimo jikoni
Walimu wamo majilisini

Katika

  1. hutumiwa kuleta maana ya Miongoni mwa
    mtu mmoja katika wale ni mgonjwa
  2. Wakati
    Tutakuwa na likizo katika mwezi wa Aprili
  3. Ujumla wa vitu
    Wote walishiriki katika michezo hiyo


Alama za Uakifishaji

Ni alama zinazotumiwa ili kuwasilisha nia halisi na maana kamili ya kwenye maandishi

Alama hizi pia hufanya kusomeka kwa sentensi kuwa rahisi
Mfano

Nusukoloni /Semikoloni/Nukta kipumuo(;)

Hutumiwa kuunganisha mawazo mawili
Mfano
Ninataka kuondoka mapemasipendi kuchelewa

Koloni/Nuktambili/Nukta pacha (:)

Hutumiwa kuonyesha orodha ndefu
Mfano
Nenda ununue vutu vifuatavyo:maziwa, mkate, sukari, mafuta na chumvi



Ukubwa, Udogo na Wastani wa Nomino

Ukubwa ni hali ya kukuza nomino na udogo ni hali ya kudunisha nomino
Wastani ni hali ya kawaida ya nomino

Nomino katika ukubwa huwekwa katika ngeli ya LI – YA na nomino katika hali ya udogo huwekwa
katika ngeli ya KI – VI

Zipo kanuni ambazo hutumiwa

  • Nomino zenye silabi mbili- dodosha moja
    Mtu- jitu
  • Nomino zinazoanza kwa ki dondosha ki pachika ji
    Kiatu-jiatu


Kukanusha

Kukanusha Amri

Wakati wa amri hukanushwa kwa kutumia si
Mifano
Aende – asiende
Nimpe – nisimpe
Ule – usile

Swali lije baadaye
Wewe kunywa dawa
Wewe usikunywe dawa

Wingi na Kukanusha

Wakati wa sasa hukanushwa kwa ha
Mifano 

unasoma – mnasoma – hamsomi
unakula – mnakula – hamli



Vivumishi

Vivumishi vya Pekee Ingine na -O-ote

Vivumishi hivi ni ote, o-ote, enye, enyewe na ingine



Vitawe

Ni maneno yaliyo na maana zaidi ya moja
Mfano

  • Vua-toa samaki majini
            Toa nguo mwilini
  • Ala-aina ya mfuko ambamo kisu hufichwa
          Tamko la kushangaa
          Aina yoyote ya chombo cha kufanyia kazi 


Viwakilishi

Ni neno linalosimama badala ya nomino kama yeye, sisi, wewe



Ngeli na Viambishi Ngeli

Mifano ya ngeli:

  • A – WA
  • U – YA
  • I – ZI
  • U – U
  • YA – YA
  • I – I

Ngeli ya A- WA

Ngeli hii inahusisha majina yenye sifa na hali ya wanyama, nyuni, malaika, samaki na wanadamu

Kutoa mifano katika umoja na wingi
Mfano
Mnyoo – minyoo
Kiwete – viwete
Nzi – nzi
Mkunga – mikunga

Ngeli ya U – I

Nomino za ngeli hii huchukua upatanisho wa U katika umoja na I katika wingi
Mifano
Mkono – mikono
Muundi – miundi
Mzigo – mizigo
Mtaa – mitaa
Muhula – mihula
Mwaka – miaka
Mlingoti – milingoti

Ngeli ya KI – VI

Nomino za ngeli hii ni vitu vya kawaida

Majina huanza kwa ‘ki’ katika umoja na ‘vi’ katika wingi

Mengine huanza kwa ‘ch’ kwa umoja na ‘vy kwa wingi
Mifano
Kiazi – viazi
Kiatu – viatu
Kioo – vioo
Kina – vina
Kikuba – vikuba
Cheti – vyeti
Chakula – vyakula
Chanda – vyanda
Chungu – vyungu

Wastani            udogo
Mlango             kilango
Mguu                 kiguu

Ngeli ya LI – YA

Maneno katika ngeli hii huanza na ma, me

Maneno yote katika hali ya ukubwa huingizwa katika ngeli hii
Mifano 
Dirisha – madirisha
Embe – maembe
Zulia – mazulia

Ukubwa

Guu – maguu
Jibwa – majibwa

Ngeli ya U – YA

Maneno katika ngeli hii huanza kwa U katika umoja na Ya katika wingi
Mifano
Ugonjwa – magonjwa
Uuaji – mauaji
Ujazi - majazi
Upana - mapana

Ngeli ya YA – YA

Nomino zote huanzia kwa ma
Mifano
Masihara - masihara
Matatu-  matatu
Makazi - makazi
Mahakama - mahakama
Maakuli - maakuli
Mawasiliano - mawasiliano

Ngeli ya I – ZI

Nomino hazibadiliki katika umoja na wingi
Mifano
Mashine - mashine
Sinia - sinia
Sahani - sahani
Ngozi - ngozi
Taa - taa
Pete - pete
Sakafu - sakafu
Shingo - shingo

Ngeli ya U – ZI

Maneno katika ngeli hii huwa na upatanisho wa U na ZI katka wingi
Mifano
Ubeti – beti
Uchane – chane
Uchega – chega
Ubavu – mbavu
Ubao – mbao
Ulimi – ndimi
Udevu – ndevu
Ujari – njari
Ujiti – njiti
Ugoe – ngoe
Uzi – nyuzi
Ufa – nyufa
Waadhi – nyaadhi
Walio – nyalio
Waraka – nyaraka

Ngeli ya U – U

Huchukua U katika umoja na U katika wingi
Kuelezea maneno hayabadiliki katika umoja na wingi
Mifano
Moto - moto
Ugali - ugali
Wema - wema
Ufisadi - ufisadi
Wizi - wizi
Ubaya - ubaya
Uzembe - uzembe

Ngeli ya KU

Maneno katika ngeli hii huchukua upatanisho wa kisarufi KU

Ngeli ya I – I

Majina ya nomino hii huchukua upatanisho wa sarufi kuwa I katika umoja na I katika wingi

Ngeli ya PA KU MU

Ni ngeli ya mahali

Huelezea hali tatu

  • Hapa/hapo/pale- mahali dhahiri
  • Huku/huko/kule – kusiko dhahiri
  • Humo/humu/humo – mahali ndani

Kuelezea viambishi tofauti

Join our whatsapp group for latest updates

Download Sarufi na Matumizi ya Lugha - Class 7 Kiswahili Revision Notes.


Tap Here to Download for 30/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Read 3137 times Last modified on Thursday, 16 September 2021 06:44