Isimu Jamii Questions and Answers

Share via Whatsapp

Swali 1

Nipe chai, andazi mbili na egg moja…

  1. Taja sajili inayorejelewa na maneno haya (alama 2)
  2. Fafanua sifa nane zinazohusishwa na sajili hiyo (alama 8)

Majibu

  1. Hotelini/mkahawani
  2.                                
    1. Lugha si sanifu
    2. Kuchanganya ndimi
    3. Utohozi
    4. Sentensi fupi
    5. Lugha ya heshima
    6. Lugha ya biashara
    7. Lugha ya ucheshi
    8. Matumizi ya jazanda
    9. Msamiati maalum k.m. menu n.k.

 Swali 2

Jadili changamoto zozote tano zinazoikumba lugha ya Kiswahili. ( alama10)

Majibu

  1. Uhaba mkubwa wa wataalamu wa Kiswahili
  2. Athari kutoka kwa lugha ya kwanza.
  3. Watu kupenda lugha nyinginezo kama vile kiingereza, kijerumani.
  4. Imani potovu – lugha ya Kiswahili ni duni
  5. Uhaba wa walimu wa Kiswahili.
  6. Uhaba wa vitabu vya Kiswahili.
  7. Kutokuwepo kwa sera ya lugha kutoka kwa baadhi ya serikali za mataifa ya Afrika mashariki.
  8. Uhaba wa pesa za kutafiti.
  9. Nchi za Afrika za kutokuza wala kuendeleza Kiswahili.

 Swali 3

…………….watu wakaunti ya Cheneo wamesahaulika kabisa Ningependa kuelezwa kinaga ubaga kama hawa ni wakenya au la. Order! Order! Mheshimiwa Kega.

  1. Hii ni sajili gani? (al2) ………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
  2. Eleza sifa nane za sajili iliyotajwa. (al 8)

Majibu

  1. Sajili ya bungeni
  2.                            
    • sentensi huwa ndefundefu
    • urudiaji wa baadhi ya maneno
    • Kuna kukatizana kauli
    • Mtindo maalumu wa kuanzisha,kuendeleza na kutamatisha mazungumzo.
    • Mtumizi ya ishara na miundoko Fulani
    • Msamiati maalamu
    • Kurejelea sheria za nchi
    • Lugha ya heshima
    • Kuchanganya ndimi (al.8)

 Swali 4

  1. Nini maana ya dhana ya usanifishaji wa lugha? (alama 2)
  2. Nchi za Afrika mashariki ziliunda kamati ya lugha ilikusafirisha na kukuza Kiswahili, eleza malengo manne makuu na mafanikio yake katika usanifishaji. (alama 8)

Majibu

  1. Ni uamuzi wakuchagua lugha moja au moja wapoyala haja za lugha ili kuifanyia marekebisho yakimatamshi, kisarufi, kimaana na kimaandishi ili itumike katika shughuli rasmi.
  2.  
    1. Malengo
      • Kusanifisha maandishi ni kuhakikisha mtindo mmoja unazingatiwa.
      • Kuchapisha vitabu.
      • Kuwahimiza na kuwasaidia wandishiwa Kiswahili.
      • Kuidhinisha vitabu vya kiada na ziada vinavyohitaji kakufundisha shuleni.
      • Kuwapasha waandishi habari zozote zile kuhusu njia tofauti au mitindo ya kusomeshea katika kila nchi. (zozote 4x1=4)
    2. Mafanikio
      • Vitabu vingi vya sarufi na hadithi vilichapishwa mf. Modern Kiswahili grama.
      • Tafsiri ilifanywa na vitabu kuchapishwa kwa kiwashili mf. Kisima chenye hazina.
      • Kamusi tatu zilichapishwa.
      • Vitabu vya kufunzwa Kiswahili viliidhinishwa. (zozote 4x1=4)

 Swali 5

  1. Eleza kwa ufupi jinsi mambo yafuatayo yanavyodhibiti mitindo ya lugha
    1. Mazingira (alama 2)
    2. Mada (alama 3)
    3. Hali (alama 2)
  2. Fafanua sera tatu ambazo zimepitishwa na serikali zinazochangia kuimarika kwa lugha ya Kiswahili. (alama 3)

Majibu

  1. Eleza kwa ufupi jinsi mambo yafuatayo yanavyodhibiti mitindo ya lugha
    1.  Mazingira (alama 2)
      • Mazingira hudhibiti ishara zinazotumika.
      • Mazingira huathiri toni/ kiimbo
      • Mzungumzaji huchota msamiati kutoka anakozungumzia
      • Mazingira hudhibiti urasmi wa lugha
        (alama 2x1=2)
    2. Madhumuni (alama 3)
      • Mada huathiri uteuzi wa msamiati
      • Mada hudhibiti toni inayotumika
      • Usanifu wa lugha hutegemea kule kunakozungumziwa
        (alama 3x1=3)
      • Hali (alama 2)
    3. Hali ya mtu huathiri toni au kiimbo k.m. mtu mwenye huzuni hutumia toni ya chini
      • Muundo wa sentensi huathiriwa na hali ya mtu
      • Hali ya mtu yaweza kuathiri usanifu wa lugha.
        (alama 2x1=2)
  2. Fafanua sera tatu ambazo zimepitishwa na serikali zinazochangia kuimarika kwa lugha ya Kiswahili. (alama 3)
    • Kiswahili kufanywa lugha rasmi
    • Kiswahili kuwa lugha ya taifa
    • Kiswahili kuwa somo la lazima shuleni
    • Kiswahili kutumiwa bungeni kama lugha rasmi
    • Kiswahili kutumiwa katika machapisho ya serikali

 Swali 6

Fafanua sifa kumi za sajili ya shuleni.         

Majibu

  1. Lugha rasmi kv Kiingereza au Kiswahili hutumika.
  2. Lugha sanifu kv Kiingereza au Kiswahili hutumika
  3. Kuhamisha msimbo- Kiingereza na Kiswahili
  4. Kuchanganya msimbo-kiingereza na Kiswahili 
  5. utohozi  k.m picha
  6. msamiati wa kimasomo. Km mitihani
  7. Lugha nyenyekevu/ upole/ adabu-  mwanafunzi kwa mwalimu
  8. Lugha amrishi/ agizi/ kali
  9. Lugha shawishi
  10. Maswali na majibu
  11. Sentensi ndefu ndefu
  12. Kauli zisizokamilika/ Kukatizana kauli
  13. Lugha ya kimafumbo/ tamathali za usemi
  14. Lugha nyepesi/ rahisi kueleweka
  15. lugha chapwa/ legevu
  16. Lugha changamfu
  17. Lugha himizi/ matumaini
  18. Takriri/ uradidi
  19. Viziada lugha/ ishara

 Swali 7

  1. Eleza maana ya lugha ya taifa. (alama 2)
  2. Eleza sababu tatu zinazofanya watu kubadili na kuchanganya ndimi. (alama 3)
  3. Eleza hatua tano ambazo zimesaidia kukuza lugha ya Kiswahili baada ya uhuru nchini Kenya. (alama 5)

Majibu

  1. Eleza maana ya lugha ya taifa. (alama 2)
    Ni lugha iliyoteuliwa kama kitambulisho cha utamaduni na ustaarabu wa taifa zima.
  2. Eleza sababu tatu zinazofanya watu kubadili na kuchanganya ndimi. (alama 3)
    1. Kusisitiza ujumbe.
    2. Upungufu wa msamiati wa lugha moja.
    3. Kutaka kudhihirisha uko kundi Fulani la watu.
    4. Kufahamu lugha Zaidi ya moja
    5. Kuficha ujumbe kwa kundi lingine katika mawasiliano (1x3=3)
  3. Eleza hatua tano ambazo zimesaidia kukuza lugha ya Kiswahili baada ya uhuru nchini Kenya. (alama 5)
    1. Kuwekwa kwa sera.
    2. Kuteuliwa kwa Kiswahili kama lugha ya taifa.
    3. Vyombo vya habari na mawasiliano mfano taifa leo.
    4. Shughuli za biashara.
    5. Uchapishaji wa vitabu.
    6. Shughuli za kidini.
    7. Kampeni za kisiasa zilitegemea matumizi ya Kiswahili. (1x5=5)

 Swali 8

MTU 1: Una shida gani?
MTU 2: Kichwa chaniwanga, tumbo lanisokota na ninahisi uchovu mwingi. Nisaidie tafadhali.
MTU 1: Pole, afya yako itakuwa shwari. Hizi tembe hapa zitakusaidia kupunguza maumivu.
Unapaswa kuzitumia mara tatu kwa siku

  1.                              
    1. Tambua sajili hii ( alama 2)
    2. Kwa kutolea mfano, andika sifa tatu ambazo zingetumika katika sajili hii ( alama 3)
  2. Umepewa jukumu la kuendesha shughuli ya mazishi kijijini mwako. Fafanua sifa tano za lugha utakayotumia wewe na waombolezaji wengine. (alama 5)

Majibu

  1.                                  
    1. sajili ya hospitalini- hizi tembe hapa zitakusaidia
    2. matumizi ya tarakimu-Meza 1x3
      Msamiati wa kitaaluma baina ya madaktari-TB
      Kuchanganya ndimi-lab
      Lugha nyepesi kwa mgonjwa ili aelewe
      Lugha ya ishara-naumwa hapa.
      Kadiria sifa nyingine ambazo hazipo kwenye muktadha
      Zozote 3x1=3
  2.                          
    1. Msamiati maalum wa mazishi, kwa mfano marehemu, waombolezaji
    2. Sentensi ndefu ili kufafanua ili kwelewika
    3. Lugha ya heshima- unapotambua waliohudhuria – kuitwa marehemu
    4. Lugha legevu
    5. Kiimbo cha chini – kwa sababu ya kuombeleza
    6. Takriri – Alikuwa mzuri, alikuwa mkarimu, marehemu
    7. Sentensi fupi - mtuambee
    8. Lugha ya maagizo-wenye magari waegeshe upande wa kushoto
    9. Lugha ya kuliwaza – usife moyo
    10. Matumizi ya nyimbo – ili lukiwaza waliofiwa 

 Swali 9

  1. Eleza maana ya usanifishaji wa lugha. (alama 2)
  2. Taja lahaja zozote mbili za kati. (alama 2)
  3. Kulingana na habari zinazotufikia hivi punde, maafisa watatu wa polisi jana walikana mashtaka ya mshukiwa wa mauaji ya watoto 13 kutoroka kutoka kituo cha polisi.
    1. Tambua sajili inayorejelewa. (alama 1)
    2. Eleza sifa tano za sajili hii. (alama 5)

Majibu

  1. Eleza maana ya usanifishaji wa lugha. (alama 2)
    • Ni uamuzi wa kuchagua lugha moja au mojawapo ya lahaja za lugha na kuifanyia marekebisho ya kimatamshi, kisarufi, kimaana na kimaandishi ili iweze kutumika katika shughuli rasmi. (alama 2/0)
  2. Taja lahaja zozote mbili za kati. (alama 2)
    • Kimvita-Husemwa Mombasa kisiwani
    • Kijomvu-Husemwa maeneo ya jomvu, nje ya Kisiwa cha Mombasa
    • Kingare-Husemwa Mombasa (alama 21=2)
  3. Maafisa watatu wa polisi jana walikana mashtaka ya mshukiwa wa mauaji ya watoto 13 kutoroka kutoka kituo cha polisi.
    1. Tambua sajili inayorejelewa. (alama 1)
      • Sajili ya matangazo/matangazo ya redio/matangazo ya runinga/ Sajili ya magazetini (alama 1/0)
    2. Eleza sifa tano za sajili hii. (alama 5)
      • Mada/anwani huwa fupi na yenye mvuto
      • Matumizi ya tarakimu mfano 13
      • Matumizi ya lugha ya kuvutia
      • Ujumbe huandikwa au husomwa kwa aya fupi fupi ili kuokoa muda.
      • Sentensi aghalabu huwa ndefu kwa lengo la kufafanua.
      • Mara nyingi hutumia wakati uliopita
      • Matumizi ya lugha sanifu
      • Matumizi ya lugha nyepesi/rahisi ili kueleweka

Swali 10

  1. Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali.
    MHUSIKA 1: Order! Order! Nidhamu, Mheshimiwa Fujo. Hili ni onyo dhidi ya tabia hiyo.
    MHUSIKA II: Nisamehe Bwana .........
    MHUSIKAI: Sasa ninakaribisha swali la tatu. Mheshimiwa Pekua, uliza swali lako.
    MHUSIKAIII: Ninaomba kufahamishwa ni kwa nini Waziri wa Maji ameshindwa kusambaza huduma za maji katika kijiji cha Majikame. 
    1. Bainisha sajili ya makala haya. (alama 1)
    2. Fafanua sifa za sajili hii kama zinavyobainika kifunguni. (alama 5)
  2. Bainisha sababu nne zilizopelekea kusanifisha lugha ya Kiswahili.

Majibu

  1.    
    1. Saliti ya bungeni
    2.    
      • Lugha ya bungeni: mheshimiwa nidhamu
      • Lugha mseto/kuchanganya ndimi:order!order!
      • Lugha ya heshima: mheshimiwa, ninaomba
      • Lugha amrishi : hili ni onyo dhidhi ya..
      • Kukatiza ndimi/kauli: nisamehe bwana..
      • Lugha dadisi: mheshimiwa pekua, uliza swali lako
      • Lugha elezi/ fafanuzi: hili ni onyo dhidhi ya tabia hiyo
  2.    
    • wingi wa lahala za kiswahili
    • haja ya kurahisha mawasilia
    • uvumbuzi wa siasa na teknolojia
    • hala ya kusawazisha tafiti katika kusulah
    • sababu ya kielimu - lugha sawazishi ya kufundishia
    • sababu za kiduni - lugha sawazishi ya mahubiri

Swali 11

Wewe ni mfanyabiashara katika soko la Chapakazi,eleza sifa tano za lugha utakayotumia kuwasiliana na wateja pamoja na washiriki wengine siku ya soko. (Alama 10)

Majibu

  • Hutumia msamiati wa biashara kama vile fedha,faida,hasara,bei,bidhaa,uchumi. Hii ni kwa sababu kila sajili huwa na msamiati wake.
  • Matumizi ya lugha shawishi na rahisi kueleweka ili kuweza kumshawishi mteja. Hii inatokana na ukweli kwamba muuzaji anataka kununua kwa bei nafuu kwa mudax mfupi uliopo.
  • Ni lugha yenye ucheshi na porojo kwa sababu ya kutaka kuvutia wanunuzi na kupata wateja wengi Zaidi kwa kuwa kuna ushindani mkubwa. Kuna ai kule kupewa Guarantee.
  • Ni lugha changamfu, kwa jinsi inayofurahisha ili kuwavutia wateja.
  • Ina kuchanganya na kubadili msimbo ili kuwavutia wanunuzi aina mbalimbali. Kwa mfano, “Nunua kwa bei nafuu,almos free!”
  • Ni lugha ya kijazanda na yenye taswira na tashbihi tele . Maelezo ambayo hutumika katika kuvutia wateja yamejaaa vifananisho na bidhaa nyingine ambazo ni bora ama duni kwa minajili ya kuhuisha na kuinua sifa za bidhaa inayohusika.
  • Ni lugha ya kupumbaza na kufurahisha,kwa mfano, ‘Utavaa hadi uzeeke!’Wakai mwingine ni lugha ya kulaghai ili kuuza.
  • Ni lugha iliyojaa matumizi ya chuku. Kwa mfano,”Dawa hii itaondoa wadudu wote nyumbani mwako mara moja!” au “Inatoka Ujapani straight!” ili kuwavutia wateja.
  • Lugha hii huchanganywa na nyimbo na hata mashairi wakai mwingine kama njia ya kuvutia wateja, hasa katika mazingia ya masoko wazi. Kwa mfano: “Ni ya leo,ahahaha,ni ya leo…”Inapotumika kwenye mabango na vipeperushi,sajili hii hutumia picha zinazopendeza kwa rangi, sitiari fiche,vifupisho na vidokezi,maana ni sajili yenye mnato.
  • Ni lugha ya mvutano/malumbano. Mteja hukosoa bidhaa ili kumshawishi muuzaji kushusha bei,naye mwenye bidhaa husifu bidhaa zake.
    Ni lugha yenye heshima na unyenyekevu kwa mnunuzi ili kuwasawishi wateja

Swali 12

  1. Eleza maana za istilahi zifuatazo : (Alama 2)
    1. sajili
    2. lahaja
  2. Taja nadharia tatu za chimbuko la Kiswahili (Alama 3)
  3.     
    1. Eleza maana ya dhana usanifishaji (Alama 1)
    2. Fafanua sababu mbili za usanifishaji wa Kiswahili. (Alama 2)
  4. Eleza dhima mbili za lugha lugha rasmi. (Alama 2)

Majibu

  1. Eleza maana za istilahi zifuatazo : (Alama 2)
    1. sajili - ni muktadha mbali mbali ya matumizi ya lugha
    2. lahaja - ni vilugha vidogo vidogo vinavyotokana na lugha moja kuu.
      (1×1=2)
  2. Taja nadharia tatu za chimbuko la Kiswahili (Alama 3)
    1. Kiswahili ni lugha ya Kiafrika yenye asili ya Kibantu
    2. Kiswahili ni lahaja ya Kiarabu
    3. Kiswahili ni lugha ya mseto
  3.    
    1. Eleza maana ya dhana usanifishaji (Alama 1)
      • Ni uteuzi na uimarishaji wa lahaja moja ya lugha miongoni mwa lahaja nyingine ili kutumika katika shughuli rasmi. (1×1=1)
    2. Fafanua sababu mbili za usanifishaji wa Kiswahili . (Alama 2)
      • Kuwepo kwa lahaja nyingi za Kiswahili
      • Kulikuwa na hati tofauti zilizotumiwa kuandika Kiswahili
      • Shughuli mbali mbali za kidini
      • Haja ya kusawazisha maandishi ya kitaaluma
      • Haja ya kuwa na lugha moja ya mawasiliano na elimu
        (1×1=2)
  4. Eleza dhima mbili za lugha lugha rasmi. (Alama 2)
    • Kuendesha shughuli zote katika ofisi za serikali
    • Kufundisha shuleni. (1×1=2)

Swali 13

  1. Ndada, mbona umerara sana na kecho akuna kazi. 
    1. Mzungumzaji ana tatizo gani? (Alama 2) 
    2. Tatizo hili limesababishwa na nini? (Alama 1)
  2. Watu wanapozungumza huenda wakafanya makosa ya sarufi na ya kimatamshi hapa na pale, na hata hutumia msamiati vibaya. 
    Eleza sababu saba za kufanywa makosa haya (Alama 7) 

Majibu

  1.  
    1. Athari za lugha ya kwanza.
    2. Ujuzi wa lugha nyingi za mzungumzaji
  2.  
    • kutofahamu kanuni za sarufi
    • kutafsiri lugha ya mama katika Kiswahili
    • upungufu wa viungo vya kutamkia kama meno, ulimi
    • ukosefu wa baadhi ya sauti za Kiswahili katika lugha ya asili
    • kuzungumza kwa haraka
    • ugonjwa
    • kutoimudu lugha vilivyo
    • kurithishwa lugha isiyo sanifu na matamshi mabaya aidha na mwalimu au wazazi.

Swali 14

Rafiki yako amezongwa na mambo magumu na anafikiria suluhu ni kujiua umepewa jukumu la kumshauri.

  1. Utatumia Lugha ya sajili gani? (Alama 2)
  2. Fafanua sifa nane za kimtindo utakazomatumia ili kufanikisha mazungumuzo yako (alama 8)

Majibu

  1. Utatumia Lugha ya sajili gani? (Alama 2)
    • Sajili ya ushauri nasaha/ya ushauri
  2. Fafanua sifa nane za kimtindo utakazomatumia ili kufanikisha mazungumuzo yako (alama 8)
    • Matumizi ya maswali ya balagha-ukijitoa uhai utanufaikaje?
    • Lugha ya ushawishi-maisha ni matamu
    • Kuchanganya msimbo/ndimi-ucommit suicide kwa nini?
    • Matumizi ya tasfida-kujitia kitanzi
    • Matumizi ya chuku-utaenda kwa shetani straight
    • Matumizi ya viziada lugha ili kusisitiza hoja’
    • Lugha ya ucheshi kama vile-mtu akihang anajiendea haja kubwa
    • Matumizi ya lugha yenye mdokezo-watu wataachwa na…
    • Matumizi yenye toni kali ya kuonya kamavile -nitakushtaki kwa polisi
    • Matumizi ya lugha dadisi -mbaona unataka kujitoa uhai
    • Matumiziya nyimbo-kumrai asijiue
    • Matumizi ya maombi-kumshawishi abadili nia
    • Matumizi ya kauli fupi-chagua Maisha.
    • Matumizi ya lugha nyepesi-hamna haja ya kujiua 

Swali 15

Kumekuwa na mijadala mingi kuhusu athari ya chanjo dhidi ya ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Kovid-19.Wewe ni Afisa wa afya katika eneo lenu umealikwa kutoa hotuba kuhusu usalama wa chanjo hii .Eleza sifa kumi za lugha utakayotumia.

Majibu

  • Lugha shawishi – Chanjo ni Salama.
  • Kujisawiri kama mmoja wa walioitumia – mimi nimepata kuambukizwa
  • Kuchanganya ndimi – Chanjo ya Covid – 19
  • Kuhamisha msimbo – we shall overcome.
  • Kutoa ahadi – serikali itatoa chanjo zaidi.
  • Chuku – waliopewa chanjo hawashikwi na magonjwa mengi .
  • Swali balagha – ni nani anayetaka kuangamizwa na ugonjwa huu?
  • Kutumia lugha ya unyenyekevu / kusihi – naomba.
  • Msamiati teule – daktari , sindano , dawa , chanjo .
  • Lugha yenye ucheshi – mtu akipiga chafya timua mbio.
  • Misimu – uviko.
  • Sentensi fupi fupi – kaa nyumbani , vaa barakoa , nawa mikono kwa sabuni na maji.

Swali 16

Maafisa 3 wakana kusaidia mshukiwa wa mauwaji ya watoto kutoroka kituoni."
Maafisa watatu wa polisi jana walikana mashtaka ya kumsaidia mshukiwa wa mauaji ya watoto 13 kutoroka kutoka kituo cha polisi…”

  1. Huku ukitoa sababu mbili, tambua sajili hii. ( alama 3) 
  2. Fafanua sifa zozote saba za sajili hii. (alama 7) 

Majibu

  1. Huku ukitoa sababu mbili, tambua sajili hii. ( alama 3)
    • Sajili ya magazetini/ matangazo
    • Sababu
      • kuwepo kwa anwani/mada yenye mvuto
      • matumizi ya usemi wa taarifa/ lugha ya kuripoti ( sajili 1, sifa 2x1)
  2. Fafanua sifa zozote nyingine saba za sajili hii. (alama 7) 
    1. mara nyingi vichwa vya habari havizingatii sarufi – ili kuokoa nafasi katika gazeti/muda
    2. baadhi ya jumbe ya mambo ya kweli – ili kuvutia wasomaji/ wanunuzi/wasikilizaji/mtazamaji 
    3. mada/ anwani huwa fupi sana na ya kuvutia- ili kuvutia wateja/ wasomaji wa gazeti/wasikilizaji 
    4. lugha inayotumika hutegemea taarifa inayotolewa- kila taaluma ina msamiati wake.
    5. ujumbe huandikwa/husomwa katika aya fupifupi/ kwa muhtasari- ili kuokoa nafasi katika magazeti/muda
    6. lugha yenye kauli/ sentensi ndefundefu- ili kufafanua hoja kikamilifu.
    7. matumizi ya tarakimu badala ya maneno- ili kuokoa nafasi/kusomeka haraka viii) lugha ya kuvutia – “mwalimu aonja asali”
    8. matumizi mengi ya chuku- “ paka amla ndovu”
    9. matumizi ya sitiari/jazanda- ili kutasfidi lugha
    10. matumizi ya lugha rahisi- ili kupasha ujumbe kwa watu wa matabaka yote.
    11. lugha ya maelezo – ili kupasha ujumbe kwa njia nyepese na kueleweka rahisi. (zozote 7x1) 
    12. matumizi ya tasfida – ili kuficha ukali
    13. lugha ya picha / michoro – ili ujumbe ueleweke

Swali 17

Wewe ni mtaalamu wa maswala ya usalama. Umepewa fursa kuhutubia warsha inayojumuisha maafisa wa usalama kutoka katika vikosi mbalimbali kuhusu jukumu lao katika kudumisha usalama,amani na maridhiano nchini.

  1. Taja sajili ambayo utatumia kisha ueleze sababu ya jibu lako. ( alama2)
  2. Andika huku ukifafanua vipengele vinane vya kimtindo utakavyotumia kufanikisha mazungumzo yako. (alama 8)

Majibu

  1. Sajili ya kitaaluma/Mazungumzo rasmi
    Hotuba kwa wataalamu,maafisa wa usalama
  2.       
    1. Nitatumia msamiati maalum
    2. Nitatumia sentensi fupifupi/ndefu ndefu ili kutoa maelezo
    3. Nitatumia lugha rasmi ya Kiswahili
    4. Nitatumia lugha sanifu
    5. Nitatumia lugha ya heshima, mabibi na mabwana
    6. Nitatumia lugha shawishi
    7. Nitatumia lugha ya ushauri
    8. Nitatumia lugha ya tasfida kuficha makali ya msamiati
    9. Nitachanganya na hau kuhamisha msimbo
    10. Nitatumia msamiati wa kutoholewa/maneno ya kukopwa kuakisi maendeleo ya kiteknolojia na zana za kivita.
    11. Nitataja na kunukuu takwimu kwa kutoa ushahidi.
    12. Nitatumia ishara 
    13. Nitatumia lugha ya kuwapa matumaini. 
    14. Nitatumia takriri ili kusisitiza mambo muhimu.
    15. Nitatumia kiimbo kuhalisi hisia tofauti tofauti 

Swali 18

(Mdundo wa muziki) kina mama mpo…..! Kina siste nanyi… are you there? Kampuni ya platinium imewaletea mafuta mpya ya silk. Mafuta hayo yana vitamin C, Sunscreen na yana marashi ya kupendeza. Ukiyatumia kwa wiki moja tu, ngozi yako itakua laini na nyororo kama ya kitoto kichanga. Nayo macho ya wote, Waaa! Yatakuwa kwako 24/7. Jinunulie! Jinunulie! Mafuta ya silk. Mafuta ya wanawake wa kisasa.

  1. Taja sajili iliyotumiwa hapa. (alama 1)
  2. Taja sifa nne za sajili hii. (alama 4)
  3. Kwa nini Wakenya wengi hupenda kuchanganya na kubadili msimbo? (alama 5)

Majibu

  1. Taja sajili iliyotumiwa hapa. (alama 1)
    • Sajili ya matangazo ya biashara.
  2. Taja sifa nne za sajili hii. (alama 4)
    • Hajaa porojo nyingi
    • Lucha huwa nyepesi na rahisi
    • Lugha haizingatii kanuni za lugha
    • Lugha ya kupiga chuku ili kushawishi wasikilizaji.
    • Mbinu ya kuchanganya na kubadili msimbo hutumika.
    • Mbinu ya picha na muziki hutumiwa nikuzidisha mvuto kwa wasikilizaji.
    • Lugha ya mshawasha mno hutumika
    • Lugha ya mkato hutumika.
  3. Kwa nini Wakenya wengi hupenda kuchanganya na kubadili msimbo? (alama 5)
    • Kuonyesha umahiri wa lugha zote mbili.
    • Kuonyesha hisia k.m chuki, huzuni, furaha n.k
    • Kufidia upungufu wa msamiati au lugha anayotumia kukosa msamiati.
    • Ili kujitambulisha na kundi linalotumia lugha Fulani.
    • Kujinasibisha na hadhi ya lugha iwapo katika jamii lugha moja ina hadhi kuliko nyingine.
    • Kutokana na ari ya kutaka kueleweka zaidi.

Swali 19

Eleza hali ya lugha ya Kiswahili nchini Kenya baada ya uhuru (alama.10)

Answers

  • Kiswahili kinafundisha  shuleni ;inatahiniwa kama somo la lazima katika shule za msingi  na sekiondari. Pia kinafundishwa katika vyuo vikuu
  • Kinatumika katika utantgazaji katika vituo vya utangazaji
  • Ni lugha rasmi
  • Serikali inatumia sambamba na Kiingereza katika kusambazia hati za serikali
  • Kinartumika kuendesha shughuli za kitawala katika vituo vya polisi , mahakamani n.k
  • Kinatuika kaika shughukli za kidini
  • Kina tumika katika shughuli za sanaa , maonyesho na muziki
  • Wanasiasa waniona afadhali katika mikutano ya hadhara                     

Swali 20

Umepewa nafasi kuwahutubia washika dau kuhusu jinsi ya kuthibiti ongezeko la vijana wanaofikishwa mahakamani kwa sababu anuai.

  1. Bainisha  sajili utakayotumia.(alama 1)
  2. Andika huku ukifafanua vipengele vinne vya kimtindo vitakavyothibiti uteuzi wa lugha katika sajili hii. (alama 4)
  3. Fafanua majukumu matano yaliyokabidhiwa Kamati ya Inter-Territorial  Language Committee iliyotarajiwa kusanifisha Kiswahili. (alama 5)

Majibu

  1. sheria/mahakamani/ kotini/ daawa
  2.         
    1. msamiati maalumu/ teule/wa kipekee- jela, rufani, hakimu,wakili, shahidi na kadhalika
    2. kuzingatia itifaki Mkuu wa usalama katika Kaunti hii,Manaibu wake,Walimu Wakuu,walimu
    3. lugha rasmi ya Kiswahili au Kiingereza
    4. kunukuu  vifungu vya sharia,sura ya sita ya sharia za nchi yetu…
    5. kuchanganya na kuhamisha msimbo, mfano,Take it from me, kijana atakayevunja sharia …
    6. sentensi ndefu ndefu ili kutoa maelezo.
    7. utohozi wa  msamiati,mfano,jaji.
    8. msamiati wa kukopa kutoka katika lugha nyinginezo kufidia upungufu wa kisayansi/kiteknolojia
    9. lugha sanifu
    10. lugha ya heshima kwa mfano, Mheshimiwa, Mshukiwa, Kiongozi wa Mastaka
    11. Lugha ya kuamuru
    12. Lugha yenye udadisi ili kushirikisha hadhira 
    13. Lugha hudhihirisha ukweli
    14. Lugha ya kushawishi 
    15. Lugha ya maagizo
    16. Lugha legevu inayoeleweka na wote
    17. Matumizi ya viziada lugha-ishara,kiimbo,miondoko na kadhalika.
  3.      
    1. Kusanifisha matumizi ya maandishi ya Kiswahili kote Afrika Mashariki 
    2. Kutunga kamusi za kutumia
    3. Kutafiti lahaja za Kiswahili
    4. Kuboresha vitabu vya shule na vingine vilivyokuwa tayari vimechapishwa.
    5. Kusoma na kuhakiki vitabu vilivyoshughulikiwa na kamati.
    6. Kufanya tafsiri ya vitabu vingine kwa lugha ya Kiswahili
    7. Kujibu maswali yanayohusu lugha ya Kiswahili na fasihi yake.
    8. Kuendeleza lugha moja kwa kuwepo maafikiano kamili katika mamlaka ya \Afrika Mashariki. 
    9. Kuleta ulinganifu wa matumizi ya maneno yaliyoko na maneno mapya kwa kusimamia uchapishaji. 
    10. Kuleta ulinganifu wa sarufi ya Kiswahili kwa kuchapishaaaaaa vitabu vifaavo vya kufundishia.
    11. Kuwatia moyo waandishi na kuwasaidia kuandika katika Kiswahili.
    12. Kuwasaidia wenyeji kuijua lugha ya Kiswahili.

Swali 21

  1. Eleza sifa tano za lugha ambayo wewe kama mnyapara wa kiwanda cha kusaga miwa cha Kimatuni utatumia ukiwahutubia wafanyakazi walio chini yako (alama 5)
  2. Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali (alama 5)
    “Polepole, Mama Mercy! Unajua si kupenda kwangu Tena si hali itakayodumu milele Baada ya siku chache tu, tutakuwa tumekamilisha mradi huo wenye dharura Kisha tutakuwa na muda wa kila kitu Hili, Mama Mercy, ni kile tunaita bad coincidence nimebanwa na kazi Unanielewa ?
    “Dadiinjaasana!”
    Fafanua sifa tano za lugha inayotumika katika huu muktadha wa familia (alama 5)

Majibu

  1. Sifa za sajili ya Viwandani
    1. msamiati teule – kutaja bidhaa zinazozalishwa kama sukari
    2. kuchanganya ndimi – Kiingereza na lugha za kieneo, duty, boiler
    3. sentensi ndefu katika kutoa taratibu na masharti kazini
    4. maswali yanayohitaji majibu moja kwa moja ili kutaka kujua ukweli kuhusu suala fulani
    5. maswali ya balagha – Ukichelewa kazini, unataka nini?
    6. lugha ya maagizo/ uamrishaji – Mtu yeyote asipige simu wakati wa kazi!
    7. ukali – Hakuna kubembelezana tena!
    8. kurejelea sehemu za sheria, katiba au mkataba wa kuajiriwa
    9. kauli kamilifu kwa sababu ni lazima kueleweka bila utata
    10. utohozi – meneja, mashine, trakta
    11. misimu – Sitaki mtu aniletee!
    12. kutozingatia sarufi/lugha legevu – Baadhi ya wafanyakazi huenda hawana kisomo kingi.
      (hoja 5 na mifano ambatani x 1 = 5)
  2. Sifa za sajili ya mazungumzo ya nyumbani baina ya wanandoa katika dondoo
    1. unyenyekevu kuashiria mapenzi – Polepole Mama Mercy!
    2. Lugha yenye ahadi - …tutakuwa na muda wa kila kitu
    3. kutotaja jina halisi mwenza na badala yake kutumiamajina ya watoto – Mama Mercy
    4. maswali elekezi- Unanilewa…?
    5. kukata kauli – Mama Mercy anamkatiza mwenzake kwa kusema ana njaa.
    6. kulumbana – Wahusika wote wawili wanazungumza.
    7. kubadili mada ghafla – Mama Mery amwita Dadii na kusema ana njaa.
    8. kuchanganya ndimi – bad coincidence
    9. kauli fupi ambazo sio sentensi – maneno ya Mama Mercy

Swali 22

  1. Terry: Liandikwalo ndilo liwalo. “Since when has man ever changed his destiny?”
    1. Tambua mtindo wa lugha uliotumiwa na mzungumzaji wa maneno haya. (alama 1)
    2. Eleza sababu nne zinazopelekea wazungumzaji kutumia mtindo huu. (alama 4)
  2. Wewe ni mfanyikazi katika kiwanda cha kutengeneza mavazi. Eleza sifa tano za lugha utayotumia unapowasiliana  na wafanyakazi wenzako. (alama 5)

Majibu

  1.      
    1. kubadili lugha/ misimbo/ndimi/kuhamisha
    2. Kuficha siri/ kutenga wengine
      1. kuelewa/ kumudu matumizi ya lugha zaidi ya moja.
      2. Kutoimudu lugha anayoitumia sawasawa
      3. Kujitambulisha na kundi fulani.
      4. kuonyesah hisia.
      5. Uzoufu wa kuchanganya ndimi.
      6. Kufidia msemaji.
      7. Kutaka kujieleza/ kufafanua zaidi.
      8. Kutafsiri lugha.
      9. Ili kusisitiza jambo Fulani. (4x1=4)
  2.      
    1. Matumizi ya  kauli – kata jora.
    2. Hutaja vyeo vya watu kwa mfano, mkuu wa idara.
    3. Msamiati unaohusiana na mavazi au vifaa vya kiwandani kwa mfano cherehani.
    4. Ukiukaji wa sarufi kwa sababu ya viwango tofauti vya kielimu.
    5. Hutumia misimu ya kiwandani hicho ili kurahisisha  mawasiliano
    6. Lugha nyenyekevu hasa wadogo wanapozungumza na wakubwa wenye hadhi kwenye kumpuni.
    7. Kuchanganya/ kubadili misimbo kwa mfano leta mashini
    8. Lugha ya kuamrisha/ kuelekeza kutoka kwa wakubwa. 

Swali 23

  1. Umechaguliwa na mgombea wa ubunge katika eneobunge lenukatika kufanya kampeni za uchaguzi. Fafanua sifa tano za lugha utakayotumia katika kuendeleza kampeni hizo.
  2. “Maulana akuzidishie baraka.”
    “Amina! Nawe akukinge na dhiki za ulimwengu na baraka ziongezeke kama mchanga baharini.”
    “Atatupa sote tukimwamini kama ilivyo katika maandiko takatifu.”
    1. Taja sajili inyahusishwa na mazungumzo haya. (alama 1)
    2. Fafanua sifa nne za lugha ziliyotumiwa katika mazungumzo haya. (alama 4)

Majibu

  1. Umechaguliwa na mgombea wa ubunge katika eneobunge lenukatika kufanya kampeni za uchaguzi. Fafanua sifa tano za lugha utakayotumia katika kuendeleza kampeni hizo.
    • Matumizi ya msamiati maalum
    • Tamathali za usemi k.v methali
    • Chuku
    • Kuchanganya ndimi
    • Matumizi ya michoro na ishara
    • Matumizi ya nyimbo
    • Lugha legevu/ isiyo zingatia sarufi
  2. “Maulana akuzidishie baraka.”
    “Amina! Nawe akukinge na dhiki za ulimwengu na baraka ziongezeke kama mchanga baharini.”
    “Atatupa sote tukimwamini kama ilivyo katika maandiko takatifu.”
    1. Taja sajili inyahusishwa na mazungumzo haya. (alama 1)
      • Sajili ya dini/ maabadini
    2. Fafanua sifa nne za lugha ziliyotumiwa katika mazungumzo haya. (alama 4)
      • Msamiati maalum- Maulana
      • Lugha yenye matumaini
      • Tashibihi- kama mchanga baharini
      • Kurejelea vitabu takatifu

Swali 24

  1. Wewe ni mtaalamu wa kutoa ushauri nasaha kwa vijana. Umealikwa na shule ya upili ya Bidii kuwazungumzia wanafunzi. Taja mambo matano uatakayozingatia kufanikisha mazungumzo yako. (alama5)
  2. Fafanua jinsi yafuatayo yanavyoathiri matumizi ya lugha. (alama2)
    1. Madhumuni
    2. Uana
  3. Taja mambo matatu yaliyofanyika kukabiliana na changamoto zinazokabili ukuaji wa kiswahili nchini kenya. (alama3)

Answers

  1.  
    1. Kutumia lugha rahisi ya kueleweka na wanafunzi.
    2. Kuchanganya ndimi ili kutaka dhana/ maelezo Fulani yaeleweke zaidi.
    3. Kutumia ucheshi ili kusisimua.
    4. Kurudia baadhi ya mambo nitayotaka kusisitiza.
    5. Kuhusisha nyimbo za mafunzo ili kufanya mazungumzo yavutie.
    6. Kuwahusisha kwa vipindi vya maswali na majibu.
    7. Kuwapa mada za kujadili katika makundi ili kila mmoja ahusike kufanya jambo.
    8. Kutoa mifano ya mambo wanayoyafahamu vizuri.
  2.  
    1. madhumuni- Watu Huteua msamiati kulingana na sababu ya mazungumzo yao. Kwa mfano ikiwa ni mazungumzo ya kumshawishi mtu, mzungumzaji huteua maneno ya kushawishi.
      Mtu hutumia toni tofauti kulingana na madhumuni.
      Madhumuni huamua lugha ambayo mtu atatumia. Kuchanganya ndimi/usanifu wa lugha n.k
    2. Uana- Kuna tofauti baina ya lugha ya wanaume na wanawake. Kwa mfano lugha ya wanawake usheheni matumizi mengi ya vihisishi kinyume na ili ya wanaume.
  3.  (alama 3)
    1. Ongezeko la walimu wa Kiswahili
    2. Vitabu na machapisho zaidi ya Kiswahili Kukifanya Kiswahili lugha ya taifa na rasmi
    3. Kiswahili ni somo la lazima shule za msingi na za upili Kiswahili kufunzwa vyuoni
    4. Kuwa na vyama vya Kiswahili katika shule Utafiti zaidi wa Kiswahili
    5. Makongamano ya kuimarisha Kiswahili kwa walimu na wanafunzi Vipindi vya maigizo kwa Kiswahili/
    6. Taarifa za habari na magazeti ya Kiswahili Kuna vituo vya redio na runinga vinavyopitisha ujumbe kwa Kiswahili tu

Swali 25

  1. Fafanua jinsi kanuni zifuatazo zinavyoathiri matumizi ya lugha katika jamii. (alama 4)
    1. Hali
    2. Uhusiano
    3. Lugha azijuazo mtu
    4. Jinsia
  2. Ukiwa shuleni ulipata nafasi ya kumsikiliza mtaalamu wa masuala ya vijana kuhusu maadili ya jamii.Ni mambo gani ambayo ungezingatia ili kuupata ujumbe wake barabara? (alama 6)

Majibu

  1.  
    1. Hali- Matumizi ya lugha hutegemea hali ya mtu. Kama vile, mtu akiwa mgonjwa, mlevi, mchangamfu, mwenye hasira n.k. Kwa mfano mlevi hutumia lugha legevu na yenye matusi. Mtu mgonjwa hutumia toni ya huruma na upole.
    2. Uhusiano- Lugha hubadilika kutegemea mahusiano ya wazungumzaji.kwa mfano, mtoto hutumia lugha ya heshima anapozungumza na mzazi wake ilhali anapozungumza na rafikize/wanahirimu atatumia lugha ya utani/mzaha.
    3. Lugha azijuazo mtu- Mtu aliye na ujuzi wa zaidi ya lugha moja, ana uwezo wa kuchanganya au hata kuhamisha ndimi anapozungumza.
    4. Jinsia- Lugha hubadilika kutegemea jinsia. Mazungunzo baina ya wanawake yatahusu mambo kama vile mapambo, mavazi,malezi n.k. Mazungumzo kati ya wanaume huenda yakahusu michezo, magari, siasa n.k. Wanawake hutumia msamiati wa heshima na adabu ilhali wanaume hutumia lugha kavu
      (4x1=4)
  2.          
    • Kuuliza maswali kuhusu yasiyoeleweka vyema
    • Kuandika mambo muhimu kwenye daftari.
    • Kusikiliza kwa makini.
    • Kuangaliana na hatibu uso kwa uso anapozungumza ili kupata kila ishara atakayoitumia.
    • Kujibu maswali iwapo atayauliza.
    • Kuketi/kusimama kwa namna itakayoniwezesha kuupata ujumbe bila kusinzia.
    • Kutulia / kuepuka maongezi na wenzangu ambayo yataninyima fursa ya kupata kila kitu kwenye hotuba yake.

Swali 26

"Baada ya mjadala mrefu kuhusu mswada huu na kuzingatia sheria za bunge hili tukufu, kifungu cha 4, kipengele cha 6, ibara ya 3, ndugu zangu ningependa kutangaza kupitishwa kwa mswada huu na sasa utawasilishwa kwa rais kusubiri sahihi yake. Kupitishwa kwa mswada huu kwa kauli moja ni tukio la kihistoria kwa bunge hili. Tutaweza kufikia the two third rule..."

  1. Sifa mbili za sajili ya bunge zinadhihirika katika kifungu hiki. Andika sifa zozote tano huku ukitoa mifano mwafaka. (alama 2)
  2. Fafanua vipengele vingine vitatu vya mitindo ya mawasiliano ambayo mbunge angetumia katika kufanikisha mawasiliano yake. (alama 3)
    Tamu sana! Very sweet! Very nutritious! Onja ujionee! Nunua. Nunua leo. Usikose mummy. Mchukulie mtoto. Fifty na Fifty! Hamsa. Fifty. Bure kwa bure! Bei ya starehe! Burudika.
  3. Tambua sajili hii (alama 1)
  4. Eleza sifa nne za sajili hii kwa kurejelea kifungu. (alama 4)

Majibu

  1.  
    • Matumizi ya sentensi ndefu. Sentensi ya kwanza ina zaidi ya maneno 30.
    • Matumizi ya msamiati maalum. "mswada, bunge"
    • Vifungu vya sheria vinarcjelewa. "kifungu cha 4..."
    • Matumizi ya lugha sanifu. "sentensi ya kwanza ina lugha sanifu"
    • Matumizi ya lugha kavu. "lugha inayotumiwa haina mapambo"
    • Matumizi ya lugha ya heshima. "sheria za bunge hili tukufu..."
    • Kuchanganya ndimi. "kufikia the one third rule..."
    • Lugha ya kuibua utangamano. "ndugu zangu" (zozote mbili)
  2. Matumizi ya uradidi/urudiaji. "mheshimiwa spika"
    • Matumizi ya viziada lugha au ishara za mwili au uso
    • Kutajwa kwa wahusika kwa majina. " Mheshimiwa Tunu"
    • Wabunge kukatizana kalima.
    • Matumizi ya lugha ya mzaha na kukejeliana.
    • Lugha ya maswali na majibu
    • Matumizi ya utohozi. "spika, bajeti"
    • Matumizi ya lugha amrishi hasa na spika. "Mheshimiwa... keti!"
    • Mtindo maalum wa kuanzisha na kuendeleza mjadala. "Mheshimiwa Bwana Spika"
    • Lugha ya kushawishi. "ndugu zangu waheshimiwa naomba"
      (zozote tano za kwanza 5x1=5)
      TANBIHI: Kila sifa iandamane na mfano au maelezo.
      Sifa bila mfano, alama nusu, mfano bila sifa sufuri.
      Tamu sana! Very sweet! Very nutritious! Onja ujionee! Nunua. Nunua leo. Usikose mummy. Mchukulie mtoto. Fifty na Fifty! Hamsa. Fifty. Bure kwa bure! Bei ya starehe! Burudika.
  3. Sajili ya biashara/ sokoni:Anasema nunua leo
  4. Eleza sifa nne za sajili hii kwa kurejelea kifungu.
    • Lugha ya kuvutia hutumiwa, bure kwa bure ili kuvutia wateja.
    • Lugha shawishi mno hutumiwa, mfano bei ya starehe sana/ usikose mummy ili kuwavutia wanunuzi.
    • Kuna matumizi ya takiriri nunua, nunua leo
    • Kuchanganya ndimi, very sweet ili kuvutia wateja wengi.
    • Huwa na ucheshi na porojo ili kuwavutia wateja. Mfano, bure kwa bure Lugha nyepesi hutumika ili kuwasilisha. Bei ya starehe
    • Ubora wa bidhaa husisitizwa, ili kuwavutia wateja. Tamu sana
    • Kuna upigaji chuku mwingi ili kuwavutia wateja. Mfano bure kwa bure.
    • Sentensi fupi fupi hutumika kurahisisha mawasiliano. Mfano nunua, nunua leo.
    • Lugha ya mafumbo-fifty na fifty (ni mia)
    • Mwanafunzi akitoa hoja kisha akose kusema ili, au akose kutoa sababu, alama zake ni nunge.

Swali 27

Bwana spika, ningependa wizara ya usafiri na miundo mbinu ieleze kwa nini ajali za barabarani zinazohusisha usafiri was imma zimeongezeka, na ni hatua gani zimechukuliwa kusitisha ajali huku ikijulikana kuwa kampuni fulani za usafiri zinavunja sheria maksuudi?Juma lililopita watu hamsini ( 50 ) walifariki katika ajali la basi lililokuwa limepata aboria 80 badala ya idadi rasmi ya 62. Ajabu ni kuwa gari hili lilikuwa limepita vizuizi kadhaa vya polisi.

  1. Bainisha muktadha wa dondoo hili. (Al. 2 )
  2. Fafanua sifa nane zinazotambulisha sajili hii. (Al. 8 )

Majibu

  1. Sajili ya bungeni (Al. 2)
  2.    
    • Sentensi fupi fupi .
    • Sentensi ndefu ndefu.
    • Lugha ya majibizano/ kudadisi / maswali na majibu.
    • Kunakili vifungu vya sheria.
    • Lugha ya tarakimu .
    • Matumizi ya msamiati maalum wa bungeni. Mfano, bwana spika, mbunge , waziri, sheria.
    • Lugha ya utohozi. Mfano, spika.
    • Matumizi ya misimu kama UDA, CDF , ODM?
    • Lugha ya adabu .Mfano, bwana spika.

Swali 28

Haya ng`ara leo, nguo moto moto. Fifty hamsa fifty hamsa fifty hamsa na nyingine. Shati shilingi
hamsini tu. Kuona ni bure…

  1. Kando na sifa zinazojitokeza katika Makala haya taja sifa zingine tano za sajili hii. (alama 5)
  2. Eleza juhudi tano zinazofanywa ili kukikuza Kiswahili nchini Kenya na dunia kwa jumla. (alama 5)

Majibu

  1.      
    1. Matumizi ya viziada lugha/ ishara
    2. Matangazo huambatana na picha au michoro
    3. Matumizi ya porojo
    4. Matumizi ya chuku
    5. lugha ya ucheshi
    6. lugha iliyosheheni taswira na tamathali za semi
    7. Lugha yenye kukatizana kauli
    8. Kujinajibisha au kujitambulisha na mteja (hoja za kwanza 5*1=5)
  2. uimarishaji wa kiswahili nchini.
    1. Uchapishaji wa baadhi ya vitabu na magazeti hufanywa kwa Kiswahili. Mfano Taifa leo
    2. Kuna vipindi mbali mbali mbali katika redio na runinga vinavyokuza Kiswahili.
    3. kiswahili kimeingizwa kwenye kompyuta n ahata simu za mkononi
    4. Kiswahili kimefanywa lugha ya taifa nchini Kenya na hata juzi kuteuliwa kule Uganda
    5. Kiswahili hutumiwa kufunzia baadhi ya masomo shuleni.
    6. Kuteuliwa kwa siku ya Kiswahili duniani ni hatua kubwa katika ukuzaji wake.

Swali 29

  1. Eleza sifa tano za lugha ambayo wewe kama mnyapara wa kiwanda cha kusaga miwa cha Kimatuni utatumia ukiwahutubia wafanyakazi walio chini yako. (alama 5)
  2. Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali. (alama 5)
    "Polepole, Mama Mercy! Unajua si kupenda kwangu. Tena si hali itakayodumu milele. Baada ya siku chache tu, tutakuwa tumekamilisha mradi huo wenye dharura. Kisha tutakuwa na muda wa kila kitu. Hili, Mama Mercy, ni kile tunaita bad coincidence... nimebanwa na kazi. Unanielewa...?
    "Dadii...njaa...sana!" Fafanua sifa tano za lugha inayotumika katika huu muktadha wa familia. (alama 5)

Majibu

  1. Sifa za sajili ya Viwandani
    1. msamiati teule - kutaja bidhaa zinazozalishwa kama sukari
    2. kuchanganya ndimi - Kiingereza na lugha za kieneo, duty, boiler
    3. sentensi ndefu katika kutoa taratibu na masharti kazini
    4. maswali yanayohitaji majibu moja kwa moja ili kutaka kujua ukweli kuhusu suala fulani
    5. maswali ya balagha - Ukichelewa kazini, unataka nini?
    6. lugha ya maagizo/uamrishaji - Mtu yeyote asipige simu wakati wa kazi!
    7. ukali - Hakuna kubembelezana tena!
    8. kurejelea sehemu za sheria, katiba au mkataba wa kuajiriwa
    9. kauli kamilifu kwa sababu ni lazima kueleweka bila utata
    10. utohozi-meneja, mashine, trakta
    11. misimu - Sitaki mtu aniletee!
    12. kutozingatia sarufi/lugha legevu - Baadhi ya wafanyakazi huenda hawana kisomo kingi.
      (hoja 5 na mifano ambatani x 1 = 5)
  2. Sifa za sajili ya mazungumzo ya nyumbani baina ya wanandoa katika dondoo
    1. unyenyekevu kuashiria mapenzi - Polepole Mama Mercy!
    2. Lugha yenye ahadi - ...tutakuwa na muda wa kila kitu
    3. kutotaja jina halisi mwenza na badala yake kutumiamajina ya watoto - Mama Mercy
    4. maswali elekezi- Unanilewa...?
    5. kukata kauli - Mama Mercy anamkatiza mwenzake kwa kusema ana njaa.
    6. kulumbana - Wahusika wote wawili wanazungumza.
    7. kubadili mada ghafla-Mama Mery amwita Dadii na kusema ana njaa.
    8. kuchanganya ndimi - bad coincidence
    9. kauli fupi ambazo sio sentensi - maneno ya Mama Mercy

Swali 30

  1. Eleza ukionyesha bayana tofauti baina ya lahaja na lafudhi. (alama 4)
  2. Taja sifa tatu tambulizi za lugha ya misimu (alama 3)
  3. Orodhesha sifa kuu za sajili ya siasa. (alama 3)

Majibu

  1. Lahaja – Tofauti katika matamshi, maumbo na matumizi ya maneno zitokanazo na tofauti za kimaeneo kwa lugha yenye asili moja.
    • Husanifiwa na kupata hadhi ya kuwa lugha; K.M chimiini na Kingazija Kiswahili
    • Yaweza kuandikwa: ndoo tulale, mato yaniuma.
    • Lafudhi- Matamshi ya mzungumzaji yatokanayo na athari za lugha yake ya kwanza,lugha jirani,maumbile au hadhi katika jamii.
    • Hujitokeza kwanza kimatamshi na wala si kimaandishi:
    • Piga ugali (pika), utaguja lini? (utakuja),ndoa la mauti (doa) na kulanga kuku(kula)
      2 x 2 = 4
  2. Sifa za lugha ya misimu:
    Misimu – maneno au semi ziibukazo mahali na zidumuzo kwa muda tu; mzee, kimwana,dot-com,kusota,kupiga ngeta n.k
    1. hupendwa na kutumiwa kwa wingi
    2. huambatana na kitushi / tukio.
    3. hurahisisha mawasiliano / mazungumzo
    4. huzuka na kutoweka baada ya muda
    5. huweza kuingizwa katika maandishi zozote 3 x 1 = 3
  3. Sajili ya siasa
    • Lugha yenye mvuto / ushawishi ari na mwamko
    • Hubeba porojo na ukinzani
    • Hudokeza ahadi na utendaji bora
    • Hupumbaza na kunata
    • Hulenga kundi / watu fulani

Swali 31

“Karibu wageni karibuni
Come and learn with us lugha ya Kiswahili
Nyote mtabenefit sana”
“Kwa nini?”
“Kwa sababu it’s a national language”

Maswali  

  1. Lugha ngapi zimetumika katika muktadha hii? (al 2)
  2. Mtindo wa kutumia lugha zaidi ya moja katika mazungumzo huitwaje? (al 2)
  3. Mzungumzaji mwenye uwezo wa kutumia lugha zaidi moja anaitwaje? (al 2)
  4. Taja sababu za wazungumzaji kutumia lugha zaidi ya moja (al 4)

Majibu

  1. Lugha ngapi zimetumika katika muktadha hii? (al 2)
    • lugha mbili
  2. Mtindo wa kutumia lugha zaidi ya moja katika mazungumzo huitwaje? (al 2)
    • kuchanganya ndimi
  3. Mzungumzaji mwenye uwezo wa kutumia lugha zaidi moja anaitwaje? (al 2)
    • Bilinguo / uwili lugha
  4. Taja sababu za wazungumzaji kutumia lugha zaidi ya moja (al 4)
    • ili kueleweka vizuri
    • kukosa msamiati katika lugha moja
    • kuwa na umahiri katika lugha zote
    • kukosa umahiri katika lugha moja/au zote
    • Kutaka kujihusisha na kundi Fulani  (zozote 4)

Swali 32

... Bwana Spika, ninaomba kufahamishwa kwa nini Waziri wa Biashara ameshindwa kuchuka hatua kukomesha uuzaji wa vileo hatari kwa watoto wa shule. 

  1. Kwa kutolea mfano taja sajili iliyodokezwa hapo juu.  (alama 2)
  2. Fafanua sifa zozote nane za sajili inayorejelewa na maneno haya   (alama 8)

Majibu

  1. Sajili ya bungeni - Bwana spika
  2.  
    1. Utohozi - spika
    2. Lugha amrishi hutumika hasa na spika
    3. Lugha ya heshima na adabu hutumika k.m Aomba
    4. Sentensi ndefundefu ili kuelezea mambo kikamilifu
    5. Wakati mwingine kuna kukatizana kauli.
    6. Lugha ni ya kimdahalo
    7. Huzingatia mtindo wa kuhutubu
    8. Kuna kuchanganya ndimi ili kujieleza vizuri
    9. Matumizi ya ishara lugha/ viziada lugha.
    10. Hutaja vifungo mbalimbali vya sheria
    11. Lugha fafanuzi/ elezi - kutoa maelezo ya kina
    12. Msamiati maalum k.v mswada
    13. Urudiaji wa kauli fulani
    14. Mtindo maalum wa kuanzisha na kuendeleza mazungumzo

Swali 33

“Mabibi na Mabwana …………. Kaunti yetu imebaki nyuma kwa sababu ua uongozi duni.  Raudi hii wababa na wamama pamoja  na vijanaa lazima mabuda maanalogue  tuwasend home.  Mkinidunga votes zenu nitamake sure ………………..

  1. Tambua sajili iliyotumika (al.2)
  2. Eleza sifa za sajili hii (al.8)

Majibu

  1.  
    1. Lugha ya kisiasa
    2. Mkutano wa kisiasa
    3. Lugha ya  kuomba kura       2 x 1 = 2
  2.  
    • Lugha isiyo  sanifu
    • Kuchanganya ndimi
    • Ahadi nyingi
    • Lugha ya kushawishi
    • Msamiati mteule
    • Kukashifu  wengine
    • Kujisifu

Swali 34

Combination ya Ndovu FC kali sana... Anaenda Kalulu. Kalulu anapiga pasi kwa Nyamavu. Nyamavuuu na kabumbu. Lo! Kwake Lukas. Lukas anakwenda. Anakwenda. Mpenzi msikilizaji kumbuka huyu Lukas ni imara kama mwamba siku zote...Anawachachawiza wachezaji wawili wa Twiga FC, anapiga chenga moja, mbili tatuuu...Mpira unakuwa mwingi na kutoka nje... Anayerusha boli ni Zungu, jamaa wa timu ya Twiga, kimo cha mbilikimo lakini ukali wa wembe. Huyu ndiye aliyeifungia timu yako mabao mengi zaidi msimu uliopita. Anaupokca pale Kayaya almaarufu Tornado. Mpira wenyewe ukimwona unaogopa. Anacheza vizuri pale. Anabingirisha ngozi kama anayewafunza wengine. Refa anapuliza kipenga. It's a foul play.

  1. Ukitolea ushahidi jibu lako, tambulisha sajili ya kifungu hiki. (alama 2)
  2. Eleza mtindo wa sajili hii kwa kurejelea kifungu. (alama 8)

Majibu

  1. Ukitolea ushahidi jibu lako, tambulisha sajili ya kifungu hiki. (Al 2)
    • Sajili ya michezo/Sajili ya uwanjani/ Matangazo ya kandanda/kabumbu/mpira wa miguu
    • Kuna kutajwa kwa wachezaji na majina yao. (Sajili alama 1. Ushahidi alama 1)
  2. Eleza mtindo wa sajili hii kwa kurejelea kifungu. (alama 8)
    1. Sentenși fupi fupi. Mfano: Anaenda Kalulu.
    2. Kuchanganya ndimi. Kwa mfano, Combination ya Ndovu FC kali sana.
    3. Kuhamisha ndimi. Kwa mfano, It's a foul play.
    4. Kuna matumizi ya utohozi wa maneno kama vile, pasi, boli
    5.  Matumizi ya tashbihi. Mfano: imara kama mwamba, ukali wa wembe
    6. Kuna mbinu rejeshi kurajelea matukio ya awali. Kwa mfano,...aliyeifungia timu yake mabao mengi zaidi msimu uliopita.
    7. Matumizi ya majina ya lakabu. Mfano Tornado
    8. Kuna matumizi ya nahau kama vile, piga chenga.
    9. Matumizi ya lugha hisishi/nidaa; Lo!
    10. Takriri/uradidi wa maneno. Kwa mfano, anakwenda.
    11. Kutumika kwa vifupisho vya maneno kama vile; refa, FC
    12. Matumizi ya chuku. Mfano: Mpira ukimwona unaogopa.
    13. Uhaishaji wa mpira; unaogopa kwa kumwona mchezaji.
    14. Taswira ya uoni; maelezo kuhusu umbile la mchezaji - kimo cha mbilikimo. Au taswira mwendo; mwendo wa wachezaji uwanjani unapoelezwa.
    15. Pana matumizi ya misimu ya uwanjani kama vile; mpira unakuwa mwingi. 

Swali 35

  1. Umeteuliwa kama mtangazaji wa mashindano ya michezo baina ya shule katika eneo gatuzi ndogo lenu. Eleza sifa tano za lugha utakayotumia. (alama 5)
  2. Jadili mambo matano yanayoathiri matumizi ya lugha katika jamii. (alama 5)

Majibu

  1.                    
    1. msamiati maalum – mpira, mchezaji, uwanja
    2. lugha yenye misimu – sare,
    3. lugha ya uradidi – anakwenda anakwenda
    4. lugha ya ucheshi –
    5. matumizi ya chuku –
    6. utohozi
    7. kuchanganya / kuhamisha msimbo –
    8. kauli fupifupi –
    9. matumizi ya vihisishi-
    10. kauli zisizokamilika (mdokezo)
      ( kadiria siafa zaidi) (zozote 5x1 )
  2.                        
    1. Umri
    2. Mazingira
    3. Uhusiano
    4. Tabaka
    5. Jinsia
    6. Mada
    7. Wakati ( zozote zilizofafanuliwa 5x 1)

Swali 36

Rafiki yako amezongwa na mambo magumu na anafikiria suluhu ni kujiua umepewa jukumu la kumshauri.Fafanua sifa kumi za lugha utakayotumia ili kufanikisha ujumbe wako.

Majibu

  • Matumizi ya maswali ya balagha-ukijitoa uhai utanufaikaje?
  • Lugha ya ushawishi-maisha ni matamu
  • Kuchanganya msimbo/ndimi-ucommit suicide kwa nini?
  • Matumizi ya tasfida-kujitia kitanzi
  • Matumizi ya chuku-utaenda kwa shetani straight
  • Matumizi ya viziada lugha ili kusisitiza hoja’
  • Lugha ya ucheshi kama vile-mtu akihang anajiendea haja kubwa
  • Matumizi ya lugha yenye mdokezo-watu wataachwa na…
  • Matumizi yenye toni kali ya kuonya kamavile -nitakushtaki kwa polisi
  • Matumizi ya lugha dadisi -mbaona unataka kujitoa uhai
  • Matumiziya nyimbo-kumrai asijiue
  • Matumizi ya maombi-kumshawishi abadili nia
  • Matumizi ya kauli fupi-chagua Maisha.
  • Matumizi ya lugha nyepesi-hamna haja ya kujiua

Swali 37

  1. Katika jamii huwa wakati mwingine kuna matumizi ya lugha isiyo ya kistaarabu. Taja mifano mitano ya lugha sampuli hiyo (alama 5)
  2. Taja mambo matano yanayoathiri jinsi tunavyoweza kutumia lugha katika jamii.  (alama 5)

Majibu

  1.  
    • Lugha hutaja sehemu nyeti za mwili wa binadamu kama vile za uzazi.
    • Kutaja mada pale isipofaa mf. Vifo, magonjwa, upimaji wa kinyesi, makamasi nk. Wakati wa kula.
    • Wanataja vilema ua wenye udhaifu wakiwepo k.v zeruzeru, kipofu, kiziwi.
    • Hutumia maneno ya kimatusi k.v mjinga, pumbavu n.k.
    • Hutumia lugha ya kulaani k.v ninakuombea ufe haraka / ufutwe kazi n.k.
      (Hoja zozote 5 x 1 = 5)
  2.  
    • Hadhira mf. wale anaowazungumzia kama ni watoto akatumia lugha yenye ucheshi.
    • Utungo / matini / muktadha – kama ni mashairi atatumia lugha yenye ukiushi.
    • Tabaka mf. la juu amezoea kiingereza hapendi mf. Kiswahili.
    • Hali – chlokoro wanatumia lugha ya kutisha, mlevi, mgonjwa lugha yake huwa tofauti.
    • Mada – zile ngumu hutumia lugha nzito, zile rahisi hutumia lugha nyepesi.
    • Matilaba mf. Mtu anapotaka wenzake wamuunge mkono atatumia lugha ambayo itawavuta kwake.
    • Umri – kundi la kiumri husababisha vilugha mf. Vijana wana mtindo wao. 

Swali 38

Wewe ni wakili katika kesi ya jinai inayoendelea katika Mahakama ya Haki na Uwajibikaji. Hata hivyo, umegundua kuwa hadhira haijamakinika kukusikiliza.  Fafanua sifa za lugha utakayotumia ili hadhira imakinike.

Majibu

  1. Matumizi ya msamiati maalum mfano kesi, mshukiwa, hakimu, mshtakiwa.
  2. Kurejelea kwa vitabu kama katiba na sheria za nchi mfano sheria kifungu nambari 3 sehemu 4…
  3. Lugha ya kudadisi au maswali na majibu ili kuweza kubaini ukweli kabla ya uamuzi kufanywa.
  4. Sentensi ndefu ndefu ili kutoa maelezo ya kina kuhusu uamuzi wa kesi husika.
  5. Matumizi ya lugha rasmi mfano Kiswahili au kiingereza.
  6. Utohozi wa misamiati mfano jaji - judge, korti - court.
  7. Matumizi ya msamiati uliokopwa mfano amicua curiae.
  8. Lugha nyepesi na rahisi kueleweka na watu wa viwango vyote vya elimu.
  9. Matumzi ya lugha sanifu ili kuepuka kupotosha ujumbe au maelezo yanayotolewa.
  10. Kuhamisha na kuchanganya ndimi kwa mfano “Mshtakiwa unaweza kujitetea sasa. Tell the court what happened on that day.”
  11. Lugha ya unyenyekeve na heshima hasa kutoka kwa mshatakiwa mfano “mheshimiwa jaji, naomba mahakama inihurumie kwa kunipunguzia kifungo…”
  12. Kuzungumza moja kwa moja na mshukiwa – wewe mshukiwa.
  13. Urudiaji au uradidi ili kuweka wazo wazi/kusisitiza.
  14. Msamiati wa kawaida kupewa maana maalum, kwa mfano, learned friend kummanisha mwanasheria.
  15. Kauli fupifupi hasa wakati wa kuhoji.
  16. Lugha ya kushawishi ili kutetea upande wako.
  17. Matumizi ya lugha chakavu/kikale.
  18. Kutumia lugha ya mapokezano.
  19. Lugha ya kutaja tareje na wakati wa tukio.
  20. Matumizi ya ishara/viziada lugha ili kusisitiza na kufafanuaa ujumbe. 

Swali 39

  1. Taja nadharia zozote mbili zinazohusiana na chimbuko la lugha ya Kiswahili. (alama 2)
  2. Kwa kutolea mifano, eleza sifa zozote nne za kimsingi za sajili inayoweza kutumika darasani. (alama 8)

Majibu

  1. Nadharia :
    1. Kiswahili kama lugha ya mseto/mchanganyiko wa lugha tofauti za kigeni na za dkiafrika. Ni zao la kuingiliana kwa lugha za kigeni kama kihindi, kiarbu, kiajemi na lugha za makabila ya wenyeji
    2. Kiswahili kama tokeo la ndoa baina ya wanawake wa pwani ya afrika mashariki na waarabu/lugha ya vizalia wa ndoa kama hio.
    3. Kiswahili ni lugha  ya kibantu kulingana na ushahidi wa kiisimu na kihistoria (alama 1 x 3 =3)
  2. Sifa za kimsingi za sajili ya darasani :
    1. Lugha sanifu
    2. Mwingiliano wa kisarufi hudumishwa
    3. Msamiati huegemea kwenye mada husika/maneno ya taaluma mbalimbali hutumika
    4. Urudiaji/takriri – ili kuhakikisha kuwa hoja imeeleweka
    5. Majibizano – kati ya mwalimu na waxnafunzi wanapouliza na kujibu maswali
    6. Sentensi huweza kuwa fupi/ndefu kutegemea mada husika
    7. Imejaa ufafanuzi – wahusika wanapoelezea hoja ili ieleweke vyema

Swali 40

Wananchi watukufu, mimi ni ndume. Wale wanaonichokoza waambiwe Kizingo hawaogopi. Wangoje mpaka next general election. Tupatane kwa debe.

  1. Eleza muktadha wa sajili hii. (alama 2)
  2. Tambua mbinu mbili za lugha zilizotumika katika kifungu hiki. (alama 2)
  3. Eleza sifa sita za sajili uliyotambua hapo juu. (alama 6)

Majibu

  1. Muktadha wa siasa – msamiati maalum umetumika, kwa mfano, next general election.
  2.  
    • Istiara – mimi ni simba
    • Kuchanganya ndimi – Wangoje mpaka next general election.
  3.  
    • Huwa ni lugha ya propaganda
    • Ni lugha ya ucheshi
    • Hutumia chuku
    • Lugha yenye ushawishi
    • Yaweza kuwa na majibizano
    • Ni yenye udanganyifu
    • Imejaa ahadi
    • Ina kudunisha
    • Yaweza kuwa na matusi/bezo
    • Ina majisifu/ majigambo
    • Ina kauli fupi fupi

Swali 41

  1. Eleza maana ya istilahi zifuatazo:
    1. Linguafranka
    2. Sajili
    3. Lahaja
    4. Uwili lugha
    5. Lugha sanifu
  2. Eleza majukumu yoyote sita ya Kiswahili nchini Kenya. (alama 6)

Majibu

  1. Eleza maana ya istilahi zifuatazo:
    1. Linguafranka                                                                                                                 (alama 1)
      • Ni lugha inayotumiwa baina ya watu ambao wanazungumza lugha tofauti kabisa za kwanza.
    2. Sajili                                                                                                                              (alama 1)
      • Ni mtindo wa lugha ambao hutumika katika muktadha mahsusi.
    3. Lahaja                                                                                                                          (alama 1)
      • Ni namna tofauti tofauti ya kuzungumza lugha moja kutegemea eneo au tabaka fulani.
    4.  Uwili lugha                                                                                                                   (alama 1)
      • Ni hali ambapo mzungumzaji mmoja anaweza kutumia lugha mbili.
    5. Lugha sanifu                                                                                                                  (alama 1)
      • Ni lugha au lahaja iliyochaguliwa na kufanyiwa marekebisho ya kimatamshi, kisarufi, kimaana na kimaandishi ili iweze kutumika katika shughuli rasmi.
  2. Eleza majukumu yoyote sita ya Kiswahili nchini Kenya.                                            (alama 5)
    • Ni chombo cha mawasiliano, maingiliano na maelewano baina ya Wakenya.
    • Ni nyenzo ya kuwaunganisha Wakenya wote wenye asili mbalimbali na kuwafanya kuwa kitu kimoja.
    • Ni chombo cha kushirikisha umma katika shughuli zote za taifa.
    • Ni kitambulisho cha Wakenya wote.
    • Hutumiwa na serikali ya Kenya kupitisha sera zake kwa wananchi\

Swali 42

  1. Eleza sifa zozote tano zinazotambulisha sajili ya mazungumzo. (alama 5)
  2. Andika sifa tano za kimtindo utakazotumia ukipata fursa ya kutangaza mchezo wa kandanda shuleni.     (alama 5)

Majibu

  1. Eleza sifa zozote tano zinazotambulisha Sajili ya mazungumzo. (alama 5)
    1. Kuzungumza kwa zamu
    2. Kukatizana kauli
    3. Msamiati maalum kutegemea mada
    4. Lugha husishi – ninakualika
    5. Matumizi ya ishara nyuso (masolugha)
    6. Matumizi ya viziada lugha kusisitiza mada.    ( za kwanza 5×1=05)
  2. Andika sifa tano za kimtindo utakazotumia ukipata fursa ya kutangaza mchezo wa kandanda shuleni. (alama 5)
    1. Kuchanganaya ndimi
    2. Msamiati maalum wa michezo
    3. Utohozi wa maneno
    4. Matumizi ya lakabu
    5. Uradidi wa maneno
    6. Sitiari  - yeye ni nyani
    7. Chuku – kimo cha kuku
    8. Sentensi fupi fupi.   
Join our whatsapp group for latest updates

Download Isimu Jamii Questions and Answers.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest