Online Video Lessons
  • Home
  • High School Notes
    • Mathematics
    • English
    • Kiswahili
    • Biology
    • Chemistry
    • Physics
    • CRE
    • IRE
    • Geography
    • History and Government
    • Agriculture
    • Business Studies
    • Computer Studies
    • Home Science
  • Past Papers
    • KCSE
    • PRE-MOCKS
    • MOCKS
    • National Schools Past Papers
    • High School Term Past Papers
    • KCSE Prediction Papers
    • Topical Revision Questions and Answers
  • Primary School Materials
    • Play Group: Activities, Homework and Syllabus
    • Pre-Primary One - PP1: Activities, Homework and Exams
    • Pre-Primary One - PP2: Activities, Homework and Exams
    • CBC Grade 1: Subjects, Syllabus and Exams
    • CBC Grade 2: Subjects, Homework and Exams
    • CBC Grade 3: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • CBC Grade 4: Exam Papers, Syllabus and Subjects
    • STD 8 Past Papers
    • Biology
    • Chemistry
    • Kiswahili
    • English
    • Mathematics
    • Business
  • Schemes of Work
Featured:
ACIDS, BASES AND INDICATORS - Form 1 Chemistry Notes - Wednesday, 23 January 2019 09:15
AIR AND COMBUSTION - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 09:04
INTRODUCTION TO CHEMISTRY - Form 1 Chemistry Notes - Friday, 11 January 2019 13:43
SIMPLE CLASSIFICATION OF SUBSTANCES - Form 1 Chemistry Notes - Thursday, 17 January 2019 08:43
WATER AND HYDROGEN - Form 1 Chemistry Notes - Tuesday, 22 January 2019 12:34
  • Home
  • Past Papers
  • KCSE
  • KCSE 2014
  • Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Kiswahili Karatasi ya Pili

Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Kiswahili Karatasi ya Pili

Share via Whatsapp
  • Be the first to comment!
« Previous - Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Biology Paper 2 Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Biology Paper 3 - Next »
Download PDF for future reference Install our android app for easier access
  1. UFAHAMU: (Alama 15)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.

    Afisa wa ukaguzi wa abiria na mizigo alimrudishia cheti chake cha usafiri na kubofya tarakilishi yake kuashiria kuanza kumhudumia mteja mwingine. Duma alikichukua cheti chake cha usafiri kwa pupa, kana kwamba anamtarajia mtu kuja kukibwakura. Moyo wake ulitweta na kukisukuma kidari chake kikembe nusura kukipasua. Baada ya kukihifadhi cheti hiki ndani ya mfuko wake mdogo wa kusafiria, alichapuka moja kwa moja hadi chumbani ambamo wasafiri hungojea kuiva kwa safari.

    Si kwamba Duma ni mwanagenzi wa safari za Ughaibuni. La! Hasha. Amekia vilele vya anga kwa muda wa miaka isiyopungua kumi sasa, tangu alipochukuliwa kijijini mwao alipokuwa na miaka kumi na miwili; mjomba wake anakuja kumtafutia kazi. Kazi aliyopata ilimtia tumbo joto mwanzoni, akataka kutoroka, atokomee kokote kule. Fikiria wewe, ndio sasa umetoka kwenye mbeleko ya mama yako, ubwabwa wa shingo ndio unaanza kukutoka, kisha uje kutoswa kwenye kazi ya kuvuna majani kwenye shamba kubwa la Bwana Mali, majani ambayo unapopata fursa ya kuyatafuna yanakufanya kujihisi kama tiara inayoelea angani! Kisha baadaye upagazwe kazi ya kuyauza majani hayo hayo, pamoja na unga unaohifadhiwa katika vifuko vidogo vya kuvutia, kwenye soko la siri na hata shuleni! Hata hivyo walisema wasemao kwamba papo kwa papo kwamba hukata jiwe, na kinolewacho hupata.

    Duma alipata walimu, akafunzwa jinsi ya kuyatumia majani na aina mbalimbali za unga ili kuituliza nadhari ya dhamiri yake ambayo awali ikimsumbua sana. Polepole ule utu na ulimbukeni aliokuwa nao uliyeyuka, akatwaa moyo wa jiwe na kuikumbatia kazi hii kwa dhati ya moyo wake, moyoni akijiambia kuwa hayo ndio majaliwa yake. "Ikiwa hii si utashi wa Mungu, kwa nini akalituma gonjwa kuwaua wazazi wangu, mmoja baada ya mwingine? Kwa nini akawaacha akina ami kunipoka kidogo kilichobakizwa na matibabu ya wazazi wangu? Kwa nini asitume mtu kuja kuniokoa nilipoingizwa kwenye biasharia hii na mjomba Papa?" Duma alijiuliza maswali haya mfululizo. Hatimaye aliihalilisha kazi yake kwa kusema, "Kazi mbi si mchezo mwema."

    Dunia alipopata tajiriba ya kutosha kupambana na walinda usalama wenye macho ya kipanga, mwajiri wake hakusita kumtumia kwenye safari za kusafirisha shehena kwenye masoko ya ng'ambo. Mara nyingi aliponea tundu la sindano kutiwa mbaroni. Wakati mwingine mashine za ukaguzi ziliweza kunusa shehena yake, akalazimika kulainisha viganja vya maafisa wakuu forodha. Kila mara alijiambia, "Hii kazi ni hatari, nikipata pesa za kutosha kuufukuza uhawinde nitang'atuka." Hata hivyo, Duma alikuwa tayari alikwisha kuwa sikio la kufa. Alikuwa amedidimia katika ulanguzi wa dawa za kulevya, ulanguzi ambao ulikuwa umemwingia kwenye mishipa jinsi dawa zenyewe zilivyokuwa zimegeuka damu inayosukuma moyo wake. Badala ya kuacha, yeye na mwajiri wake walizua mikakati mipya ya kusafirisha shehena.

    Safari ya leo ilipoiva, Duma alifanya kama alivyoagizwa na mwajiri wake. Asubuhi na mapema alibugia shehena yake, koo ikakubali kuisafirisha hadi tumboni ambapo uchango wake uliomba kuihifadhi hadi utakapofika wakati wa kuitapika shehena hiyo Ughaibuni. Fungu lililobaki lilitiwa ndani ya begi la kusafiria, katikati ya nguo. Duma alitarajia kwamba atapata jamaa wake wa kawaida kwenye forodha. Akajiambia kwamba hata asipompata huyo jamaa anaweza kuitoa shehena hiyo hiyo kama kafara kwa maafisa wa usalama. Duma alikuwa na bahati ya mtende kumpata huyo jamaa wake, pamoja na afisa wa usalama aliyejuana naye kwa vilemba, akafanikiwa kupitisha shehena zake bila kujua kuwa yake ya arubaini imefika.

    Mara tu Duma alipotua kwenye uwanja wa ndege wa Kamata, Polisi wa Kimataifa walimzingira. Mimwero ya kamera za wanahabari ilitishia kuyapofua macho ya mtumwa huyu ambaye alikuwa sharti auwawe kwa kukubali kutumwa. Vikuku viwili vikubwa vilivirembesha viwiko vya mikono yake ambayo aliikabidhi kwa maafisa hawa kama anayekubali kuwajibikia kosa lake. Nchini mwake mwajiri wake alipiga kidoko alipotazama kadhia hii kwenye runinga. Akasema, "Bloody coward! How can he allow himself to be caught?"

    1. Huku ukitoa mifano mitano, onyesha jinsi haki za binadamu zililivyokiukwa katika kifungu hiki. (alama 5)

    2. Andika vyanzo vinne vya maovu ya kijamii kwa mujibu wa taarifa. (alama 4)

    3. "Yaliyompata Duma ni mwiba wa kujichoma." Thibitisha kauli hii kwa kutoa mifano minne. (alama 4)

    4. Eleza maana ya msamiati ufuatao kulingana na kifungu:(alama 2)
      1. wenye macho ya kipanga
      2. zimegeuka damu inayosukuma moyo wake


  2. UFUPISHO: (alama 15)

    Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.

    Suala la jamii kujitosheleza wa mahitaji ya chakula na lishe ni jambo ambalo halina budi kushughulikiwa kwa dhati. Chakula ni mojawapo ya mahitaji ya kimsingi ya binadamu na kila mja ana haki kupata chakula, na si chakula tu, bali chakula chenye virutubisho muhimu. Nchi isiyowakimu raia wake kwa chakula ni sawa na ng'ombe aliyeshindwa kumnyonyesha ndama wake.

    Kwa muda mrefu, viongozi wamekuwa wakipambana na tatizo la ukosefu wa chakula. Msimu wa kiangazi unapobisha hodi, watu wengi, hasa wale wahitaji, hupukutika kutokana na mng'ato wa njaa. Japo serikali na wafadhili hutuma vyakula vya msaada kwa jamii zilizoathirika zaidi, chakula hiki huwa kama nguo ya kuazima, na bila shaka ya kuazima haikidhi haja.

    Mojawapo ya vyanzo vikuu vya uhaba wa chakula ni kiwango cha chini cha uzalishaji na uhifadhi wa chakula chenyewe. Zipo sehemu nyingi nchini ambazo ni kame. Sehemu hizi hukabiliwa na ukosefu wa maji kwani, ama mvua hainyeshi, au inaponyesha haitoshelezi mahitaji ya mimea. Mimea mingi hujikaukia ikiwa michanga ya kudhihaki juhudi za wapanzi. Zipo sehemu katika nchi hii ambazo huenda kwa misimu hata zaidi ya mitano bila kupata zao lolote kutoka mashambani. Hali ikiwa hivi makali ya uhitaji huzidi na wakazi wa sehemu hizi hulazimika kuwa wategemezi kwa majirani na serikali. Wengine wakikosa chakula huazimia kula visivyoliwa. Wanaamwa la mbwa baada ya kukosa la mama.

    Hali kadhajika, japo zipo sehemu nyingine ambazo hazina tatizo la ukame, mbinu hasi za kilimo husababisha utoaji wa mavuno haba, hivyo kutojitosheleza kwa chakula. Bila shaka wanapopanda ovyo, wanavuna ovyo. Kuna wakulima ambao hupalilia mmomonyoko wa udongo kwa kulima kandokando ya mito, kupanda zao lile lile katika sehemu ile ile ya ardhi miaka nenda miaka rudi, na kutopanda mimea ambayo hukinga tabaka la juu ya udongo dhidi ya kumomonyelewa na maji au upepo. Matokeo ya haya yanaweza kutabiriwa; udongo wenye rutuba huoshwa na mashamba kutwaa utasa ambao huzidisha kuzalishwa kwa chakula haba. Wakulima wengine hukaidi wito wa kupanda mimea ambayo hustahimili ukame kama vile mibaazi, mihogo, mtama, ulezi na wimbi. Baadhi ya wafugaji hufuga mifugo wengi ambao hushindwa kustahimili kiangazi. Si ajabu kupata kwamba katika baadhi ya maeneo, mizoga ya ng'ombe na hata ngamia imezagaa kote, tanuri la kiangazi linapofanya kazi yake.

    Sehemu nyingine zimebarikiwa kwa ukwasi wa chakula. Hata hivyo, baadhi ya wakazi wa sehemu hizi hawana mwao kuhusu umuhimu wa lishe bora. Wapo wanaodhani kuwa chakula ni chakula, bora tumbo lipate haki. Hawa hula vyakula kama vile viazi, mahindi, na wengine nyama bila kujua wanahitaji vyakula vyenye virutubisho muhimu, yaani, wanga, protini, vitamini na madini. Wapo wanaodhani proteni pekee ni nyama. Hawa hula nyama mawio na machweo, matokeo yakiwa kuambulia magonjwa kama vile shinikizo la damu.

    Katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa chakula, serikali, kupitia wizara husika, imeanzisha miradi ya kuhakikisha kuwa kuna uzalishaji wa chakula kwa kiwango cha kuridhisha. Visima vya maji na mabwabwa yamechimbwa katika sehemu kame ili kunyunyuzia mashamba maji. Baadhi ya wakulima wameanza kupanda mimea ambayo inapevuka na kutoa mazao haraka. Ipo mimea ya kuatika ambayo hutoa matunda baada ya muda mfupi, hivyo kusaidia kupunguza makali wa njaa. Wafugaji wengine wameanzisha miradi ya kufuga kuku wa kututumuliwa. Hawa hukua na kukomaa kwa muda mfupi na huweza kutoa nyama na mayai. Wafugaji wa kuku hawa huweza kuwauza kununua aina nyingine ya vyakula.

    Wakulima pia wanahimizwa kutumia njia za kisasa za kuzalisha na kuhifadhi chakula. Chakula kinapohifadhiwa vyema, hata mvua isiponyesha, raia huweza kujitegemea. Ikiwa maghala ya halmashauri ya kuhifadhi chakula nchini hayahifadhi chakula, mara nyingi nchi hulazimika kuagiza chakula kutoka nje kiangazi kinapoajiri. Aidha, chakula kisipohifadhiwa vyema huishia kuharibika na kuhasiri wanaokila, ikawa msiba juu ya mwingine.

    Ni muhimu kufahamu kuwa jukumu la kupambana na ukosefu wa chakula ni la kila raia. Hali ya kungojea kila mara kulishwa na serikali inatufanya kuwa wategemezi zaidi. Wakulima wadogowadogo ambao huuza vyakula vyao kwa bei ya chini sana mara tu wanapovitoa mashambani wanapaswa kujiasa dhidi ya mazoea haya na kujua kuwa akiba haiozi. Wanaoishi katika sehemu zenye vinamasi wasaidiwe kuzitunza sehemu hizi na kuzitumia kwa njia endelevu. Vijana wahimizwe wawaunge wazee mkono kushughulikia kilimo katika sehemu za mashambani badala ya kuhamia mjini kutafuta kazi za ajira ambazo ni haba. Wanaoishi mjini nao wajifunge nira kutumia nafasi walizo nazo kuendeleza kilimo cha bustani.

    1. Fupisha ujumbe wa aya tano za kwanza kwa maneno 100 (alama 9,1 ya mtiririko)

    2. Kwa kurejelea aya tatu za mwisho, eleza njia sita za kukabiliana na uhaba wa chakula. (maneno 85) (alama 6, 1 ya mtiririko)

  3.  MATUMIZI YA LUGHA: (Alama 40)

      1. Eleza maana ya silabi. (alama 2)
      2. Andika neno lenye muundo ufuatao: (alama 1)
        irabu + konsonanti + irabu

    1.  Ainisha vitenzi katika sentensi: (alama 3)
      Ndege yu taabani, hata hivyo anajaribu kujinasua.

    2. Geuza sentensi ifuatayo kwa kufuata maagizo.(alama 2)
      Wachezaji hawakucheza mpira kwa sababu ya mvua.
      Anza kwa: Mpira

    3. Andika sentensi ifuatayo katika wakati ujao hali timilifu.
      Dobi huwapigia watu nguo pasi. (alama 2)

    4. Andika sentensi ifuatayo upya ukizingatia kinyume cha maneno yaliyopgiwa mstari. (alama 2)
      Ubora wa kazi zao ulifichuka baada ya kuanzishwa kwa mradi ule.

        1. Eleza maana ya kirai. (alama 2)
        2. Ainisha virai vilivyopigiwa mstari. (alama 1)
          Zana hizi zimeundwa na mafundi wenye stadi mkubwa.
    5. Kinga ni hali ya kuzuia madhara fulani. Andika maana nyingine mbili za 'kinga'. (alama 2)

    6. Changanua sentensi ifuatayo kwa kielelezo cha matawi. (alama 2)
      Lililimwa vizuri sana.

    7. Bainisha maana mbili zinazojitokeza katika sentensi ifuatayo: (alama 2)
      Wakimbizi walisema kuwa walitamani kurudi kwao mwaka huo.

    8. Eleza maana mbili za sauti ifuatayo: dh. (alama 2)

    9. Andika sentensi ifuatayo katika umoja. (alama 2)
      Hao wenyewe hawakuzingatia mafunzo ya lishe bora.

    10. Tunga sentensi moja kubainisha tofauti ya kimaana kati ya gharama na karama. (alama 2)

    11. Kanusha sentensi ifuatayo: (alama 2)
      Wanafunzi waliingia darasani, wakatoa vitabu wakaanza kusoma.

    12. Tunga sentensi mbili kuonyesha matumizi mawili tofauti ya nukta pacha. (alama 2)

    13. Tumia nomino ya jamii kuwakilisha maneno yaliyopigiwa mstari. (alama 1)
      Nzige wengi sana walivamia na kuharibu mimea.

    14. Onyesha visawe vya maneno yaliyopigiwa mstari. (alama 2)
      Washiriki wote walituzwa medali baada ya mchuano huo.

    15. Nomino zifuatazo ziko katika ngeli gani? (alama 1)
      1. Furaha...
      2. Nyasi.......

    16. Uganisha sentensi hizi ukitumia kiunganishi cha kinyume. ( alama 2)
      Wananchi walikabiliwa na hatari.
      Wananchi waliendelea kuwaokoa majeruhi.

    17. Andika upya sentensi ifuatayo ukianzia kwa yambwa tendwa. (alama 2)
      Wafugaji waliwakatia ng'ombe wote majani ya mti huo.

  4.  ISIMU JAMII: (Alama 10)

    1. Umepewa jukumu la kuwazungumzia vijana wenzako kuhusu umuhimu wa uwekezaji. Fafanua sifa tano za lugha utakayotumia. (alama 5)

    2. Eleza sifa tano za sajili ya kidini. (alama 5)

Please download this document as PDF to read all it's contents.

Why PDF Download?

  • You will have the content in your phone/computer to read anytime.
  • Study when offline.(No internet/data bundles needed.)
  • Easily print the notes to hard copy.

Either

Click here to download the pdf version of "Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Kiswahili Karatasi ya Pili", and read the full contents of this page

OR

CLICK HERE to get "Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Kiswahili Karatasi ya Pili" on Whatsapp

OR




Read 2330 times Last modified on Thursday, 18 October 2018 17:29
Ask a question related to this topic in the comment section below.

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.

« Previous - Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Biology Paper 2 Kenya Certificate Of Secondary Education(KCSE 2014) Biology Paper 3 - Next »
Print PDF for future reference Join our whatsapp group for latest updates
Published in Kenya Certificate of Secondary Education ( KCSE ) 2014
back to top

EasyElimu Banner

Join our telegram group Download Notes

  • KCSE Revision Questions
  • Privacy Policy
  • Mobile App Privacy Policy
  • Elimuza
CSS Valid | XHTML Valid | Top | + | - | reset | RTL | LTR
Copyright © Dailynews 2021 All rights reserved. Custom Design by Youjoomla.com
KCSE 2014