Kiswahili Questions and Answers - Form 1 Mid Term 2 2022

Share via Whatsapp

MASWALI

  1. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali. (alama 10)
    Malenga mlotukuka, kwa tungo zenu teule
    Tungo zenye kusifika, zenye na nasaha tele
    Naomba la uhakika, jawabu enyi wavyele
    Wa kuume tangu lini, kuukata wa kushoto !
    Tangu dahari miaka, mikono ina upole
    ‘Meungana pasi shaka, ni miwili vile vile
    Mmoja ukisumbuka, mwingine hujaa ndwele
    Wa kuume tangu lini, kuukata wa kushoto !
    Wa kuume ukicheka, wa kushoto nao vile
    Ulipofanya dhihaka, kwamba unao upele
    Wa kushoto hutanzuka, kuukuna kwa vidole
    Wa kuume tangu lini, kuukata wa kushoto !
    Kimako leo amaka, kushoto haoni mbele
    Kumbe kuume kushika, kudhibiti mtale
    Misuli ‘metutumuka, hajali hana simile
    Wa kuume tangu lini, kuukata wa kushoto !
    Tamati ninaondoka, nawachia wakale
    Uamuzi wa haraka, ufanyike msilale
    Umenijaa wahaka, mwanzo wa ngoma ni lele
    Wa kuume tangu lini, kuukata wa kushoto !
    Maswali
    1. Shairi hili ni la aina gani? (Alama 1)
    2. Eleza vina vya shairi hili. (Alama 2)
    3.      
      1. Mizani ni nini ? (Alama 1)
      2. Shairi hili lina mizani ngapi katika ubeti wa nne mshororo wa tatu ? (Alama 1)
    4. Taja na ueleze maana ya kibwagizo cha shairi hili. (Alama 2)
    5. Taja jambo ambalo hufanywa na mikono yote miwili kwa pamoja. (Alama 1)
    6. Toa maana ya maneno haya kama yaliyotumiwa katika shairi. (Alama 2)
      1. Dahari
      2. Kuume
  2. MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 20)
    1. Taja konsonanti ,mbili za ufizi. (Alama 2)
    2. Taja irabu mbili za nyuma. (Alama 2)
    3. Toa mifano mitatu ya ala tuli za kutamkia. (Alama 3)
    4. Ni nini maana ya kiyeyusho/nusu – irabu ? (Alama 1)
    5. Andika maneno mawili kwa kila mojawapo ya sauti hizi mwambatano. (Alama 2)
      1. Nj
      2. Sw
    6.    
      1. Eleza maana ya silabi. (Alama 1)
      2. Onyesha silabi za neno parapanda. (Alama 2)
    7. Taja aina moja ya kamusi. (Alama 1)
    8. Mtu anayehudumu maktabani huitwaje ? (Alama 1)
    9. Tambua aina za maneno katika sentensi hii. (Alama 2)
      Mtoto mtukutu ameadhibiwa vibaya.
    10. Nomino hizi ziko katika ngeli gani ? (Alama 1)
      1. Mkoba
      2. Ngao
    11. Kamilisha methali hizi. (Alama 1)
      1. Kikulacho ……
      2. Jambo usilolijua …
    12. Onyesha matumizi mawili ya nukta pacha/koloni. (Alama 1) 


MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. Tarbia
  2. Kina cha kati/ndani – ka, kina cha mwisho/nje – le
  3.          
    1. Sauti yenye mdundo katika shairi.
    2. Mizani kumi na sita
  4.    
    • Wa kuume tangu lini, kuukata wa kushoto !
    • Tangu lini mkono wa kulia ukaukata wa kushoto ?
  5. Kucheka, kusumbuka
  6.    
    1. Zamani, kale
    2. Kulia
  7. MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 20)
    1. /d/,/t/,/n/,/l/,/r/,z/,/s/
    2. /o/,/u/
    3. kaakaa laini, kaakaa ngumu, ufizi, meno, koo, pua
    4. Konsonanti inayotamkwa bila ya hewa kufungiwa/ kuzuiliwa/ kubanwa
    5.    
      1. Njema, njumu, njama, njuga, njenje, njiiti, njozi (mtahini ahakiki jibu)
      2. Swali, swara, sweta, Kiswahili, swila (mtahini ahakiki jibu)
    6.    
      1. Tamko linalotolewa kwa mpigo katika neno/ mpigo mmoja wa sauti katika neno.
      2. Pa-ra-pa-nda
    7.    
      • Kamusi ya kiswahili sanifu
      • kamusi ya semi na nahau
      • kamusi ya methali
      • kamusi ya vitendawili
      • kamusi ya sayansi (mtahini ahakiki jibu)
    8. Mkutubi
    9. Mtoto mtukutu ameadhibiwa vibaya.
         N        V             T                   E
    10.      
      1. U – I
      2. I – ZI
    11.      
      1. Ki nguoni mwako
      2. Ni kama usiku wa kiza
    12.      
      • Hutumika kabla ya kutoa orodha
      • Kuandika tarehe
      • Kuandika saa
      • Kuonyesha masomo ya Biblia
      • Kutoa mada ya barua rasmi
      • Katika mazungumzo ya moja kwa moja/ mchezo wa kuigiza ( Baada ya jina la msemaji)
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Questions and Answers - Form 1 Mid Term 2 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest