Maagizo
- Jibu maswali yote.
MASWALI
- SEHEMU YA A-TAMTHILIA:KIGOGO (Pauline Kea)
“Oooh bebi,miaka yaenda mbio sana,nayo sura yako inachujuka…”- Weka dondoo hili katika muktadha wake.(alama 4)
- Mhusika anayehusishwa na wimbo huu ana msimamo gani wa kimapinduzi?(alama 8)
- Eleza sifa zozote nane za mhusika huyu.(alama 8)
- SEHEMU YA B-DIWANI YA TUMBO LISILOSHIBA NA HADITHI ZINGINE (Wah. Dumu Kayanda Na Alifa Chokocho)
Shibe Inatumaliza:Salma Omar- Jazanda ni mbinu mojawapo ya mbinu za lugha zilizotumiwa kwa ukamilifu.ukirejelea hadithi shibe inatumaliza fafanua mifano kumi.(alama 10)
- “…lakini kula kunatumaliza vipi?
- Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)
- Eleza jinsi kula kunavyo tumaliza kwa mujibu wa hadithi.(alama 6)
- SEHEMU YA C- RIWAYA YA CHOZI LA HERI (Assumpta K. Matei)
“…Maisha yangu yalijaa shubiri tangu utotoni.”- Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)
- Kwa kutolea mfano,bainisha tamathali ya usemi inayojitokezakatika kauli hii.(ala2)
- Jadili athari za vita katika jumuia ya chozi la heri.(alama 14)
MWONGOZO
- ”oooh bebi,miaka yaenda mbio sana,nayo sura yako inachujuka…
- Weka dondoo hili katika muktadha wake.(alama 4)
- Ni wimbo wa daudi kabaka anaouimba ngurumo.
- Anamwimbia tunu
- Wako mangweni pahali pa ulevi
- Alikuwa anamdhihaki tunu na wanaharakati wengine kuwatembelea ili kuwahamasisha kuhusu udhalimu wa majoka na kuwa ni vyema waupinge.
- Mhusika anayehusishwa na wimbo huu ana msimamo gani wa kimapinduzi?(alama 8)
- Ana msimamo dhabiti.Tunu anasimama kidete bila uoga kupambana na udhalimu wa utawala wa Majoka.
- Ni mfano bora wa watu wa jamii:kuwajibika na kuchukua jukumu la kuikomboa jamii inayokandamizwa.
- Anafanikiwa kushawishi wananchi wasihudhurie sherehe za uhuru na badala yake wakusanyike katika eneo la soko la Chapakazi ili wadai uhuru wa kweli.
- Mateso ya kupigwa na kudhulumiwa na utawala havikatizi ari yake katika kuleta mapinduzi.
- Baadaye kutokana na jitihada zake pamoja na wanaharakati wengine,uongozi wa Majoka unaondolewa na soko linafunguliwa tena.
- Anakataa kuozwa kwa lazima
- Ni mwanamke jasiri kwani hamuogopi Majoka.
- Ni mwanaharakati wa kimapinduzi.
- Eleza sifa zozote nane za mhusika huyu.(alama 8)
- jasiri na mkakamavu
- mwenye busara
- mwenye msimamo dhabiti
- Ni mzalendo mwenye mapenzi ya dhati kwa nchi yake.
- Mshawishi
- Mwajibikaji
- Msomi
- Mwenye utu/mkarimu
- King’anga’nizi-aling’ang’ania kudai haki mpaka akaangusha utawala wa Majoka.
- Mtetezi
(mwanafunzi lazima aweze kufafanua sifa zozote )
- Weka dondoo hili katika muktadha wake.(alama 4)
-
- Mifano kumi ya jazanda katika “shibe inatumaliza”. (alama 10)
- "sasa” na “mbura”-kusasambura(kumaliza kila kitu ,kupora mali yote.)
- sherehe-mipango isiyo na maana ya kufilisi mali ya umma.
- mchele wa Mbeya-bidhaa za humu nchini za zenye manufaa makubwa/rasilmali za kiasili.
- mchele wa basmati-bidhaa duni za kigeni.
- kupakua vyakula-kupora mali ya umma.
- kupika-kuzalisha mali
- magonjwa-matatizo yanayokumba nchi
- shibe-tamaa inayosababisha ufisadi.
- kula-kufisidi nchi
- Sherehe-unyakuzi wa mali za umma
- wapishi-wafanyakazi/wanaozalisha mali.
- vyakula-rasilmali za nchi
- “…lakini kula kunatumaliza vipi?
- Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)
Haya ni maneno ya sasa akimwambia mbura katika sherehe baada ya kula .wanazumzia ile hali ya matumbo yao kushiba ilhali wengine wanadhikika tu. - Eleza jinsi kula kunavyo tumaliza kwa mujibu wa hadithi.(alama 6)
- Magonjwa-sukari,presha,saratani,obesity,madonda ya tumbo.
- Vifo-kuuana kwa mabomu,risasi,kunyongana,kuuana kifikra.
- Kunyang’anyana vinavyoonekana na visivyoonekana-haki,utu,heshima,uhuru.
- Kutochunguza vyakula
- Kutochunguza utendakazi wa wafanyikazi.
- Kutowajibikia kazi zao
- kuwalipa watu hawafanyi kazi mishahara.
- Kukosekana kwa dawa
- Kuchangia kuzorotesha uchumi.
- Mali ya umma kunyakuliwa.
- Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)
- Mifano kumi ya jazanda katika “shibe inatumaliza”. (alama 10)
- SEHEMU YA C. RIWAYA YA CHOZI LA HERI.
“maisha yangu yalijaa shubiri tangu utotoni.”- Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)
- Haya ni maneno ya chandachema.anawaambia kairu,umu,zohali na mwanaheri.wako katika shule ya tangamano.
- Chandachema anawasimulia wenzao dhiki alizopitia maishani mwake baada ya kuzaliwa.
- Kwa kutolea mfano,bainisha tamathali ya usemi inayojitokeza katika kauli hii.(alama 2)
- Msemo/nahau-kujaa shubiri
- Jazanda-kujaa shubiri:maisha yake yalikuwa na matatizo mengi.
- Jadili athari za vita katika jumuia ya chozi la heri.(alama 14)
- Vifo:vitabaina ya pande za mwekevu na yule mpinzani wake wa kisiasa vilisababisha mauaji.
- Uharibifu wa mali.aila ya Ridhaa kuangamizwa katika moto:nyumba na mali kuteketezwa.
- Ukosefu wa makazi bora.kaizari na wenzake wamekosa makazi bora kule msitu wa mamba walikotorokea.vibanda vinasongomana.
- Huzuni –ridhaa alihuzunika sana baada ya aila yake na mali zake kuteketezwa kwa moto.
- Hasara kwa wafanyabiashara.wahalifu waliingia katika maduka ya kibiashara za kihindi,kiarabu na kiafrika na kupora mali ya wenyewe.
- Kutiwa nguvuni:waporaji waliopora maduka wakati wa vita walitiwa nguvuni na kukabiliana na mkono wa kisheria hapo baadaye.
- Watu kutoroka Makwao:wahafidhina walihama makwao wakati wa vita bila kujua walikokuwa wakielekea.
- Utegemezi:kukosekana kwa chakula katika kambi yam situ wa mamba kulifanya watu kutegemea msaada wa chakula kutoka kwa wahisani k.v shirika la msalaba mwekundu.
- Majeruhi. Kuna mwanamme aliyevamiwa na kuumizwa kwenye mgogoro wa kupigania ardhi katika eneo la tamuchungu.Alilazwa katika kituo cha mwanzo mpya.
- Kukatizwa masomo.mfano lime na mwanaheri
- Kusababisha uyatima-vita katika kambi yam situ wa mamba vinasababisha walinda usalama kuua wazazi na kuwaacha watoto peke yao.
- Kubakwa-baada ya fujo kuzuka lime na mwanaheri wanabakwa na wahuni.
- Magonjwa-ridhaa aliugua shinikizo la damu kutokana na mshtuko wa kupoteza jamaa yake.
- Kusambaratishwa kwa jamaa.mfano selume
- Athari za kisaikolojia
- Eleza muktadha wa dondoo hili.(alama 4)
Join our whatsapp group for latest updates
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Download Kiswahili Questions and Answers - Form 4 Mid Term 2 Exams 2023.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students