Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 4 End Term 2 Exams 2023

Share via Whatsapp
MAAGIZO:
  • Andika insha mbili. Insha ya kwanza na ya lazima.
  • Kisha chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia.
  • Kila insha isipungue maneno 400.
  • Kila insha ina alama 20.
  • Kila insha lazima iandikwe kwa lugha ya Kiswahili.
  1. Umetangazwa  kuwa  mwanafunzi  bora katika  mtihani  wa kitaifa. Mwalimu Mkuu wa shule ya upili ya Tujitahidi  amekualika  katika shule  hii  yake kuwahutubia  wanafunzi  kuhusu  kilichochangia ufanisi  wako. Toa  hotuba  yako.
  2. Ufisadi umekuwa  tatizo sugu katika nchi  ya  Kenya. Jadili  kuhusu  madhara yake huku ukipendekeza njia za kuukabili.
  3. Tunga kisa  kitakachodhirisha  maana  ya  methali:
    Ukiona vyaelea vimeundwa.
  4. Tunga  kisa  kitakachomalizika  kwa: . . .Hapo  ndipo  nilipotambua  kuwa ukitenda  wema umetendea nafsi yako.  

MARKING SCHEME

  1. Huu ni utungo kiuamilifu Vipengele viwili vikuu vya insha ya aina hii viweze kushughulikiwa. Vipengele hivi ni:
    1. Maudhui
    2. Muundo
      • Muundo wa hotuba. Mtahiniwa azingatie mundo au sura ya hotuba. Vipengele vifuatavyo vya kimsingi vizingatiwe.
    3. Anwani ya hotuba.
    4. Anwani itaje kuwa ni hotuba.
    5. Anwani itaje mada na hotuba.
Utangulizi
Huanza kwa salamu au mwito wa kuhamasisha hadhira inayohutubiwa .Hatibu huanza kwa kutaja waliofika kwa vyeo vyao. Aliye na cheo cha juu zaidi ndiye hutangulia kwanza. Maamkizi hufuatwa na lengo la hotuba.
 
Mwili
Maudhui yenyewe hutolewa. Kila hoja hufafanuliwa kwa aya yake. Hoja hupangwa vyema ili mawazo yatiriirike vyema. Mtahiniwa aliyejitosheleza kimaudhui awe na hoja tano au zaidi zilizofafanuliwa vilivyo.
 
Hitimisho
Hatibu anaweza kurejelea aliyoyahutubu kwa muhtasari. Anaweza pia kushukuru hadhira.
 
Maudhui

Mtahiniwa anaweza kuibuka na hoja zinazohusiana na mada. Baadhi ya hoja hizo ni:
  1. Kuwa na nidhamu ya hali ya juu.
  2. Jitihada katika masomo.
  3. Kuwaheshimu walimu, wazazi na wanafunzi.
  4. Kufuata ushauri nasaha wa wakubwa.
  5. Kumcha Mungu.
  6. Kushughulikia kazi ya ziada na kudurusu vitabu vingi.
  7. Kutopoteza wakati wowote.
  8. Kuamka na kuingia darasani mapema.
  9. Kukamilika kwa mtaala mapema.
  10. Kuepuka kukwaruzana na mamlaka shuleni.

Tanbihi

Mtahiniwa akikosa sura ya hotuba aadhibiwe kwa kutolewa alama nne za sura  4s.

  1. Hii ni insha ya kujadili au kufafanua hoja.
    Hoja ziweze kuzungumziwa madhara ya ufisadi na vilevile suluhu.
    Baadhi ya hoja za madhara ni:
    1. Kutopata huduma muhimu bila hongo.
    2. Kusambaratika kwa uchumi wa taifa.
    3. Kutupiliwa mbali kwa mitihani ya kitaifa.
    4. Watu kufutwa kazi kwa sababu ya ufisadi.
    5. Kuharibu mazingira.
    6. Kufungwa jela kwa wahusika.
    7. Viongozi kupoteza nyadhifa zao.
    8. Kuleta fedheha kwa familia.

Baada ya hoja za suluhu: 

  1. Kuhamasisha wananchi kuhusu athari za ufisadi.
  2. Kutia mbaroni wahusika na kuwashtaki.
  3. Kutaifisha mali iliyonyakuliw kwa njia ya ufisadi.

Tanbihi:

Mtahiniwa aweze kufafanua angaa hoja tano kikamilifu.

  1. Hii ni insha ya methali
    \Kisa kidhidhirishe maana ya methali. Maana ni kwamba ukiona vyombo vya bahari vikielea vimeundwa kisayansi. Tunapoona mambo ya watu yakifanikiwa tukumbuke wameyafanyia kazi. Methali hii inahimiza juhudi na bidii maishani.

    Kisa kinaweza kudhihirisha hali zifuatazo:
    1. Mhusika awe amefanikiwa kimaisha kwa sababu ya juhudi zake.
    2. Anaweza kuwa tajiri kwa sababu ya bidii yake ya kikazi.
    3. Mtahiniwa aibuke kuwa bora zaidi katika mtihani kwa sababu ya kusoma kwa bidii.
    4. Kampuni ifanikiwe kwa sababu ya kazi ambzo zimefanywa na wafanyikazi .

Tanbihi: 

Kisa kionyeshe upande wa kuundwa na upande wa kuelea. Yaani upande wa bidii na upande kufanikiwa. Kisa kikikosa kuoana na maana ya methali mtahiniwa atakuwa amepotoka. Akiandika kuhusu upande mmoja atakuwa amepungukiwa kimaudhui.

  1. Hii ni insha ya mdokezo

Maneno kiini ni kutenda mema na kuwa umetendea nafsi yako. Mtahiniwa atunge kisa ambacho kitaoana na mdokezo. Mtahiniwa anaweza kutumia mbinu rejeshi ili kuonyesha wema mhusika aliutenda. Hatimaye aonyeshe vile mhusika huyu aliweza kutendewa wema kama alivyotenda.

Tanbihi:

Mtahiniwa atakuwa amepotoka pale tu kisa chake kitakuwa kimekosa kuoana na mdokezo.
Atakapokosa kumalizia na kidokezo atakuwa tu amepungukiwa kimtindo lakini hajapotoka.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 4 End Term 2 Exams 2023.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest