Kiswahili Paper 3 Questions - Maseno Mock Examinations 2022

Share via Whatsapp

MASWALI

SEHEMU A: FASIHI SIMULIZI

  1. Lazima
    Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali
    Mabibi na mabwana. Siku hii ya leo nina furaha riboribo. Furaha ghaya. Furaha inayoshinda mwanamke aliyepata salama. Mbona nisiwe na furaha na buraha katika jamii hii iliyotuka ikashinda utukufu wenyewe? Jamii hii yetu imedumu kwa miaka na mikaka. Kisa na maana? Umoja wetu. Mshikamano wetu. Undugu wetu. Muungano wetu. Sote twafahamu fika bila chembe chochote cha walakini kwamba umoja ni nguvu utengano ni udhaifu. Nani asiyejua utu ni ubinadamu? Kwamba kinachotutofautisha na hayawani ni utu? Utu imara na dhabiti usiotikisika wala kusukasuka katika mawimbi na dhoruba za aushi. Hakuna adinasi anayeweza kusimama tisti kama mbuyu akiwa pekee. Asiyejua kifai kwamba jifya moja haliinjiki chungu nani?
    1. Tambua kipera hiki cha mazungumzo cha fasihi simulizi. (alama 1)
    2. Huku ukitoa hoja tano, fafanua umuhimu wa kipera. (alama 5)
    3. Bainisha vipengele vya kimtindo vilivyotumiwa kuwasilisha ujumbe. (alama 3)
    4. Unanuia kutumia mbinu ya mahojiano kukusanya habari kuhusu kitanzu hiki.
      Eleza manufaa matano ya kutumia mbinu hii. (alama 5)
    5. Eleza maana ya ngomezi. (alama 1)
    6. Fafanua sifa tano za ngomezi. (alama 5)
  2. SEHEMU B: RIWAYA
    A. Matei: Chozi la Heri
    Jibu swali la 2 au la 3
    “Hajui vipi, lakini moyoni ametia nia, na penye nia bila shaka njia hupatikana. Ataanzia hapa kuyabadilisha maisha yake ya dhiki kuwa ya heri.”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
    2. Bainisha vipengele viwili vya kimtindo. (alama 2)
    3. Fafanua sifa sita za mrejelewa. (alama 6)
    4. Kwa kurejelea riwaya ya Chozi la Heri eleza jinsi wahusika wanabadilisha maisha yao ya dhiki kuwa ya heri. (alama 8)
  3. “Sijui kama umewahi kujawa na hisia za kukataliwa, ukajihisi kama mkoma aliyesiribwa kinyesi usoni?”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
    2. Bainisha tamathali mbili za usemi kwenye dondoo hili. (alama 2)
    3. Eleza namna kukataliwa kunajitokeza katika riwaya. (alama 8)
    4. “Mhitaji siku zote ni mtumwa”. Jadili ukweli wa kauli hii ukirejelea riwaya ya Chozi la Heri. (alama 6)
  4. SEHEMU C: TAMTHILIA
    P. Kea: Kigogo
    Jibu swali la 4 au la 5
    “… naona watia vyanda kwenye mdomo wa simba – huo ni mchezo hasi.”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
    2. Fafanua umuhimu wa mbinu ya kimtindo kwenye dondoo hili. (alama 2)
    3. Eleza sifa sita za anayeambiwa maneno haya. (alama 6)
    4. Kwa kurejelea tamthilia onyesha namna kutia vyanda kwenye mdomo wa simba ni mchezo hasi. (alama 8)
  5. “Kuishi ni nini kama si kuabiri katika chombo cha usakaji nafsi na majaliwa? Misimu mingine ikatunyeshea fanaka, na siku pia zikaja za kiangazi cha kadhia, chombo chenye rubani imara huhimili vishindo na hasira ya mawimbi makali. Hata hivyo, mwenye woga wa dhoruba hubakia ufukweni asibanduke, asidiriki katu kuionja shubiri na tamu ya mapambano. Ni lazima kama ibada kuisoma bahari na kusonga mbele kwa mpango, kwa kuwa hatuna budi kuishi. Kuishi kwa kutojali ni muhali, kutakuletea ajali, ajali nayo ilivyo haijali, hasara zake zitakuhasiri. Uwe si mtu tena, bali gofu la mtu linaloishi leo kama kwamba ni mwisho wa maisha. Linaloisifia jana bila kufikiria kesho yake. Linasahau kuwa safari ya kesho hupangwa leo, na jana haitarudi tena. Nasema kwa tashtiti, wa kunikosoa asimame!”
    1. Changanua vipengele vya kimtindo katika kifungu hiki. (alama 10)
    2. Hali duni ya maisha katika jamii huchangiwa pakubwa na viongozi. Jadili kauli hii ukirejelea tamthilia ya Kigogo. (alama 10)
  6. SEHEMU D: USHAIRI
    Jibu swali la 6 au la 7
    Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
    Kindumbwendumbwe cha kandanda
    Ndio mwanzo kasi kimeshika
    Na vumbi kutifuliwa
    Safu ya ushambulizi naona
    Imeanza makali kukosa
    Nalo shinikizo kuelemea upande mmoja
    Kila mtu anashangilia
    Maana
    Hata mvua inyeshapo
    Mkondo wa maji hupenya palipo dhaifu.
    Ni kipindi cha lala salama
    Na si ishara nzuri kwa waliolemewa
    Chenga wanapigwa na kanzu kuvishwa
    Na washangiliaji maelfu
    Sauti wakipaaza na kelele kupiga
    Ni kilele cha wendawazimu
    Wa binadamu kujidhiki na jasho kumwaga
    Kwa kuufukuzia upepo alioutia mateka
    Kwa ngome kuujengea.
    Upande mmoja umenywea
    Na kutegemewa kurambishwa
    Ila nitazamapo kwa tuo
    Naona walinda ngome
    Misuli yao bado imara
    Miguu yao bado haijawasaliti
    Mbinu zao bado hazijapata kutu
    Nguvu zao bado hazijanywea
    Hawawezi kushambulia kwa makali
    Lakini ngome yao bado ni tisti.
    “Endeleeni kuimarisha ngome
    Na yao mikwaju kuzuia
    Kipindi cha majeruhi bado kiko mbali
    Wala hiki sidhani kitalala salama
    Karibuni nao wataanza kunywea
    Na tamaa kukata kwa bao kukosa.”
    Nani asiyejua binadamu aliyetamauka
    Dhaifu alivyo kwa tumaini kukosa?
    Nani asiyejua kuwa bao
    Kimiani haliingii pasi ngome kusalitika?
    Tangu lini mechi kushindwa
    Kwa wingi wa mashambulizi?
    Hata ngome imara ni ushindi tosha!
    Najua watasema, “msikize huyo mwendawazimu
    Na kauli zake za kiwendawazimu.”
    Kwangu lililo muhimu ni kusikilizwa
    Maana maisha yenyewe ni wendawazimu.
    Kuna urazini gani kuifukuzilia pumzi
    Kama mtoto mdogo aliyepagawa?
    Kuna urazini gani kurushiana makonde lingoni
    Jasho kumwaga na damu kutoana?
    Na mtu asiye hasimu yako
    Kwa kusingizio cha burudani?
    Kuna urazini gani kujilimbikizia mali
    Ilhali mchapa kazi ananyongwa na njaa?
    Wendawazimu wangu daima unanituma
    Shindano la miereka kushabikia
    Uhayawani huo kushangilia kwa vicheko
    Maana
    Maisha na uhayawani
    Ni kama theluji na barafu
    Kwangu mimi mzaliwa wa hapa jangwani.
    (T. Arege)
    1. Maisha ni wendawazimu na uhayawani. Thibitisha kwa kutoa hoja tano kwenye shairi. (alama 5)
    2. Fafanua mbinu tatu ambazo mshairi ametumia kuwasilisha ujumbe katika shairi hili. (alama 3)
    3. Eleza muundo wa shairi hili. (alama 4)
    4. Bainisha aina mbili za urudiaji katika shairi hili. (alama 2)
    5. Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
    6. Bainisha nafsineni katika shairi hili. (alama 2)
    7. Huku ukitoa mifano, eleza mbinu mbili ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika ubeti wa tano. (alama 2)
  7. Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
    Ujana wa kisasa!
    Mtu akiwa kijana, hudhania hazeeki
    Mzee akimuona, kwake ni kama kisiki
    Anafikiri ujana, daima haufutiki
    Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    Ukimuona kijana, apita hatikisiki
    Mzee wakipishana, amuona kama dhiki
    Utadhania hapana, uzee haumfiki
    Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    Kuringia uvulana, ukaona iliki
    Na kusahahu kijana, uzee haukingiki
    Kwa kweli hiyo ni lana, nakwambia Ludoviki
    Fahamu kwamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    Huo wako usichana, ukiitwa huitiki
    Unapoitwa kwa jina, na mzee mamluki
    Wamuona ni kichana, hata nywele hazisuki
    Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    Umbo ulivyojazana, usiseme ni bureki
    Nyama hazitakunjana, na ngoziyo sio feki
    Wala haitavutana, mfano wa pulastiki
    Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    Si vyema kumtukana, mzee kwa chukichuki
    Akipita wamguna, useme hahesabiki
    Wewe ni mtu wa jana, hata ukungwi huoki
    Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    Walituambia sana, ujana haushikiki
    Si mwida hutauona, usambe hauponyoki
    Ukiponyoka ni shina, uzee umediriki
    Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    Sifurahi kuoana, ujana ukawa tiki
    Kuna mambo mengi sana, hupitia halaiki
    Amina Rabbi Amina, na Mola akubariki
    Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
    (Ludovick Mbogholi)
    1. Fafanua kwa kutoa hoja tano mtazamo wa nafsineni kuhusu ujana wa kisasa kwa mujibu wa shairi hili. (alama 5)
    2. Fafanua dhamira ya mtunzi wa shairi hili. (alama 2)
    3. Eleza aina tatu za taswira zinazojitokeza katika shairi hili. (alama 3)
    4. Bainisha aina tatu za urudiaji zilizotumiwa kwenye shairi hili. (alama 3)
    5. Tambua nafsineni katika shairi hili. (alama 1)
    6. Eleza umuhimu wa mbinu mbili ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika ubeti wa tano. (alama 2)
    7. Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
    8. Andika ubeti wa saba katika lugha nathari. (alama 2)
  8. SEHEMU E: HADITHI FUPI
    A. Chokocho na D. Kayanda (Wah.): Tumbo Lisiloshinba na Hadithi Nyingine
    A. Chokocho: Tulipokutana Tena
    “Ingawa mimi nilikuwa kitoto cha miaka mitano, nilihisi siku ile ilikuwa mbaya kwangu.
    Siku tofauti kabisa katika maisha yangu.”
    1. Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
    2. Fafanua umuhimu wa mzungumzaji katika kuijenga hadithi hii. (alama 5)
    3. Eleza namna mbinu ya kinaya inajitokeza katika hadithi ya Shibe Inatumaliza. (alama 5)
    4. Hadithi, Mtihani wa Maisha inahimiza uwajibikaji. Jadili. (alama 6)
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 3 Questions - Maseno Mock Examinations 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?