MASWALI
SEHEMU A: FASIHI SIMULIZI
- Lazima
Soma utungo ufuatao kisha ujibu maswali
Mabibi na mabwana. Siku hii ya leo nina furaha riboribo. Furaha ghaya. Furaha inayoshinda mwanamke aliyepata salama. Mbona nisiwe na furaha na buraha katika jamii hii iliyotuka ikashinda utukufu wenyewe? Jamii hii yetu imedumu kwa miaka na mikaka. Kisa na maana? Umoja wetu. Mshikamano wetu. Undugu wetu. Muungano wetu. Sote twafahamu fika bila chembe chochote cha walakini kwamba umoja ni nguvu utengano ni udhaifu. Nani asiyejua utu ni ubinadamu? Kwamba kinachotutofautisha na hayawani ni utu? Utu imara na dhabiti usiotikisika wala kusukasuka katika mawimbi na dhoruba za aushi. Hakuna adinasi anayeweza kusimama tisti kama mbuyu akiwa pekee. Asiyejua kifai kwamba jifya moja haliinjiki chungu nani?- Tambua kipera hiki cha mazungumzo cha fasihi simulizi. (alama 1)
- Huku ukitoa hoja tano, fafanua umuhimu wa kipera. (alama 5)
- Bainisha vipengele vya kimtindo vilivyotumiwa kuwasilisha ujumbe. (alama 3)
- Unanuia kutumia mbinu ya mahojiano kukusanya habari kuhusu kitanzu hiki.
Eleza manufaa matano ya kutumia mbinu hii. (alama 5) - Eleza maana ya ngomezi. (alama 1)
- Fafanua sifa tano za ngomezi. (alama 5)
- SEHEMU B: RIWAYA
A. Matei: Chozi la Heri
Jibu swali la 2 au la 3
“Hajui vipi, lakini moyoni ametia nia, na penye nia bila shaka njia hupatikana. Ataanzia hapa kuyabadilisha maisha yake ya dhiki kuwa ya heri.”- Eleza muktadha wa dondoo hili (alama 4)
- Bainisha vipengele viwili vya kimtindo. (alama 2)
- Fafanua sifa sita za mrejelewa. (alama 6)
- Kwa kurejelea riwaya ya Chozi la Heri eleza jinsi wahusika wanabadilisha maisha yao ya dhiki kuwa ya heri. (alama 8)
- “Sijui kama umewahi kujawa na hisia za kukataliwa, ukajihisi kama mkoma aliyesiribwa kinyesi usoni?”
- Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
- Bainisha tamathali mbili za usemi kwenye dondoo hili. (alama 2)
- Eleza namna kukataliwa kunajitokeza katika riwaya. (alama 8)
- “Mhitaji siku zote ni mtumwa”. Jadili ukweli wa kauli hii ukirejelea riwaya ya Chozi la Heri. (alama 6)
- SEHEMU C: TAMTHILIA
P. Kea: Kigogo
Jibu swali la 4 au la 5
“… naona watia vyanda kwenye mdomo wa simba – huo ni mchezo hasi.”- Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
- Fafanua umuhimu wa mbinu ya kimtindo kwenye dondoo hili. (alama 2)
- Eleza sifa sita za anayeambiwa maneno haya. (alama 6)
- Kwa kurejelea tamthilia onyesha namna kutia vyanda kwenye mdomo wa simba ni mchezo hasi. (alama 8)
- “Kuishi ni nini kama si kuabiri katika chombo cha usakaji nafsi na majaliwa? Misimu mingine ikatunyeshea fanaka, na siku pia zikaja za kiangazi cha kadhia, chombo chenye rubani imara huhimili vishindo na hasira ya mawimbi makali. Hata hivyo, mwenye woga wa dhoruba hubakia ufukweni asibanduke, asidiriki katu kuionja shubiri na tamu ya mapambano. Ni lazima kama ibada kuisoma bahari na kusonga mbele kwa mpango, kwa kuwa hatuna budi kuishi. Kuishi kwa kutojali ni muhali, kutakuletea ajali, ajali nayo ilivyo haijali, hasara zake zitakuhasiri. Uwe si mtu tena, bali gofu la mtu linaloishi leo kama kwamba ni mwisho wa maisha. Linaloisifia jana bila kufikiria kesho yake. Linasahau kuwa safari ya kesho hupangwa leo, na jana haitarudi tena. Nasema kwa tashtiti, wa kunikosoa asimame!”
- Changanua vipengele vya kimtindo katika kifungu hiki. (alama 10)
- Hali duni ya maisha katika jamii huchangiwa pakubwa na viongozi. Jadili kauli hii ukirejelea tamthilia ya Kigogo. (alama 10)
- SEHEMU D: USHAIRI
Jibu swali la 6 au la 7
Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Kindumbwendumbwe cha kandanda
Ndio mwanzo kasi kimeshika
Na vumbi kutifuliwa
Safu ya ushambulizi naona
Imeanza makali kukosa
Nalo shinikizo kuelemea upande mmoja
Kila mtu anashangilia
Maana
Hata mvua inyeshapo
Mkondo wa maji hupenya palipo dhaifu.
Ni kipindi cha lala salama
Na si ishara nzuri kwa waliolemewa
Chenga wanapigwa na kanzu kuvishwa
Na washangiliaji maelfu
Sauti wakipaaza na kelele kupiga
Ni kilele cha wendawazimu
Wa binadamu kujidhiki na jasho kumwaga
Kwa kuufukuzia upepo alioutia mateka
Kwa ngome kuujengea.
Upande mmoja umenywea
Na kutegemewa kurambishwa
Ila nitazamapo kwa tuo
Naona walinda ngome
Misuli yao bado imara
Miguu yao bado haijawasaliti
Mbinu zao bado hazijapata kutu
Nguvu zao bado hazijanywea
Hawawezi kushambulia kwa makali
Lakini ngome yao bado ni tisti.
“Endeleeni kuimarisha ngome
Na yao mikwaju kuzuia
Kipindi cha majeruhi bado kiko mbali
Wala hiki sidhani kitalala salama
Karibuni nao wataanza kunywea
Na tamaa kukata kwa bao kukosa.”
Nani asiyejua binadamu aliyetamauka
Dhaifu alivyo kwa tumaini kukosa?
Nani asiyejua kuwa bao
Kimiani haliingii pasi ngome kusalitika?
Tangu lini mechi kushindwa
Kwa wingi wa mashambulizi?
Hata ngome imara ni ushindi tosha!
Najua watasema, “msikize huyo mwendawazimu
Na kauli zake za kiwendawazimu.”
Kwangu lililo muhimu ni kusikilizwa
Maana maisha yenyewe ni wendawazimu.
Kuna urazini gani kuifukuzilia pumzi
Kama mtoto mdogo aliyepagawa?
Kuna urazini gani kurushiana makonde lingoni
Jasho kumwaga na damu kutoana?
Na mtu asiye hasimu yako
Kwa kusingizio cha burudani?
Kuna urazini gani kujilimbikizia mali
Ilhali mchapa kazi ananyongwa na njaa?
Wendawazimu wangu daima unanituma
Shindano la miereka kushabikia
Uhayawani huo kushangilia kwa vicheko
Maana
Maisha na uhayawani
Ni kama theluji na barafu
Kwangu mimi mzaliwa wa hapa jangwani.
(T. Arege)- Maisha ni wendawazimu na uhayawani. Thibitisha kwa kutoa hoja tano kwenye shairi. (alama 5)
- Fafanua mbinu tatu ambazo mshairi ametumia kuwasilisha ujumbe katika shairi hili. (alama 3)
- Eleza muundo wa shairi hili. (alama 4)
- Bainisha aina mbili za urudiaji katika shairi hili. (alama 2)
- Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
- Bainisha nafsineni katika shairi hili. (alama 2)
- Huku ukitoa mifano, eleza mbinu mbili ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika ubeti wa tano. (alama 2)
- Soma shairi lifuatalo kisha ujibu maswali
Ujana wa kisasa!
Mtu akiwa kijana, hudhania hazeeki
Mzee akimuona, kwake ni kama kisiki
Anafikiri ujana, daima haufutiki
Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
Ukimuona kijana, apita hatikisiki
Mzee wakipishana, amuona kama dhiki
Utadhania hapana, uzee haumfiki
Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
Kuringia uvulana, ukaona iliki
Na kusahahu kijana, uzee haukingiki
Kwa kweli hiyo ni lana, nakwambia Ludoviki
Fahamu kwamwe hubaki, humo ndani ya ujana
Huo wako usichana, ukiitwa huitiki
Unapoitwa kwa jina, na mzee mamluki
Wamuona ni kichana, hata nywele hazisuki
Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
Umbo ulivyojazana, usiseme ni bureki
Nyama hazitakunjana, na ngoziyo sio feki
Wala haitavutana, mfano wa pulastiki
Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
Si vyema kumtukana, mzee kwa chukichuki
Akipita wamguna, useme hahesabiki
Wewe ni mtu wa jana, hata ukungwi huoki
Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
Walituambia sana, ujana haushikiki
Si mwida hutauona, usambe hauponyoki
Ukiponyoka ni shina, uzee umediriki
Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
Sifurahi kuoana, ujana ukawa tiki
Kuna mambo mengi sana, hupitia halaiki
Amina Rabbi Amina, na Mola akubariki
Fahamu kamwe hubaki, humo ndani ya ujana
(Ludovick Mbogholi)- Fafanua kwa kutoa hoja tano mtazamo wa nafsineni kuhusu ujana wa kisasa kwa mujibu wa shairi hili. (alama 5)
- Fafanua dhamira ya mtunzi wa shairi hili. (alama 2)
- Eleza aina tatu za taswira zinazojitokeza katika shairi hili. (alama 3)
- Bainisha aina tatu za urudiaji zilizotumiwa kwenye shairi hili. (alama 3)
- Tambua nafsineni katika shairi hili. (alama 1)
- Eleza umuhimu wa mbinu mbili ambazo mshairi ametumia kutosheleza mahitaji ya kiarudhi katika ubeti wa tano. (alama 2)
- Eleza toni ya shairi hili. (alama 2)
- Andika ubeti wa saba katika lugha nathari. (alama 2)
- SEHEMU E: HADITHI FUPI
A. Chokocho na D. Kayanda (Wah.): Tumbo Lisiloshinba na Hadithi Nyingine
A. Chokocho: Tulipokutana Tena
“Ingawa mimi nilikuwa kitoto cha miaka mitano, nilihisi siku ile ilikuwa mbaya kwangu.
Siku tofauti kabisa katika maisha yangu.”- Eleza muktadha wa dondoo hili. (alama 4)
- Fafanua umuhimu wa mzungumzaji katika kuijenga hadithi hii. (alama 5)
- Eleza namna mbinu ya kinaya inajitokeza katika hadithi ya Shibe Inatumaliza. (alama 5)
- Hadithi, Mtihani wa Maisha inahimiza uwajibikaji. Jadili. (alama 6)
Join our whatsapp group for latest updates
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Download Kiswahili Paper 3 Questions - Maseno Mock Examinations 2022.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students