- Jibu maswali yote katika karatasi hii.
- Thibitisha kuwa anayerejelewa katika makala haya alikuwa fukara. Alama 1
- Otii alikuwa Maarufu sana kabla ya kuwa mgonjwa. Fafanua. Alama 2
- Eleza maana ya: “Jamaa zake si watu wa kusubiri mvua kunyesha ndipo waanze kutafuta pahala pa kununua mwavuli”. Alama 1
- Chama cha watu wa nyumbani walifanya kinyume na matakwa ya Otii. Eleza. Alama 1
- Taja sifa zozote mbili zinazojitokeza za wahusika wanaopanga mikakati ya mazishi. Alama 1
- Andika na ueleze misemo yoyote miwili iliyotumika hatika hadithi hii. Alama 2
- Eleza maana ya msamiati.
- Kilichotalizwa
- Muwele Alama 2
SEHEMU YA ‘C’ SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA ALAMA 40
- Taja sauti zenye sifa zifuatazo
- Kikwamizo ghuna cha menoni
- Irabu ya nyuma kati
- Kiyeyusho cha midomo Alama 3
- Kwa kutoa mifano tofautisha kati ya mizizi funge na mizizi huru. Alama 2
- Andika kwa ukubwa wingi:
Mji mkubwa umejengwa nyumba za kifahari. Alama 2 - Yakinisha sentensi ifuatayo;
Usipojikakamua kiume hutafaulu katika mitihani. Alama 1 - Tita ni la kuni ilhali ________________ ni kwa mizigo. Alama 1
- Weka nomino zifuatazo katika ngeli zake. Alama 2
- Kijakazi
- Petroli
- Kwa kutoa mfano, onyesha matumizi matatu ya kiakifishi:
Parandesi Alama 3 - Andiika sentensi ifuatayo katika usemi wa taarifa.
“Leo jioni tutamtembelea shangazi yako jijini”. Mama akamwambia Alama 2 - Changanua sentensi ifuatayo kwa mstari.
Sisi wawili tutatuzwa tuzo. Alama 2 - Tunga sentensi katika wakati uliopita hali timilifu. Alama 2
- Ainisha mofimu katika neno: Alama 3
Apikaye - Tunga sentensi ukitumia vivumishi vinavyotoa maana zifuatazo: Alama 2
- Kutobagua
- Kutobakiza
- Unda nomino dhahania kutokana na vitenzi
- Safari
- Lima Alama 2
- Tunga sentensi ukitumia kivumishi kisisitizi cha mbali kidogo ukitumia nomino ya ngeli ya I-ZI Alama 2
- Tunga sentensi ukitumia kihusishi chochote cha wakati Alama 2
- Kamilisha jedwali. Alama 2
Kutenda Kutendesha Kutendesha Cheza Lia - Banisha vitenzi katika sentensi; Alama 2
Babu yangu alikuwa akisafiri jana jioni - Weka shadda kwenye maneno yafuatayo ili kubadilisha maana kwenye mabano. Alama 2
- Walakini (dosari)
- Barabara (shwari)
- Unganisha sentensi ifuatayo ili kupata sentensi ambatano Alama 2
Walimu hao walipewa uhamisho.
Walimu wengine hawakupewa - Andika katika wingi
Ndizi hili langu limeoza. Alama1
SEHEMU YA ‘D’ ISUMUJAMII ALAMA 10
- Tambua sajili ya makala uliyosoma. Alama2
- Eleza sifa sita za sajili uliyotaja hapo juu. Alama 6
- Istilahi zifuatazo za isimujamii zina maana gani? Alama 2
- Lahaja
- Uwililugha
SEHEMU YA E: FASIHI SIMULIZI ALAMA 10
- Eleza maana ya:
- Ushairi simulizi Alama1
- Taja vipera viwili vya Ushairi simulizi Alama2
- Mbolezi huwa na umuhimu katika jamii. Eleza umuhimu wake kwa hoja tatu. Alama 3
- Fafanua aina zifuatazo za hadithi. Alama 2
- Mighani
- Hurafa
- Eleza aina mbili za hadhira. Alama 2
SEHEMU YA F: USHAIRI ALAMA 10
- Taja sifa zozote mbili za binadamu kama zinavyojitokeza katika shairi. Alama 2
- Hii ni shairi ya aina gani kwa mujibu wa aina mbili kuu za mashairi. Alama 1
- Eleza umbo la ubeti wa tatu Alama 4
- Shairi hili linaweza kuwekwa katika bahari mbalimbali. Zitaje bahari mbili. Alama2
- Eleza maana ya msamiati ufuatao kama ulifyotumika katika shairi.
- Mafatani Alama 1

MARKING SCHEME
SEHEMU YA A INSHA ALAMA 20
- Hii ni insha ya mdokezo. Maneno kiini katika insha hii ni kung’amua kuwa kungali na watu wenye ukarimu na utu.
- Mtahiniwa anaweza kutumia mbinu rejeshi na kutunga kisa ambacho kinaonana na mdokezo.
- Anaweza kurudi nyuma na kuelezea labda shida ambazo zilikuwa zimemulemea.
- Hali zifuatazo zinaweza kujitokeza.
- Mhusika anaweza kuwa na mrudukano wa madeni ambayo ameshindwa kulipwa. Hatimaye mtu mwenye utu akaja kusaidia.
- Anaweza kuwa alikuwa amelemewa na mzigo wa kukidhia familia mahitaji ya kimsingi mfadhili akajitokeza kumuauni.
- Anaweza kuwa katika mazingira hatari lakini msamaria mwema akajitokeza na kamsaidia.
- Tanbihi.
- Mtahiniwa akitunga kisa ambacho hakionani na mdokezo,atakuwa amepotoka.
- Mtahiniwa akikosa kuandika mdokezo atakuwa amepungukiwa kimtindo lakini hajapotoka.
SEHEMU YA B UFAHAMU ALAMA 10
- Aliishi kwenye kibanda kilichotalizwa udongo na kuzekwa makuti machakavu. Alama 1
-
- Alisakatia kadanda timu ya Bandari F.C.
- Alichezea timu ya Harambee Stars
- Alikuwa anakanyanga ardhi inatetemeka Alama 2
- Walianza kupanga mikakati ya mazishi ya Otii hata kablaya kifo chake. Alama 1
- Wanapanga kumzika otii Kisumu kubwa Sidindi lakini yele alitaka azikwe Kisumu Ndogo Mombasa. Alama 1
-
- Wenye ushirika
- Wenye mapuuza
- Watamaduni Alama 1
- Misemo
Misemo ni- pata afueni-kupata nafuu
- kupiga chafya-kuchemua Alama 2
-
- Kilichotalizwa - Kilichopakwa udongo
- Muwele - mgonjwa Alama 2
SEHEMU YA C SARUFI NA MATUMIZI YA LUGHA (ALAMA 40)
-
- Kikwamizo ghuna cha menoni ‘dh’
- Irabu ya nyuma kati ‘o’
- Kiyeyusho cha midomo ‘w’ Alama 3
-
- Mzizi huru ni ule ambao unaweza kusimama kama neno kwa mfano samehe, Sali.
- Mizizi funge ni mzizi ambao hauwezi kusimama kama neno. Kwa mfano; -chez- -pig- Alama 2
- Ukubwa wingi
- Majiji makuu yamejengwa majumba ya kifahari. Alama 2
- Kuyakinisha
- Ukijikakamua kiume utafaulu katika mtihani. Alama 1
- Shehena ya mizigo Alama 1
-
- Kijakazi A-WA
- Petroli I-I Alama 2
- Parandesi/mabano/vifungo
- Kuhifadhi maelezo ya nyongeza
- Kutoa maelekezo ya mwandishi
- Kuonyesha maneno yenye maana sawa. Alama 3
- Usemi wa taarifa
- Mama alimwambia kuwa siku hiyo jioni wangemtembelea shangazi yake jijini. Alama 2
- Mstari
Sisi wawili tutakatazwa tuzo- S → K N (W+V) + KT (T+N) . Alama 2
- Wakati uliopita hali timilifu mfano
- Kasisi alikuwa amewahubiria waumini. Alama 2
- Apikaye
- A – nafsi/ngeli
- PIK ] Mzizi
- A- Kauli/Kiishio
- Ye-Kirejeshi Alama 3
-
- kutobagua – o – ote
- Kutobakiza - ote Alama 2
-
- Usafiri
- Ukulima Alama 2
- Sahani au Nyumba iyo hiyo ama zizo hizo Alama 2
- Kabla ya, baada ya, mpaka Alama 2
- Kamilisha jedwali
Kutenda Kutendesha Kutendesha Cheza Chezesha Chezeshea Lia Liza Lizia -
- Alikuwa - Kitenzi Kisiaidizi Ts
- Akisafiri - Kitenzi kikuu Alama 2
-
- Walakini (dosari)
- Barabara (Shwari) Alama 2
- Walimu hao walipewa uhamisho lakini wengini hawakupewa. Alama 2
- Ndizi hizi zetu zimeoza. Alama 1
SEHEMU YA D ISIMU JAMII Alama 10
- Sajili ya vijana Alama 2
- Sifa za sajili ya vijana
- Kutumia lugha legevu
- Kuchanganya ndimi
- Kuna matumizi ya sheng
- Matumixi ya sentensi fupi
- Kuna matumizi ya misimu
- Huwa kuna kukatizana kauli Alama 6
-
- Iahaja
- Ni viijilugha ya lugha moja
- Uwililugha
- ni uwezo wa mtu kuzungumza lugha mbili. Alama 2
- Iahaja
SEHEMU YA E FASIHI SIMULIZI ALAMA 10
-
- Ushairi simulizi ni tungo za ushairi ambazo huasilishwa mbele ya hadhira kwa kusemwa au kwa kusemwa au kwa njia ya mdomo.
- Vipera vya ushairi simulizi Alama 1
- Nyimbo
- Maghani Alama 2
-
- Huwafariji waliofiwa
- Huwapa waliofiwa matumaini
- Huleta utangamano baina ya waliofiwa na jama za marafiki.
- Huhimiza wetu wasiogope bali wawe na ujasiri
- Huimbwa kama njia ya kudumisha utamaduni Alama 3
-
- Mighani – Hadithi za mashujaa
- Hurafa – Hadithi za wahusika
Wanyama pekee Alama2
-
- Hadhira hai – hadhira inayoshirikishwa
- Hadhira tuli – Hadhira isiyoshirikishwa Alama 2
SEHEMU YA F USHAIRI ALAMA 10
- Sifa za binadamu
- Binadamu ni haini
- Binadamu ni wafitini
- Binadamu ni waongo
- Binadamu ni mbaya Alama 2
- Shairi la Kiarudhi Alama 1
-
- Umbo la ubeti wa tatu
- Ubeti una mishororo minne
- Ubeti una migao miwili – ukwapi na utao
- vina vya ubeti huu ni
- Se - ni
- Se- ni
- Se – ni
- Wa – ni
- Kila kipande kina mizani miine Alama 4
- Bahari
- Tarbia – kila ubeti una mishororo miine
- Mathinau – kila mshororo una migao miwili.
- Ukara – vina vya kati vinatofatiana katika kila ubeti lakini vya nje vinafanana Alama 2
- Watu mafatani – wachochezi Alama 1
Download Kiswahili Questions and Answers - Form 3 Mid Term 1 Exams 2023.
Tap Here to Download for 50/-
Get on WhatsApp for 50/-
Why download?
- ✔ To read offline at any time.
- ✔ To Print at your convenience
- ✔ Share Easily with Friends / Students
Join our whatsapp group for latest updates