Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 4 End Term 1 Exams 2021

Share via Whatsapp

KISWAHILI
MTIHANI WA MWISHO WA MUHULA
MUHULA WA 1 2021
KIDATO CHA NNE
KARATASI YA 1
MUDA SAA 2 

MAAGIZO

  • Jibu maswali mawili
  • Swali la kwanza ni la lazima
  • Chagua swali moja kati ya matatu yaliyobaki
  • Kila insha isipungue maneno 400
  1. Swali la LAZIMA
    Ukiwa Gavana Mtajika wa Kaunti yako umealikwa kuwazungumzia wanafunzi wa kidato cha nne katika shule ya Mafanikio. Andika Tawasifu utakayowasilisha. (alama 20)

  2. Eleza jinsi udanganyifu katika mitihani utaathiri maisha ya kizazi kijacho. (alama 20)

  3. Andika kisa kitakachothibitisha maana ya methali: Mtenda mema kwa watu atendea nafsiye. (alama 20)

  4. Kamilisha tukio kwa maneno yafuatayo:
    “…waliwasili saa tatu baadaye. Uharibifu wa mali na maisha ulikuwa umeshatendeka wala kufika kwao hakukusaidia kwa lolote.”(alama 20)

MAAKIZO

  1. Muundo
    Zingatia lugha ya mtiririko.
    1. KujitambulishaJina
      • Kuzaliwa/Eneo/Kaunti n.k
      • Malezi yake
      • Elimu
      • Msingi
      • Sekondari
      • Vyuo mbalimbali alivyosomea.
    2. Tajriba
      • Kazi aliyofanya/alizofanya kabla ya kuwa Gavana.
      • Siasa – kiwango/viwango gani?
      • Anatajika kwa jambo/mambo gani
      • Mifano: - Elimu ya juu – shahada kadha
      • Miradi ya maendeleo
      • Ziara alizofanya.
      • Uwajibikaji wake/maadili kazini
      • Falsafa yake ya maisha.
      • Malengo yake
      • Changamoto alizopitia.
      • Ruwaza/maazimio yake.
      • Lugha – mtahiniwa atumie nafsi ya kwanza.
      • Usemi ya taarifa.
      • Lugha rasmi itumiwe.
  2. Hoja.
    1. Maadili yatazorota
    2. Njia za mkato maishani
    3. Uzembe kazini
    4. Ukosefu wa uwajibikaji
    5. Mapuuza
    6. Kutothamini mitihani
    7. Elimu kudorora
    8. Kuathirika kwa taaluma mbalimbali
    9. Utendekazi utaathirika
    10. Nidhamu kutoweka
  3. Mtenda mema kwa watu atendea nafsiye
    1. Maana: Kuwafanyia wema watu ni sawa na kujiwekea akiba. Huenda nao wakakutendea wema utakapouhitaji.
    2. Funzo: Usidhani unafanya kazi ya bure unapomfaa mtu Fulani.
    3. Matumizi: Inaweza kuhimizwa anayefikiria kuwa wema uatendao ni wa bure na kuwa hatafaidika hata akiendelea.
    4. Mtahiniwa aandike kisa kitakachodhihirika pande zote mbili.
  4. Mambo ya kuzingatiwa
    1. Kisa kinafaa kuwa katika wakati uliopita.
    2. Mtahiniwa azingatie kumaliza kisa chake kwa maneno yote yaliyodokezwa.
    3. Mahali pa tukio patajwe.
    4. Baadhi ya matukio;
      • Moto
      • Wizi
      • Ugaidi
      • Baharini/majini
      • Ajali barabarani.
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili Paper 1 Questions and Answers - Form 4 End Term 1 Exams 2021.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest