Displaying items by tag: kiswahili

MASWALI

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne hapo.

Chagua jibu lifaalo zaidi kati va yale ulivopewa

Sikukuu ya Krismasi ilishangiliwa        1           Makundi ya wakristo        2           makanisani ili          3          Ndugu na jamaa         4         waliziwahi sehemu         5           burudani ili kuburudika kwa furaha na buraha. Watu wengine          6          ili kuwapa mkono waliokuwa hawajiwezi.        7          walizingatia kwamba        8         .

1.A. kwa hamu na ghamu  B. kwa uti wala mauti  C. kwa shangwe na nderemo  D. kwa udi na uvumba 
 2.A. walimiminika  B. yalimiminika  C. watamiminika  D. yatamiminika
 3.A. kusheherekea  B. kushehekea  C. kureshehekea  D. kusherehekea
 4.A. pia  B. ilhali  C. madhali  D. angalau
 5.A. ya  B. kwa  C. za  D. wa
 6.A. walijitolea kibwebwe  B. walijitolea mhanga  C. walijitolea kingoto  D. walijitolea kiguu
 7.A. Kwa kwamba  B. Kwa ajili  C. Kwa hakika  D. Kwa moja
 8.A. kutoa ni moyo, usambe ni utajiri  B. cha mfupi huliwa na mrefu  C. mtegemea cha nduguye hufa maskini  D. fimbo ya mbali haiui nyoka

 

Kiswahili ni lugha mojawapo,        9          katika mazungumzo ya kawaida. Lugha hii       10       sana         11         nyanja anuwai. Wanafunzi shuleni hufundishwa      12        thelathini. Aidha, kuna sauti ghuna ambazo pia huitwa        13         Sauti hizi huunda         14         Mathalani, neno 'kilichoundwa' lina silabi        15          

9.A. zilizotumika  B. iliyotumika  C. zinazotumika   D. inayotumika 
10.A. inadhaminiwa  B. kinathaminiwa  C. inathaminiwa D. kinadhaminiwa
11.A. katika  B. kati ya  C. kwenye D. katikati ya
 12.A. konsonati  B. alfabeti  C. vokali  D. irabu
 13.A. nyepesi  B. sighuna  C. kwaruzo  D. mwambatano
 14.A. neno  B. sentensi  C. silabi  D. aya
 15.A. sita  B. tano  C. kumi na mbili  D. nane

Kutoka swali la 16-30, jibu swali kulingana maagizo uliyopewa.

  1. Chagua matumizi ya 'kwa' kurejeleamchanganyiko
    1. Walitembea kwa miguu hadi shuleni.
    2. Wazee kwa vijana walihudhuria sherehe hizo.
    3. Timu hizo zilifungana mabao matano kwa sita.
    4. Aliadhibiwa kva utundu wake.
  2. Hazama ni kwa puani kama vile ni kwa sikio.
    1. mkufu
    2. kidani
    3. kipete
    4. mapete
  3. Chagua wingi wa sentensi hii Ua wa dobi ulinivutia sana
    1. Maua ya madobi yalituvutia sana.
    2. Nyua za madobi zilinivutia sana.
    3. Maua ya dobi yalituvutia sana.
    4. Nyua za madobi zilituvutia sana.
  4. Chagua kiambishi 'ku' cha ukanusho
    1. Kusoma huku kunafurahisha
    2. Hakusoma kitabu hicho cha hadithi
    3. Aliyekupiga ametiwa mbaroni
    4. Mchezo huo ulichezwa kule.
  5. Fidia ni
    1. malipo ya kumvunjia mtu heshima
    2. malipo ya kwanza ya kumshika mtoto
    3. malipo kwa ajili ya hasara au maumivu
    4. malipo ya kwanza ya kukinunua kitu dukani.
  6. Kanusha:
    Jengo lililojengwa kwa uhafifu limebomolewa
    1. Jengo lisilojengwa kwa uhafifu limebomolewa
    2. Jengo lililojengwa kwa uhafifu halijabomolewa
    3. Jengo halikujengwa kwa uhafifu limebomolewa
    4. Jengo lisilojengwa kwa uhafifu halijabomolewa.
  7. Ni nini maana ya msemo huu?
    Kumvisha mtu kilemba cha ukoka
    1. Kumtegemea mtu kwa kila jambo.
    2. Kumsema mtu katika mafumbo.
    3. Kumweka mtu katika hatari.
    4. Kumdanganya mtu kumhusu.
  8. Chagua jibu lenye ala za muziki pekee
    1. Filimbi, udi, mvukuto, chapuo.
    2. Siwa, zeze, upatu, nembo..
    3. Njuga, tari, kinubi, fidla.
    4. Harimuni, marimba, msondo, maleba.
  9. 5/6 kwa maneno ni
    1. sudusi sita
    2. humusi sita
    3. sudusi tano
    4. humusi tano.
  10. Ni kundi lipi la nomino ambalo lipo katika ngeli ya LI-YA?
    1. Maji, marashi.
    2. Gitaa, povu.
    3. Maskani, mavazi.
    4. Maagizo, maarifa.
  11. Onyesha sentensi yenye kielezi cha mahali
    1. Mwajuma alisafisha nyumba alfajiri.
    2. Kule kuna miti mirefu.
    3. Wawili walisajiliwa chuoni.
    4. Gari limefika asubuhi.
  12. Chagua jibu lenye nomino ya makundi isiyofaa
    1. Mzengwe wa wagomaji.
    2. Numbi ya nyuki.
    3. Shungi la moto.
    4. Thurea ya nyota
  13. Kauli, 'Jedi ni sungura maishani; imetumia tamathali gani ya usemi?
    1. Jazanda.
    2. Kinaya.
    3. Tashhisi.
    4. Nahau.
  14. Ikiwa juzi ilikuwa Jumanne, mtondo itakuwa
    1. Ijumaa.
    2. Jumatatu.
    3. Jumapili.
    4. Jumamosi.
  15. Chagua jibu lenye kivumishi kilichoundwa kutokana na kitenzi.
    1. Ita -  mwito
    2. Vumilia - uvumilivu
    3. Agiza - maagizo
    4. Sahau - sahaulifu.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31 - 40.

Kuku aliketi nje ya nyumba yake huku amejishika tama. Moyo wake ulijawa na huzuni mpwitopwito. Je, angewezaje kuujenga urafiki wake upya na mwewe mwandani wake wa chanda na pete? Tatizo sugu lililokuwa limeubomoa urafiki wao wa kufa kuzikana ni wembe. Kuku alishangaa namna ambavyo kitu kidogo kama hicho kingesababisha mgogoro kama huo mkubwa. Mawazo kedekede yalizidi kumzunguka akilini mithili ya pia.

Mwewe naye kwa upande wake pale kiotani alitabasamu kwa furaha mzomzo. Aliurarua mnofu wa nyama wake kifaranga mtoto wa kuku. Kwake alijiambia kuwa, “Sasa ninazidi kujilipa deni langu la wembe. Mtu hawezi kuwa ananipotezea rasilimali zangu pasipo kuzingatia hisia zangu pia. Bado atakuja kunitambua! Atabaki mzazi bila vikembe hadi atakapolipa deni lote!"

Giza la usiku lilikumbatia siku yenyewe. Sauti za mbwa zikawa zinasikika kwa umbali. Bado kuku pamoja na vifaranga wake watatu walikuwa hawajalala. Biwi la simanzi liliwaangukia kuku. Mtoto wake wa kiume alikuwa amenyakuliwa na mwewe. Mwewe asiye na utu wala msamaha. Mbona asingengoja hata siku moja imalizike kabla ya kuanza kujilipa yeye mwenyewe? Kwa nini basi asingekuja wapange mikakati namna ya kulipwa? Utitiri wa mawazo ulimtembea akilini mwake bighairi ya kuwa na mwisho. Hatimaye, kuku aliwageukia wana wake ambao ndio chanzo cha kupotea kwa wembe wake mwewe. Aghalabu, alikuwa amewakanya dhidi ya kuchezea vitu vya wenyewe bila ya ruhusa. Kuku alijua siku moja mchezo wao huo ungewatumbukiza katika kidimbwi cha moto. Sasa moto huo ulikuwa umeanza kuwateketeza mno. Kuku akaishia laiti ningalijua na vyanda vi mkononi. Hata hivyo, akaamua kulitafuta suluhisho la kudumu ifikapo asubuhi.

Jua la asubuhi liliramba umande wa alfajiri huku likimzizimua kobe ambaye alitoka nyumbani mwake asteaste. Mzee kobe alisifika sana kwa maarifa yake na akili tambuzi alizokuwa nazo hasa katika kuyatatua mambo baina ya wenzake. Aliketi pale nje huku akibukua tabu kubwa kuhusu migogoro. Kuku jirani yake aliwasili kwake kwa kishindo. Hapo kobe akatambua ya kwamba lazima kuna jambo. Huku amenyong'onyea kama mkufu. Kuku alimpasulia mbarika mzee kobe kuhusu tatizo lake. Jungu kuu halikosi ukoko. Baada ya kikao hicho cha saa tatu naye mzee kobe, kuku alirudi nyumbani akiwa na matumaini kwamba suluhu limepatikana. Mzee kobe alibaki katika kina kirefu cha fikra ili kulipata suluhisho hilo la kudumu na kumpiga jeki jirani yake. Kwa hakika, ni heri jirani kuliko ndugu yako wa toka nitoke wa mbali.

  1. Chagua maana ya ‘kushika tama' kwa mujibu wa kifungu. |
    1.  kuhangaika
    2. kuhuzunika
    3. kunung'unika
    4. kukasirika
  2. Kulingana na aya ya kwanza, kuku
    1.  aliketi ndani ya kiambo chake
    2. alikuwa jasiri na mkakamavu
    3. aliwazia kiini cha ufa uliokuwa umetokea
    4. hakushangaa kiini cha mgogoro..
  3. Kulingana na aya ya pili, mwewe anaonekana kuwa
    1. mwenye ubinafsi
    2. mwenye urafiki wa dhati
    3. mwenye huzuni nyingi
    4. mwenye maarifa chungu nzima.
  4. Kitendo cha mwewe kuamua kujilipishia deni lake kinaweza kulinganishwa na methali gani?
    1. Asante ya punda ni mateke.
    2. Tamaa mbele mauti nyuma.
    3. Mtu ni watu.
    4. Uzuri wa mkakasi ndani kipande cha mti.
  5.  "Biwi la simanzi lilimwangukia kuku,"
    imetumia tamathali gani ya usemi?
    1. Ishara.
    2. Sitiari.
    3. Chuku.
    4. Tashhisi. 
  6. Kwa nini mzee kobe alisifika? 
    1. Kwa sababu alipenda kusoma mabuku.
    2.  Kwa sababu alikuwa mstahimilivu.
    3. Kwa sababu alikuwa mwenye akili pevu.
    4. Kwa sababu alipenda kuliota jua.
  7. Kulingana na aya ya mwisho si sahihi kusema
    1. kikao hakikuzalisha matunda.
    2. jirani anaonekana kuwa na umuhimu.
    3. mzee Kobe aliwazia jambo hilo.
    4. kikao kilichukua saa tatu.
  8. Kifungu kinabainisha kwamba
    1. mwewe alikuwa mwandani wa dhati.
    2. kuku hakuwajali watoto wake.
    3. mzee kobe hakupenda kisomo kwa dhati.
    4. kuku alimwelezea kobe mambo dhahiri.
  9. Maana ya, "biwi la simanzi' kulingana na kifungu ni
    1. mkusanyiko wa hasira
    2. mkusanyiko wa taka
    3.  kuwa na kiasi kikubwa cha huzuni
    4.  kuwa na kiasi kikubwa cha uka.
  10. Kichwa kifaacho kifungu hiki ni sana ni
    1. Mzee Kobe mwenye magamba.
    2. Elimu nyingi huondoa maarifa.
    3. Urafiki wenye unafiki.
    4. Vifaranga vya kompyuta.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 41 - 50.

Afya au siha ni hali ya kutokuwa na maradhi. Hali hii humwezesha mtu kuhifadhi nguvu zake za mwili na kumwezesha kufanya kazi katika mawanda mbalimbali. Mtu mwenye afya bora huweza kutekeleza mengi bila masumbuko. Kwa mfano, yeye huweza kujirausha na kujishughulisha hadi jioni bila kuhisi uchovu mwingi.

Chombo hakiendi ila kwa makasia, nayo afya nzuri haimjii tu mtu. Afya hustahili kupaliliwa na kutunzwa kwa namna anuwai kama vile kula vyakula vyenye viinilishe, kufanya mazoezi na kuandama mienendo miadilifu. Usafi wa mv ili na mazingira pia huchangika katika kuimarisha afya. Ni bayana kwamba mazingira yakiwa machafu hukosa kuvutia na kusababisha kusambaa kwa harufu inayokirihisha. Isitoshe, uchafu huwa hali mufti ya kuzaana kwa wadudu kama vile chawa, nzi, kunguni na mbu ambao ni maadui wakuu wa afya. Tabia ya binadamu huathiri afya yake. Wapo watu ambao wameambulia magonjwa kama vile saratani ya mapafu na kifua kikuu kutokana na mazoea ya pombe, sigara na dawa za kulevya. Wengine hujiponza kwa kuingilia vitendo viovu kama vile kushiriki mapenzi kiholela na kujisababishia magonjwa. Magonjwa haya ni kama vile kisonono na ukimwi ambao umewapukutisha watu kama majani makovu kutoka mtini.

Aidha, watu hujiharibia afya kwa kufanya kazi mfululizo bila kupumzika. Licha ya kwamba bidii ni muhimu katika maendeleo ya jamii yoyote ile, utendaji kazi pasipo kupumzika huweza kuwa na athari hasi. Kuna baadhi ya watu ambao wamewahi kupata maradhi ya moyo, ya kiakili na hata shinikizo la damu kutokana na hali kama hii. Wengine hujihasiri kwa kula vyakula vingi kupindukia. Kadhalika, wapo wengine ambao hupata magonjwa kwa kula vyakula visivyofaa katika kundi hili kwa wale ambao hawadiriki kufanya kazi wala mazoezi. Hawa hujinenepea na kudhoofisha utendakazi wao.

Hali ya umaskini pia huchochea kuzoroteka kwa afya. Asilimia kubwa ya watu nchini humu haimudu huduma bora za afya na lishe bora kutokana na hali ya ufukara. Wengine, kwa kukosa fedha hawapati elimu ya kimsingi kuhusu afya. Hawa huweza kujizulia magonjwa kwa kutojua na kutofuata sheria za afya. Pamoja na hayo, kuna wale ambao wanarithi magonjwa ya kiukoo kama vile bolisukari kutoka kwa wazazi wao. Umuhimu wa afya hauwezi kupuuzwa. Nchi yenye kizazi chenye afya hustawi kiuchumi. Afya ikidumishwa wanajamii huweza kutumia fedha zao kuwekeza katika miradi badala ya kuzitumia kujiunga na kuwauguza wenzao. Ni jukumu la kila raia kuhakikisha kwamba anailinda afya yake na ya wengine kwa vyovyote vile. Walio na mazoea ya kupuuza ushauri wa wanaotoa huduma za afya na lishe wajiase, la sivyo watakuja kujiuma vidole.

  1. Kulingana na aya ya kwanza siha
    1. hukuza maendeleo katika maeneo mbalimbali
    2. humwondolea mtu matatizo mwilini
    3.  humpunguzia mtu mazoea ya uchovu
    4. huimarisha matokeo ya utendakazi.
  2. Ni muhimu kutunza mazingira kwa kuwa
    1.  tutamaliza vikwazo tofauti tofauti vya afya
    2.  tutazuia ongezeko la wadudu waharibifu
    3. tutaepuka kuenea kwa harufu
    4. tutarudisha hali ya kupendeza.
  3. Mwandishi anapinga hali gani hasa katika aya ya tatu?
    1. Uambukizaji wa magonjwa.
    2. Kuhusiana bila mpango.
    3. Vifo vya watu wengi.
    4. Matumizi mabaya ya mihadarati.
  4. Chagua jibu ambalo ni sahihi kulingana na aya ya nne
    1. Jambo jema husababisha maradhi
    2. Kazi nyingi husababisha moyo kuharibika
    3. Mazoezi hayawezi kudhibiti afya.
    4. Mapumziko huimarisha hali ya mtu kiakili.
  5. Kufanya kazi kidindia
    1. huboresha maendeleo ya taifa
    2.  huweza kusababisha uharibifu wa afya
    3. huwa na athari chanya
    4. hupunguza shinikizo la damu.
  6.  Maana ya 'inayokirihisha' ni
    1.  inayochukiza
    2. inayoenea
    3.  inayoaibisha
    4. inayodhuru.
  7. Maana ya "chombo hakiendi bila ya makasia' imejitokeza vipi katika kifungu?
    1. Wanaonyoosha viungo vyao huwa wakakamavu.
    2. Wanaozingatia mienendo mizuri hudumisha afya.
    3. Wanaoepuka kazi hawapati shinikizo la damu
    4.  Wanaokula vyakula vyenye viinilishe huzuia kunenepa.
  8. Chagua funzo linalojitokeza katika aya ya mwisho
    1. Wanaokosa kuzingatia maelekezi hupata majuto.
    2. Mtu hawezi kufaidika kiafya bila kupata ushauri.
    3. Wanaodharau watu wenye hekima hupata magonjwa.
    4. Nchi haiwezi kupiga hatua bila raia wote kuzingatia maradhi.
  9. Umuhimu wa afya hauwezi kupuuzwa kwa vile
    1. mipango nchini hukwama wahudumu wakikosekana
    2. watu wagonjwa hawawezi kuizalisha mali
    3. maradhi husababisha kuzorota kwa maendeleo
    4. pesa nyingi hutumiwa kuwatunza walio hospitalini.
  10. Kisawe cha 'kujiuma vidole" ni
    1. kupiga vijembe
    2. kutia nanga.
    3. kupigwa butwaa.
    4. kujuta hatimaye.

INSHA

Andika insha ya kusisimua ukiendeleza kwa maneno haya:

Nilikuwa nimeketi sebuleni nikisoma kitabu cha hadithi

MWONGOZO 

  1. C
  2. B
  3. D
  4. A
  5. C
  6. B
  7. C
  8. A
  9. D
  10. C
  11. A
  12. B
  13. C
  14. C
  15. B
  16. B
  17. D
  18. D
  19. B
  20. C
  21. B
  22. D
  23. C
  24. C
  25. B
  26. C
  27. B
  28. A
  29. C
  30. D
  31. B
  32. C
  33. A
  34. D
  35. D
  36. C
  37. A
  38. D
  39. C
  40. C
  41. D
  42. A
  43. D
  44. D
  45. B
  46. A
  47. B
  48. A
  49. C
  50. D

 

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne hapo. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya uliyopewa.

Tunapotia guu katika __1__ __2__, walimu wetu wapendwa wanaendelea kutupa__3__huku tukifunzwa mengi kama vile __4__ ambavyo hutoa taarifa kuhusu vitenzi, vivumishi na hata vielezi. Huku hayo yakiendelea, tumepata __5__ kufahamu akisami pia, __6__, __7__ ambayo ni sehemu moja ya saba. Kwa moyo wa shukrani, __8__ kuwapa kongole mzomzo.

   A   B   C   D 
 1.   kidato cha nane    darasa la kwanza   kidato cha kwanza   darasa la nane 
 2.  mwakani  mwaka ujao   mwaka huu   mwaka kesho 
 3.  motisha  vitisho   mazoezi   talaka 
 4.  viarifa  vibadala   viwakilishi   vielezi 
 5.  nafsi ya  fursa ya   nafasi wa   wasaa ya 
 6.  mathalani  mithili ya   mifano   madhali 
 7.  tusui  sudusi   subui   humusi 
 8.  haitulazimu  hatuna budi  ina bidii  tuna budi


Kristina alipojiangalia tena__9__ kioo, aligundua kuwa uso wake uliokuwa __10__na kufanya mabaka sasa ulianza kurudisha unyevuunyevu wa awali. __11__ mauti ya mume wake yapata majuma mawili __12__ yalimdhoofisha, __13__ kuwa __14__. Kwa vyovyote vile, ilimpasa kuyazika ya kale na kuendelea na safari ya maisha japo kwa kuuma __15__.

   A     B      C    D 
 9.   ndani ya   katikati ya   na   kwa 
 10.  ukimeremeta   umenawiri   umesawijika   umeiva 
 11.   hata hivyo  Hata ingawa   Hivyo   Kwa hivyo 
 12.  zilizopita  yaliyopita   yalipita   zilipita 
 13.  alijipa moyo  alipiga mwayo   alikonga roho   alipiga mtindi  
 14.  mavi usioyala wayawingiani kuku?  mavi ya kale hayanuki   kuchamba kwingi ni kuondoka na mavi   mavi ya kale hayaachi kunuka
 15.  meno   shida   ulimi   chanda 

 

Kutoka swali la 16 hadi 30, jibu swali kulingana na maagizo   

  1. Chagua maelezo yaliyo sahihi. 
    1. Arafa: ujumbe wa maandishi unaotumwa kwa simu.
    2. Kipepesi: chombo cha kutuma na kupokea barua.
    3. Kikokotoo: chombo cha kutuma ujumbe kwa sauti.
    4. Mtandao: mfumo wa mawasiliano kupitia tarakilishi.
  2. Chagua silabi.
    1. Sh
    2. Dha
    3. Ng
    4. Th
  3. Upi ni usemi halisi wa sentensi ifuatayo?
    Mwalimu kwa hasira aliwaamuru wanafunzi wote wapige magoti na kumaliza kazi yao ya ziada. Mwalimu
    1. alifoka, "Pigeni magoti na mmalize kazi yenu ya ziada!"
    2. alisema, "Mpige magoti na mmalize kazi yenu ya ziada."
    3. alifoka, "Malizeni kazi yenu ya ziada na mpige magoti!"
    4. alisema wanafunzi wote wapige magoti na wamalize kazi yao ya ziada.
  4. Tambua sentensi yenye kivumishi cha idadi.
    1. Mtumwa huyu ni mtiifu sana. 
    2. Kitabu cha kasisi si cheusi.
    3. Jino langu linauma sana.
    4. Kiatu cha kwanza hakifai.
  5. Ni jozi gani iliyokosewa?
    1. Skrubu - bisibisi.
    2. Mpini - jembe.
    3. Mchi - kinu.
    4. Mkufu - kipini.
  6. Ni kiunganishi gani kisichoweza kukamilisha sentensi ifuatayo?
    Kauleni aliadhibiwa vikali ________________________ kufukuzwa shuleni.
    1. licha ya
    2. fauka ya
    3. bighairi ya
    4. pamoja na
  7. Tambua sentensi yenye a unganifu.
    1. Cha walimu ni safi.
    2. Kitabu cha mwalimu kimeanguka.
    3. Msipoziba nyufa mtajenga kuta.
    4. Nilimwona alipokuwa akienda maktabani.
  8. Ni kundi gani lenye nominoambata?
    1. Maji, marashi, mate.
    2. Njugumawe, batamzinga, askarikanzu.
    3. Safu ya milima, umati wa watu, kichala cha matunda.
    4. Kenya, Juma, Agosti.
  9. Nomino maskani huwa katika ngeli gani?
    1. PAKUMU
    2. YA-YA
    3. U-YA
    4. LI-YA
  10. Paka huyu ndiye alaye buku katika wingi ni paka hawa
    1. ndiyo walaye buku.
    2. ndio walao buku.
    3. ndiyo walao mabuku.
    4. ndio walao mabuku.
  11. Tambua sentensi yenye kielezi.
    1. Katika debe tanna maji.
    2. Kilichosimama ni hiki.
    3. Niliitika kwa sauti.
    4. Mtoto aliyesimama kando ya mto ni mwoga.
  12. Banati ni kwa msichana kama vile ___________________________ ni kwa kaptura.
    1. kinyasa
    2. bombo
    3. mvuli
    4. mshipi
  13. Chagua nahau iliyo tofauti kimaana.
    1. Aga dunia
    2. Kata kamba
    3. Konga roho
    4. Enda na ulelengoma
  14. Kamilisha methali: Wema
    1. haiozi.
    2. haigombi.
    3. hauozi.
    4. haukomi.
  15. Kitendawili:
    Mzungu analala na ndevu ziko nie.
    1. Mwiko.
    2. Hindi.
    3. Mvi.
    4. Unga

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31 hadi 40.

Hadithi! Hadithi! Hapo zamani za kale kabla ya majabali kukauka, kuku na mwewe walikuwa marafiki wa dhati. Usahibu wao ulikuwa ule wa kufa kuzikana. Waliishi pamoja kwa miaka na mikaka. Walishirikiana na kusaidiana katika lolote lililotokea, la furaha na la majonzi.

Walifanya kazi pamoja. Kila mmoja alijitahidi kadiri ya uwezo wake. Walishirikiana kama kinu na mchi. Bega kwa bega, walifanya kazi zao. Mwewe alijitwika jukumu la kulisha familia zote mbili naye kuku alikuwa na jukumu la kuwalinda watoto wao. Kuku alihakikisha wameshiba na kutulia.

Ndege hawa waliishi kwa amani na utulivu bila kukumbwa na tatizo lililowashinda kutatua. Urafiki wao ulifanya wakati mwingine walale njaa ili watoto wao washibe.

Siku moja walipata barua ya ualishi kutoka kwa ndege wenzao. Karamu ya kukata kwa shoka ilikuwa iandaliwe. Mwewe aliwatayarisha wanawe kwa sherehe. Kuku aligundua kuwa vifaranga wake walikuwa na kucha ndefu zilizowaaibisha. Hivyo, aliamua kumwomba mwewe wen.be. Mwewe alimpa wembe bila kusita kisha akamwambia, "Hakikisha kwamba umerudisha wembe wangu mara moja."

Kuku alitekeleza wajibu wake kwa haraka. Muda si muda, familia hizo mbili zikang'oa nanga kwa furaha. Karamun, kila mmoja na watoto wake alibugia mapochopocho. Vinywaji vilikuwa tele. Baada ya sherehe, walirejea nyumbani.

Siku iliyofuata, mwewe alimtuma mtoto wake kwa kuku kuuchukua wembe ili wanyolewe. Kuku alipigwa na butwaa alipogundua kwamba wembe wa mwewe haukuwapo. Wasiwasi ulimvamia mara moja. Huku na kule, alianza kuchakurachakura. Jasho lilimtiririka lakini wapi! Juhudi zake hazikumfaa.

Mtoto wa mwewe aliripoti haya kwa mama yake. Bila kungoja, mwewe alifika nyumbani kwa kuku. "Aka! Hujui wewe kuwa wembe huo ni mmoja kama moyo? Lazima nitwae fidia. Nitawala vifaranga wako mmoja mmoja hadi unirejeshee wembe wangu." Maneno hayo yalimchoma kuku moyoni kama mkuki. Tangu siku hiyo, kuku huchakurachakura huku na kule akiutafuta wembe wa mwewe. Naye mwewe huruka juu akiwasaka vifaranga wa kuku.

  1. Aya ya kwanza inaudokezea kwamba
    1. urafiki wa mwewe na kuku ulikuwa wa unafiki.
    2. mwewe na kuku walitengana sana.
    3. urafiki wa ndege hawa haukuwa wa ukweli.
    4. kuku na mwewe walipendana sana
  2. Neno lililopigiwa mstari mwishoni mwa aya ya kwanza lina maana sawa na
    1. huzuni.
    2. ufanisi.
    3. furaha.
    4. ugomvi.
  3. Katika kifungu ulichosoma, ni nani aliyekuwa akitafuta chakula?
    1. Kuku.
    2. Mwewe.
    3. Wote wawili.
    4. Watoto wao.
  4. Mwewe na kuku walishirikiana kama kinu na mchi. Methali inayoafikiana na hali hii ni
    1. bendera hufuata upepo.
    2. baniani mbaya kiatu chake dawa.
    3. kidole kimoja hakivunji chawa.
    4. adui mpende.
  5. Ni nini ambacho kinaonyesha kuwa ndege hawa waliwajali watoto wao?
    1. Kuwatafutia chakula kila siku. 
    2. Kuwatetea kila siku.
    3. Kulala njaa ili watoto washibe.
    4. Kwenda karamuni pamoja.
  6. Barua waliyoipata mwewe na kuku
    1. iliandikiwa watoto wao.
    2. iliwaalika katika karamu.
    3. iliwafurahisha sana.
    4. iliwaletea chakula.
  7. Ni kweli kuwa
    1. mwewe alikuwa mwaminifu.
    2. kuku hakuwapenda watoto wake.
    3. watoto wa mwewe walikuwa wachafu.
    4. kuku alikuwa mzembe.
  8. zikang'oa nanga..." ni sawa na
    1. zikaanza safari.
    2. zikakamilisha safari.
    3. zikafika sherehení.
    4. zikasherehekea.
  9. Kulingana na kifungu ulichokisoma, ni nini kilichomtia kuku wasiwasi alipogundua kuwa wembe haukuwapo? 
    1. Kuvunjika kwa urafiki wao.
    2. Kunyakuliwa kwa watoto wake.
    3. Onyo alilokuwa amepewa awali.
    4. Kukosa kuhudhuria karamu.
  10. Tabia ya mwewe ya kuruka juu ili kuwasaka vifaranga wa kuku inaonyesha tabia ya
    1. kuonyesha mapenzi. 
    2. kutoa onyo.
    3. ulafi.
    4. kulipiza kisasi.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 41 hadi 50.

Je, ni mnyama yupi mwenye nyayo kama za kasuku, awezaye kutazama pande zote kwa wakati mmoja na mwenye ulimi wenye kasi isiyomithilika? Si ndege, si chura bali ni kinyonga. Kwa makini ukichunguza vidole vya kinyonga, utagundua kuwa, kiaina, vinafanana na vya kasuku. Kila mguu unavyo vidole vitano vyenye upekee wa kuyakamata matawi sawasawa. Aidha, kila kidole kinao ukucha, hivyo, kuwafanya vinyonga wakwezi hodari.

Si miguu yao tu ambayo huajabiwa katika miili yao. Kwa mtazamo wa makini, itadhihirika kuwa katika kila moja ya macho yao, ukope wa juu na wa chini hukaribiana kiasi cha kuacha nafasi ya mboni pekee. Kinyume na binadamu, kinyonga huweza kutazama na kuona pande mbili tofauti mara moja, kwa wakati mmoja. Hili humwezesha kuona kwa nyuzi mia tatu na sitini bila tatizo. Vile vile, wao huwa na uwezo mkubwa wa kuona hususan wakiyaelekeza macho yao yote mawili katika azma moja. Wana uwezo wa kuwaona wadudu wadogo wadogo hata wakiwa mbali. Hili huwasaidia sana wakati wa mawindo.

Ili kulipiza katika utaratibu wao wa kutembea, vinyonga huwa na ndimi ndefu ajabu. Wakati mwingine, ndefu kuliko urefu wa miili yao kwa jumla! Yasemekana kuwa ndimi hizo zao huwa na kasi kiasi kuwa ni vugumu binadamu kuufuatilia mwondoko huo kwa macho. Ni kwa vipi ambavyo ndimi zao huwa na kasi hivyo? Hakika, ndimi zao huwa kama upote na mshale au manati. Jinsi ambavyo upote hurusha mshale ndivyo ambavyo ulimi wa kinyonga hutoka na kuingia kinywani mwake na hivyo kumsaidia kulinasa windo lake.

Talanta nyingine maarufu ya kinyonga ni uwezo wake wa kubadilibadili rangi ya ngozi yake. Anao uwezo wa kujibadili hadi rangi zote za upinde wa mvua na hata zambarau, waridi, nyeusi na hudhurungi. Uwezo huu huwasaidia kujificha kwa kujifananisha na mazingira waliyomo. Hata hivyo, sababu kuu ya uwezo huu huwa kudhibiti kiwango cha joto mwilini na kuelekeza hisia zao. Wao hutumia mabadiliko haya ya rangi kuonyesha hali ya kutamalaki na utetezi katika maeneo wanamoishi. Mabadiliko haya ya rangi aidha hutumika kuwavutia vinyonga wa jinsia tofauti.

Vinyonga wengi hupatikana Afrika. Hata hivyo, matabaka mengine machache yamewahi kushuhudiwa kwingineko kama vile Asia na pia majangwani. Maadamu vinyonga hawana masikio, wao hutumia hisia za mirindimo katika mazingira yao. Hayo yote ya kuajabia kuhusu kinyonga humfanya awe mwanajamii wa kuvutia mno miongoni mwa wanyama jamii ya mamba na mburukenge.

  1. Ni gani hapa si kweli kuhusu kinyonga?
    1. Anao ulimi wenye kasi ya juu.
    2. Nyayo zake hufanana na za kasuku.
    3. Huweza kutazama pande nyingi kwa wakati mmoja.
    4. kwa kiwango fulani, hufanana na chura.
  2. Badala ya kutumia neno lililopigiwa mstari katika aya ya kwanza, mwandishi angetumia
    1. kenge.
    2. lumbwi.
    3. ngwena.
    4. nyoka
  3. Ni nini huwafanya vinyonga kuwa wakwezi hodari?
    1. Miili yao miembamba.
    2. Vidole vyao vitano. 
    3. Kucha zao.
    4. Utaratibu wao katika kutembea.
  4. Kwa maoni yako, nafasi za mboni hubakia kwa nini? Ili
    1. kudhibiti kiwango cha nuru. 
    2. kuwawezesha vinyonga kuona. 
    3. kutenganisha kope za juu na za chini.
    4. kuajabiwa na mwanadamu.
  5. Ni uwezo gani wa vinyonga ambao mwanadamu anaweza kuiga?
    1. Kutazama pande kadhaa kwa wakati mmoja. 
    2. Kasi ya ulimi.
    3. Kujibadili rangi.
    4. Utaratibu katika kutembea.
  6. Je, ni gani hapa si sababu ya vinyonga kujibadili rangi?
    1. Kutambulisha hisia zao.
    2. Kupima viwango vyao vya jotomwili.
    3. Kujitofautisha na mazingira wanamoishi.
    4. Kutafuta wenza.
  7. Mwandishi ametaja mambo mangapi ya kuajabia kuhusu kinyonga?
    1. Manane
    2. Saba
    3. Matano
    4. Sita
  8. Sababu kuu ya kinyonga kubadilibadili rangi ni
    1. kujifananisha na mazingira.
    2. kuvutia jinsia tofauti. 
    3. kuonyesha hisia zao.
    4. kudhibiti jotomwili.
  9. Mwandishi ametaja uwezo gani wa vinyonga unaowafanya kuwa maarufu?
    1. Uwezo wao wa kukwea miti. 
    2. Kasi ya ndimi zao.
    3. Uwezo wao wa kujibadili rangi.
    4. Urefu wa ndimi zao.
  10. Kulingana na msemaji, vinyonga huweza kupatikana katika mabara yapi?
    1. Majangwani na misituni.
    2. Asia na Marekani.
    3. Asia, Afrika, Marekani, misituni na majangwani.
    4. Asia na Afrika.

INSHA

Umepewa dakika 40 kuandika insha yako. Andika insha ya kusisimua ukianzia kwa maneno haya:

Baada ya kupata maakuli, kila mmoja wetu alielekea ukumbini ili kupata burudani ya muziki. Kufunba na kufumbua,......................................................................

MARKING SCHEME

  1. D
  2. C
  3. A
  4. D
  5. B
  6. A
  7. C
  8. B
  9. D
  10. C
  11. B
  12. B
  13. A
  14. B
  15. A
  16. A
  17. B
  18. A
  19. D
  20. D
  21. C
  22. B
  23. B
  24. B
  25. D
  26. C
  27. B
  28. C
  29. C
  30. B
  31. D
  32. A
  33. B
  34. C
  35. C
  36. C
  37. D
  38. A
  39. A
  40. D
  41. D
  42. B
  43. C
  44. B
  45. D
  46. C
  47. D
  48. D
  49. C
  50. D

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne hapo. Jaza kila pengo kwa kuchagua jawabu lifaalo zaidi.

Nilisikia kuwa Zakayo alikuwa seremala aliyejulikana kijijini __1__. Samani __2__ mara kwa mara ziliwafaa na kuwapendeza wengi. Ungefika katika__3__ yake, usingekosa kupata __4__ waliofika ama kujionea __5__ kununua fanicha. Kila mmoja alifahamu kuwa ufanisi __6__ haukuja hivihivi tu. La hasha! Alikuwa mja mwenye kujituma na __7__. Daima alifahamu kuwa ___8___.

       A                   B              C               D 
 1.   pote   mote   chote   kote 
 2. zilizotengeneza    zilizotengenezwa    alizotengeneza   alizotengenezwa 
 3.  majilisi   makavazi   maabara   karakana 
 4.  watu anuwai   umati wa watu   mlolongo wa watu   safu ya watu 
 5.  au   wala  ila  bali
 6.  yake  huu  huo  hiyo
 7.  kulaza damu   kujitolea mhanga    kula mwande   kufa moyo 
 8.  mgaagaa na upwa hali wali mkavu   simba mwenda pole ndiye mia nyama   mkono mmoja hauchinji ng'ombe   mwana wa mhunzi asiposana huvukuta


Kila mtoto ana uwezo wa __9__ mambo mengi sana ikiwa atapewa nafasi inayofaa. Si vyema __10__ watoto kwa madai kuwa ni wa kike au wa kiume. Jinsia __11__ kutumika kama kigezo cha kuamua uwezo wa mtoto. Siku hizi, si __12__ kuwaona binadamu wa kike au kiume wakifanya kazi sawa. Hapo zamani, watu wangeshangaa kumpata mwanamke akifanya kazi ya __13__; yaani kufua vyuma. __14__ limekuwa jambo la kawaida kwani uwezo wao __15__ katika kazi za aina zote.

          A          B          C            D 
 9.   kutekeleza   kutendesha   kutelekeza   kutekelezwa 
 10.   kuwapendelea   kuwabagua   kuwatunukia   kuwashauri 
 11.  haufai   haifai   halfai   hamfai 
 12.  kawaida  muhimu   ajabu   rahisi 
 13.  ujume   unajimu   uhandisi   uhunzi 
 14.  Hiki   Huu   Hii   Hili 
 15.  unadhihirika  unadidimia  unadunishwa   unadhihirisha 

 

Kuanzia nambari 16 hadi 30 jibu kulingana na maagizo. 

  1. Tambua aina za maneno yaliyopigiwa mistari.
    Ambaye alikamilisha kazi asubuhi amefurahi.
    1. kivumishi, nomino
    2. kivumishi, kielezi
    3. kiwakilishi, kielezi
    4. kiwakilishi, nomino
  2. Sentensi gani iliyotumia nomino ambata?
    1. furaha
    2. mbwakoko
    3. thureya ya nyota
    4. kitambaa
  3. Chagua maelezo ambayo ni sahihi.
    1. Mjume hufanya kazi ya kufua visu.
    2. Kinu na mchi hutumika kukunia nazi.
    3. Bomba la kutolea moshi jikoni huitwa dohani.
    4. Nyonga hupatikana kati ya goti na paja. 
  4. Koloni hutumika kwa njia gani?
    1. Kuunganisha sentensi mbili zinazokaribiana kimaana.
    2. Kuonyesha kuwa maneno yaliyokuwa yakisemwa hayakukamilika.
    3. Kuonyesha mwisho wa sentensi kamilifu.
    4. Kutanguliza orodha katika sentensi. 
  5. Sentensi gani ambayo ni sahihi kati ya sentensi zifuatazo?
    1. Maji chafu hayafai kunywewa.
    2. Taifa lenye linaendelea vizuri ni hili. 
    3. Mimea yote yalimea vizuri.
    4. Madaktari wamewatibu wagonjwa hao.
  6. Ugonjwa gani ambao hutokana na baridi kati ya magonjwa yafuatayo?
    1. saratani
    2. waba
    3. unyafuzi
    4. kichomi
  7. Chagua sentensi iliyo na kitenzi katika hali ya kufanyiza
    1. Aliyauza matunda yake katika soko la Kongowea.
    2. Tendo la kuwaoza wasichana wachanga limepigwa marufuku.
    3. Matunda yaliyooza yarnetupwa mbali.
    4. .Aliuliza swali hilo kwa wanafunzi wawil 
  8. Tambua matumizi ya 'kwa' kwenye sentensi ifuatayo.
    Alipofika kwa mjomba wake alipokelewa kwa furaha.
      1. kifaa, namna
    1. namna, ala
    2. kihusishi, matumizi
    3. kihusishi, jinsi
  9. Sentensi gani iliyotumia kivumishi kiashiria?
    1. Kalamu nzuri iliwekwa ndani ya mkoba.
    2. Nyumba yake imejengwa ikakamilika.
    3. Kijana mwenyewe atapewa kitabu hicho.
    4. Wanafunzi wengi wamepanda miti. 
  10. Onyesha sentensi iliyo katika hali timilifu.
    1. Ungefuata masharti ungekuwa mshindi.
    2. Hakuelewa kuwa usafi ni muhimu.
    3. Nguo hazijakauka kwa njia nzuri.
    4. Sitaki kujihusisha na matumizi ya dawa za kulevya.
  11. Tambua maamkuzi ambayo ni ya wakati ulio tofauti.
    1. umeshindaje 
    2. sabalheri 
    3. umeamkaje
    4. chewa
  12. Chagua ukanusho wa:
    Aliyewasili alipigiwa makofi. 
    1. Asiyewasili hakupigiwa makofi.
    2. Aliyewasili hajapigiwa makofi. 
    3. Aliyewasili hakupigiwa makofi. 
    4. Asiyewasili hajapigiwa makofi.
  13. Mwanzele alipokuwa akielekea nyumbani wakati wa jioni, kivuli chake kilikuwa nyuma yake. Je, nyumbani kwao ni upande gani wa dira?
    1. mashariki
    2. kaskazini
    3. kusini
    4. magharibi
  14. Tambua ukubwa wa;
    Mbuzi mwenye uso mdogo amelala chini ya mti.
    1. Buzi lenye juso dogo limelala chini ya jiti.
    2. Kibuzi chenye kijuso kidogo kimelala c hini ya kijiti.
    3. Kibuzi chenye kijuso kidogo kimelala chini cha kijiti.
    4. Buzi lenye juso dogo limelala chini la jiti.
  15. Mvulana ni kwa msichana kama vile jogoo ni kwa _______________________________.
    1. jimbi
    2. kikwara
    3. koo
    4. kipora

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata.  

Ukiitathmini jamii yetu kwa makini, utagundua kuwa maovu yanazidi kuzagaa na kushamiri kote. Ni nadra sana kwa siku kumalizika bila kusikia habari za maovu kama vile ubakaji, mauaji, wizi, utapeli, vita na kadhalika. Wengi wamekuwa wakijisaili mara kwa mara ili kupata suluhu. Kuwategemea maafisa wa polisi nako kumekuwa kazi ya bure bilashi. Hii ni kwa kuwa polisi wenyewe nao wana matatizo yaliyowazidi nguvu. Kuna nyakati ambapo polisi huwafyatulia risasi na kuwaua raia wanaofaa kuwalinda. Ajabu iliyoje! Nyakati zingine, maafisa wa usalama huwaua jamaa zao na kujiua wao wenyewe. Hali ya polisi kuchukua hongo na kupuuza sheria imekuwa jambo la kawaida. Chambilecho marehemu babu yangu, Mola ailaze roho yake mahali pema peponi, baadhi ya maafisa wa usalama wamekuwa kama paka waliojukumishwa kuyatunza maziwa. Kazi yao ikawa kuyanywa bila kujali.

Je, maovu haya yanachangiwa na nini? Inadaiwa kuwa jambo la msingi ni kupanda kwa kiwango cha maisha. Wataalam wanasema kuwa kupata mahitaji ya kimsingi kama vile chakula, makazi na mavazi kumekuwa kama kumtafuta paka mweusi katika giza. Wengi wanapozidiwa na mzigo wa maisha, wanakata shauri kuiba, kuwatapeli wenzao au kuua ili wapate pesa za kuzikimu aila zao. Wengine nao huona kuwa kuwaua watoto na kujiua ni njia rahisi ya kujiondoa na kuwaondoa wapendwa wao katika ulimwengu huu wenye madhila na mizingile chungu nzima. Lile wanalofaa kujua ni kuwa njia hizo hazifai kabisa. Awali ya yote, ni jambo la busara kufahamu kuwa Mungu ndiye mwenye mamlaka juu ya uhai wa mja yeyote. Kujiua au kumwua mtu ni dhambi mbele ya mwenyezi Mungu. Maovu mengine kama vile wizi na utapeli humletea mtu majuto tele.

Sababu nyingine ni tamaa. Kuna wengi katika jamii ambao hawatosheki na kile wanachokipata. Kwa nini afisa wa polisi aliye na mshahara ajiingize katika shughuli za ufisadi? Kuna haja gani kwa gavana anayelipwa kitita cha pesa kupora mali ya umma? Daktari wa hospitali ya umma anaibaje dawa katika hospitali na kuziuza kama si kuongozwa na tamaa? Bila shaka, wanaongozwa na tamaa. Tamaa humfanya mtu asitosheke. Anapopata nne, hutamani kuwangepata nane. Pale anapojaliwa kupata sita, huona kuwa ingekuwa afadhali kama angepewa tisa. Japo ni vyema kupiga hatua maishani, ni vyema hatua hizo zipigwe katika mipaka ya kisheria na kanuni zilizowekwa.

Isitoshe, wapo wengi walio na mazoea ya kupuuza sheria. Naam, hawa ni wale wenye hulka za kuenda kinyume na maagizo. Wao hufurahia sana wanapokiuka kanuni zilizowekwa. Yamkini, watu wa sampuli hii hutaka kuona lile litakalotokea baada ya kuvunja sheria. Nimewahi kusikia visa vya watu waliowapa sumu na kuwaua mifugo wa mwingine bila sababu. Furaha yao ni kuona maovu yakitokea na hasara kumpata mtu. Wengine hutembea na rungu na mijeledi usiku wa manane ili kuwacharaza wapitanjia bila sababu maalum. Ajabu ni kwamba wao hawawezi wakatamani kufanyiwa maovu kama hayo.

Aidha, kuna wengi ambao hukosa utt. Kukosa utu humfanya mtu asimjali mwenzake wala kumwonea huruma. Kukosa utu husababisha mtu asijiulize, "Je, nikifanyiwa hivyo nitahisi vipi?" Mwizi anayemwibia mtu pesa, simu, mkoba, kumpokonya mavazi na kisha kumpiga huwa anaongozwa na nini? Huo si unyama? Mtu anawezaje kumkatakata mume au mkewe kwa kigezo kuwa yeye ni mkizi? Je, haelewi kuwa hasira hasara?

Ili kupata suluhisho la kudumu, serikali na jamii kwa jumla ina jukumu la kubuni nafasi nyingi za kazi. Hili litachangia katika kupunguza gharama ya maisha. Matumizi ya dawa za kulevya nayo yanafaa kupigwa marufuku. Walevi au waraibu wa mihadarati husababisha maovu mara kwa mara. Zaidi ya yote, ni jambo la busara kuiombea nchi yetu kucha kutwa ili Mola aiauni.

  1. Kwa mujibu wa aya ya kwanza, ni kweli kuwa;
    1. Msomaji amekuwa akifanya uchunguzi kuhusu kutokea kwa maovu.
    2. Siku hata moja haiwezi ikapita bila visa vya kutokea kwa maovu kutangazwa. 
    3. Maovu yamekuwa yakitokea mara kwa mara katika jamii.
    4. Ni vigumu kusikia kuwa kumetokea maovu mbalimbali katika jamii yetu.
  2. Neno 'wakijisaili' lina maana gani jinsi lilivyotumika katika kifungu?
    1. wakishangaa
    2. wakijiuliza
    3. wakijirekebisha
    4. wakijituliza
  3. Yafuatayo ni maovu yaliyotajwa katika aya ya kwanza isipokuwa;
    1. ufisadi
    2. ubakaji
    3. mauaji
    4. anas
  4. Aya ya pili inadokeza kuwa,
    1. Kupanda kwa gharama ya maisha ndio msingi wa kutokea kwa maovu.
    2. Kila anayezidiwa na mzigo wa maisha hujiingiza katika maovu kama vile wizi.
    3. Baadhi ya watu hutekeleza maovu wanaposhindwa kutatua matatizo yanayowakumba.
    4. Mungu pekee na serikali ndio wenye mamlaka juu ya uhai wa mja yeyote.
  5. Kauli 'polisi huwafyatulia risasi na kuwaua raia wanaofaa kuwalinda' inaonyesha;
    1. kinaya
    2. majazi
    3. kejeli
    4. tabaini
  6. Msimulizi wa makala haya anaeleza kuwa mara nyingi ufisadi hutokana na;
    1. kutotosheka.
    2. kutamauka.
    3. kukosa utu.
    4. kuzoea kuvunja sheria.
  7. Msimulizi ana maana gani anaposema kuwa 'kumekuwa kama kumtafuta paka mweusi katika giza'?
    1. ni nadra
    2. ni muhali
    3. ni shani
    4. ni sahili
  8. Kauli 'wao hawawezi wakatamani kufanyiwa maovu kama hayo' inaashiria ukweli wa methali gani?
    1. Baniani mbaya kiatu chake dawa.
    2. Mkuki kwa nguruwe kwa binadamu uchungu.
    3. Ndugu mui heri kuwa naye.
    4. Mui huwa mwema.
  9. Maneno 'yeye ni mkizi' yana maana gani jinsi yalivyotumika katika kifungu?
    1. ana hasira
    2. ni mkali
    3. ni katili
    4. ni mwenye tovu
  10. Kulingana na kifungu, ubunifu wa nafasi za kazi:
    1. ndiyo njia bora zaidi ya kukabiliana na maovu katika jamii.
    2. ni jukumu la serikali ya nchi husika. 
    3. ndiyo njia kuu ya kupunguza maovu katika jamii.
    4. unaweza kuchangia katika upunguzaji wa maovu.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata.   

Wakazi wa Ihonje walikusanyika katika kikao cha kumpa heshima za mwisho Bwana Kapombe. Japo awali alijulikana na kila mmoja kama Adili, hulka zake za kukumbatia ulevi zilifanya akabatizwa jina la Kapombe. Jina halisi alilopewa na wazazi wake likayeyuka kama barafu kikaangoni na kupotea kama moshi hewani. Boma lao lilijaa watu kutoka janibu za mbali na karibu. Wapo waliolia na kulalamikia namna kifo kilivyoipokonya jamii mtu wa maana. Wengine waligalagala mchangani na kutishia kujitupa katika kaburi lililochimbwa ikiwa hapakujitokeza yeyote wa kuwazuia. Ukweli ni kuwa kijana wa watu alikuwa ameacha mkono kulingana na maoni ya wanajamii hao.

Japo mwili wake haukuwa umepatikana, ilikuwa wazi kuwa asingekuwa hai kwa namna yoyote ile. Kiwango chake cha ulevi kilikithiri na kupita mipaka. Walifahamu kuwa kama hakugongwa na gari, basi alianguka mtoni na kufa au alikunywa pombe kupita kiasi. Kijana huyo alikuwa ametoweka siku kadhaa zilizotangulia. Ndugu, jamaa na marafiki walimsaka kwa siku tatu mtawalia. Hata hivyo, juhudi zao hazikuzaa matunda. Msako huo ulilenga sehemu mbili kuu, vituo vya polisi na vituo vya kuuzia pombe haramu. Ilikuwa desturi kwake kupatikana katika makao ya wagema tangu macheo hadi machweo, kucha kutwa. Alifanya kibarua na kulipwa hela kidogo, zote zilikuwa zawadi kwa mgema. Alipokosa kibarua, aliiba kuku, shati la mtu au sufuria la mama yake na kuuza. Wakati mwingine hakupatikana akiwa kwa mgema. Huo ulikuwa wakati ule aliotiwa mbaroni ama kwa kupatikana akibugia pombe haramu au kushukiwa kwa wizi wa vitu vya wanajamii.

Alipokosekana katika maeneo hayo mawili, iliamuliwa kwa kauli moja kuwa alikuwa amefariki. Kwa mujibu wa mila na desturi za jamii hiyo, walilazimika kuuzika mgomba na kufanya matanga yake. Siku hiyo ya mazishi', boma la akina Kapombe lilijaa: si wake, si waume, si vijana, si wazee, si matajiri, si wachochole. Vyakula ainati viliandaliwa: ugali, nyama, pure, chai ya maziwa, chai ya mkandaa, kitoweo cha kuku miongoni mwa vyakula vingine.

Harakati za mazishi zilipokuwa zimenoga, mtu mmoja karibu na lango la boma alipiga ukelele wa hofu. Wengine walipoangalia, walimwunga mkono kwa kupiga unyande, kamsa, nduru na mayowe. Ya Mungu ni mengi! Kapombe alionekana akijikokota kurudi nyumbani kwao. Alikuwa mnyonge, mngonge kama utumbo. Alikuwa mchafu mithili ya kilihafu. Alinuka fee ungedhani kuwa ni fondogoo. Wapo waliopiga mbio kwa kasi ya umeme. Masufuria ya vyakula yaligongwa na kukimwaga chakula. Wengine nao walibeba chakula kicho hicho, hasa kuku. Palikuwa na hali ya kuchanganyikiwa katika boma lote. Wachache waliokuwa na ujasiri walitulia tuli kama maji mtungini. Utulivu uliporejea, Kapombe alipewa nafasi ya kujieleza. Kumbe hakuwa ameaga dunia. Mtoto wa watu alilewa chakari bin chordo. Maadamu hakuwa amekula kwa muda, pombe ilimzidi nguvu na kusababisha kuzimia kwake. Alinyooka twaa kando ya barabara kama mzoga.

Alifafanua kuwa alizinduka na kujipata katika chumba kilichoogofya. Hali iliyokuwa mie ndani haikuelezeka kwa maneno yoyote. Alikata shauri kutoka nje. Alipoufungua mlango wa chumba, mabawabu waliokuwa pale nje walipiga mbio kwa hofu na woga wa kunguru. Kumbe alipopatikana akiwa amezimia njiani, alidhaniwa kwamba ameaga dunia, akapelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti. Msamaria mwema alimfanyia hisani na kumpeleka hospitalini alikolazwa kwa siku tatu akifanyiwa matibabu. Kapombe alikula yamini kuwa asingelewa tena. Asingemwamkua wala kumwangalia mgema. Asingewaza kuhusu pombe wala kileo chochote. Hewaa! Alikuwa amepata funzo la mwaka.

  1. Jina halisi ambalo kapombe alipewa na wazazi liliyeyushwa na nini?
    1. mazoea ya wakazi
    2. tabia zake za ulevi
    3. mabadiliko ya maisha
    4. dawa za kulevya
  2. Eleza maana ya 'janibu' jinsi lilivyotumika katika kifungu.
    1. matabaka
    2. sehemu
    3. viwango
    4. safari
  3. Kulingana na aya ya pili, ni kweli kuwa;
    1. wakazi walithibitisha kuwa Kapombe alikuwa amefariki.
    2. ilisemekana kuwa Kapombe alionekana katika kituo cha polisi na kituo cha kuuzia pombe haramu.
    3. ndugu, jamaa na marafiki walianza kumsaka baada ya siku tatu.
    4. Kapombe alitumia kila njia ili apate pesa za kununulia vileo.
  4. Ni kweli kuwa waliokuwa wakilia nyumbani kwa akina Kapombe walikuwa;
    1. wanafiki.
    2. waombolezaji.
    3. majirani.
    4. masahibu.
  5. Msimulizi anaposema kuwa juhudi zao hazikuzaa matunda', ana maana kuwa;
    1. ziligonga mwamba.
    2. zilifua dafu.
    3. zilishamiri.
    4. zilikuwa maarufu.
  6. Kapombe alifafanua jinsi;
    1. alivyozinduka.
    2. alivyolala.
    3. alivyozimia.
    4. alivyoshtua watu.
  7. Kwa maoni yako, kwa nini watu wengi walifika nyumbani kwa akina Kapombe wakati wa 'mazishi' yake?
    1. walitaka kumwona akirudi nyumbani.
    2. walijua kuwa hakuwa amekufa bali alikuwa tu hospitalini.
    3. walizingatia mila na desturi za jamii yao.
    4. walijua kuwa kungekuwa na chakula kingi cha kufurahia.
  8. Yawezekana kuwa Kapombe aliamua kuuacha ulevi kutokana na:
    1. kuogopa kushikwa na polisi mara kwa mara.
    2. kuchoshwa na hali ya kudharauliwa na wanakijiji kila wakati.
    3. ushauri aliopewa na madaktari alipokuwa hospitalini.
    4. dhiki nyingi alizopitia kutokana na ulevi wake.
  9. Wakazi walitarajia kuwa Kapombe angepatikana katika;
    1. kituo cha polisi, makao ya mgema 
    2. kituo cha polisi, hospitali
    3. chumba cha kuhifadhi maiti, makao ya mgema
    4. chumba cha kuhifadhi maiti, hospitali 
  10. Ujumbe katika kifungu hiki unaweza ukarejelewa kwa methali kuwa;
    1. Mgema akisifiwa tembo hulitia maji. 
    2. Mtoto umleavyo ndivyo akuavyo.
    3. Mtegemea cha nduguye hufa maskini. 
    4. Hakuna marefu yasiyokuwa na ncha.

INSHA   

Andika Insha ya kusisimua itakayoanzia kwa maneno yafuatayo

Niliposikia jina langu likiitwa, nilishangaa. Sikuyaamini masikio yangu. Moyoni nilijawa na ................................................

MARKING SCHEME

  1. D
  2. C
  3. D
  4. A
  5. A
  6. C
  7. B
  8. A
  9. A
  10. B
  11. B
  12. C
  13. D
  14. D
  15. A
  16. C
  17. B
  18. C
  19. D
  20. D
  21. D
  22. B
  23. D
  24. C
  25. C
  26. A
  27. C
  28. D
  29. D
  30. C
  31. C
  32. B
  33. A
  34. C
  35. A
  36. A
  37. B
  38. B
  39. A
  40. D
  41. B
  42. B
  43. D
  44. A
  45. A
  46. A
  47. C
  48. D
  49. A
  50. D

Soma mazungumzo haya kisha ujibu maswali 1 hadi 5

Mwalimu: Hamjambo wanafunzi?
Wanafunzi: Hatujambo sana mwalimu Lydia! Shikamoo?
Mwalimu? Marahaba watoto wangu! ketini.
Wanafunzi: Asante sana mwalimu!
walimu: Leo nataka kwanza kuangalia kucha ya kila mtu. Sasa kila mtu aende mbele kisha nikague kama kucha ni safi na fupi. Nitaanza na wasichana kwanza.
Mwanafunzi. 1: Tafadhali mwalimu, mama hana pesa ya kununua wembe. Nitakata kesho unisamehe!
Mwalimu: Ngoja pale kwa mlango ungoje kiboko.
Mwanafunzi 2: Mwalimu makucha zangu ni fupi na safi sana. Ebu angalia.
Mwalimu: Ni vizuri Angela. Rudi kwenye kiti chako.
Mwanafunzi 3: Mwalimu makucha zangu ni refu lakini safi sana.
Mwalimu: Nitakusamehe leo lakini uikate kesho.
Mwanafunzi 3: Asante mwalimu.

  1. Lydia alikuwa             
    1. Mwanafunzi
    2. Mwalimu mkuu
    3. Mwalimu wa darasa
    4. Mpishi
  2. Kinyume cha neno "wasichana" ni
    1. wavulana 
    2. msichana 
    3. walimu 
    4. watoto
  3. Ni neno lipi la adabu aliotumia mwanafunzi wa tatu katika mazungumzo haya?
    1. Tafadhali 
    2. Pole
    3. Labda
    4. Asante
  4. Watoto wangapi waliokaguliwa na mwalimu?
    1. wanne
    2. watatu 
    3. wawili 
    4. mmoja
  5. Mtoto yupi alikuwa na kucha fupi na safi?
    1. Angela
    2. Lydia
    3. Mwanafunzi 3 
    4. Mwanafunzi 1

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 13.
KSWSQN6

Mama Jamila alimaliza kupika chamcha, yaani chakula cha mchana. Alikuwa amewapikia wanawe ugali na kuku. Aliwapakulia watoto wake. Kila mmoja akapata kipande kimoja kikubwa cha kuku na ugali wake. Aliwaita wakae chumbani wale chakula chao. Jamila alipopewa chakula chake alikataa kukaa na nje na chakula chake. wengine na kutoka alisimama kwa mshangao. Mamake alipogundua kilichofanyika, alimwuliza, "Jamila nyama iko Mara alipotoka nje akaja mwewe na kuchukua nyama yake kutoka sahanini. Jamila wapi?" Jamila akakosa la kusema. Alilia na kujuta kwa nini hakumtii mamake kwa kuketi chumbani kula chakula na wengine.

  1. Mwewe alichukua nini?              
    1. Jamila
    2. Sahani
    3. Nyama
    4. Ugali
  2. Mwewe ni aina ya
    1.  ndege
    2. simba
    3. mwizi
    4. nyoka
  3. Chamcha ni chakula cha saa kama 
    1.  asubuhi 
    2. saa saba
    3.  jioni
    4. usiku
  4. Tunasema: Mama Jamila alikula ugali               kuku.
    1. na
    2. kando na
    3.  kwa
    4. pamoja na
  5. Wingi wa neno "chakula" ni
    1. chakula
    2. viakula
    3. vyakula
    4. mavyakula
  6. Kuku hutaga
    1. nyama
    2. ugali
    3. maziwa
    4. mayai
  7. Kwa nini Jamila alisimama kwa mshangao? Kwa sababu
    1. alipewa chakula kidogo. 
    2. alipigwa na Mwewe
    3. chakula chake kilichukuliwa na Mwewe 
    4. hakushiba
  8. Ni nani aliyekuwa amepika chakula?
    1. Jamila
    2. Mwewe
    3. Hatujaambiwa
    4. Mama Jamila

Kutoka nambari 14 hadi 18, jaza mapengo ukitumia maneno uliopewa chini.

Wanyama wa nyumbani wana faida        14         kwetu. Ng'ombe na mbuzi        15        nyama na maziwa.          16        wanyama hao wanatupatia ngozi           17        hutumika        18            kutengeneza ngoma. Punda na farasi hutubebea mizigo. Kuku na bata hutupa mayai

  A      B      C      D   
 14.  mingi    nyingi    kingi    wengi  
  15. hutupatia       hutupitia      hutupatiwa      hutupata   
  16.halafu      kisha      ndio      baadaye   
 17. ambayo       ambaye      ambao      ambacho  
 18. zigo      mizigo      mizigo      mazigo   

Kutoka swali 19 hadi 30, jibu kulingana na maagizo.

  1. Tambua akisami hii kwa maneno.
    KSWSQN19
    1. Robo 
    2. Thuluthi
    3. Nusu
    4. Sudusi
  2. Kamilisha methali
    Bendera                 
    1. ni baraka 
    2. hufuata upepo
    3.  ina rangi nne
    4. ni maridadi
  3. Umbo hili huitwa?
    KSWSQN21
    1. mraba
    2. mstatili
    3. duara
    4. duara dufu
  4. Mpira iko                 ya meza.
    1. chini ya
    2. ndani ya
    3. juu ya
    4. kando ya
  5. Andika sentensi kwa wingi.
    Mtoto huyu ni mgonjwa.
    1. Watoto hawa ni wagonjwa.
    2. Watoto hao ni wagonjwa.
    3. Watoto hawa ni mgonjwa.
    4. Matoto hawa ni wagonjwa.
  6.  "Kikapu" iko katika ngeli gani?
    1. LI-YA
    2. U-ZI 
    3. M-WA
    4. KI-VI
  7. Sentensi hii iko katika wakati gani?
    Mgeni atakuja kwetu.
    1. uliopo
    2. ujao
    3. uliopita
    4. wowote
  8. Nyasi mbichi zina rangi ya
    1. nyeusi
    2. nyekundu
    3. samawati
    4. kijani.
  9. Nikiwa na njaa nitaenda kwa
    1. mpishi
    2.  mkulima
    3. mwalimu
    4. nahodha
  10. Kanusha sentensi ifuatayo.
    Unywe maji safi                     maji chafu.
    1. usikunywe 
    2. ukunywe 
    3. usinywe
    4. usimeze
  11. Kinyume cha neno "cheka" ni
    1.  chekea
    2. chekelea 
    3. lia
    4. furahia
  12. Sehemu ya dira imeandikwa Q ni
    KSWSQN30
    1. magharibi 
    2. kusini
    3. mashariki
    4. kaskazini 

Andika insha murwa kuhusu 

DARASA  LETU MPYA

MWONGOZO 

  1. C
  2. A
  3. D
  4. B
  5. A
  6. C
  7. A
  8. B
  9. C
  10. C
  11. D
  12. C
  13. D
  14. B
  15. A
  16. C
  17. A
  18. C
  19. A
  20. B
  21. C
  22. C
  23. A
  24. D
  25. B
  26. D
  27. A
  28. C
  29. C
  30. C
Tagged under

Soma vifungu vifuatavyo, vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne. Jaza kila pengo kwa kuchagua jawabu lifaalo zaidi.   

Siku hiyo___1___Jumamosi niliamka nikiwa mzima kama ___2___. Mzazi wangu alikuwa ___3___ katika maonyesho ya kilimo. Tulipofika katika lango kuu, ilitubidi kulipa ___4___ baada ya kupanga ___5___ kwa muda wa nusu saa. ___6___  na wanyama wa kuvutia humo kwa mfano ___7___ farasi, twiga simba, chui na wengineo. Nilivutiwa pia na ___8___ mpya ya kilimo. Ulipowadia wakati wa ___9___ tulirudi nyumbani nikiwa na furaha ___10___.

   A   B   C   D 
 1.   za   la   wa   ya 
 2.  kigongo   kaburi   kinyonga   ibada 
 3.  atanipeleka   angenipeleka   akinipeleka   hunipeleka 
 4.  nauli  kiingilio  fola  karo
 5.  laini  nguo  vyombo  foleni
 6.  Mlikuwa  Palikuwa  Kulikuwa  Pangekuwa 
 7.  ; . : /
 8.  uinjinia  teknolojia  ufundi  maarifa
 9.  macheo  mawio  alfajiri  machweo
 10.  riboribo  kwikwikwi  tiki  pomoni

 

Ajali za barabarani ___11___ shida kubwa humu nchini. Idadi kubwa ya watu ___12___ maisha yao huku wengine wakijeruhiwa ___13___. Sababu kuu ni kuwa madereva wamekuwa ___14___ sana.  Tushirikiane ili kupunguza ajali nchini kwani ___15___.

   A   B   C   D 
 11.   limekuwa   zingekuwa   ilikuwa   zimekuwa 
 12.  haijapoteza   imepoteza   haipotezi   wamepoteza 
 13.  vizuri   vyema   vibaya   zaidi 
 14.  wapotovu  waaminifu   waangalifu   wema 
 15.  ajali haina kinga   jifya moja halinjiki chungu   haraka haraka haina baraka    jungu kuu halikosi ukoko.

 

Kutoka swali la 16 hadi 30 jibu kulingana na maagizo.

  1. Chagua sentensi iliyo katika hali timilifu
    1. Mvua ilinyesha tukapanda.
    2. Nchi ingelindwa ingestawi
    3. Mashindani yakikamilika tutaondoka
    4. Mgeni wetu hajawasili
  2. Andika akisami  6/7 kwa maneno
    1. Tusui sita
    2. Thumuni saba
    3. Subui sita
    4. Tusui saba
  3. Ni orodha ipi yenye vitenzi pekee?
    1. Cheza, imba, soma
    2. Mtiifu, zuri, karimu
    3. Polepole, vibaya, haraka
    4. Juu ya, katika, kwenye
  4. Chagua nomino iliyoundwa kutokana na kitenzi nyamaa
    1. nyamazia
    2. unyamavu
    3. nyamaza
    4. nyamavu
  5. Ni mdudu yupi husababisha ugonjwa wa malale?
    1. Mbu
    2. Chawa
    3. Mbung'o
    4. Konokono
  6. Shairi lenye mishororo mitatu katika kila ubeti huitwa
    1. Tarbia
    2. Takhmisa
    3. Tathnia
    4. Tathlitha
  7. Andika kwa wingi:
    Rafiki yangu amemkamata koo na jogoo.
    1. Rafiki zetu wamewakamata koo na jogoo
    2. Marafiki zetu wamewakama makoo na majogoo
    3. Rafiki wetu wamewakamata makoo na majogoo
    4. Marafiki zangu wamewakamata koo na jogoo
  8. Ni orodha ipi yenye vitate?
    1. Baba-papa
    2. Mvulana - barobaro
    3. Jenga - bomoa
    4. Panda - vua
  9. Ni methali ipi yenye maelezo kuwa vitendo vizuri hupongezwa na mtu husifiwa kwa matendo yake mema?
    1. Dua la kuku halimpati mwewe
    2. Haba na haba hujaza kibaba
    3. Chanda chema huvikwa pete
    4. Kinga na kinga ndipo moto uwakapo
  10. Kanusha sentensi ifuatayo
    Mwalimu aliyefika ametufunza vyema
    1. Mwalimu asiyefika hakutufunza vyema
    2. Mwalimu hakufika wala hakutufunza vyema
    3. Mwalimu aliyefika hajatufunza vyema
    4. Mwalimu aliyefika hatatufunza vyema
  11. Msimu wa baridi nyingi bila ya mvua huitwa
    1. kiangazi
    2. masika
    3. vuli
    4. kipupwe
  12. Maneno, waraka, nyasi na uo huwa katika ngeli gani?
    1. U-ZI
    2. I-ZI
    3. U-YA
    4. I-I
  13. Mtu huyu ni kinyonga. Maneno haya yametumia fani ipi ya lugha?
    1. Tashbihi
    2. Istiara
    3. Msemo
    4. Nahau
  14. Tegua kitendawili
    Huku mwamba na kule mwamba.
    1. Giza
    2. Ardhi
    3. Jeneza
    4. Kaburi
  15. Karibu imetumikaje katika sentensi?
    Darasa letu lina karibu wanafunzi thelathini.
    1. Kuonyesha wakati
    2. Kuonyesha nusura
    3. Kuonyesha takribani
    4. Kuonyesha makaribisho

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31 mpaka 40.

Hapo zamani za kale, paliishi mzee mmoja aliyeitwa Maarifa. Maarifa alimwoa mke mmoja na kuweza kufanikiwa kupata mwana aliyeitwa pendo. Pendo alikuwa mtoto wa pekee katika aila hiyo. Mabonge ya nasaha aliyopewa na baba yake yaliangukia masikio yaliyotiwa nta.

Maarifa, mke wake na mtoto wao Pendo waliishi katika jamii iliyokuwa na ushirikiano kwa wema na mabaya. Jamii hii ilishi kwa kutegemea mifugo na kulima mashamba madogo madogo. Pendo alipoendelea kukua alijihisi ameerevuka kiasi cha kuwajaribu wakuu wake akili. Kweli aliyesema akili nyingi huondoa maarifa hakukosea.

Baadhi ya mafunzo aliyopewa na baba yake ni kuwa akienda kulisha kondoo apige ukemi pindi mbwa mwitu watokeapo na atapata usaidizi haraka sana. Siku moja Pendo alienda kulisha mifugo mbali kidogo na nyumbani. Alifikiri na akaona ni bora apige ukemi aone kutatokea nini.

"Uuuwi! Uuuwi! Uuuwi! Njooni haraka, mbwa mwitu wamevamia kondoo." Punde si punde wanaume wa miraba minne, mashunjaa wa kijiji walifika huku wamejihami kwa nyuta na mishale. Waliduwaa kuona Pendo akicheka huku akiwa na raha. Ni ibra iliyoje?

Wanaume walirejea nyumbani na kumweleza Maarifa kisa chote. Pendo alipowasili alioswa na kukemewa na wazazi wake. Mwana muwi haongeleki mara moja. Pendo alirudia tendo lake mara ya pili. Nao wanaume wakaja kama safari ya kwanza. Tukio hilo lilikuwa mchezo mbaya wa kuchezea watu wazima.

Siku ya tatu, Pendo alipokuwa akilisha mifugo, mbwa mwitu walitokeza ghafla. Alipiga mayowe lakini hakuona hata mtu mmoja aliyekuja kumsaidia. Watu walidhani ni mzaha ule wake wa kawaida. Maskini Pendo, mbwa mwitu waliwala kondoo wote na hatimaye kumjeruhi vibaya. Pendo alijuta kwa kutofuata mawaidha aliyopewa na wakuu wake.

  1. Ni nini maana ya maneno Pendo alikuwa mtoto wa pekee kulingana na habari?
    1. Pendo alikuwa na tabia tofauti na wenzake
    2. Pendo alizaliwa wa kwanza katika jamaa yake
    3. Pendo hakuwa na dada wala kaka
    4. Pendo alikuwa wa mwisho kuzaliwa kwao
  2. Mawaidha ambayo pendo alipewa na baba yake
    A hakuyasikiliza wala hakuyafuata
    B. aliyatilia maanani
    C. hakuyasikiliza bali aliyafuata
    D. aliyazingatia yote 
  3. Ala ya mzee Maarifa ilishi katika
    1. jamii iliyotangamana wakati wa furaha
    2. jamii iliyoishi kwa utengano
    3. jamii iliyoshirikiana wakati na dhiki pekee
    4. jamii iliyoshirikiana wakati wa heri na shari
  4. Tendo la Pendo kujihisi ameerevuka kiasi cha kuwajaribu wakuu wake linaonyesha
    1. ni kawaida watoto kufanya hivyo
    2. alikuwa mkaidi
    3. alikuwa mwerevu kuliko watoto wa rika lake
    4. alikuwa ameerevuka kuliko wavyele wake
  5. Baadhi ya mafunzo aliyopewa Pendo ni yapi?
    1. Akiwa malishoni apige mayowe akiwaona mbwa mwitu
    2. Akipiga mayowe wakati wowote akiwalisha kondoo
    3. Asithubutu kwenda malishoni peke yake
    4. Mbwamwitu wakitokea apambane nao
  6. Ni nini maana ya maneno wanaume wa miraba minne kulingana na habari?
    1. Wanaume jasiri na dhaifu
    2. Wanaume dhaifu na shujaa
    3. Wanaume wanene na wenye nguvu
    4. Wanaume wenye nguvu na woga
  7. Unadhani ni kwa nini wazazi walimkemea Pendo baada ya kupashwa habari?
    1. Alikuwa amefanya jambo la aula
    2. Alikuwa ameonyesha ushujaa 
    3. Kondoo wote waliliwa na mbwamwitu 
    4. Alikuwa ameonyesha utovu wa nidhamu
  8. Ni jambo lipi linaloonyesha kuwa wanakijiji walikuwa wamechoshwa na tabia za Pendo? 
    1. Kutoenda kumsaidia safari ya mwisho
    2. Kutomjulisha baba yake kuhusu tabia zake 
    3. Kumsaidia alipopiga ukemi mara ya pili
    4. Kutomfahamisha baba yake kuhusu kuvamiwa na mbwamwitu
  9. Mwana muwi haongeleki mara moja ina maana kuwa
    1. Mtoto mzuri hawezi kuharibika kwa kosa moja
    2. Mtoto mbaya haachi tabia zake mbovu
    3. Kumbebeleza mtoto si vyema.
    4. Mtoto mwenye nidhamu hafai kukanywa
  10. Kichwa mwafaka cha habari hii ni kipi?
    1. Maarifa na Pendo
    2. Kikulacho ki nguoni mwako.
    3. Majuto ni mjukuu
    4. Dawa ya moto ni moto

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 41 mpaka 50.

Kilimo ndicho uti wa mgongo nchini Kenya. Ukulima huchangia pakubwa katika jumla ya pato la taifa. Asilimia sabini na tano ya Wakenya walio katika umri wa kufanya kazi ni wakulima ingawa nusu ya mzao haya hutumika kwa kukidhi mahitaji ya kimsingi.

Nchi ya Kenya ikiwa na chini ya asilimia ishirini ya ardhi inayofaa kwa ukulima ndiyo inayoongoza katika ukuzaji wa kitunguu na maembe kwa mataifa ya nje. Kwa ujumla, sekta ya kilimo inachangia takriban asilimia sitini na tano ya bidhaa za nchi zinazouzwa katika mataifa ya nje.

Hata hivyo ukulima wa nchi ya Kenya umekabiliwa na changamoto ainati. Ukosefu wa mvua hutatiza wakulima nchini. Hii ni kwa sababu kilimo nchini hutegemea mvua. Majira ya mvua yanaendelea kubadilika kwa kiasi cha kuyafanya yasitegemewe. Mvua inayonyesha haitoshi na mimea hukauka kabla ya kukomaa na kupata mazao. Iwapo wakulima wametayarisha mashamba na kupanda mbugu, huweza kupata hasara kubwa.

Wakulima wengi nchini hawatumii teknolojia ya kisasa ili kuboresha mapato yao. Hii ni kwa sababu utafiti hauhusishi wakulima ili kuboresha mapato yao. Wakulima wengi hivyo basi huendelea kutumia njia zilizopitwa na wakati katika uzalishaji wa mazao na hivyo kupata mapato yasiyoweza kukidhi haja ya mkulima na nchi kwa jumla.

Wadudu na magonjwa yanayoathiri mimea ni changamoto nyingine inyokabili wakulima. Wengi wao wamekosa elimu kuhusu jinsi ya kuzuia magonjwa na wadudu wanaoharibu mimea na mazao au mavuno yao. Wengi hawajui jinsi ya kuzuia wadudu wanaoyaharibu. Mahali wanamoweka mazao au mavuno yao hamfai na husababisha uharibifu unaoleta hasara kuu. Wataalamu wanaowatembelea wakulima ni wachache sana na hawafikii wakulima wengi. Jambo hili husababisha ukosefu wa ujuzi wa kutosha wa kuendeleza kilimo kwa njia za kisasa.

Wakulima wanaweza kuwa na ujuzi wa kuzuia magonjwa na wadudu wanaoharibu mimea na mazao au hata matumizi ya teknolojia ya kisasa lakini wakose fedha za kutekeleza mambo haya. Gharama ya mbegu, viuadudu na mbolea yaweza kuwa juu kwa mkulima wa kawaida.

Ukosefu wa miundomsingi mathalani barabara umesababisha usafirishaji wa mazao ya mkulima kuwa ghali. Hili hufanya mazao kuharibika mashambani na yakifika sokoni yanauzwa kwa bei duni kwa kuwa hali yake si nzuri. Hivyo basi wakulima wanaendelea kupata hasara zaidi. Serikali inafaa isaidie sekta ya kilimo kwa kuongeza wataalamu zaidi wanaotembea mashambani kuwaelekeza wakulima. Wakulima wapewe mikopo ya kukidhi mahitaji ya zaraa. Miundomsingi pia iboreshwe.

  1. Kilimo ndicho uti wa mgongo ina maana
    1. kimefanikiwa sana
    2. ni tegemeo kubwa
    3. wananchi wengi ni wakulima
    4. kina faida na hasara nchini
  2. Chagua jibu sahihi
    1. Asilimia sabini na tano ya Wakenya ni wakulima
    2. Takribani Wakenya wote hupenda kilimo
    3. Zaidi ya nusu ya mapato ya nchi ni ya wakulima
    4. Robo tatu ya wafanyakazi nchini ni ya wakulima
  3. Nchi ya Kenya inaongoza kwa
    1. asilimia kubwa ya ardhi ya kulima 
    2. uuzaji wa kahawa na chai kwa wenyeji 
    3. ukuzaji wa kahawa na majani chai 
    4. kilimo bora cha kitunguu na maembe
  4. Ni kweli kusema kwamba
    1. Kenya hutegemea tu mauzo ya bidhaa za kilimo
    2. Kenya hainunui bidhaa za kilimo maadamu ziko tele
    3. Bidhaa nyingi zinazouzwa nje ya nchi ni za kilimo
    4. Nchi yetu imeweza kujitosheleza kupitia kilimo
  5. Ipi si mojawapo ya changamoto zinazowakabili wakulima nchini?
    1. Mvua kunyesha kupita kiasi
    2. Ukosefu wa mvua ya kutosha
    3. Ukosefu wa soko la bidhaa
    4. Kupungua kwa thamani ya bidhaa
  6. Elimu humsaidia vipi mkulima
    1. kuimarisha mazao na kupunguza hasara
    2. kujifanyia utafiti na kupiga hesabu za pesa
    3. kutumia njia za kiasili na kuepuka hasara
    4. kufahamu manufaa ya kilimo na kuboresha miundomsingi
  7. Ni methali ipi inayolingana na ya sita?
    1. La kuvunda halina ubani
    2. Jitihada haiondoi kudura maelezo katika aya
    3. Kidole kimoja hakivunji chawa
    4. Dau la mnyonge haliendi joshi
  8. Miundomsingi inahitaji zaidi katika
    1. utoaji wa elimu
    2. uchukuzi wa bidhaa
    3. uimarishaji wa soko 
    4. uuzaji wa bidhaa
  9. Serikali inafaa kuwapa wakulima mkopo ya kukidhia mahitaji ya kilimo. Mkopo usiotozwa riba huitwaje?
    1. Arbuni
    2. Ridhaa 
    3. Karadha
    4. Fidia
  10. Kichwa kinachofaa zaidi kifungu hiki ni kipi?
    1. Umuhimu wa kilimo nchini
    2. Ukulima nchini na changamoto zake
    3. Namna ya kuinua uchumi nchini
    4. Faida za ukulima

INSHA

Umepewa dakika 40 kuandika Insha yako.

Endeleza insha hii

Ulikuwa ni usiku wa manane ambapo niliamshwa na mayowe.............................

MARKING SCHEME

  1. D
  2. A
  3. C
  4. B
  5. D
  6. A
  7. C
  8. B
  9. D
  10. A
  11. D
  12. B
  13. C
  14. A
  15. B
  16. D
  17. C
  18. A
  19. B
  20. C
  21. D
  22. B
  23. A
  24. C
  25. C
  26. D
  27. A
  28. B
  29. D
  30. C
  31. C
  32. A
  33. D
  34. B
  35. A
  36. C
  37. D
  38. A
  39. B
  40. C
  41. B
  42. D
  43. C
  44. C
  45. A
  46. A
  47. D
  48. B
  49. C
  50. B

MASWALI

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswall 1-5.

(Chura na Jongoo wamekutana karibu na mto)
Chura: Hujambo rafiki yangu Jongoo? Sijakuona tangu tulipouanza mwaka huu. Kwema?
Jongoo: Sijambo kaka. Hali yangu shwari tena kwema kweli kweli. Mwaka huu nimeamua kutulia. Sipendi kutembeatembea ili ngozi yangu isichomwe na jua.
Chura: Oh! Umenikumbusha. Nilitaka unipe siri ya kuwa na ngozi laini, nyororo na inayomeremeta kama kioo.
Jongoo: (Akicheka kwa dhihaka) Ni rahisi sana bwana. Nyanya yangu alinieleza siri hii. Kwanza chukua mafuta ya uto, yachemshe kabisa kisha uruke ndani na ukae humo kwa muda.
Chura:(Akionyesha umakinifu zaidi) Eh! Kisha baadaye nifanyeje?
Jongoo: Hamna jingine. Tayari utakuwa na ngozi kama yangu.
Chura: (Huku akirukaruka na kuondoka) Asante sana rafiki yangu. Hebu nikajaribu mtindo huu mpya.
Jongoo: (Akiangukia kwa kicheko) Haya bwana. Kila la heri.

  1. Ni kwa nini Chura alitaka kujua ikiwa kwa Jongoo kulikuwa kwema?
    1. Walipendana kama chanda na pete.
    2. Hawakuwa wameonana kwa muda mrefu.
    3. Alitaka aibiwe siri ya ngozi nyororo.
    4. Walikuwa wamekutana ghafla bin vuu.
  2. Je, Jongoo alitoa sababu gani iliyomfanya asipende kutembeatembea?
    1.  Hali ya anga haikuwa shwari.
    2. Aliogopa hali ilivyokuwa baridi.
    3. Mara nyingi alikuwa mchovu.
    4. Aliogopa kuchomwa na jua.
  3. Ni nini ambacho Chura alikuwa amesahau akakumbushwa?
    1. Siri ya ngozi laini, nyororo na inayomeremeta.
    2. Jinsi ya kuchemsha mafuta ya uto.
    3. Jinsi ya kuwa na ngozi iliyoparara.
    4. Namna ya kuwa na mtindo mpya wa kuvutia.
  4. Kulingana na Jongoo, ni nani aliyemfunza kuwa na ngozi nyororo?
    1. Wazazi wake
    2. Nyanya yake
    3. Rafiki zake
    4. Mama yake
  5. Unadhani Jongoo alikuwa rafiki wa aina gani?
    1. Wa dhati.
    2. Mwaminifu.
    3. Mnafiki.
    4. Wa chanda na pete. 

Soma kifungu kifuatacho kisha uilbu maswali 6 hadi 8.
Shule yetu inaitwa shule ya msingi ya Mambosasa. Ina madarasa makubwa. Kutokana na ukubwa wake na idadi ya wanafunzi, kila darasa lina walimu wawili waangalizi. Walimu wetu ni mahiri sana katika ufunzaji. Ninasema hivi kwa sababu Mambosasa imeongoza na kushika usukani kwa miaka mitatu sasa. Kuna mabustani ya maua shuleni humu. Katika mabustani haya mmepandwa maua kama vile mawaridi na milangilangi. Katika maktaba yetu kuna vitabu vingi. Wanafunzi wengi huvisoma vile vya hadithi. Ua umejengwa kuizunguka shule letu. Ua huu hutuhakikishia usalama wetu. Uta wenyewe unavutia kwani ulijengwa kwa mawe na ustadi wa hali ya juu.

  1. Kila darasa shuleni Mambosasa lina walimu wawili waangalizi kwa sababu
    1. madarasa ni mengi.
    2. wanafunzi ni wengi.
    3. shule yenyewe ni kubwa.
    4. matokeo yake huwa mazuri.
  2. Kinachoonyesha kuwa walimu wa Mambosasa ni mahiri ni
    1. ukubwa wa madarasa shuleni humo.
    2. kuwapo kwa walimu wawili katika kila darasa.
    3. bidii za wanafunzi.
    4. matokeo bora katika mitihani.
  3. Badala ya kutumia neno mahiri, mwandishi angetumia neno
    1. wazembe.
    2. stadi.
    3. wazuri.
    4. wavivu.
  4. Kulingana na taarifa hii, wanafunzi huenda maktabani
    1. ili wakasome.
    2. kutazama video.
    3. ili wakafanye mikutano.
    4. kutamba hadithi.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 10 hadi 12.
Ajira ya watoto ni kazi ambazo zinawatumikisha na kuwaathiri watoto kati ya miaka mitano hadi kumi na saba. Kwa namna fulani wao huathirika kiakili, kimwili, kimakazi na kimaadili. Pia ajira hizi ni kizuizi cha watoto hawa kupata elimu. Mateso yanayowapata watoto katika ulimwengu wa ajira ya watoto duniani ni mengi. Ajira hizi huweza kuwa za nyumbani kwa watu wengine, mashambani au viwandani. Kazi wanazozifanya watoto hawa ni pamoja na kulisha mifugo, kuchimba mawe, kufyatua matofali, kuchonga mawe, ujenzi wa barabara, kuvuta au kusukuma mikokoteni na za ndani ya nyumba. Zote hizi ni kinyume na haki za binadamu kwa jumla.

  1. Tumearifiwa kuwa ajira za watoto huweza kuwaathiri watoto
    1. kimaadili, kimakazi na kidini.
    2. kiakili, kimavazi na kidini.
    3. kimakazi, kiakili na kimaadili.
    4. kiakili, kimwili na kiukoo.
  2. Kulingana na kifungu, ajira za watoto haziwezi kuwa
    1. nyumbani kwa wengine.
    2. katika viwanda.
    3. mashambani.
    4. shuleni.
  3. Haki za binadamu hazimkubali mtoto
    1. kuosha vyombo nyumbani kwao.
    2. kuvuta mikokoteni kwa malipo.
    3. kulifagia darasa lao.
    4. kufua sare zake. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswall
Malaria ni ugonjwa hatari unaosambazwa na aina fulani ya mbu. Si mbu wote husambaza malaria. Aliyewahi kuugua malaria hawezi kuyasahau makali yake. Masaibu yake huanza kwa baridi kali. Mhasiriwa hutetemeka sana. Baadaye joto la mwili hupanda na kufuatiwa na homa kali. Baada ya muda, mhasiriwa hutokwa na jasho.
Malaria ikitibiwa kwa dawa za kisasa, mhasiriwa hupata nafuu na hatimaye kupona. Isipotibiwa kwa wakati, husambaa mwilini na huweza hata kusababisha kifo kwa muda wa siku chache. Kwa miaka mingi, malaria imekuwa tishio katika maeneo mengi. Imewahi kuwaua wengi kwa kipindi kifupi huko India, Ugiriki, Roma na katika mataifa ya Afrika Magharibi. Takribani miaka mia tatu iliyopita, dawa ya malaria iitwayo kwinini ilivumbuliwa.

  1. Kulingana na habari, si kweli kusema kuwa
    1. si mbu husambaza malaria
    2. mtu aliyewahi kuugua malaria hasahau makali yake upesi.
    3. dawa za kisasa haziwezi kutibu malaria.
    4. kwinini ni dawa ya malaria.
  2. Ni gani hapa si dalili ya malaria kulingana na kifungu?
    1. Kutapika
    2. Joto jingi
    3. Kutetemeka
    4. Homa kali
  3. Taarifa inasema kwamba mataifa yaliyorekodi vifo vya wengi kwa muda mfupi kutokana na malaria si pamoja na
    1. Roma
    2. Ugiriki
    3. India
    4. Ajentina 

Soma kifungu kifuatacho. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa.

Wiki iliyopita, shule yetu iliandaa sherehe kubwa sana. Sherehe hiyo ilikuwa ya kuwazawidi wanafunzi _16_ waliofanya vizuri_17_ mashindano ya uandishi wa insha. Mashindano hayo yaliyoandaliwa na gazeti _18_Jichopevu yalijumuisha shule mia moja. Shule yetu ikawa ya __19__na kuzishinda nyingine tisini na___20___

  1.                    
    1. watukutu
    2. wazembe
    3. hodari
    4. wakali
  2.                  
    1. kwa
    2. katikati
    3. katika
    4. kua
  3.                          
    1. wa
    2. la
    3. ya
    4. za
  4.                
    1. kwanza
    2. kuanza
    3. mbili
    4. moja
  5.                      
    1. sita
    2. saba
    3. nane
    4. tisa

Kutoka swali la 21-30, jibu swali kulingana na maasizo uliyopewa.

  1. Teua sentensi iliyo katika kauli ya kutendwa.
    1. Machoine na dada yake waliandikiana barua.
    2. Mwalimu amesaidiwa kubeba vitabu.
    3. Yeye hupenda kulia bila sababu.
    4. Uzi wa Mwanaidi ndio uliokatika. 
  2. Ni majina yapi yaliyo katika ngeli moja?
    1. Uyoga, ua, upishi.
    2. Kijiko, kiongozi, kiwavi.
    3. Chepeo, kiazi, vitu.
    4. Marashi, magonjwa, makosa.
  3. Kisawe cha neno kinyonga ni
    1. kenge.
    2. nyoka.
    3. mjusi.
    4. lumbwi.
  4. Meza ya seremala imevunjika katika wingi ni
    1. Meza za maseremala zimevunjika.
    2. Meza za seremala zimevunjika.
    3. Mameza za maseremala zimevunjika.
    4. Meza za waseremala zimevunjika.
  5. Katika maneno uliyopewa, ni lipi litakuwa la mwisho katika kamusi?
    1. Mshikaki
    2. Mswaki
    3. Msaada
    4. Msaragambo
      1. i
      2. iii
      3. iv
      4. ii
  6. Kanusha sentensi ifuatayo:
    Juma anaimba polepole
    Juma ..................
    1. haimbi polepole.
    2. hataimba polepole.
    3. hakuimba polepole.
    4. hajaimba polepole.
  7. Chagua sentensi iliyo katika nafsi ya tatu.
    1. Mlitutembelea jana kwa sherehe.
    2. Alinunuliwa mwanasesere maridadi.
    3. Nimeamua kufanya bidii masomoni.
    4. Mwalimu aliyekuwa darasani ametoka.
  8. Kidani ni pambo la
    1. kichwani.
    2. miguuni.
    3. kifuani.
    4. mikononi.
  9. Lo! Nyoka mrefu ameingia ndani ya shimo polepole. Kivumishi ni kipi hapa?
    1. Lo!
    2. Mrefu
    3. Ndani ya
    4. Polepole
  10. Chagua ukubwa wa neno mji.
    1. Miji
    2. Majiji
    3. Kijiji
    4. Jiji

MAJIBU

swa

 

Tagged under

MASWALI

KISWAHILI: INSHA
Umepewa dakika 40 kuandika insha yako
Andika insha ya kusisimua kuhusu mada ifuatayo:

DAKTARI NIMPENDAYE

KISWAHILI: LUGHA
SEHEMU YA KWANZA
Kusikiliza na kuzungumza   (Alama 5)
Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali.
Baraka: Masalkheri Furaha?
Furaha: Akheri Baraka. umeshindaje sahibu?
Baraka: Vyema. (akimtazama kwa makini.) Umetoka wapi?
Furaha: Nimetoka zahanatini.
Baraka: Kwani unaugua?
Furaha: Ndiyo. Juzi nilikaa nje jioni na wenzangu bila sweta na baridi ilikuwa kali. Nilianza kukohoa na nilipozidiwa nikaamua kwenda kutafuta matibabu.
Baraka: Natumai umefanyiwa uchunguzi mzuri ili kujua hasa unakoumia.
Furaha: Ndiyo, nilifanyiwa vipimo na ikabainika kuwa nina kichomi.
Baraka: Kichomi ni nini?
Furaha: Ugonjwa huu pia unaitwa mkamba au nimonia. Unaathiri mapafu na kumfanya mtu awe na shida ya kupumua.
Baraka: Sasa nimeelewa. Je, umepewa dawa?
Furaha: (Akitikisa kichwa) Naam. Ndizo hizi hapa mkobani. Aidha nimepewa maagizo na nitahakikisha nimeyafuata vizuri.
Baraka: Pia uhakikishe umejikinga na baridi.
Furaha: Sasa ninajua kuwa nisipowajibika kujikinga ninaweza kuwa mgonjwa.
Baraka: Ninakutakia afueni ya haraka.
Furaha: Asante sahibu. Ningetaka sasa niende nyumbani ili niweze kunywa dawa na kupumzika. Kwaheri!
Baraka: Kwaheri ya kuonana. (Wote wanaondoka.)

  1. Baraka na Furaha walikutana wakati gani?
    1. Asubuhi
    2. Machweo
    3. Adhuhuri
    4. Usiku wa manane
  2. Ni neno lipi la adabu alilotumia Furaha katika mazungumzo haya?
    1. Nimetoka
    2. Hakika
    3. Asante
    4. Naam
  3. Ni kauli gani si kweli kulingana na mazungumzo haya?
    1. Furaha alikuwa na ugonjwa ulioathiri viungo vya ndani ya mwili
    2. Furaha aliugua kwa sababu ya baridi kali.
    3. Furaha alitibiwa katika hospitali ndogo.
    4. Furaha alitibiwa katika hospitali kuu
  4. Je, ungeyasikiliza mazungumzo ya Baraka na Furaha, ungejifunza nini?
    1. Ni sharti tuwajibikie afya zetu.
    2. Mtu akiugua si lazima atafute matibabu.
    3. Tukijikinga tutapata magonjwa.
    4. Dawa si muhimu katika mili yetu.
  5. Neno lingine ambalo lina maana sawa na daktari ni:
    1. Tabibu
    2. Rafiki
    3. Ndugu
    4. Jirani

Swali la 6 hadi la 8
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.
KIJIJI CHA FANAKA
Timu ya kandanda ya Nyota inapatikana katika kaunti ya Nawiri. Nyota ina wachezaji hodari. Nahodha wa timu hiyo anaitwa Sakata. Timu hii huwavutia na
kuwashangaza wengi. Wachezaji wa Nyota ni wenye bidii ya mchwa. Aidha husaidiana katika shughuli zao zote. Huwa wanaamka alfajiri na mapema kufanya mazoezi. Huwa wanakimbia na kupiga kwata uwanjani. Baadaye hucheza mechi ya mazoezi. Wanaamini kuwa mtaka cha mvunguni sharti ainame.
Wakati wa mashindano huwa wanashirikiana ili kupata ushindi. Timu hi haijawahi kushindwa. Hata wakicheza na timu kali namna gani huwa hawashindwi. Ukiwauliza vipi huwa wanapata ushindi, wao hukuambia kuwa jitihada hufaidi. Wachezaji wa nyota hupata mapato makubwa kutokana na mchezo wa kandanda. Wanaweza kujipatia mahitaji yao pamoja na familia zao.

  1. Ni jibu lipi sahihi kulingana na aya ya kwanza?
    1. Timu ya nyota hucheza mchezo wa chesi.
    2. Timu ya nyota haina kiongozi.
    3. Wachezaji wa Nyota ni wazembe.
    4. Timu ya Nyota hucheza mpira wa miguu.
  2. Kifungu kinaonyesha kwamba wachezaji wa Nyota wana bidii kwani:
    1. Huamka mapema kufanya mazoezi na kucheza mechi
    2. Huwa wanashirikiana.
    3. Huamka alfajiri na mapema.
    4. Huwa wanakimbia na kupiga kwata.
  3. Kifungu hiki kimetumia Methali ngapi?
    1. Moja
    2. Tatu
    3. Mbili
    4. Nne

Swali la 9 hadi la 12
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.
MALEZI YA MTOTO
Baada ya mtoto kuzaliwa, Mungu humpatia walimu wengi. Mwalimu wa kwanza wa mtoto ni mama. Yeye ndiye anayeanza kuujaza ukurasa mtupu wa ubongo wa mwanawe. Baba pia ana jukumu kubwa katika kumfunza na kumlea mtoto. Sitakosea nikisema kuwa yeye ndiye mwalimu wa pili.
Kazi yake pia ni nyingi. Ni wajibu wake ahakikishe kuwa ameshirikiana na mama malezini kwani mkono mmoja haulei mwana.
Mazingira ya mtoto yanapopanuka yeye huanza kuwa na walimu wengi. Walimu hawa hupatikana shuleni, kanisani, msikitini, nyumbani na mahali kwingine ambako watoto hukutana na watu. Aidha vyombo vya habari na mawasiliano kama vile: Runinga, redio, simu na vinginevyo pia humfundisha mtoto mambo mengi. Hivi vinafaa kutumiwa kwa tahadhari kubwa.
Ikumbukwe kuwa ikiwa mazingira anapokulia mtoto yatamfunza maadili yeye atakuwa na tabia njema. Tuwape watoto mazingira bora ya kujifunza maadili nasi tutafurahia kuwa katika ulimwengu wenye watu waadilifu.

  1. Kwa mujibu wa aya ya kwanza mwalimu wa pili wa mtoto ni nani?
    1. Baba
    2. Mama
    3. Kasisi
    4. Imamu
  2. Ili mtoto apate malezi mema ni lazima baba na mama wawe na:
    1. Utengano
    2. Uzembe
    3. Ushirikiano
    4. Walimu wengi
  3. Kulingana na kifungu, walimu wa mtoto hupatikana katika sehemu hizi zote isipokuwa:
    1. Shuleni
    2. Porini
    3. Kanisani
    4. Msikitini
  4. Watoto wakifunzwa maadili:
    1. ulimwengu utakosa watu wenye tabia mbaya.
    2. tutafurahia kukosa maadili.
    3. tabia njema hazitapatikana.
    4. nidhamu itakosa.

Swali la 13 hadi la 15
Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.
Amina, Maria, Zuhura, Musa na Malaika walimtembelea nyanya yao kijijini. Nyanya hutengeneza mikeka, vikapu na fagio. Yeye hutumia vifaa hivi nyumbani na vingine huvipeleka sokoni kuviuza.
Vijana hawa walimsaidia nyanya yao katika shughuli hiyo. Amina, Maria na Malaika walifuma mikeka. Maria, Musa na Malaika walitengeneza fagio. Wote, isipokuwa Amina na Malaika walifuma vikapu. Wavulana wote walileta vifaa vya kufanyia kazi. Baada ya kumaliza kazi, vijana wote isipokuwa Zuhura walifagia eneo walilofanyia kazi. Vijana wote isipokuwa Maria walimsaidia nyanya kupeleka bidhaa walizotengeneza sokoni.

  1. Nikijana yupi alitengeneza vifaa vitatu?
    1. Zuhura
    2. Musa
    3. Maria
    4. Amina
  2. Ni nani hakumsaidia nyanya kupeleka bidhaa sokoni?
    1. Malaika
    2. Maria
    3. Musa
    4. Amina
  3. Kulingana na kifungu:
    1. Musa, Maria na Zuhura walifuma vikapu.
    2. Malaika, Musa na Amina walifuma mikeka.
    3. Zuhura, Maria na Malaika walifuma mikeka.
    4. Amina, Mariana Musa walifuma vikapu.

Swali la 16 hadi la 20
Soma kifungu kifuatacho. Kwa kila swali umepewa majibu manne. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa.
Johari alisomea shule______16_______Katika ofisi _____17______mwalimu mkuu kulikuwa na _______18______ dirishani. Pia kuna viti vya kukalia. Viti hivi huifanya ofisi _______19______. Kila siku sakafu ya ofisi hiyo_____20_______ili kuondoa vumbi.

  1.                    
    1. nzuri
    2. kuzuri
    3. vizuri
    4. mzuri
  2.                    
    1. kwa
    2. mwa
    3. ya
    4. la
  3.                            
    1. fremu
    2. pazia
    3. kizingiti
    4. Zulia
  4.                  
    1. kupendea
    2. kupendeza
    3. kupendezwa
    4. kupendezana
  5.                    
    1. hupigwa mswaki
    2. hupunga hewa
    3. hupigwa maji
    4. hupigwa deki 

Swali la 21 hadi la 30
Chagua jibu sahihi.

  1. Ni kiungo gani cha mwili hakijaambatanishwa vizuri na kazi yake?
    21 aihdada
  2. Hili ni jedwali la maneno. Chagua jibu linaloonyesha vivumishi vimilikishi pekee?
    22 auygduada
  3. Kati ya maneno haya ni gani litakuja mwisho yakipangwa kialfabeti?
    1. Kabumbu
    2. Gori
    3. Hoki
    4. Jugwe
  4. Kati ya sentensi hizi ni gani imetumia kivumishi kirejeshi 'amba-'kwa usahihi?
    1. Mlango ambayo umefungwa ni huu.
    2. Mgeni ambaye amekuja ni wangu.
    3. Kiatu ambayo kinapendeza ni changu. 
    4. Mti ambaye umekatwa ni mrefu.
  5. Ni sentensi gani iliyoakifishwa vizuri?
    1. Lo! Nyumba imechomeka.
    2. Ngo'mbe ni mnyama mzuri.
    3. Nilinunua kalamu: Winona daftari.
    4. Je, kandanda ni sawa na soka.
  6. Ni sentensi gani yenye kiwakilishi? 
    1. Mpira huu unapendeza.
    2. Watoto wanacheza kibemasa vizuri.
    3. Mimi nitaogelea kesho.
    4. Mabao matano yalifungwa katika mechi hiyo.
  7. Chagua jibu linalounganisha sentensi hizi kwa usahihi.
    1. Imani alimwokea Amara keki.
    2. Amara alimwokea Imani Keki.
      1. Amara aliokewa keki kwa Imani.
      2. Imani aliokea keki kwa Amara.
      3. Amara na Imani waliokewa keki.
      4. Imani na Amara waliokeana Keki.
  8. Chagua sentensi ambayo ni ukanusho wa: Mtoto analilia uji.
    1. Mtoto hatalilia uji.
    2. Mtoto hakulilia uji.
    3. Mtoto halilii uji.
    4. Mtoto hajalilia uji.
  9. Ni sentensi ipi iliyo katika hali ya ukubwa?
    1. Kijia hiki ni kikubwa.
    2. Dege hili limepaa angani.
    3. Kigamia kina njaa kwa sababu ya ukame.
    4. Nyumba yetu ina sebule kubwa.
  10. Chagua jibu lenye nahau iliyoambatanishwa sawasawa na maana yake.
    Piga deki  Pangusa na kusafisha sakafu 
    B Piga mswaki Toka nje ili kujipumzisha
    C Tia mbia Safisha meno kwa mswaki
    D Punga hewa Toa miche ilipomea na kuipanda kwingineko

MAJIBU

kiswahili

 

Tagged under

 Soma kifungu kifuatacho na ujaze nafasi zilizoachwa.

Mama Rehema alienda sokoni kununua nyama na kusaga mahindi,         1         kwenye         2           aliuweka mkoba wake chini. Alijiunga na wanunuzi wengine, ili apimiwe nyama kwa         3          .Alilipa          4        kidogo na akaelekea kusaga mahindi

1. A.Walipofika    B. Watapofika    C. Alifika     D. Zilifika  
 2. A. buchari    B. hospitali    C. jikoni    D. shambani  
 3. A. kipimio   B. ratili     C.meza     D. kinu  
 4. A. vikombe    B. sarufi   C. pesa    D. mapeni  

Jaza kwa kutumia kihusishi sahihi.

  1. Paka yuko               mti
    GD4ST4KISW5
    1.  ndani ya 
    2. juu ya
    3.  kando ya
    4. chini ya . 
  2. GD4ST4KISW6
     kikombe kiko                 meza
    1. juu ya
    2. chini ya 
    3. mbele ya 
    4. ndani ya
  3. GD4ST4KISW7
    maji yamo                   bilauri
    1. mbele ya
    2. ndani ya 
    3. kati ya 
    4. juu ya 
  4. Rangi za bendera ni nyekundu, nyeusi, kijani kibichi na                  
    1. nyeupe 
    2. samawati 
    3. zambarau
    4. hudhurungi 

Chaqua jawabu sahihi kujaza nafasi

  1. Kiatu                    ni kizuri.
    1. hiki
    2. hili
    3. hizi
    4. huyu
  2. Nyumba                   inapendeza
    1. wao
    2.  lao
    3. yao
    4. hao
  3. Wazazi                   wameingia sasa.
    1. yenu
    2. zenu
    3.  lenu
    4. wenu
  4. Nguo                      zilifuliwa na mama.
    1. yao
    2. zao
    3. wao
    4. lao
  5. Matunda                   yameiva yote.
    1. hawa
    2.  huu
    3. hili
    4. haya
  6. Ni ndege yupi hapatikani mwituni?
    1. Kasuku
    2. Kuku
    3. Chiriku
    4. Mbayuwayu
  7. Kifaa hiki huitwa:-
    GD4ST4KISW15
    1. shoka
    2. plau
    3. bendera 
    4. jembe
  8. Kifaa ambacho hutumika kufyeka nyasi huitwa:-
    1. reki
    2. jembe
    3. kifyekeo
    4. plau

Andika kinyume cha neno lililopigwa mstari

  1. Wasichana walipanga viti vizuri.
    1.  watapanga
    2. walipangua
    3. walipenda
    4. watapangua
  2. Mtoto atalia baada ya kuachwa.
    1. atalala
    2. atacheza
    3. atasheka
    4. atacheka
  3. Mama ataingia.
    1. ataenda
    2. atatoka
    3.  atakimbia
    4. atakaa
  4. Yaya hutandika kitanda chake.
    1. hutanfua 
    2. hutenda
    3. hupanga
    4. hulala
  5. Kaka alianika nguo zake.
    1.  hutandua
    2. alianua
    3. alichukua
    4. alichezea

Andika jibu sahihi

  1.  Pahali ambapo pesa huhifadhiwa ni:-
    1. benki
    2. soko 
    3. kanisani
    4. dukani

Kanusha vitenzi vifuatavyo

  1. Alicheza
    1. atacheza
    2. hatacheza
    3. hakucheza
    4. halichezi
  2.  hutibu
    1. anatibu
    2.  hakutibu
    3. hatibi
    4. hatibu
  3. Alisoma
    1.  hakusoma
    2. anasoma
    3. atasoma
    4. anasoma
  4. Atakaa
    1.  halikaa
    2. hatakaa
    3. hakai
    4. hakukaa

Andika vifungu hivi kwa wingi.

  1.  Ua hili
    1. nyua hii
    2. maua hii
    3. maua haya
    4. ua haya
  2. Kiberiti hiki
    1. viberiti hivi
    2. viberiti hii
    3. kiberiti hivi
    4. viberiti hawa
  3. Nyumba hii
    1. nyumba hii
    2. nyumba hiyo
    3. nyumba hizi
    4. nyumba hiyo
  4. Kiota hiki
    1. viota hawa
    2. viota hivo
    3. viota hivi 
    4. viota hili

Soma hadithi kisha ujibu maswali yafuatayo.

Teknolojia ya kisasa imetuwezesha kuweka pesa kwenye simu. Huna haja ya kubeba pesa mfukoni unapoenda dukani. Unaweza kulipia bidhaa dukani kwa njia ya simu. Unaweza kufanya hivyo wakati wowote na mahali popote. Wanaotumia teknolojia hii hufanya mambo mengi zaidi kuliko walio na pesa taslimu. Kuna baadhi ya huduma zinazoweza kununuliwa kwa kutumia pesa kwenye simu.

  1. Je, teknolojia ya kisasa imetuwezesha kufanya nini kulingana na hadithi?
    1.  Kuweka pesa kwenye simu 
    2. Kuchora kwa simu
    3. Kupiga picha 
    4. Kufanya hesabu
  2. Ni njia gani inaweza tumika kulipia pesa?
    1. ya benki 
    2. ya kukopa 
    3. njia ya sim
    4. kubadilishana bidhaa
  3. Kuna faida gani kulipa pesa kwa kutumia simu?
    1. Mtu hafanyi jambo lolote 
    2. Mtu hufanya mambo mengi 
    3. Mtu hufanya mambo kidogo
    4. Mtu hasaidiki

Soma hadithi kisha ujibu maswali yafuatayo.

Nyanyiro alikuwa mvuvi aliyeishi karibu na soko la sokomoko. Alifanya kazi yake ya uvuvi kwa bidii. Asubuhi na mapema aliamka na kwenda mtoni. Pale mtoni palikuwa na aina mbalimbali ya samaki kama vile ngege na mkunga. Nyanyiro alivua samaki kila siku na mara nyingine alipenda kunadi samaki wake kwa kupaza sauti.

  1. Je, nyanyiro alikuwa anafanya kazi gani?
    1. Mpishi
    2. Mvuvi 
    3.  Msusi
    4. Mlevi
  2. Je, Nyanyiro alienda mtoni saa ngapi?
    1. Asubuhi na mapema
    2. Jioni
    3. Usiku
    4. Alasiri
  3. Samaki wale walipatikana mtoni ni kama:
    1. mbayuwayu
    2. njiwa
    3. mkunga
    4. kasuku
  4. Nyanyiro aliwauza samaki wake kwa:-
    1. kupeana
    2. kunadi
    3. kukopesha
    4. kimoyomoyo
  5. Kazi ya Nyanyiro ilikuwa ya:- 
    1. uvuvi 
    2. uvivu
    3. ualimu
    4. ukulima
  6. Ni mnyama yupi hapatikani nyumbani?
    1. Kondoo
    2. Ndovu
    3. Kima
    4.  Paka
  7. Samaki huishi:-
    1. ardhini
    2. mtini
    3. mwituni
    4. majini

KUSIKILIZA NA KUZUNGUMZA

Mwalimu amwamkue mwanafunzi, Habari yako?

(Mwanafunzi ajibu)

Mwalimu amtayarishe mwanafunzi kujibu maswali kuhusu vitendawili.

(Mwanafunzi azitegue)

  1. Huku ng'o kule ng'o
  2. Askari mlangoni
  3. Kisima changu hakitindiki maji
  4. Kamba yangu ndefu lakini haifungi kuni
  5. huku mwamba kule mwamba
  6. Nyumba yangu ina mlango mdogo
  7. Juu ya mlima kuna msitu mweusi

KUSOMA

Soma kifungu kifuatacho kwa sauti huku ukizingatia matamshi bora

Soko la mwembeni lililoko kwenye Kaunti ya Kwale lina bidhaa nyingi. Kuna sehemu zilizotengwa kulingana na bidhaa zinazouzwa. Kuna vibanda vya kuuzia matunda, nyama, nguo na mboga. Wafanyabiashara hupanga na kulinda bidhaa hizo kwa uangalifu mkubwa utafikiri ni kuku anayelinda kifaranga wake ndani ya kizimba. Wafanyabiashara hukata leseni na kupewa risiti. Bila leseni, huwezi kunadi au kuuza bidhaa zozote. Watu wa kila rika huja sokoni kwa sababu mbalimbali. Wengine huja kuuza na kununua bidhaa. Wengine huja kutazama bei za bidhaa. Wengine huja kwa matembezi na kujistarehesha tu. Wengine hawana sababu.

ANDIKA INSHA YA KUSISIMUA KUHUSU

RAFIKI NIMPENDAYE

MWONGOZO 

  1. C
  2. A
  3. B
  4. B
  5. C
  6. A
  7. B
  8. A
  9. A
  10. C
  11. D
  12. B
  13. D
  14. B
  15. A
  16. C
  17. B
  18. D
  19. B
  20. A
  21. B
  22. A
  23. C
  24. B
  25. A
  26. D
  27. C
  28. A
  29. C
  30. C
  31. A
  32. C
  33. B
  34. B
  35. A
  36. C
  37. B
  38. A
  39. B
  40. D

Kusikiliza na kuzungumza

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali 1-5

G4swaT1T23002P1

Chichi:   (akibisha mlango) Hodi!
Jabari:   (kwa furaha) karibu! Ni nani tafadhali?
Chichi:   Rafiki yako Chichi.
Jabari:   Karibu sana sahibu. Nimekungojea sana ufike ili tushinde pamoja leo.
Chichi:   Asante kwa makaribisho. Sebule yenu inafurahisha sana.
Jabari:   Namshukuru Mungu kwa kuwasaidia wazazi wangu kununua meza ya kisasa, makochi, televisheni, mazulia na mapazia mazuri.
Chichi:   (Akiangalia juu) Balbu zenu za stima zinapendeza sana.
Jabari:   (akiwasha umeme) Tazama, zina rangi tofautitofauti.
Chichi:   (akiikagua meza) Matendegu haya ya meza yametengenezwa kwa ufundi sana.
Jabari:   Seremala aliyeyatengeneza ni hodari. Pia alitengeneza fremu ya mlango wetu. Angalia vile inavutia.
Chichi:   Kusema kweli nyumba yenu inapendeza. Kabla sijarudi kwetu leo nitakusaidia kuipiga deki.
Jabari:    Asante Chichi. Usafi ni kitu muhimu.
(wote wanaketi na kupanga shughuli za siku hiyo)

  1. Ni jambo gani la heshima ambalo Chichi alifanya alipofika kwa rafiki yake?
    1. Kubisha hodi
    2. Kufurahi
    3. Kukaribishwa
    4. Kungojewa
  2. Kulingana na mazungumzo haya neno rafiki ni sawa na:
    1. Chichi
    2. Jabari
    3. Sahibu
    4. Karibu
  3. Sebule ya akina Jabari ina vitu hivi vyote isipokuwa?
    1. Makochi
    2. Balbu
    3. Meza
    4. Picha
  4. Gani kati ya vitu hivi huwa na matendeguu?
    1. Zulia
    2. Pazia
    3. Meza
    4. Balbu
  5. Ni shughuli gani ambayo Jabari na Chichi watafanya ili kutunza usafi?
    1. Kupiga deki
    2. Kuketi
    3. Kupanga shughuli za siku
    4. Kula pamoja

Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali 6-9    

G4swaT1T23002P2

Chui na punda walikuwa marafiki wa chanda na pete. Walikuwa wakiishi msituni. Wakati mwingine walikuwa wakitofautiana kuhusu mambo fulani.

Siku moja Punda alimwambia Chui kuwa nyasi ni za rangi ya samawati. Chui alimpinga na kusema kuwa nyasi ni za rangi ya kijani. Walizozana sana kuhusu rangi ya nyasi mpaka
wakakosana.

Ili kupata suluhisho walienda kwa Simba ambaye alikuwa mfalme wa wanyama. Punda alikimbia mbele ya Chui na kumwambia Simba, "Nyasi ni za rangi ya kijani, kweli ama si kweli?" Simba akasema ni kweli. Chui naye akaja na kusema, "Nyasi ni za rangi ya kijani." Simba akamuuliza, "Ni nani hajui hivyo?"

Chui aliposikia hivyo alifurahi sana na kumwomba Simba amwadhibu Punda. Simba alimwadhibu Chui licha ya kuwa alisema ukweli. Aliadhibiwa kwa sababu ya kuzozana na punda ambaye alichukuliwa kuwa mnyama mjinga kuliko Chui.

  1. Punda na Chui walitofautiana kuhusu nini?
    1. Mfalme na wanyama
    2. Rangi ya nyasi
    3. Msituni
    4. Chakula
  2. Kulingana na kifungu mfalme wa wanyama alikuwa nani?
    1. Simba
    2. Chui
    3. Punda
    4. Nyasi
  3. Ni wanyama wangapi waliotajwa katika kifungu hiki?
    1. Mmoja
    2. Wawili
    3. Wanne
    4. Watatu
  4. Kulingana na kifungu hiki tunajifunza nini?
    1. Hatufai kuzozana na Punda kwani tunaweza kuadhibiwa na Simba.
    2. Mtu akiwa mwerevu kuliko mwingine anaweza kuadhibiwa.
    3. Simba, Chui na Punda ni wanyama wa msituni.
    4. Hatufai kuzozana na watu wasioelewa mambo kwani tunaweza kuingia hatarini.

Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali 10-12   

Siku moja Jawabu aliambiwa na wazazi wake aeleze kuhusu nidhamu ya mezani. Pia aliambiwa aeleze faida zake. Aliwaomba kwa heshima wamruhusu aandike kwenye karatasi.

 Tabia yenye nidhamu   Faida zake 
 Kumshukuru Mungu  Huonyesha heshima kwa Mungu  
 Kunawa mikono kabla ya kula   Kuepuka magonjwa
 Kula kwa utaratibu  Huwezi ukatapika
 Kula bila kuongea  Hutachafua chakula cha wengine 
 Kunawa mikono baada ya kula   Kutunza usafi wa mtu binafsi

Wazazi wake waliposoma walifurahi sana kwa sababu mtoto wao anaelewa nidhamu mezani na umuhimu wake.

  1. Jawabu aliambiwa na wazazi wake aeleze kuhusu nini?
    1. Nidhamu
    2. Nidhamu mezani
    3. Nidhamu ya mezani na faida zake.
    4. Mezani
  2. Mtu akikosa kunawa mikono kabla ya kula atapata hasara gani?
    1. Atatapika
    2. Atachafua nguo zake
    3. Hatashiba
    4. Anaweza kunata maad
  3. Ni tabia gani nyingine ambayo Jawabu angeongeza kwenye orodha yake?
    1. Kutazama runinga ukila chakula.
    2. Kutumia simu wakati wa kula.
    3. Kula ukiwa umeketi vizuri na kutulia.
    4. Kula ukisoma kitabu cha hadithi.

Soma kifungu kifuataccho kisha ujibu maswali 13 - 15.  

G4swaT1T23002P3

Wekeza ni mfanyabiashara hodari katika Jiji la Mtaji. Ana duka kubwa sana la mavazi. Watu wote; wazee kwa vijana, matajiri kwa maskini, wanawake kwa wanaume hununua mavazi katika duka hilo.

Mavazi hayo yamepangwa ya kiume kando na ya kike kando. Sehemu ya mavazi ya kiume ina suruali, kaptura, mashati, tai, suti, soksi, chupi na mavazi mengineyo. Upande wa mavazi ya kike kuna; marinda, blauzi, chupi, suti, sketi, sidiria, mitandio na mengineyo.

Duka hilo pia lina mavazi ya wakati wa baridi kama vile makoti na sweta. Aidha kuna mavazi ya wakati wa kazi kama vile ovaroli. Isitoshe kuna sehemu ya viatu, mishipi, kofia, soksi na sare za wanafunzi.

Wanunuzi wengi huenda katika duka hilo kwani bidhaa huuzwa kwa bei nafuu.

  1. Duka lililoelezewa liko katika jiji gani?
    1. Hodari
    2. Mfanyabiashara
    3. Wekeza
    4. Mtaji
  2. Kulingana na kifungu ni mavazi gani yameambatanishwa vizuri na wanaoyavaa? 
    1. Blauzi-wanaume
    2. Shati- wanawake
    3. Sare- wazee
    4. Ovaroli-wafanyakazi
  3. Kwa nini wanunuzi wengi huenda katika duka la Wekeza?
    1. Lina bidhaa nyingi.
    2. Bidhaa huuzwa kwa bei nafuu.
    3. Duka liko jijini.
    4. Duka hilo lina mavazi yote.

Soma kifungu kifuatacho. Kina nafasi 16 hadi 20. Umepewa majibu manne hapo. Chagua jibu lifaalo Zaidi kati ya yale uliyopewa.

Nyumba ___16___ ni ___17___. Jikoni kuna mawe ___18___ ya kupikia yanayoitwa ___19___. Sisi huitunza nyumba yetu ___20___.

   A   B   C   D 
 16.   wetu   yetu   chetu   letu 
 17.  nzuri  mzuri   zuri   mizuri 
 18.  watatu   mitatu   tatu  matatu 
 19.  mchi  mvungu   mafiga   makochi 
 20.  nzuri  vizuri   mzuri   wazuri 

 

Kutoka swali 21-30, chagua jibu sahihi. 

  1. Ni maamkuzi gani ambayo hayajajibiwa vizuri?
    1. U mzima?- ni mzima
    2. Alamsiki-binuru
    3. Makiwa- tunayo au yamepita
    4. U hali gani?- nawe pia
  2. Ni kundi gani la maneno yaliyoambatanishwa sawasawa na aina yake? 
    1. Zuri, -baya-,refu, -fupi- vivumishi
    2. Soma, andika, keti, simama- nomino
    3. Mvungu, tumbuu, kizingiti, globu- viwakilishi
    4. Mimi, wewe, yeye, wao- vitenzi
  3. Ni sentensi gani haina kielezi?
    1. Nilikula wali jana.
    2. Mwalimu mzuri anafundisha.
    3. Wanafunzi wanacheza uwanjani.
    4. Mtoto alikula polepole.
  4. Ni kifaa gani cha nyumbani kimeambatanishwa sawasawa na jina lake?
    G4swaT1T23002P4
  5. Ni kundi gani lina mpangilio mzuri wa maneno kama yanavyofuatana katika kamusi?
    1. Kinu, kisu,mwiko,mchi
    2. Zulia,tumbuu,pazia,fremu
    3. Kula,nawa,pakua,pika
    4. Salamu, salama, salimu,sala
  6. Badilisha sentensi hii katika umoja: vyakula vyao vimepikwa.
    1. Chakula chake kimepikwa.
    2. Vyakula vyake vimepikwa.
    3. Chakula chao kimepikwa.
    4. Chakula changu kimepikwa.
  7. Ni sentensi gani si kitanzandimi?
    1. Baba alivua papa.
    2. Mama alitoa doa.
    3. Kuku alikula gugu.
    4. Jana aliandika jina.
  8. Unapoandika insha unafaa kuzingatia haya yote isipokuwa
    1. Anwani
    2. Mpangilio mzuri wa mawazo
    3. Hati safi
    4. Michoro mizuri
  9. Ni sentensi gani yenye kiulizi?
    1. Wewe una nidhamu mezani? C
    2. Seremala alitengeneza mtoto wa meza.
    3. Wacha kula ovyoovyo!
    4. Alifagia, akapiga deki na kupanga nyumba.
  10. Tazama picha kisha ujibu swali
    G4swaT1T23002P5
    Chombo hiki kinaitwaje?
    1. Tarakilishi
    2. Televisheni
    3. Redio
    4. Simu

INSHA

Kuandika (Alama 10)

Umepewa dakika 40 kuandika insha yako. Andika insha juu ya:

                                                                       RAFIKI YANGU

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

MARKING SCHEME

  1. A
  2. C
  3. D
  4. C
  5. A
  6. B
  7. A
  8. D
  9. D
  10. C
  11. D
  12. C
  13. D
  14. D
  15. B
  16. B
  17. A
  18. D
  19. C
  20. B
  21. B
  22. A
  23. B
  24. C
  25. C
  26. C
  27. D
  28. D
  29. A
  30. A

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali 1-5

G4swaT1T23001P1

Amani: (Kwa furaha) Hujambo Johari!
Johari: (Akitabasamu) Sijambo Amani. Umeamkaje? Amani: Vyema labda wewe.
Johari: Ningetaka tujadiliane vile tutakavyoyatunza mazingira ya shule yetu muhula huu.
Amani: Aha! Naona unayajali mazingira yetu.
Johari: Naam! Baada ya likizo ndefu takataka zimeenea kila mahali, nyasi ni ndefu na madarasa yamejaa vumbi.
Amani: Ni jukumu letu kama wanafunzi kuhakikisha tumeifanya shule yetu kuwa safi.
Johari: Tunafaa kutafuta fyekeo, reki na fagio ili kutekeleza shughuli yetu.
Amani: Mwalimu wetu wa darasa atatusaidia kupata vifaa hivyo katika stoo ya shule.
Johari: Tunafaa tuongee na wanafunzi wenzetu ili tujipange  vizuri kutekeleza shughuli hii.
Amani: Tutajigawa katika vikundi mbalimbali ili kila mahali shuleni pawe safi.
Johari: Haya basi twende tukaongee na wenzetu.

  1. Mazungumzo uliyoyasoma yalifanyika wakati gani?
    1. Jioni
    2. Adhuhuri
    3. Asubuhi
    4. Usiku
  2. Amani na Johari wanazungumza kuhusu nini?
    1. Usafi wa mazingira ya shule
    2. Usafi wa nyumbani kwao
    3. Usafi wa darasa lao
    4. Usafi wa uwanja wa shule
  3. Wanafunzi watatumia kifaa gani kufyeka nyasi ndefu?
    1. Ufagio
    2. Reki
    3. Jembe
    4. Fyekeo
  4. Ili kila mwanafunzi apate kazi yake wanafaa kufanya nini? 
    1. Kujigawa katika makundi. 
    2. Kuzungumza
    3. Kumwomba mwalimu awapatie vifaa
    4. Kuosha darasa kwanza
  5. Ni gani kati ya hizi si shughuli ya kutunza usafi wa mazingira
    1. Kufagia
    2. Kufyeka
    3. Kuoga
    4. Kuokota takataka

Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali 6-9   

G4swaT1T23001P2

Bwana Bakari alikuwa mfugaji hodari wa kuku. Alikuwa na majogoo watano na kuku arubaini na watano wa kutaga mayai. Kuku hawa huitwa koo.

Koo walikuwa wameanza kutaga na kwa hivyo baada ya siku kadhaa wangeyalalia mayai na kuangua vifaranga.

Bwana Bakari aliwatunza kuku wake vizuri. Aliwapatia chakula na maji ya kutosha. Pia aliwachanja kila mara ili wasipate magonjwa.

Wanafunzi hupenda kumtembelea Bwana Bakari ili kujifunza ufugaji wa kuku.

  1. Bwana Bakari hufanya kazi gani?
    1. Kulima
    2. Kuuza mayai
    3. Kufuga kuku
    4. Kuangua vifaranga
  2. Kuku anayetaga mayai huitwaje?
    1. Koo
    2. Jogoo
    3. Kifaranga
    4. Pora
  3. Bwana Bakari hakuwatunza kuku wake kwa _________________________
    1. kuwapa chakula
    2. kuwapa maji
    3. kuwachanja
    4. kuwaosha
  4. Kwa nini Bwana Bakari aliwachanja kuku wake?
    1. Ili wasipate magonjwa
    2. Ili wapate vifaranga
    3. Ili watage mayai mengi
    4. Ili waongezeke

Soma hadithi ifuatayo kisha ujibu maswali 10-12

G4swaT1T23001P3
Mwema alitumwa dukani na mama yake kununua bidhaa. Alipewa noti ya shilingi mia mbili. Alimpata mwuzaji na kuagiza bidhaa zifuatazo:

  1. Sukari nusu kilo - shilingi sabini na tano.
  2. Mkate - shillingi sabini
  3. Maziwa pakiti moja - shilingi hamsini

Baada ya kupewa bidhaa hizo alipatiana pesa, akapewa risiti na baki ya pesa.

  1. Tunaweza tukamwita Mwema nani?
    1. Mnunuzi 
    2. Muuzaji
    3. Mchuuzi
    4. Dalali
  2. Ni bidhaa gani ghali kuliko zote?
    1. Mkate
    2. Sukari
    3. Maziwa
    4. Zote
  3. Mwema alipewa baki ya shillingi ngapi?
    1. Kumi
    2. Kumi na tano
    3. Tano
    4. Hatujaambiwa

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 13-15.

Mcheshi alisafiri na kwenda marekani. Aliishi katika nchi hiyo kwa miaka mitano. Hata hivyo hakuwahi kuisahau nchi yake ya Kenya. Kila wakati alipoikumbuka nchi yake alitamani siku ya kurudi ifike haraka.

Mcheshi alikuwa na sababu nyingi za kuipenda Kenya. Nchi ya Kenya ina wananchi wanaopenda amani. Kuna milima na mabonde ya kupendeza. Kuna mito, maziwa na bahari. Isitoshe Kenya ina wanyamapori wengi kama vile: Simba, ndovu, chui, kifaru na twiga.

Siku ya kurudi ilipofika, Mcheshi alipanga mizigo yake, akaenda katika uwanja wa ndege, akaiabiri na kurudi Kenya. Alipofika aliwapata baba na mama yake wamemsubiri. Walikumbatiana kwa furaha kisha wakaenda nyumbani.

  1. Mcheshi alisafiri kwenda nchi gani?
    1. Kenya
    2. Marekani
    3. Uingereza
    4. Ethiopia
  2. Kulingana na kifungu gani kati ya hizi si sababu ya Mcheshi kuipenda Kenya?
    1. Wananchi wenye amani
    2. Milima na mabonde
    3. Wanyamapori
    4. Kilimo
  3. Katika uwanja wa ndege, Mcheshi alikuwa amesubiriwa na _______________________
    1. wazalendo
    2. wazazi wake
    3. ndugu zake
    4. marafiki

Jaza pengo kwa kutumia majibu yafaayo

Bendera ___16___ Kenya ina rangi ___17___. Rangi iliyo juu kabisa ni ___18___ katikati ya bendera yetu kuna mikuki ___19___ na ngao. Shuleni huwa tunaipandisha bendera ili kuonyesha ___20___ wetu.

   A   B   C   D 
 16.   wa   ya   cha   la
 17.  nne   minne   wanne   minne 
 18.  nyeupe   nyeusi   nyekundu   kijani 
 19.  mbili  wawili   mbili   miwili 
 20.  uzalendo   urafiki   uadui   uhodari 
  1. Tazama picha hizi kisha ujibu swali
    G4swaT1T23001P4
    Vifaa hivi hutumika wapi?
    1. Shuleni
    2. Sokoni
    3. Shambani
    4. Dukani
  2. Musa amemsindikiza rafiki yake hadi kituo cha mabasi. Wanapoagana Musa atamwambiaje?
    1. Kwaheri
    2. shikamoo
    3. Usiku mwema
    4. majaliwa
  3. Ni sentensi gani si sahihi?
    1. Mimi ninacheza. 
    2. Wewe unasoma
    3. Yeye anaandika
    4. Wewe anacheka
  4. Tazama picha hii kisha utumie kihusishi mwafaka.
    G4swaT1T23001P5
    Maua yako __________________ meza.
    1. juu ya
    2. kando ya
    3. chini ya
    4. mbele ya
  5. Kanusha sentensi ifuatayo: Uliwasimulia wanafunzi hadithi.
    1. Hutawasimulia wanafunzi hadithi.
    2. Hatawasimulia wanafunzi hadithi.
    3. Hukuwasimulia wanafunzi hadithi. 
    4. Huwasimulii wanafunzi hadithi.
  6. Badilisha sentensi hii katika wingi: Kitabu chake kimepotea.
    1. Vitabu vyao vimepotea.
    2. Vitabu vyake vimepotea.
    3. Kitabu chao kimepotea.
    4. Vitabu vyetu vimepotea.
  7. Ni kitendo gani hakijaambatanishwa na kinyume chake?
    1. Cheka - lia
    2. Enda-rudi
    3. Kubali-kataa
    4. Andika - soma
  8. Jaza mapengo kwa jibu sahihi:
    Farasi alikimbia _________________________ naye kobe alitembea ______________________________.
    1. polepole, haraka
    2. haraka, polepole
    3. polepole, polepole
    4. haraka, haraka
  9. "Ni sentensi gani yenye kikomo?
    1. Unataka nini hapa?
    2. Kesho nitatuzwa zawadi:
    3. Kumbe unanidanganya.
    4. Nilikula wali, chapati, ugali.....
  10. Tazama picha kisha ujibu swali.
    G4swaT1T23001P6
    Ndege huyu and twa nani? 
    1. Tausi
    2. Mbuni
    3. Bata
    4. Njiwa

INSHA

Kuandika(Alama 10)

Umepewa dakika 40 kuandika insha yako. Andika insha juu ya 

                                                 MWALIMU WANGU WA DARASA

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

______________________________________________________________________________________

MARKING SCHEME

  1. C
  2. A
  3. D
  4. A
  5. C
  6. C
  7. A
  8. D
  9. A
  10. A
  11. B
  12. C
  13. B
  14. D
  15. B
  16. B
  17. A
  18. B
  19. D
  20. A
  21. C
  22. A
  23. D
  24. A
  25. C
  26. A
  27. D
  28. B
  29. C
  30. B
Page 7 of 14