Displaying items by tag: kiswahili

MASWALI

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali 1-5.
(Wanafunzi kadhaa wanajadiliana kuhusu vyakula wavipendavyo na manufaa yavyo mwilini).

Lulu: Juzi sote tulielewana kuwa vyakula kama vile vibanzi au chipsi havina manufaa yoyote mwilini. Ingawa wengi hawakukubali, huo ndio ukweli wa mambo.

Pendo: Ni kweli Lulu. Sasa leo kila mmoja atataja chakula akipendacho na umuhimu wa chakula hicho mwilini.

Ali: Baada ya kuacha kula vibanzi kwa wingi, nimeamua kupenda mboga za majani kama vile mchicha. Mboga hizi hunikinga dhidi ya magonjwa mbalimbali. Vile vile karoti huyaimarisha meno yangu na kuyapa nguvu macho yangu.

Rama: (Akitikisa kichwa kukubaliana na Ali) Mimi kwa upande wangu nilipoacha kula chipsi kwa wingi, siku hizi mimi ni mpenzi wa vyakula vyenye asili ya mizizi kama vile mihogo na viazi. Vyakula hivi hunipa nguvu ya kucheza mchezo wangu niupendao. Si mnaujua?

Wote: Naam, kandanda.

Rama: Ndiyo. Tena vyakula hivi hunipa joto la kutosha mwilini(akirukaruka na kurusha miguu ovyoovyo) Na wewe Lulu? (wote wanamgeukia Lulu)

Lulu: Baada ya kupunguza ulaji wa vibanzi au chipsi, siku hizi napenda sana maziwa, hasa ya ngamia. Maziwa haya huvikuza viungo vya mwili wangu hivyo kunifanya kukua na kuwa mkubwa. Nayapenda mno maziwa ya ngamia.

Pendo: Kwa upande wangu, siku hizi mimi napenda sana kula dagaa hasa wakiandaliwa pamoja na ugali. Dagaa huukuza mwili wangu na kunifanya kuongezeka kimo.

Lulu: Licha ya hayo yote, tusisahau kufanya mazoezi ya kutosha na kunywa maji safi na salama.

Wote: Sawa Lulu.

  1. Kulingana na mazungumzo haya, watoto hawa walikuwa wakipenda chakula gani kitambo?
    1. Maziwa ya ngamia
    2. Chipsi.
    3. Mboga za majani.
    4. Vyakula vya mizizi.
  2. Ali alisema anapenda mchicha kwa sababu
    1. huyapa nguvu macho yake. 
    2. humpa joto na nguvu ya kucheza. 
    3. humkinga asipate magonjwa. 
    4. huufanya mwili wake kukua.
  3. Kati ya watoto hawa, ni yupi mchezaji hodari wa kandanda?
    1. Rama
    2. Pendo
    3. Lulu
    4. Ali
  4. Kulingana na mazungumzo haya, ni chakula gani hapa hutupa nguvu? 
    1. Dagaa
    2. Mboga za majani
    3. Maziwa ya ngamia 
    4. Viazi
  5. Mwishoni mwa mazungumzo haya, Lulu anawakumbusha wenzake
    1. kunywa maji na kufanya mazoezi. 
    2. kufanya mazoezi na kunywa maji safi na salama.
    3. kufanya mazoezi.
    4. kunywa maji yaliyo safi na salama. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 8.
Naikumbuka vizuri siku yangu ya kwanza katika Gredi ya nne. Ilikuwa Jumanne asubuhi. Baada ya kuchukua virago vyangu kutoka katika darasa tuliloliacha pamoja na wengine, tuliandamana hadi Gredi ya nne kusini. Kwa kuwa nilikuwa mfupi zaidi, niliamua kukaa mbele kabisa katika safu ya kati. Kipindi cha kwanza kilikuwa cha Kiswahili. Tofauti na Gredi ya tatu, hapa tungefunzwa na walimu tofauti. Mwalimu wa Kiswahili alikuwa mwanadada mwembamba. Alikuwa na tabasamu angavu usoni. Aliongea Kiswahili sanifu. Nilikifurahia kipindi chake. Baada ya somo hili, nilikuwa na hamu ya kutaka kuwajua walimu wale wengine pia.

  1. Nini ambacho mwandishi bado anakumbuka?
    1. Mwalimu wa Kiswahili wa Gredi ya nne.
    2. Siku yake ya kwanza shuleni
    3. Siku yake ya mwisho katika Gredi ya tatu.
    4. Siku yake ya kwanza katika Gredi ya nne.
  2. Mwandishi aliamua kukaa mbele zaidi kwani
    1. alikuwa mfupi wa kimo.
    2. alizoea kukaa katika nafasi kama hiyo. 
    3. mwalimu alimtaka kufanya hivyo. 
    4. nafasi za nyuma zilikuwa zimejaa.
  3. Tumeambiwa tofauti gani iliyo kati ya Gredi ya tatu na ya nne? 
    1. Mpangilio wa darasani. 
    2. Ratiba ya mafunzo. 
    3. Idadi ya walimu. 
    4. Idadi ya wanafunzi.
  4. Ni wazi kuwa mwalimu wa Kiswahili wa Gredi ya nne alikuwa
    1. mnene kama nguruwe.
    2. mcheshi.
    3. mwanamume mwembamba mwenye tabasamu.
    4. mzembe kupindukia. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 9 hadi 12.
Watoto wachanga wanafaa kukanywa dhidi ya kucheza na vitu kama vile sarafu na gololi. Hivi ni kwa sababu watoto wengine huvitia vitu hivi hatari masikioni au hata puani. Ajabu ni kuwa, wengine hata huweza kuvimeza vidude hivi. Mtoto anapofanya hivyo, si vyema kujaribu kukitoa hicho kilichoingizwa sikioni au puani. Huenda ikawa hatari hata zaidi. Muhimu ni kumpeleka mtoto katika kituo cha afya kilicho karibu haraka iwezekanavyo ili kuokoa hali.

  1. Taarifa inasema kuwa kuvitia vitu hatari masikioni na puani si vizuri kwa kuwa huweza
    1. kusababisha hatari.
    2. kusababisha mauti. 
    3. kuleta hasara.
    4. kuzua ugomvi.
  2. Mtoto akimeza sarafu, cha kwanza kufanya ni nini?
    1. Kujaribu kumtapisha. 
    2. Kumpeleka hospitalini.
    3. Kujaribu kuiondoa.
    4. Kumnywesha maji kwa wingi
  3. Ili ajali ya aina hii isitokee, watoto wachanga
    1. wasipewe safaru bali noti za kuchezea.
    2. wafumbwe midomo na pua wasitie vitu hatari.
    3. wasiruhusiwe kabisa kucheza.
    4. wakanywe dhidi ya kuchezea vifaa hatari.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 13 hadi 15.
Wanyama ambao huishi misituni huitwa wanyamapori. Wengi wao huwa wakali na hivyo hawawezi kuishi na wanadamu. Ndovu au tembo ndiye mnyama mkubwa zaidi. Mnyama aliye na mbio zaidi kupita wote ndiye duma. Mwenye shingo ndefu kupita wote huitwa twiga huku yule aliye mkali zaidi na ambaye huitwa mfalme wa nyika ni simba. Wanyama hawa pamoja na wengine huwavutia watalii ambao hujaajaa humu nchini ili kuwatazama. Wanapokuja, wao hulipa pesa za kigeni ambazo husaidia kuuinua uchumi wa nchi yetu.

  1. Binadamu hawawezi kuishi na wanyamapori kwa sababu ya
    1. ukubwa wao.
    2. ukali wa baadhi yao.
    3. mbio zao.
    4. upole walio nao.
  2. Tembo ndiye mnyama 
    1. mkali kuliko wote.
    2. mwenye mbio zaidi. 
    3. mwenye shingo ndefu ajabu. 
    4. mkubwa zaidi.
  3. Chagua sifa za simba kulingana na ufahamu huu.
    1. Mwenye mbio na shingo ndefu.
    2. Ukali na ufalme.
    3. Ukali na shingo ndefu. 
    4. Ukubwa na mbio.

Soma kifungu kifuatacho. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa.
Karimu ra nyanya yake wanaishi ..................16.................... mto Riva. Mto huo huwasaidia na ..................17.................... wakati wa ukame. Huu ni wakati ambapo hakuna ..................18.................... Kila siku ya ..................19.................... Karim huwa haendi shuleni. Yeye humsaidia nyanya yake shambani palipo na migomba. Shughuli za shambani huwa za kupalilia migomba hiyo. Nyanya wa Karim humpenda kwa sababu Karim ..................20.................... mvivu.

  1.                    
    1. ndani ya
    2. karibu na
    3. juu ya
    4. chini ya
  2.                
    1. maji
    2. moto
    3. mchanga
    4. kuni
  3.            
    1. jua
    2. joto
    3. kelele
    4. mvua
  4.                    
    1. Jumatatu
    2. Alhamisi
    3. Jumamosi
    4. Jumanne
  5.                
    1. ni
    2. huwa
    3. si
    4. ndiye

Katika swali la 21-30. jibu swall kulingana na maagizo uliyopewa.

  1. Ni neno gani hapa ambalo si nomino?
    1. Darasa
    2. Chaki
    3. Chupa
    4. Ruka
  2. Chagua orodha ya vitenzi pekee.
    1. Mdogo, chota, watu.
    2. Mdudu, okoa, Ala!
    3. Ona, chukua, leta.
    4. Kalamu, andika, chini ya.
  3. Katika sentensi mbuzi wanono walipelekwa sokoni jana, kivumishi ni kipi?
    1. Wanono
    2. Jana
    3. Walipelekwa
    4. Sokoni
  4. Maneno ambayo hutumiwa badala ya nomino huitwa
    1. viwakilishi.
    2. vielezi.
    3. vihisishi.
    4. vihusishi.
  5. Ni maneno yapi ambayo yote ni vielezi? 
    1. Darasa, ubao, chati.
    2. Pika, uza, sema.
    3. Nje ya, kando ya, ndani ya.
    4. Ovyoovyo, polepole, haraka.
  6. Chagua kiunganishi bora kukamilishia sentensii hii:
    Maimuna hakuja shuleni - alikuwa mgonjwa.
    1. na
    2. lakini
    3. kwa sababu
    4. ingawa
  7. Chagua nomino za ngeli ya A- WA pekee.
    1. Kiongozi, kijana, kitana.
    2. Nyoka, njiwa, kiroboto.
    3. Motokaa, majani, tawi. 
    4. Meza, kalamu, karatasi.
  8. Tegua kitendawili hiki.
    Kamba yangu ndefu lakini haifungi kuni.
    1. Mkufu
    2. Maji ya mto
    3. Siafu
    4. Barabara
  9. Chagua mfano wa kihisishi.
    1. Nje ya
    2. Beba
    3. Lo!
    4. Kwa makini
  10. Chagua wingi wa sentensi ifuatayo: Kondoo mgonjwa atatibiwa. 
    1. Kondoo wagonjwa watatibiwa. 
    2. Makondoo wagonjwa watatibiwa. 
    3. Kondoo mgonjwa watatibiwa.
    4. Kondoo wagonjwa atatibiwa. 

MWONGOZO

kiswahili ms

Tagged under

MASWALI

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali 1-5.
Kaka Mbweha: (Akicheka kwa kejeli) Bi Ngiri, mkulima hodari wa mihogo anayeheshimika katika ukanda huu, hujambo?

Bi Ngiri: (Akihema kwa uchovu) Sijambo, lakini nina swali. Unacheka nini? Ama ndio njia yako ya kumfariji anayetoka kuchanika kwenye mpini siku nzima?

Kaka Mbweha: (Anacheka zaidi) Eti kuchanika kwenye mpini? Wachapakazi kama mimi hawana haja ya kujichosha. Wanafanya kazi kwa kutumia akili.

Bi Ngiri: (Kwa dharau) Mhh! Heri nyinyi mabingwa wa kutumia akili. Sisi wengine inabidi tujikaze kisabuni ili tupate riziki.

Kaka Mbweha: (Kwa mshangao) Nyinyi wengine? Wewe na kina nani? Je, huna habari kwamba rafiki zako sungura na fisi hawapandi wala kuvuna lakini daima wana shibe?

Bi Ngiri: (Kwa sauti ya chini) Hayo ya kina sungura hayanihusu ndewe wala sikio. Isitoshe, unavyoona nimechoka. Shamba langu la mihogo liko mbali na kwangu. Bado nina mlima mmoja wa kukwea ndipo nifike.

Kaka Mbweha: Haya basi niazime vipande viwili vya mihogo. Nitarejesha nitakapovuna.

Bi Ngiri: Kaka Mbweha, umesahau kuwa tayari una deni langu la mihogo? Lípa hilo kwanza.

Kaka Mbweha: (Kwa unyenyekevu) Nitalipa tu.

Bi Ngiri: Utanilipa vipi ilhali wewe mwenyewe hukuvuna? Unastahili kufanya kazi kwa bidii. Kumbuka ajizi ni nyumba ya njaa.

  1. Kulingana na mazungumzo haya, Bi Ngiri anasifika kwa sababu ya nini? 
    1. Kutembea mwendo mrefu kwenda shambani mwake.
    2. Ukulima wa mihogo.
    3. Bidii katika shughuli za shambani. 
    4. Kuwashauri wakulima wenzake.
  2. Chagua sifa inayomfaa zaidi kaka Mbweha kulingana na mazungumzo haya.
    1. Mchapakazi
    2. Mnyenyekevu
    3. Mwerevu
    4. Mvivu
  3. Mazungumzo haya yanaweka wazi kuwa anayejitegemea ili kujilisha kikamilifu ni
    1. fisi.
    2. sungura.
    3. kaka Mbweha.
    4. Bi Ngiri.
  4. Ni kwa nini Bi Ngiri alimwambia kaka Mbweha kuwa bado alikuwa na mlima mmoja wa kukwea? Ili 
    1. kumjulisha kuwa kulikuwa na milima huko.
    2. waandamane kuelekea kwake. 
    3. akatize mazungumzo na amruhusu aende akapumzike.
    4. kumweleza umuhimu wa kuwa na shamba mbali na nyumbani.
  5. Mazungumzo haya yanatufunza kuhusu
    1. ubaya wa uzembe.
    2. umuhimu wa kutumia akili. 
    3. kilimo cha mihogo. 
    4. matumizi ya mashamba. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 9.
Ni wajibu wa kila mkenya, awe kijana au mzee, kushiriki katika uhifadhi na ulinzi wa misitu yetu. Kila mmoja ana nafasi yake ya kutekeleza kulingana na umri na uwezo wake. Upanzi wa miti unafaa kuongozwa na vijana kwa sababu wana nguvu ya kutosha. Msimu mzuri wa kupanda miche ni msimu wa mvua nyingi.
Ili kuipanda miti mingi nchini, serikali imetenga siku moja kwa mwaka iwe ya upanzi wa miche, yaani miti michanga. Wengi hivi karibuni wamekosa kuitilia maanani siku hii muhimu. Hapo awali, shughuli hii ilikuwa ikichangamkiwa na kila mmoja katika jamii.

  1. Kulingana na ufahamu, uhifadhi wa misitu ni wajibu wa
    1. vijana.
    2. watu wazima. 
    3. watu wote.
    4. wanafunzi.
  2. Je, ni kwa nini vijana ndio wanaofaa kuongoza katika upanzi wa miti?
    1. Wana nguvu ya kutosha.
    2. Wanajua kupanda miche zaidi. 
    3. Wao ndio wengi nchini.
    4.  Hiyo ni sheria ya nchi yetu.
  3. Katika mwaka mzima, siku ngapi zimetengewa upanzi wa miti?
    1. 3
    2. 2
    3. 4
    4. 1
  4. Kulingana na ufahamu, 
    1. hata sasa, wanajamii wanachangamkia upanzi wa miche.
    2. miti michanga sana huitwa miche.
    3. hapo awali, watu hawakupenda kupanda miche.
    4. miti ina faida kwa vijana pekee. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 10 hadi 12.
Mayowe aliketi kando ya ghala lake tupu. Tumbo lilimnguruma kwa njaa. Aliishi hivyo kwa siku tatu. Mtama aliokuwa ameuweka katika ghala uliibwa na manyani na tumbili waliotoka katika msitu wa Marura. Mahindi nayo yaliyokuwa tele humo ghalani yaliliwa yote na kuchakulo. Kando yake kulikuwa na kibuyu. Kibuyu hicho kilisoma akili yake haraka na kumwambia kwa sauti, "Fanya chaguo!" Mayowe alisema kwa sauti, "Ninataka chakula!" Ghafla bin vuu, ghala likajaa mihogo na viazi. Mayowe alifurahi kuliko siku zote za maisha yake.

  1. Mwanzoni mwa ufahamu, ghala la Mayowe lilikuwa na nini?
    1. Mihogo na viazi.
    2. Lilikuwa tupu.
    3. Mahindi na mtama.
    4. Mtama na viazi.
  2. Tumeambiwa kuwa Mayowe alihisi njaa kwa muda wa
    1. wiki tatu.
    2. miaka mitatu.
    3. saa tatu
    4. siku tatu.
  3. Manyani na tumbili wezi walitoka wapi?
    1. Katika kijiji jirani.
    2. Mlimani.
    3. Mtoni Marura.
    4. Msituni Marura.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 13 hadi 15.
Kuna umuhimu mkuu wa kudumisha afya bora. Binadamu akiwa na afya bora huweza kufanya shughuli zote vizuri na kwa wakati unaofaa. Ili kuwa na afya bora, ni vizuri kuzingatia lishe bora. Chakula tunachokila lazima kiwe na kabohaidreti, protini na vitamini kwa viwango vinavyofaa mwilini. Vilevile, ni vizuri kunywa maji safi na salama kila siku. Je, wajua kuwa matunda hutukinga tusiwe wagonjwa? Wapishi na watu wote wanaoandaa chakula ni lazima wawe safi ili tusipatwe na magonjwa.

  1. Taarifa hii inasema kuwa inatulazimu kudumisha
    1. lishe bora.
    2. chakula bora.
    3. afya bora.
    4. usafi wa hali ya juu.
  2. Tumean.biwa kuwa chakula chetu ni vyema kiwe na
    1. kabohaidreti na protini.
    2. vitamini na kabohaidreti.
    3. kabohaidreti na protini.
    4. vitamini, kabohaidreti na protini.
  3. Kulingana na taarifa hii, matunda
    1. hutuletea magonjwa.
    2. hutukinga dhidi ya magonjwa.
    3. huwa na ladha ya kuvutia.
    4. yanafaa kuwa safi na salama. 

Soma kifungu kifuatacho. Chagua libu lifealo zaidi kati ya yale uliyopewa

Wapo wanyama mbalimbali ...................16................. katika mbuga zetu. Kuna wale ambao huwawinda wenzao kama vile simba, chui na  ...................17.................. Hawa huwa  ...................18................. mchana wote.  ...................19.................kuwaona, lazima ufike mbugani mapema kabla ya  ...................20.................kuchomoza.

  1.                        
    1. zilizo
    2. iliyo
    3. aliye
    4. walio
  2.                
    1. farasi
    2. ngamia
    3. duma
    4. ndovu
  3.            
    1. hawalali
    2. hawaamki
    3. wamelala
    4. wanalala
  4.            
    1. Hili
    2. Ili
    3. Hii
    4. Kwa sababu
  5.              
    1. giza
    2. mwezi
    3. nyota
    4. jua

Katika swall la 21-30, libu swall kulingana na maagizo uliyopewa. 

  1. Chagua kundi la nominoambata pekee. 
    1. Umati, kicha, mlolongo.
    2. Mjombakaka, mjusikafiri, mlariba.
    3. Huzuni, furaha, hasira.
    4. Meza, kalamu, darasa.
  2. Chagua nomino iliyo tofauti na nyingine.
    1. Alhamisi.
    2. Upendo.
    3. Agosti.
    4. Jumanne.
  3. Chagua sentensi iliyoakifishwa ipasavyo.
    1. Alisema kuwa amemaliza kazi. 
    2. Kwani mzazi wako hajafika. 
    3. Wanafunzi wenzangu ni Timami, Maimuna na Recho.
    4. Naam, nimekuelewa sasa.
  4. Je, ni pambo gani hapa linaloweza kuvaliwa masikioni?
    1. Bangili.
    2. Kipuli.
    3. Ushanga.
    4. Hina.
  5. Chagua nomino zilizo katika ngeli ya I-ZI.
    1. Gari, tunda, tausi
    2. Uzi, ushanga, ukuta.
    3. Kinyonga, kiwavi, kinda.
    4. Pua, shingo, karatasi.
  6. Umepewa maneno manne hapo. Chagua litakalokuwa la kwanza katika kamusi.
    1. Kofia
    2. Konsonanti
    3. Koleo
    4. Kondakta
  7. Mwenzako akikuambia alamsiki utamwambiaje?
    1. Nawe pia 
    2. Binuru
    3. Jaala
    4. Inshallah
  8. Kanusha sentensi ifuatayo: Nilimwona akiingia.
    1. Nilimwona akiondoka. 
    2. Sikumwona akiondoka. 
    3. Sikumwona akiingia. 
    4. Nilimwona akija.
  9. Ukubwa wa nomino mti ni
    1. miti.
    2. jiti.
    3. kijiti.
    4. vijiti.
  10. Kamilisha tashbihi ifuatayo:
    Mzee Mapunda ni mkali kama
    1. wembe.
    2. shubiri.
    3. pilipili.
    4. simba.

MWONGOZO

swa ad

Tagged under

MASWALI

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswall 1-5.
(Mwanasiasa na wananchi wamekutana katika ukumbi wa Ulimisukari ili kutathmini maendeleo yaliyofanywa na ahadi zilizotimizwa tangu mwanasiasa alipotwaa uongozi.)

Mwanasiasa: Ni matumaini yangu kuwa hamjambo. Nina furaha mpwitompwito kwa kuitikia wito huu wa kujumuika nanyi hapa. Kwanza, asanteni sana kwa kura zenu.

Mkulima: Mheshimiwa, ulituahidi mbolea ya bei nafuu. Hadi leo hatujaiona. Je, kulikoni?

Mwanasiasa: (Kwa kiburi) Wizara husika imegundua kuwa serikali iliyotangulia ilitumia vibaya pesa, hivyo, bado hatuna pesa. Tumieni samadi. Kunjeni mashati jamani. Endeleeni kukaza misuli!

Mzazi: Bwana Tumbo, hali ya masomo je? Uliahidi kuwa wanafunzi wetu watafanyia majaribio mwezini.

Mwanasiasa: Kuhusu hilo, naomba mnipe muda kidogo niwasafirishe wanangu warudi shuleni ng'ambo kwanza. Kuhusu majaribio mwezini, tumegundua kuwa hali ya anga huko si shwari. Watasalia chini ya miti kwa muda.

Mwalimu: Hatujaona mabadiliko katika sekta ya wafanyakazi wa umma. Ulituahidi magari kwa mkopo, sasa...."

Mwanasiasa: Baiskeli hujui kuendesha, utaendeshaje gari? Mimi naona bora tufungue vyuo vya mafunzo ya udereva kwanza, ama vipi wenzangu? (akiangazaangaza)

Mjenzi: Mheshimiwa, ulituahidi vyakula bila malipo kila mwezi, kugawana mali yako na mifereji ya maziwa. Umeyafumbia macho. Mheshimiwa huoni haya?

Mwanasiasa: Jamani, naomba tuulize maswali ya kiutuuzima! Wewe uliona wapi mifereji ya aina hiyo? Hakuna cha bure! Imeandikwa kila mbuzi atakula kulingana na urefu wa kamba yake. Kuhusu kugawana mali yangu, nadhani hamkunisikia vizuri. Hali ni ngumu jamani. Tugawanaje mali yangu? (kimya) Mimi nadhani hamna mliloniitia. Tuonaneni baada ya miaka mitano. (wanafumukana kwa huzuni)

  1. Kuhusu mbolea ya bei nafuu, mwanasiasa alitoa kisingizio gani?
    1. Hakuwa na pesa za kuigharimia.
    2. Bado serikali yake haikuwa na pesa. 
    3. Mbolea ilikuwa ya bei ghali katika masoko ya kimataifa.
    4. Alitaka wakulima watumie samadi.
  2. Kuhusu hali ya masomo, mwanasiasa alitaka apewe muda ili
    1. ahakikishe usalama mwezini.
    2. akakamilishe masomo yake ng'ambo. 
    3. awasafirishe wanawe ng'ambo wakasome.
    4. wanafunzi waendelee kusomea chini ya miti.
  3. Dhana ya dharau inajitokeza pale ambapo mwanasiasa
    1. anadai kuwa wafanyakazi wa umma hawajui hata kuendesha baiskeli.
    2. anapinga ahadi zote alizoahidi.
    3. anawaahidi wananchi chakula cha bure.
    4. watu wanafumukana kwa hasira na huzuni
  4. Mwanasiasa alimaanisha nini aliposema kuwa kila mbuzi atakula kulingana na urefu wa kamba yake?
    1. Kila familia itapata chakula kulingana na hali yake.
    2. Watu wote huwa na uwezo sawa wa kujipatia riziki.
    3. Mbuzi mwenye kamba fupi hula katika eneo dogo.
    4. Kila mmoja atajipatia riziki kulingana na bidii yake.
  5. Kulingana na mazungumzo haya, ni wazi kuwa
    1. wananchi waliridhishwa na mwanasiasa huyu.
    2. mwanasiasa aliwahadaa wananchi kumpigia kura.
    3. Bwana Tumbo alikuwa kiongozi mwadilifu.
    4. Bwana Tumbo alitimiza baadhi ya ahadi alizotoa.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6 hadi 8.
Serikali inapaswa kuwaelimisha wakulima nchini. Hivi ni kwa sababu ya upungufu wa mazao ya kilimo. Wakulima wengi wamepungukiwa na ujuzi wa shughuli za ukulima. Hivyo basi, kuna haja ya kuwafunza njia za kunyunyizia mazao yao dawa. Pia inafaa wafunzwe njia bora za upanzi. Kwa wengine, kutumia mbolea huwa ni jambo wasilolijua wala kulithamini.

Kwa wanaofuga wanyama na ndege kama vile kuku, wanapaswa kufundishwa mbinu za kukabiliana na magonjwa kama vile sotoka kwa ng'ombe na kideri kwa kuku. Maafisa wa kilimo hawana budi kuwa katika mstari wa mbele katika kuwapa wakulima misaada ya kila aina maana kilimo ni uti wa mgongo wa taifa letu.

  1. Kulingana na taarifa, ni kwa nini mazao ya kilimo yamepungua?
    1. Wakulima hawafanyi bidii.
    2. Wakulima hawana ujuzi unaohitajika. 
    3. Kuna upungufu mkubwa wa mvua. 
    4. Kwa sababu kuna ukame uliokithiri nchini.
  2. Taarifa hii inasema kuwa kwa wakulima wengine, matumizi ya mbolea
    1. ni kitu muhimu mno.
    2. ni jambo geni wasilolielewa.
    3. hustahili kufunzwa na maafisa wa kilimo.
    4. ni jambo walilo na mazoea makuu nalo.
  3. Kulingana na ufahamu, si kweli kusema kuwa
    1. serikali haina budi kuwapa wakulima mafunzo kemkem.
    2. mashamba yasiyo na rutuba huhitaji mbolea.
    3. sotoka huwaathiri sana kuku huku ng'ombe wakiugua kideri.
    4. si wakulima wote wanatambua mbinu bora za kilimo.
  4. Sehemu iliyopigiwa mstari mwishoni mwa taarifa hii ina maana gani?
    1. Taifa letu linategemea sana kilimo.
    2. Wananchi wengi wa nchi hii ni wakulima.
    3. Wananchi wote wa nchi hii ni wakulima. 
    4. Wakulima wa humu nchini hawana budi kuongeza bidii kazini.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 10 hadi 12.
Ajira za watoto ni kazi ambazo zinawatumia na kuwaathiri vibaya watoto wa kati ya miaka mitano hadi kumi na saba. Kwa namna fulani, watoto huathirika kiakili, kimwili, kimakazi na kimaadili. Pia, ajira hizi ni kizuizi cha watoto kupata elimu. Mateso yanayowapata watoto katika ulimwengu wa ajira duniani ni mengi. Ajira hizi huweza kuwa za nyumbani kwa watu wengine, mashambani au viwandani. Kazi wanazozifanya watoto hawa ni kulisha mifugo, kuchimba mawe, kufyatua matofali, kuchonga mawe, ujenzi wa barabara, kuvuta au kusukuma mikokoteni na za ndani ya nyumba. Zote hizi ni kinyume na haki za binadamu kwa jumla

  1. Tumearifiwa kuwa ajira ya watoto huweza kuwaathiri watoto
    1. kimaadili, kimakazi na kidini. 
    2. kiakili, kimavazi na kimwili. 
    3. kimakazi, kiakili na kimaadili. 
    4. kiakili, kimwili na kiukoo.
  2. Kulingana na kifungu, ajira ya watoto haiwezi kuwa
    1. nyumbani kwa wengine. 
    2. katika viwanda.
    3. mashambani.
    4. shuleni.
  3. Haki za binadamu hazimkubali mtoto 
    1. kuosha vyombo nyumbani kwao. 
    2. kuvuta mikokoteni kwa malipo. 
    3. kulifagia darasa lao.
    4. kufua sare zake.

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 13 hadi 15.
Juzi tulipokuwa sebuleni tukitazama runinga, mjomba alianza kutusimulia kuhusu umuhimu wa miti. Alianza kwa kusema kuwa mwalimu wao alisema kuwa miti huwa ni maskani ya wanyama mbalimbali, sanasana nyuni ambao hutengeneza viota vyao na kutagia mayai yao humo. Aliendelea kutuambia kuwa wanyama wengine wanaotegemea miti kama makazi ni wanyamapori kama vile simba, chui, pundamilia na wengine. Si hayo tu, aidha, alisema kuwa miti huweza kutumiwa kujengea, kuundia samani na pia kutumika kama dawa ambapo sehemu mbalimbali za miti hutumika kutibia magonjwa mbalimbali. Tulipokuwa tumechoka kumsikiliza, alituaga na kila mmoja wetu akaelekea kulala ili turauke siku iliyofuata.

  1. Msimulizi na wenzake walikuwa wakisimuliwa kuhusu nini? 
    1. Madhara ya wanyama. 
    2. Matumizi ya maji. 
    3. Umuhimu wa miti.
    4. Wanyama wa porini.
  2. Yawezekana kuwa masimulizi haya yalifanyika 
    1. adhuhuri.
    2. asubuhi.
    3. alasiri.
    4. usiku.
  3. Kulingana na habari hii, miti hutusaidia katika haya yote ila kutupatia
    1. dawa. 
    2. kuni.
    3. vifaa vya ujenzi
    4. vifaa vya kutengenezea samani

Soma kifungu kifuatacho. Chagua Jibu faalo zaidi kati ya vale uliyopewa
Visa vya watu kuwaua wake, waume au watoto wao vimekuwa......................16................. sana siku hizi. Si jambo ......................17................. mtu kufikia hatua kama ......................18................. Hakika, ni......................19................. mkubwa. Si hayo tu, wengine hufikia hatua ya kujiangamiza wao wenyewe kwa kujitoa uhai. Binadamu wanafaa kujua njia......................20................. za kusuluhisha matatizo yao kuliko kuchinjana na kuuana.

  1.                  
    1. mingi
    2. wengi
    3. nyingi
    4. vingi
  2.                      
    1. jema
    2. nzuri
    3. baya
    4. mbaya
  3.                
    1. hili
    2. hiyo
    3. hizi
    4. huo
  4.              
    1. mnyama
    2. wanyama
    3. unyama
    4. kinyama
  5.                    
    1. mzuri
    2. fupi
    3. ndefu
    4. bora

Kutoka swali la 21-30. jibu swali kulingana na maagizo uliyopewa.

  1. Chagua sentensi iliyotumia amba kwa usahihi.
    1. Ugonjwa ambayo ulitibiwa ulikuwa hatari.
    2. Wanafunzi ambao waliojiunga nasi walikuwa werevu.
    3. Cherchani ambacho kilinunuliwa ni hiki.
    4. Masomo ambao tulisomeshwa yametufaa.
  2. Je, ni sentensi gani hapa imetumia kivumishi kiulizi ipasavyo?
    1. Kondoo wapi aligongwa na gari? 
    2. Wageni gani watakaolakiwa jioni? 
    3. Unataka nyumba yako ijengwe vipi?
    4. Ufisadi katika nchi hii utakoma lini?
  3. Mikoba hii ni mipya bali ile pale ni mikuukuu. Sehemu iliyopigiwa mstari ni 
    1. kiwakilishi kiashiria.
    2. kivumishi kiashiria.
    3. kielezi cha mahali.
    4. kiwakilishi cha mahali.
  4. Chagua sentensi iliyoakifishwa kwa usahihi.
    1. Wanyama wafugwao ni pamoja na: ng'ombe, mbuzi na kondoo.
    2. Ukienda ng'ambo uniletee haya: vikoi, saa na mkufu.
    3. Ala, kumbe unajua kuendesha baiskeli.
    4. Mwalimu alipoingia darasani! alikuwa na furaha.
  5. Ni sentensi gani haijatumia kivumishi kimilikishi kwa usahihi?
    1. Jirani yangu anaitwa Kenge.
    2. Madarasa yao yalikuwa na vumbi.
    3. Kina mama yao walituzwa kwa usafi wao.
    4. Mwalimu wetu anapenda kutabasamu.
  6. Chagua majina yaliyo katika ngeli ya KI-VI pekee.
    1. Kinu, kisu, choo.
    2. Uzi, utepe, kiazi.
    3. Chanzo, chenza, chupa.
    4. Kijana, kiongozi, kipofu.
  7. Ukuta umepakwa rangi katika wingi ni
    1. nyuta zimepakwa rangi.
    2. makuta yamepakwa marangi. 
    3. ukuta zimepakwa rangi. 
    4. kuta zimepakwa rangi.
  8. Nomino ndizi, nyumba na habari hupatikana katika ngeli ya
    1. LI-YA
    2. U-I
    3. I-ZI
    4. U-ZI
  9. Kamilisha methali
    Mgeni njoo
    1. mwenyeji apite. 
    2. mwenyeji apone. 
    3. kibaya chajitembeza. 
    4. usimwangalie usoni.
  10. Kupiga miguu ni sawa na 
    1. kukimbia kwa kasi. 
    2. kutuliza miguu.
    3. kuteleza matopeni. 
    4. kutembea.

MWONGOZO

kiswahili sdsd

 

Tagged under

MASWALI

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata.
Kuna aina nyingi za simu. Simu ambayo hutumika sana ni simul ya mkononi. Simu ya mkononi huitwa rununu, rukono, simutamba au selula. Watu wengi sana hutumia simu siku hizi. Hii ni tofauti na kitambo ambapo watu waliotumia simu walikuwa wachache. Kazi kubwa ya simu ya mkononi ni mawasiliano. Mawasiliano ni kupitisha. ujumbe kutoka kwa mtu mmoja hadi kwa mwingine. Faida ya mawasiliano ya kuzungumza kwa simu ni kuwa hata watu wasiojua kusoma na kuandika huweza kuwasiliana.
Simu pia huweza kutumika kuandika arafa. Arafa ni ujumbe mfupi unaoandikwa na kutumwa kutumia simu. Vilevile, simu hutumika kucheza muziki. Nyimbo mbalimbali huchezwa kwa kutumia simu. Hata hivyo, ni vyema. kuwa mwangalifu unaposikiliza nyimbo kwa kutumia simu. Unapotumia vidude viwekwavyo masikioni wakati wa kusikiliza muziki, hakikisha kuwa sauti ni ya kiwango cha chini. Kusikiliza muziki wa sauti ya juu kwa muda mrefu ukitumia vidude vya masikioni huweza kuyaharibu masikio. Ni muhimu mno kuchagua nyimbo zenye mafunzo mazuri. Baadhi ya nyimbo huwa na maneno machafu yasiyofaa. Nyimbo kama hizo hazifai kusikilizwa hata kidogo.
Kunao watu ambao husikiliza redio kupitia simu. Watu hao husikiliza taarifa za habari na mambo mengine kupitia redio iliyo kwenye simu. Simu pia hutumika kupiga hesabu kwa kutumia kikokotoo, kupiga picha na kucheza video. Hakika, simu ina umuhimu mkubwa katika maisha. Hata hivyo, simul pia ina madhara yake. Kutumia simu kila wakati kunaleta shida mbalimbali. Kwa mwanafunzi, kutumia simu kila wakati humpotezea mwanafunzi huyo nafasi ya kufanya mambo muhimu. Mambo muhimu. kwa mwanafunzi ni kusoma na kufanya kazi za ziada.

  1. Gani si jina la simu ya mkononi kulingana na kifungu?
    1. runinga
    2. simutamba
    3. selula
    4. rukono
  2. Kwa nini watu wengi hununua simu za mkononi kulingana na kifungu?
    1. Ili wasikilize muziki
    2. Ili watazame video
    3. Ili wasikilize redio
    4. Ili wawasiliane na wenzao
  3. Kulingana na aya ya kwanza, ni kweli kuwa;
    1. Watu walio na simu si wengi mno
    2. Hata watu wasiojua kusoma na kuandika huwasiliana kwa kutumia simu
    3. Kitambo, watu wengi mno walikuwa na simu kuliko siku hizi
    4. Kazi pekee ya simu ya mkononi ni mawasiliano 
  4. Ukitaka kutumia simu kuwasiliana na mtu aliye na shida ya kusikia utafanya nini?
    1. Utamwandikia arafa
    2. Utampigia simu
    3. Utamwandikia barua
    4. Utatuma mtu aongee naye
  5. Kutumia vidude vya masikioni kusikiliza muziki wa sauti ya juu kwa muda mrefu. huweza kumfanya mtu akawa;
    1. kipofu
    2. kiziwi
    3. bubu
    4. kiwete
  6. Kulingana na ufahamu, ni kweli kuwa;
    1. Simu haina manufaa yoyote
    2. Simu haina madhara yoyote
    3. Simu ina faida na madhara
    4. Simu ina madhara pekee
  7. Simu hutumika kufanya mambo yafuatayo. isipokuwa;
    1. kuwasiliana
    2. kusafiri
    3. kupiga picha
    4. kusikiliza muziki
  8. Aya ya mwisho inaeleza kuwa jambo muhimu kwa mwanafunzi ni kufanya nini?
    1. kucheza na wenzake
    2. kutumia rununu
    3. kusoma na kufanya kazi ya ziada
    4. kuwasaidia wazazi

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali yanayofuata.
Simba ndiye aliyekuwa mfalme wa mwituni. Wanyama wote walifurahia kuongozwa na simba. Siku moja Simba alitangaza kwamba alikuwa mgonjwa mahututi na kwamba alikaribia kuaga dunia. Hivyo aliwaalika wanyama wote waende nyumbani kwake kumwona na kusikia maneno yake ya mwisho. Hali hiyo iliwafanya wanyama wote wawe na woga kama kunguru.Wanyama wengi waliingiwa na wasiwasi kwa sababu walimpenda sana mfalme wao na hawakutaka afe.
Hivyo mbuzi alienda kwenye pango alimoishi Mfalme Simba ili kumjulia hali. Alisimama kwenye sehemu ya kuingilia pangoni na kusikiliza kwa muda mrefu. Kisha kondoo alikuja na akaingia pangoni moja kwa moja. Kabla hajatoka mwanafarasi naye alikuja kupokea ushauri wa mwisho wa mtalme, akaingia pangoni. Mbuzi alipoona kuwa wenzake hawakutoka nje, aliondoka. Baada ya muda mfupi simba alijitokeza nje akionekana kupata nafuu ya haraka, akaja kwenye lango lake la kuingilia pangoni ili apunge upepo wa nje. Alipopiga macho kushoto na kulia alimwona mbweha, akiwa amejiinamia akisubiri nje ya pango kwa muda mrefu.
"Kwa ini ewe mbweha hujaja ndani ya pango kutoa heshima zako za mwisho kwangu? Mbona unakaa tu apa nje ukicheza?" Simba alimwuliza.
"Nisamehe Bwana Mkubwa," Mbweha alijitetea, "ila katika kuja kwangu hapa nimegundua alama za nyayo za wanyama wengi ambao wamekwisha kukutembelea pangoni mwako; na nikichunguza kwa makini zaidi naona alama nyingi za kwato zikiingia ndani, na sioni zitokazo nje. Hadi hapo nitakapowaona wanyama waliokwishaingia pangoni mwako wakitoka nje, sitaingia. Ninaona ni heri nibaki huku huku nje kwenye uwazi na hewa safi.
Ujumbe ulipowafikia wanyama wengine, walimpeleka Simba mahakamani na kumshtaki. Simba alihukumiwa kifungo cha mwongo mmoja. Vilevile, alinyang'anywa mamlaka ya kuwa mfalme. Mbweha alichaguliwa kuwa kiongozi kwa kuwa alisema ukweli na kukomesha uovu uliokuwa ukiendelea.

  1. Simba alimaanisha nini aliposema kuwa
    'alikaribia kuaga dunia"?
    1. afya yake ilikuwa sawa
    2. halikuwa akihisi njaa
    3. alikuwa karibu kufa
    4. alikuwa karibu na dunia
  2. Ufahamu huu unaonyesha kuwa simba alikuwa mnyama mwenye;
    1. busara
    2. tamaa
    3. uchoyo
    4. ujanja
  3. Maneno 'woga kama kunguru' ni mfano wa; Tuulinde wetu mwili, kuwe maisha mazuri.
    1. nahaù
    2. kitendawili
    3. methali
    4. tashbihi
  4. Kwa nini mbweha hakuona nyayo za wanyama ambao walitoka nje?
    1. pengine alikuwa na shida ya macho.
    2. wanyama hao waliliwa na simba
    3. wanyama hao hawakujua njia ya kutoka nje
    4. wanyama walitoka mbweha akiwa ameangalia chini
  5. Mnyama gani aliyeelewa kuwa 'polepole ndiyo mwendo'?
    1. mbuzi
    2. chui
    3. mwanafarasi
    4. kondoo

Soma ubeti ufuatao kisha ujibu maswali yanayofuata.
Kuwa nayo nzuri siha, ni jambo muhimu sana,
Hufanya tuwe na raha, tufanye mengi mapana,
Huondolea jeraha, leo vilevile jana,
Tuulinde wetu mwili, kuwe maisha mazuri

  1. Ubeti huo una mizani mingapi?
    1. 4
    2. 64
    3. 32
    4. 8
  2. Kina cha mwisho cha ubeti huu ni kipi?
    1. ha
    2. li
    3. ri
    4. na

Jaza nafasi zilizoachwa kwa jibu linalofaa zaidi.
Mwanafunzi ................16................... , awe mvulana au msichana ................17................... kuhakikisha kuwa anatia bidii katika masomo yake. Mwanafunzi ambaye ................18................... masomoni hufaulu wakati  ................19................... mtihani wake. Bidii si jambo la wakati  ................20...................  tu, la hasha! Ni jambo la kila wakati.

  1.                                  
    1. yoyote
    2. wowote
    3. yeyote
    4. lolote
  2.            
    1. hafai
    2. anafaa
    3. anafai
    4. wanafaa
  3.                                  
    1. anazembea
    2. anajilegeza
    3. anajitolea
    4. anafifia
  4.                            
    1. anapoufanya
    2. anapoifanya
    3. anapoyafanya
    4. anapomfanya
  5.                        
    1. umoja
    2. wamoja
    3. moja
    4. mmoja

Jibu maswali yanayofuata kulingana na maagizo.

  1. Tambua aina za vivumishi vilivyopigiwa mistari.
    Wanafunzi wale wamenunua madaftari mawili.
    1. kimilikishi, cha idadi
    2. kiashiria, cha idadi
    3. cha sifa, kimilikishi
    4. kiashiria, kimilikishi 
  2. Onyesha ukubwa wa;
    Ngamia wa mtoto amelala chini ya mti.
    1. Jigamia la jitoto limelala chini ya jiti.
    2. Kigamia cha kitoto kimelala chini ya kijiti.
    3. Gamia wa toto amelala chini ya jiti.
    4. Gamia la toto limelala chini ya jiti.
  3. Panga maneno yafuatayo jinsi yanavyofuatana kwenye kamusi.
    1. muhebi
    2. muhtasari
    3. muhula
    4. muhogo
      1. i, iv, iii, ii
      2. i, iv, ii, iii
      3. i, ii, iv, iii
      4. iii, ii, i, iv
  4. Chagua maneno mawili yenye maana sawa na 'figo'.
    1. nso, buki
    2. mtima, moyo
    3. kifua, kidari
    4. paji, panda
  5. Maelezo gani yaliyo sahihi kuhusu matumizi ya koloni?
    1. Hutumika kutanguliza orodha.
    2. Hutumika kuonyesha sauti zenye ving’ong’o.
    3. Hutumika mwanzoni mwa sentensi.
    4. Hutumika kuonyesha visawe.
  6. Onyesha wingi wa;
    Ukuta wenye ufa umeangukia ubua.
    1. Nyuta zenye nyufa zimeangukia mabua.
    2. Kuta zenye nyufa zimeangukia mabua.
    3. Kuta zenye nyufa zimeangukia bua.
    4. Nyuta zenye nyufa zimeangukia bua. 
  7. Tambua ishara itumikayo kwenye tarakilishi kuonyesha 'chapa koza'.
    1. U
    2. I
    3. B
    4. C
  8. Sentensi ifuatayo itaandikwaje katika kauli ya kutendewa?
    Mama amepika chakula cha mtoto.
    1. Chakula cha mtoto kimepikwa na mama.
    2. Mama amempikia mtoto chakula.
    3. Mtoto amepikiwa chakula na mama.
    4. Mama amepikiwa chakula na mtoto.
  9. Mpole ni kwa 'njiwa' kama vile mwaminifu ni kwa ...............................
    1. kunguru
    2. malaika
    3. chiriku
    4. mchana
  10. Tambua aina za maneno yaliyopigiwa mistari.
    Yule anatembea polepole.
    1. kivumishi, kielezi
    2. kiwakilishi, kielezi
    3. kivumishi, kiwakilishi
    4. kiwakilishi, kivumishi

INSHA

Andika insha ya masimulizi kuhusu mada ifuatayo.
SIKU YA MICHEZO SHULENI

MARKING SCHEME

swa adad

 

Tagged under

SEHEMU YA KWANZA   (Alama 5)

Kusikiliza na kuzungumza 

Soma mazungumzo yafuatayo kisha ujibu maswali. 

G6SwaT1TW23003P1

(Mama ameketi kochini akifuma sweta. Anaiwacha shughuli yake anapomwona Amara

Amara: (akimkaribia mama) Shikamoo mama? 
Mama:  (kwa tabasamu) Marahaba binti yangu! Umeshindaje shuleni?
Amara: Vyema mama! (kimya) Nikwambie tuliyoyasoma?
Mama:  Naam, niambie mwanangu
Amara: Tulifunzwa kuhusu mabadiliko ya hali ya anga. 
Mama:  Mafunzo mazuri sana. Ni kweli kuwa hali ya anga hubadilikabadilika na kuleta misimu mbalimbali. 
Amara: Lakini mama, sikuelewa vizuri kwa sababu nilikuwa nikisinzia kwa sababu ya mafua. 
Mama:  Pole! Nitajaribu kukuelezea. Kwanza kuna msimu wa kiangazi ambao huwa na jua kali. Hali hii huleta ukame.
Amara: Je, kuna kipupwe? 
Mama:  Naam mwanangu. Hukupitwa na kila kitu. Kipupwe ni majira ya baridi kali. Wakati huu watu wanafaa kuvaa mavazi                             mazito ili kupata joto. 
Amara: Ninaelewa mama. Nakumbuka pia kuna msimu wa mvua nyingi bali sikumbuki jina lake. 
Mama:  Msimu au majira haya huitwa masika. Sanasana wakati huu wakulima hupanda kwa sababu kuna maji ya kutosha. Isitoshe                  huwa kuna mafuriko na watu hufaa kutahadhari. 
Amara: Kuna msimu unaitwa kivuli? 
Mama:  Sio kivuli mwanangu. Ni vuli au mchoo. Wakati huu mvua huwa ndogondogo. 
Amara: (Kwa furaha) Umeelezea misimu minne na ninakumbuka mwalimu akisema kuwa angetufunza minne. 
Mama: Nina furaha kuwa nimeweza kukusaidia kuelewa zaidi yale mliyofunzwa shuleni leo. 
Amara: Asante mama! Hakika umenifaa sana. 

  1. Amara alipoulizwa na mama alivyoshinda shuleni alimjibu vipi? 
    1. Naam 
    2. Vyema 
    3. Shikamoo 
    4. Marahaba
  2. Maneno yafuatayo yametumiwa katika mazungumzo. Lipi halionyeshi adabu? 
    1. Pole 
    2. Naam
    3. Asante 
    4. Je 
  3. Ni jibu lipi linaloonyesha misimu ambayo mama alimfunza Amara?
    1. Kivuli, ukame, mchoo, masika 
    2. Ukame, kiangazi, masika, kipupwe 
    3. Kipupwe, kiangazi, vuli, masika 
    4. Masika, kivuli, kiangazi, kipupwe 
  4. Ni kauli gani si sahihi kulingana na mazungumzo haya? 
    1. Amara hakuelewa chochote darasani. 
    2. Amara alikuwa na ugonjwa wa malaria 
    3. Akina amara walifundishwa kuhusu misimu mbalimbali. 
    4. Mama yake Amara anaelewa misimu vizuri.
  5. Neno misimu limetumika katika mazungumzo kisawe chake ni gani?
    1. Anga 
    2. Majira 
    3. Ukame 
    4. Mabadiliko 

Swali la 6 hadi la 9 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali.

G6SwaT1TW23003P2

Hospitali kuu ya Ubora inapatikana katika kaunti ya Kinga. Hii ni mojawapo ya hospitali nyingi katika kaunti hii. Hospitali hii imegawanywa katika sehemu tofauti kila moja ikishughulikia ugonjwa mmoja. Hospitali hii ni ya kipekee. Wagonjwa wengi huenda hapa wanapougua. 

Madaktari wa Ubora ni wenye bidii ya mchwa. Huwa wanashughulika kama nyuki mzingani. Kila mmoja huwa anahudumia wagonjwa wake kwa upendo na heshima. Wauguzi pia husaidiana na madaktari ili kuhakikisha wagonjwa wamepata tiba inayofaa na kwa haraka. Hakuna anayefanya uzembe kazini kisa na maana wanaamini kuwa bidii huleta ufanisi. Wapo wanaoshughulikia magonjwa ya kuambukiza, matatizo ya macho, shida za mifupa, ndwele za mfumo wa hewa, moyo na magonjwa mengineyo. Hakika, kila mmoja huwa na shughuli yake. 

Jitihada za wafanyakazi wa hospitali hii huwasaidia wagonjwa wengi kupata matibabu na kuwa na afya bora. Hakujawahi kuwa na visa vya wagonjwa kutohudumiwa vyema hapa. Magonjwa ya aina zote hukabiliwa. Isitoshe huwashauri watu kujikinga na maradhi kwani kinga ni bora kuliko tiba. Aidha huwatuma madaktari kufundisha umma kuhusu umuhimu wa afya bora na za kuzuia magonjwa. Kusema kweli hakuna hospitali nyingine katika kaunti ya Kinga inaishinda hii. 

  1. Ni jibu lipi sahihi kulingana na aya ya kwanza? 
    1. Katika kaunti ya Kinga kuna hospitali moja tu. 
    2. Magonjwa yote hutibiwa sehemu moja. 
    3. Hospitali ya Ubora hushughulikia magonjwa machache. 
    4. Hospitali ya Ubora ndiyo bora zaidi kauntini.
  2. Kulingana na aya ya pili ni sehemu gani ndani ya mwili huathiriwa na shida ya mfumo wa hewa? 
    1. Figo 
    2. Kibofu 
    3. Mapafu
    4. Moyo
  3. Ni njia gani madaktari. huwasaidia wananchi kujikinga na magonjwa?
    1. Kuwashauri kujikinga na maradhi.
    2. Kuwatibu haraka.
    3. Kushirikiana na wauguzi. 
    4. Kuwafundisha kuhusu lishe bora. 
  4. Ni Methali gani imetumika katika kifungu hiki?
    1. Bidii ya mchwa 
    2.  Kila mmoja huwa na shughuli yake
    3. Shughulika kama nyuki mzingani
    4. Kinga ni bora kuliko tiba 

Swali la 10 hadi la 12 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali. 

G6SwaT1TW23003P3

Wanafunzi wa gredi ya sita katika shule ya msingi ya Busara wamegawanywa katika makundi manne.Makundi haya ni: Upendo, Amani, Subira na Umoja. Kila kikundi huwa na sehemu tatu za kutunza usafi kila juma. 

Tazama jedwali la juma hili kisha ujibu maswali. 

 VIKUNDI   JUMATATU   JUMATANO   IJUMAA 
 Upendo  darasani   chumba cha maakuli   msalani 
 Amani  msalani   majilisini  darasani 
 Subira  chumba cha maakuli   msalani   majilisini
 Umoja  majilisini  darasani   chumba cha maakuli 
  1. Ni kikundi kipi hakikusafisha darasa? 
    1. Subira 
    2. Amani 
    3. Umoja 
    4. Upendo
  2. Ni kikundi kipi hakikusafisha majilisi? 
    1. Subira 
    2. Umoja
    3. Upendo
    4. Amani
  3. Ni kikundi kipi hakikusafisha chumba cha maakuli
    1. Upendo
    2. Amani
    3. Subira 
    4. Umoja 

Swali la 13 hadi la 15 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali. 

G6SwaT1TW23003P4

Ugali ni chakula kinachopendwa na watu wengi sana. Njia ya kupika si ngumu. Kwanza, lazima uwe na unga wa mahindi, maji, sufuria, mwiko na jiko la kupikia lenye moto. Pima kiasi cha maji unayohitaji na kuyatia kwenye sufuria safi. Injika sufuria. Yapatie maji muda yachemke. Tia unga kidogo kidogo ndani ya maji yanayochemka, huku ukikoroga kwa mwiko.Ongeza unga kulingana na unavyotaka ugali wako uwe. Ukitaka ugali mgumu, endelea kuongeza unga. Ngoja ugali uive kwa joto la wastani. 

Ugali huandaliwa kwa vitoweo vya aina mbalimbali kama vile: Maziwa yaliyochachuka, mboga za kiasili kama vile mchicha, samaki au nyama.Kusema kweli ugali ni chakula cha kipekee. 

  1. Hatua ya kwanza ya kupika ugali ni ipi? 
    1. Kuwa na vitu utakavyohitaji kupika ugali.
    2. Kuinjika sufuria yenye maji jikoni.
    3. Kuchukua mwiko na kuanza kukoroga.
    4. Kuwa na kitoweo ambacho unahitaji.
  2. Neno injika lina maana gani
    1. Kuosha 
    2. Kuweka sufuria jikoni
    3. Kuchoma 
    4. Kuchemsha
  3. Ugali humwongeza mtu ___________________________ mwilini.
    1. Udhaifu
    2. Urefu
    3. Unyonge 
    4. Nguvu 

Swali la 16 hadi la 20 

Soma kifungu kifuatacho. Kwa kila swali umepewa majibu manne. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa

Johari alishiriki ___16___ michezo tofauti tukiwa shuleni. Michezo ___17___ alipenda sana ni kandanda na kuogelea. ___18___ na timu ya mchezo wa kandanda alipoingia gredi ___19___nne. Alifanya bidii na kuiletea timu yake ushindi. Alifahamu kuwa ___20___.

   A   B    C   D 
 16.   kwa   kwenye   katika   ndani ya 
 17.  ambapo   ambayo   ambazo   ambako 
 18.  Alikuunga   Aliwaunga   Alijiunga   Alituunga 
 19.  ya  wa  la  za
 20.  kidole kimoja hakivunji chawa   mtaka cha mvunguni sharti  ainame    asiyesikia la mkuu huvunjika  guu   mtoto umleavyo ndivyo  akuavyo 

Swali la 21 hadi la 30 

Chagua jibu sahihi. 

  1. Kiungo hiki cha mwili kinaitwaje?
    G6SwaT1TW23003P5 
    1.  Figo
    2.  Ini
    3. Moyo
    4. Pafu
  2. Nomino hizi ni za aina gani? Wingu la nzige, pakacha la matunda, bunda la noti na robota la pamba. 
    1. Kawaida 
    2. Wingi
    3. Makundi
    4. pekee
  3. Chagua wingi wa: Ukuta mrefu umejengwa na fundi mzuri. 
    1. Kuta ndefu zimejengwa na mafundi wazuri. 
    2. Kuta ndefu zimejengwa na fundi wazuri.
    3. Ukuta mrefu zimejengwa na fundi wazuri.
    4. Kuta ndefu zimejengwa na mafundi wabaya.
  4. Tenda ni kwa tendea, chora ni kwa _____________________ 
    1. Choresha 
    2. Chorea 
    3. Choreshwa 
    4. Choreshea 
  5. Ni kauli gani sahihi kuhusu bendera ya Kenya?
    1. Ina rangi tano
    2. Katikati imechorwa mkuki na ngao 
    3. Rangi ya juu ni kijani
    4. Rangi ya chini ni nyeusi
  6. Kati ya Maneno haya gani si la adabu? 
    1. Asante
    2. Tafadhali
    3. Karibu
    4. Ninataka
  7. Chagua ukubwa wa sentensi ifuatayo: Mlango wa nyumba yake unapendeza. 
    1. Lango la jumba lake linapendeza.
    2. Mlango wa jumba lake linapendeza. 
    3. Lango la nyumba yake linapendeza.
    4. Mlango wa nyumba yake linapendeza.
  8. Chagua jibu lisilo sahihi.
    1. Watano ni kivumishi cha idadi
    2. Mimi ni kiwakilishi cha nafsi
    3. Huyu ni kivumishi kiashiria
    4. Gani? ni kivumishi cha sifa 
  9. Ni nini maana ya msemo kupiga chafya
    1. Kuchemua.
    2. Kukohoa. 
    3. Kutema. 
    4. Kupenga.
  10. Sentensi hii imetumia tamathali gani ya lugha. Bawabu wetu ni mkali kama simba. 
    1. Istiara 
    2. Methali
    3. Tashbihi
    4. Kitendawili

INSHA

Andika insha ya kusisimua kuhusu mada ifuatayo: 

SIKU YA MICHEZO SHULENI MWETU 

MARKING SCHEME

  1. B
  2. D
  3. C
  4. B
  5. B
  6. D
  7. C
  8. A
  9. D
  10. A
  11. C
  12. B
  13. A
  14. B
  15. D
  16. C
  17. B
  18. C
  19. A
  20. B
  21. C
  22. C
  23. A
  24. B
  25. B
  26. D
  27. A
  28. D
  29. A
  30. C

 

Soma taarifa ifuatayo kisha ujibu maswali 1-5. 

Kila mwaka shuleni kwetu huwa na sherehe za kutoa tuzo kwa walimu, wanafunzi, wafanyakazi na mtu yeyote yule aliyefanya jambo lolote jema au kitendo chochote cha manufaa shuleni. Walimu hutuzwa tuzo kutokana na juhudi zao za kufunza vizuri. Wapishi hutuzwa kwa kuandaa mlo mtamu, usafi na kupika kwa wakati bila kuchelewa. Madereva nao hutuzwa kwa kuendesha magari ya shule kwa utaratibu, kuwa na nidhamu kwa wanafunzi wala kutosababisha ajali yoyote. 

Wafagiaji na wahudumu wengine kama vile mabawabu, waktubi, mahazili na mtarishi pia hutuzwa. Muhula uliopita, sisi wanafunzi tulituzwa kwa maadili, usafi, bidii na matokeo bora katika kila somo. Waliofanya vizuri katika somo la michezo na uhusiano mwema baina ya wanafunzi pia walituzwa. Mimi nilituzwa kwa kuwa bora katika Kiswahili, kuwa na nidhamu kuliko wote, kuwa safi mwaka mzima na pia nikapata tuzo ya kutumia muda wangu vizuri. Nawe pia unaweza ukapata zawadi hata zaidi yangu. Usife moyo kwa sababu ipo siku! 

Maswali 

  1. Kila mwaka shuleni kuna sherehe zipi? Za
    1. kutwezwa 
    2. kutwazwa 
    3. kutuzwa
    4. kutozwa. 
  2. Wafagiaji wa shuleni ni
    1. wapishi
    2. wahazili
    3. waktubi 
    4. matopasi. 
  3. Msimulizi alipata tuzo ngapi? 
    1. Nne 
    2. Nyingi
    3. Moja 
    4. Tano.
  4. Wapishi hupewa zawadi kwa kuzingatia yafuatayo isipokuwa
    1. kupika vyakula vitamu
    2. kupika kwa wakati 
    3. kupika vyakula nadhifu  
    4. kupika haraka.
  5. Ni kweli kusema kuwa
    1. wanafunzi walipewa zawadi za kufuzu masomoni tu
    2. wanafunzi walituzwa kwa kufanya vyema katika nyanja zote shuleni
    3. walimu walipata tuzo kwa kufunza na kuvalia vizuri
    4. madereva walizawadiwa kwa kuendesha magari kwa kasi. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 6-10. 

Katika familia au ukoo kuna utaratibu wa maisha. Kuna watu wa rika tofauti. Kuna jinsia tofauti pia. Watu wa familia huishi kwa adabu, heshima na nidhamu zinazofuata umri na jinsia. Kwa hivyo, kuna jinsi ya kusalimiana kwa kuzingatia umri na jinsia. Binadamu ni jamii yenye nidhamu na isiyotenda mambo ovyoovyo kama wanyama wafanyavyo. 

Hata utaratibu wa kula hufuata kanuni na sera maalum. Huo ndio ubinadamu na ubinadamu ndio utu wa watu. Tusifanye mambo shaghalabaghala kama hayawani. Familia isiyo na utaratibu wa nidhamu si familia tena! Familia nyingine hazina salamu wala habari. Hawajiheshimu, hawaheshimu wenzao wala kuheshimiana. Hakuna babu, nyanya, mtoto, baba, mavyaa, halati wala dada. Tukiishi hivyo, yule ng'ombe mwenye mkia na pembe ataishi vipi? 

  1. Ukoo ni kikundi cha watu wanaotokana na
    1. kabila moja
    2. dini moja
    3. nasaba moja
    4. kijiji kimoja.
  2. Binadamu wenye utu na ubinadamu hufanya mambo yao kwa njia gani?
    1. Taratibu 
    2. Ovyoovyo 
    3. Shaghalabaghala 
    4. Kiholela. 
  3. Familia au ukoo ni sawa na
    1. kabila
    2. kijiji
    3. jamii
    4.  jumla.
  4. Ni maamkuzi yapi hutumiwa kulingana na umri? 
    1. Habari 
    2. Sabalheri
    3. Hujambo 
    4. Cheichei. 
  5. Halati ni
    1. dada ya mama
    2. dada ya baba 
    3. kaka ya mama
    4. kaka ya baba. 

Soma shairi hili kisha ujibu maswali 11-15. 

Mkono wa mkulima, ni mgumu kama chuma,
Chakula cha mkulima, ni maharage na sima,
Mtazame mkulima, hatulii juma zima,
Bali huyu mkulima, ndiye mama wa uzima. 

Maisha ya mkulima, ni ya shida tangu zama,
Kibanda cha mkulima, huvuja na kutetema,
Mgongo wa mkulima, daima umeinama,
Bali huyu mkulima, ndiye mama wa uzima. 

Nafasi ya mkulima, mara nyingi ni ya nyuma,
Magarini mkulima, kazi yake kusimama,
Hadharani mkulima, huambiwa hana jema,
Bali huyu mkulima, ndiye mama wa uzima. 

Maswali 

  1. 'Ni mgumu kama chuma' ni fani gani ya Lugha? 
    1. Kitendawili 
    2. Istiara 
    3. Methali 
    4. Tashbihi. 
  2. Kwa nini mgongo wa mkulima daima umeinama? Kwa sababu 
    1. ya kazi yake 
    2. ni mzee
    3. ana shida
    4. nyumba yake ni ndogo.
  3. Hili ni shairi la aina gani? 
    1. Tathlitha 
    2. Tarbia
    3. Ngonjera 
    4. Ukulima.
  4. Kibwagizo cha shairi hili kina maana gani? 
    1. Mkulima ndiye atupaye uhai. 
    2. Kwa chakula cha mkulima tunaishi. 
    3. Mkulima ni mama yetu. 
    4. Mtoto wa mkulima anaitwa Uzima.
  5. Kuna uwezekano mkubwa wa mkulima kupanda mbegu msimu upi? 
    1. Kiangazi 
    2. Kipupwe
    3. Mchoo 
    4. Mafuriko. 

Jaza mapengo kwa majibu mwafaka. 

Kila mnyama ____16____meno ____17____  ya juu na ya chini. Binadamu mtu mzima huwa na meno thelathini na ___18___ .Wanyama wote wana meno ____19____ambayo ____20____sumu kali. 

   A   B    C    D 
 16.   ako na   yuko na   ana   anazo 
 17.   makali  kali   mikali   kubwa 
 18.  miwili  mbili   mawili   viwili 
 19.  mengi  nyingi   mingi   mwingi 
 20.  zina  yana   una   ina 

 

Jibu maswali kulingana na maagizo. 

  1. Maskani  ________________________ hufagiliwa.
    1. zetu
    2. mwetu
    3. petu
    4. yetu 
  2. Baba akikasirika huwa mkali kama ______________________
    1. moto
    2. pilipili
    3. simba
    4. jua
  3. Andika ukubwa wa sentensi ifuatayo. 
    Ndoo zetu zimepasuka.
    1. Mandoo zetu zimepasuka.
    2. Madoo yetu yamepasuka. 
    3. Ndoo zetu zimepasuka.
    4. Mandoo yetu yamepasuka.
  4. Tumia kiashiria sahihi. 
    Ugonjwa _____________________ ni hatari. 
    1. hiyo 
    2. ile 
    3. huo 
    4. iyo 
  5. Nilipokuwa katika ziara, niliona _____________________ ya milima.
    1. safu
    2. mabunda
    3. msafara
    4. milolongo 
  6. Baba yangu amenunua gari _____________________
    1. mpya 
    2. kipya
    3. zipya
    4. jipya.
  7. Chagua kiwakilishi cha idadi katika sentensi ifuatayo. 
    Watu wengi wana gari moja lakini wachache wana pikipiki mbili.
    1. wengi
    2. moja
    3. wachache
    4. mbili.
  8. Kati ya viwakilishi vifuatavyo, ni kipi cha nafsi ya tatu katika wingi? 
    1. Zao 
    2. Yeye 
    3. Nyinyi
    4. Wao.
  9. Tambua kivumishi katika sentensi hii.
    Mama huyo alitembea haraka akafika vizuri.
    1. mama
    2. huyo 
    3. haraka
    4. vizuri 
  10. Kipi si kiungo cha kusafisha damu?
    1. Pafu
    2. Buki
    3. Figo 
    4. Nso. 

INSHA 

Umepewa dakika 40 kuandika insha yako. 

Andika insha ya kusisimua kuhusu mada ifuatayo; 

UCHAGUZI SHULENI MWETU. 

MARKING SCHEME

  1. C
  2. D
  3. A
  4. D
  5. B
  6. C
  7. A
  8. C
  9. D
  10. A
  11. D
  12. A
  13. B
  14. B
  15. C
  16. C
  17. A
  18. C
  19. A
  20. B
  21. D
  22. C
  23. B
  24. C
  25. A
  26. D
  27. C
  28. D
  29. B
  30. A

MASWALI

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne. Chagua ibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa.

Klabu ..............1.................. Kipaumbele yaendelea kujipinda  ..............2.................. kuhakikisha kuwa tuzo  ..............3.................. msimu  ..............4.................. wa  ..............5.................. la mwadhamu Changuchetu imetwaliwa. Vijana  ..............6.................. wameapa kwa  ..............7.................. vipana kuwa wataendeleza vipaji  ..............8.................. kwa kusakata gozi kuanzia mashinani hadi kwenye ngazi za kimataifa. Kutokana na uchechefu wa ajira, ni muhimu vijana kujisakia  ..............9.................. vya kujipatia  ..............10.................. wa kila siku badala ya kungojea kuajiriwa.

  1.                      
    1. cha
    2. ya
    3. za
    4. la
  2.                  
    1. mkono
    2. kichwa
    3. mgongo
    4. mguu
  3.                
    1. iliyotengewa
    2. lilitengewa
    3. zilizotengewa
    4. yaliyotengewa
  4.                  
    1. hii
    2. hizi
    3. hiyo
    4. huu
  5.                  
    1. kikombe
    2. kombe
    3. nishani
    4. medali
  6.                  
    1. vingi
    2. wengi
    3. kwingi
    4. pengi
  7.                
    1. vinywa
    2. vidomo
    3. ndimi
    4. matamshi
  8.                
    1. chao
    2. vyao
    3. yao
    4. zao
  9.                  
    1. vitegauchumi
    2. sera
    3. nyenzo
    4. mawanda
  10.                        
    1. pato
    2. riziki
    3. mkate
    4. bahati

Tangu utotoni,  ..............11.................. nikijitenga ..............12.................. matumizi ya dawa za kulevya kwa vyovyote vile. Dawa ..............13.................. za kulevya zimedhoofisha maisha ya wengi  ..............14.................. chipukizi na larwatia kichaa, kisha kuwasafirisha  ..............15.................. Dawa zenyewe zina madhara chungu furiko kwa watumizi na wasio watumizi wa moja kwa moja.

  1.                      
    1. nilikuwa
    2. nimekuwa
    3. ningekuwa
    4. nishakuwa
  2.                    
    1. katika
    2. kwa
    3. na
    4. dhidi
  3.                  
    1. hii
    2. hiyo
    3. hizi
    4. haya
  4.                
    1. halisi
    2. hususan
    3. mahsusi
    4. hasi
  5.                    
    1. mbinguni
    2. peponi
    3. jongomeo
    4. mawinguni

Kutoka swali la 16-30, jibu swali kulingana na maagizo?

  1. Je, ni sentensi gani iliyotumia o-rejeshi tamati kwa usahihi?
    1. Mifugo -inyweshayo ndio wetu.
    2. Malango yafunguliwayo ndiyo yaliyopambwa.
    3. Watoto wanaoimba wana sauti nyororo ajabu.
    4. Sisi tusiyo na vitabu vya hadithi tusome nini?

Tumia kiunganishi bora zaidi kujazia kihasho

  1. Walijizatiti vilivyo ...................................... hawakufua dafu mbioni.
    1. lau
    2. seuze
    3. na
    4. ingawaje
  2. Ni pambo gani lililo tofauti na mengine kimatumizi?
    1. Kipini
    2. Shemere
    3. Kishaufu
    4. Kifumanzi
  3. Chagua sentensi iliyotumia "kwa" ya kimilikishi.
    1. Kushinda kwa mbunge wetu uchaguzini kulitiliwa shaka.
    2. Walisamehewa kwa kuwa walikuwa na mtetezi hodari.
    3. Tukifika kwake tutampokeza zawadi kochokocho.
    4. Mgonjwa akizidiwa mumpeleke kwa mganga.
  4. Kinyume cha: Ajuza alianika nguo asubuhi ni.
    1. Shaibu alianua nguo jioni.
    2. Ajuza alianika nguo jioni.
    3. Shaibu hakuanika nguo asubuhi.
    4. Ajuza alianua nguo asubuhi.
  5. Teua sentensi iliyoakifishwa vilivyo. 
    1. Ala! kwani unanikumbuka? 
    2. Mama we! kumbe leo ni sikukuu? 
    3. Acheni uzembe. Mkiendelea hivyo... 
    4. Njooni twende kwa kina Rosa
  6. Ni sentensi ipi iliyo sahihi kisarufi? 
    1. Mtainunua mitamba ipi?
    2. Minana waliotegwa walikuwa wangapi?
    3. Garini mlikuwa na abiria kumi na nane na dereva.
    4. Ikiwa hautanisaidia, nami pia sitakusaidia.
      Kamilisha methall ifuatayo kwa ustadi,
  7. Nguo ya kuazima
    1. matako hulia mbwata.
    2. ni kuondoka na mavi.
    3. hakistahimili kilemba. 
    4. haisitiri matako.
      Ni upi ukanusho sahihi wa sentensi ifuatayo?
  8. Mtungi ulionumuliwa umepotea. 
    1. Mtungi ulionunuliwa haujapotea.
    2. Mtungi usionunuliwa haujapotea. 
    3. Mtungi usionunuliwa hujapotea. 
    4. Mtungi usionunuliwa hujapotea.
  9. Kitenzi kutokana na nomino mfinyanzi ni
    1. ufinyanzi. 
    2. finyanzi.
    3. finyanga.
    4. finya.
  10. Ukitaka kukaza au kulegeza parafujo, unashauriwa kutumia
    1. keekee.
    2. bisibisi.
    3. nati.
    4. fuawe.
  11. "Miti hii ina matunda" kwa ukubwa ni
    1. Majiti haya yana matunda.
    2. Majiti haya yana majitunda. 
    3. Miti hii ina majitunda.
    4. Majimiti haya yana majitunda.
  12. Tegua kitendawili kifuatacho. Tandika mkeka tule kunazi.
    1. Jahazi na tanga 
    2. Ugali
    3. Mbingu na nyota
    4. Maji ya mto
  13. Chagua sentensi yenye matumizi sahihi ya "-nge".
    1. Tungelisukuma lingeenda
    2. Wangesoma wasingelianguka mtihani. 
    3. Tusingalionana tusingalisaidiana. 
    4. Ningelijua ningelijitahidi.
  14. Bingwa wa kufua vyuma huitwa
    1. dobi.
    2. sonara.
    3. mjumu.
    4. mhunzi.

Soma kifungu kisha ujibu maswall 31-40.

Waja huwa na akili razini na tambuzi ya kukabiliana mkabala na matatizo yao lakini utekelezaji ndio huwa changamoto. Hebu tuangalie kuhusu ajali barabarani. Baada ya kugundua chanzo cha ajali, hatua muhimu zilichukuliwa. Vidhibitimwendo viliwekwa ili kuzuia magari yasiende kasi zaidi. Alikanda ya usalama ilikuwa na jukumu ili pakitokea ajali, abiria wasirushwe nje kupitia viooni na madereva kupewa vibali vinavyoonyesha kuwa wao ni raia wema ili mshikausukani asiwe ni jambazi anayetafutwa na polisi. Hayo yote ni mema. Lakini ajali zimeisha au bado watu wanaangamia barabarani? Tatizo lipo wapi?

Nilifanya utafiti na kugundua penye tatizo. Nimegundua kuwa matatizo yangalipo, nayoni nyeti. Kubwa mno likiwa jangamizi la uzungukaji wa mbuyu. Kupokea rushwa kwa maafisa wa usalama kunachangia sana. Wahudumu wengi hubeba abiria wengi kupita kiasi na kuwahonga maafisa ili wasitiwe nguvuni. Kwa sababu hiyo abiria wengi hawawezi kufunga mikanda ya usalama. Ajali inapotokea watu wengi huangukiana kwa sababu ya kusongamana.

Kuna wale waliovitoa vidhibitimwendo na magari yao huenda kwa kasi sana. Wakati mwingine wenye magari huwafanyisha kazi kwa muda mrefu madereva na wasaidizi wao. Hilo niligundua siku moja ambapo nilikarwa nikisafiri kwa basi. Niliketi karibu na dereva na kujionea vituko ambavyo siwezi kusahau. Gari lilikuwa likienda kwa kasi ungedhani lingepaa. Niliingiwa na wasiwasi mpaka nikaamua kumsaili dereva.

"Mbona unaendesha gari hivyo?" Hakunijibu.

"Huoni kuwa unayahatarisha maisha yetu?"

"Unataka nikupishe uendeshe gari? Sitaki kufunzwa kazi. Unadhani maisha yako pekee ndiyo yaliyo humu garini? Mimi nina haki ya kuenda kwa kasi. Nilitoka Mombasa usiku. Sikulala. Nilifika Nairobi alfajiri na ba do ninarudi Mombasa mapema angaa nilale."

Sikuwa na la kujibu. Mshale wa kasi ulikuwa umelalia mia moja na arubaini. Sikuongea neno. Tulipofika Mtito Andei, nilishuka. Sikuliabiri gari hilo tena. Niliamua heri kupoteza pesa kuliko kupoteza maisha, uhi niuthaminio. Nilijipa moyo kwa kusema "kwa mwoga huenda kicheko". Nililiacha likaenda na kuliahiri jingine. Tulipofika Manyani, tuliwakuta watu wakilia kando ya barabara na kuomba msaada. Basi lilikuwa msituni. Tulisimama na kuwasaidia majeruhi. Wengi walikuwa wamekufa. Nilipashwa habari kuwa dereva alisinzia na kupoteza mwelekeo.

Tunapaswa kushirikiana sote kama tunataka kukabiliana na matatizo kama vile ajali barabarani. Hata kama tunajua kuwa ajali haina kinga, ajali haitokei yenyewe bali husababishwa na binadamu.

  1. Tatizo kubwa la binadamu ni lipi? 
    1. Kutekeleza mawazo mazuri waliyo nayo.
    2. Kuwa na mawazo mazuri ambayo yanaweza kutatua matatizo waliyo nayo. 
    3. Kujua chanzo cha matatizo ambayo yanawakabili katika nyanja mbalimbali. 
    4. Kutotekeleza mawazo mema waliyo nayo.
  2. Kazi ya vidhibitimwendo ni
    1. kufanya magari yasiende.
    2. kuhakikisha kuwa magari yanaenda kwa mwendo uliokubalika.
    3. kufanya magari yaende polepole ili ajali isitokee.
    4. kuzuia ajali isitokee wakati wowote..
  3. Kwa nini madereva hupewa vibali vya uraia mwema?
    1. Ili waendeshe magari kwa ustadi mkubwa 
    2. Kuhakikisha kuwa si wahalifu wanaojificha katika udereva.
    3. Kuhakikisha kuwa gari lina vidhibitimwendo na mikanda ya usalama.
    4. Ili kumzuia dereva asiendeshe gari bila kuzingatia sheria.
  4. Kutoa au kupokea rushwa kunachangia vipi kwa kuongezeka kwa ajali?
    1. Askari wanawaruhusu madereva kuendesha magari kwa kasi maana hawawaangalii.
    2. Idadi ya wanaonusurika ajalini huongezeka maradufu.
    3. Maafisa na madereva wengi hupoteza ajira zao.
    4. Sheria za barabarani huvunjwa ovyoovyo
  5. Kulingana na taarifa hii, ni nini kinachoshababisha ajali nyingi za barabarani?
    1. Ubebaji wa abiria kupita kiasi. 
    2. Magari kuendeshwa kwa kasi mno.
    3. Madereva walevi na barabara mbovu. 
    4. Magari kupasuka magurudumu.
  6. Wenye magari wanaweza kufanya nini ili kupunguza ajali barabarani?
    1. Kuwaamuru madereva na wasaidizi wao kuzunguka mbuyu.
    2. Kuwaajiri madereva wakongwe wenye ujuzi kuliko vijana.
    3. Kuwawekea mipaka nafuu ya nyakati za utendakazi wafanyakazi wao.
    4. Kununua magari mengi ili abiria wasihangaike.
  7. Kulingana na jinsi dereva alivyomjibu mwandishi, ni wazi kuwa
    1. alikuwa na hasira kwa sababu ya kufanya kazi kwa muda mrefu.
    2. aligundua kuwa mwandishi hakujua kuendesha gari.
    3. alikuwa na tabia ya ujeuri na ufidhuli. 
    4. mwandishi hakuwa na haki ya kuuliza lolote.
  8. Ni kweli kusema gari la kwanza alilosafiria mwandishi
    1. liliwabeba abiria wengi waliobanana kama ndizi.
    2. halikuwa na kidhibitimwendo.
    3. liliendeshwa na dereva mlevi.
    4. liliwafikisha abiria salama.
  9. Aya ya mwisho yaenda sambamba na methali ipi hapa?
    1. Mkono mmoja hauchinji ng'ombe.
    2. Ajali haina kinga wala kafara.
    3. Zinguo la mtukutu ni ufito.
    4. Heri kufa kuliko kufariki.
  10. Kichwa bora zaidi cha habari hii ni
    1. Kwa mwoga huenda kicheko, kwa shujaa kilio.
    2. Ajali barabarani.
    3. Jinsi ya kuzuia ajali barabarani 
    4. Siku njema huonekana asubuhi.

Soma kifungu kisha ujibu maswali41-50.

Msonge ni nyumba ya mviringo yenye paa lenye umbo la pia. Zamani wenyeji walikuwa wakijenga nyumba za namna hii. Kitu kikubwa cha kushangaza juu ya nyumba hizi ni kuwa zina sehemu tumbi nzima.

Ukianzia chini ya nyumba hizo utakuta msingi. Hapa wenyeji walikuwa wakichimba chini na kupatandaza vizuri kwa kupapigilia kwa kutumia vijiti maalumu. Baadhi ya makabila yalivihifadhi vijiti hivyo ili kutumiwa kwa ujenzi mwingine. Sehemu hizo zimalizikapo, huwa sakafu za nyumba hizo.

Ukienda juu kidogo kuna ukuta. Ukuta huu ulijengwa kwa kusimamishwa nguzo katika mviringo kufuatana na sakafu na kukingamana na boriti zilizosimamishwa. Baada ya hapo udongo ulikandikwa katikati ili kukamilisha ukuta. Ukuta wa nyumba ya msonge ulikuwa na sehemu mbili. Sehemu ya chini iliitwa kiuno cha nyumba nayo sehemu ya juu haikuwa na jina lakini haikuwekewa mawe kama kiuno cha nyumba.

Ulipojengwa ukuta, uliwekwa mti wa juu kabisa ambao kazi yake ni kushikilia paa. Mti huu huitwa kombamoyo au mtambaapanya. Mbali na kuwa na mtambaapanya, pia ukuta huo uliwekewa vizingiti vya milango na madirisha na hatimaye milango yenyewe na madirisha.

Hatua ya mwisho katika ukuta ilikuwa ni kuusiriba. Ukuta huo ulitupiwa udongo uliokuwa umekanyagwakanyagwa na kulainishwa kwa mikono au mwiko maalumu ili kuufanya upendeze.

Katikati ya ukuta na paa, lilijengwa dari. Zilichukuliwa boriti upande hadi upande. Boriti hizo zilifungwa fito pia. Baada ya kufungiwa fito nyingi sana dari hilo lilikandikwa na haikuachwa nafasi ya kupanda juu kama madari ya kizungu. Hii ni kwa sababu hakuna kitu chochote kilichowekwa juu. Sehemu iliyowekewa kitu chochote ilikuwa uchaga. Uchaga ulikuwa sehemu ya mekoni ambako kuliwekwa kuni. Sehemu hiyo ilijengwa juu ya meko ili kupika kufanyiwe chini na kuni ziwekwe juu. Hii ilikuwa kwa sababu wakati wa masika, ilikuwa shida kwenda kuchanja kuni kwa sababu ya kuloa maji ya mvua.

Sehemu ya juu kabisa ya msonge kulikuwa na paa. Ujenzi wa paa ulihitaji fundi kuliunda na kuliczeka. Paa lililojengwa kivoloya halikudumu kwa muda mrefu maana liliharibiwa na mvua na upepo baada ya siku chache.

Katika ujenzi wa paa, yalihitajika mapau ambayo yaliwekewa fito pia. Fito hizo zilifungwa kwa kamba maalumu. Baada ya kufungwa fito, paa liliezekwa na fundi. Uczekaji ulianzia chini kuelekea juu hadi kilele cha mlingoti. Hapa kumbuka kuwa ule mlingoti ulisimamishwa kutoka katikati ya sakafu hadi katikati ya paa. Fundi wa kuezeka alitakiwa kuwa na ujuzi wa kukanyaga sehemu alizoezeka bila kuzitia dosari. Pili, paa lilitakiwa lisivuje kabisa na mwisho kabisa, lilihitajika likae hivyo hivyo miaka nenda miaka rudi bila kuezekwaezekwa mara nyingi.

Kuna nyasi za aina nyingi zilizotumiwa kuezeka. Sehemu za pwani, makuti yalitumika zaidi na bara zilitumika nyasi tofautitofauti. Kilichofanya nyasi hizo kuwa sawa sawa ni kuwa wenyewe walizichagua kwa makini. Zilihitajika kuwa nyasi ambazo hazikuchakaa haraka na zilizopatikana kwa urahisi.

Baada ya paa kuisha, fundi aliweka namna ya kofia kileleni. Lilichukuliwa bonge la udongo na kukatwa katika mviringo mzuri. Kwisha yote hayo, kijiti chenye ncha ndefu kiliwekwa kileleni na kupitishiwa lile bonge ili likae pale pale sawa sawa. Ujenzi huo ulikuwa wa kuzuia mvua isiingie ndani kupitia kileleni.

Ndani ya nyumba hamkuwa na vyumba lakini ilipobidi nyumba hizo ziligawanyika sehemu mbili tu. Yaani sebule na sehemu ya kulala.

  1. Nyumba ya msonge iligawanywa katika sehemu mbili, nazo ni
    1. sebule na jikoni.
    2. jikoni na sehemu ya kulala. 
    3. sehemu ya kulala na sebule. 
    4. uchaga na sakafu.
  2. Ni kitu gani kilichostaajibisha kuhusu msonge?
    1. Ustadi uliotumika katika kuujenga.
    2. Umbo la pia katika paa na sakafu ya mviringo.
    3. Vyumba mbalimbali vilivyopatikana katika msonge.
    4. Sehemu nyingi zilizokuwa katika nyumba hii.
  3. Ni kweli kusema kuwa:-
    1. sakafu ya nyumba ilichimbwa, kutandazwa kisha ikapigiliwa
    2. vijiti vilivyotumiwa kupigilia sakafu vilihifadhiwa na makabila yote
    3. vijiti maalumu vilichimbiwa chini vikawa sakafu
    4. ujenzi wa sakafu ulikuwa na hatua mbili zilizofuatwa.
  4. Hatua ya mwisho katika ujenzi wa kiambaza ilikuwa gani?
    1. Kusimamisha nguzo katika mviringo kulingana na sakafu.
    2. Kufungwa kwa fito nje na ndani.
    3. Kukandikwa kwa udongo katikati ya fito. 
    4. Kukisiriba kwa udongo laini.
  5. Ni nini kilichotumika kuufanya ukuta wa msonge kuwa imara na kushikilia paa? 
    1. Kuwekwa kwa mtambaapanya katika kombamoyo
    2. Kwa kuweka bonge la udongo katika mviringo
    3. Kwa kuweka kijiti chenye ncha ndefu 
    4. Kuwekwa kwa mtambaapanya
  6. Ni gani ni tofauti kuu ya dari la msonge na lile la kisasa?
    1. Dari la msonge ilikandikwa kwa udongo. 
    2. Dari la msonge huwa na uchaga. 
    3. Dari la kisasa huachiwa nafasi ya kupandia juu.
    4. Dari la kisasa huhifadhiwa kuni.
  7. Fundi wa ujenzi wa paa alionyesha ujuzi wake katika yafuatayo isipokuwa
    1. kujenga paa lililodumu kwa muda mrefu.
    2. kukanyaga sehemu zilizoezekwa bila kuzitia dosari.
    3. kuczeka paa lisilovuja.
    4. kuezeka paa lililoonekana maridadi.
  8. Ni wazo lipi ambalo ni sahihi kuhusu paa?
    1. Mapaa yote ya msonge yaliezekwa kwa makuti.
    2. Mapaa yote ya msonge yaliezekwa kwa nyasi pekee.
    3. Nyasi zilizopatikana kwa urahisi katika eneo fulani ndizo zilizotumika kuezekea mapaa.
    4. Nyasi zozote zingetumika kuezekea mapaa. 
  9. Mvua ilizuiliwaje isiingie ndani kupitia kileleni?
    1. Kwa kutumia bonge la udongo lililokatwa katika mviringo mzuri.
    2. Kwa kuezekwa nyasi ambazo hazikuchakaa kwa urahisi.
    3. Kwa kupitishia kijiti kirefu chenye ncha ndefu kilichopitishwa katika bonge la udongo kuliweka sawa sawa.
    4. Kwa kukanyaga kwa makini sehemu hiyo yenye bonge na kijiti kirefu.
  10. Ni kichwa kipi kifaacho zaidi taarifa hii?
    1. Msonge.
    2. Fundi wa kujenga msonge.
    3. Ujenzi wa nyumba za kale.
    4. Ujenzi wa msonge.

INSHA

Umepewa dakika 40 kuandika insha yako. Andika insha ya kusisimua ukiamalizia kwa maneno haya:

....................................................................................................Tangu siku hiyo, wanafunzi wote wa darasa letu waliamini kuwa hakuna mafanikio yanayoweza kupatikana bila bidii.

MWONGOZO

swa adad

 

MASWALI

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi, umepewa majibu manne. Chagua jibu lifaalo zaidi kati ya yale uliyopewa.

Wahenga na wahenguzi hawakukanyaga chechele walipolonga kuwa Mungu ...................1.................. Ama kwa ....................2.................. Mungu si mtovu. Yeyote anayemwamini atajibiwa ...................3.................. yake. Mara nyingi tumewasikia watu akitoa ...................4.................. kuhusu nasaha waliyokwisha kupokea kutoka kwa wajuzi wa nyanja mbalimbali. Ukweli ni kwamba, wenye ...................5.................. ,wote huishia kubarikiwa. Yote tuyafanyayo bila kumtegemea Rabuka huwa ni kazi  ...................6..................  hata ingawa tutatia bidii ya mchwa.

  1.                          
    1. hamwachi mja wake
    2. huwabariki waja wake
    3. hawaachi waja wao
    4. humwacha mja wake
  2.                          
    1. yamkini
    2. lakini
    3. yakini
    4. makini
  3.                
    1. ombi
    2. dau
    3. doa
    4. dua
  4.                
    1. ushahidi
    2. shahidi
    3. ushuhuda
    4. shahada
  5.                  
    1. amani
    2. amana
    3. dhamana.
    4. imani
  6.                  
    1. bure bilashi
    2. kuntu kabisa
    3. nzuri zaidi
    4. nyingi mno

Siku ..............7..................., sote tulibakia uwanjani huku tukicheza mchezo wa ..............8.................. yaani kibe. Mara tulimwona akiwa amesimama mlangoni. Mmoja wetu alitudokezea tukakimbia, tukaingia darasani na ..............9.................. Tulijua kuwa mambo yalikuwa ..............10.................. Tulingojea huku tukiwa na huzuni ..............11.................. sisemi wasiwasi. ..............12.................. kuhusu makosa yetu na ..............13.................. kuwa tulikuwa tumemkosea mwalimu wetu. Mdarisi alipoingia tulisimama tisti na kumwomba msamaha. Mwalimu alifurahi na kutufunza ..............14.................. badala ya kipindi cha Kiswahili alichokiandaa. Alitukumbusha kuwa heshima ..............15..................

  1.                            
    1. hilo
    2. hio
    3. hizo
    4. hiyo
  2.                
    1. kukimbizana na kuangushana
    2. kuiga na kuigiza majukumu ya wazazi nyumbani
    3. watoto wa kujificha na kutafutana
    4. kuvuta kamba kwa kushindania
  3.                      
    1. kukimya
    2. kunyamazana
    3. kunyamaza
    4. kuropokwa
  4.                  
    1. yamezidi unga
    2. yametumbukia nyongo
    3. yametengenea sana
    4. yameimarika zaidi
  5.                      
    1. mwingi
    2. mingi
    3. wingi
    4. nyingi
  6.                        
    1. Tulichunguzwa
    2. Tulikumbuka
    3. Tulitafakari
    4. Tulisahau
  7.                
    1. kukiri
    2. kukana
    3. kukanusha
    4. kukataa
  8.                  
    1. maadili
    2. madili
    3. adhabu
    4. utundu
  9.                      
    1. utumwa
    2. haidumu kamwe
    3. si utumwa
    4. inadumu daima.

Kuanzia swali la 16 hadi la 30. jibu kulingana na maagizo.

  1. Maneno yafuatayo yatapangwaje katika kamusi?
    1. Pasa
    2. Paka
    3. Pakua
    4. Paku
      1. ii, iv, iii, i
      2. i, iii, iv, ii
      3. iii, i, ii, iv.
      4. iv, ii, iii, i
  2. Kamilisha sentensi ifuatayo kwa maneno yafaayo.
    ___wake amemnunulia___ ____ nguvu _____
    1. Mzazi, fahali, enye, malindandi
    2. Msasi, fahari, mwenye, malidandi
    3. Mzazi, fahali, mwenye, maridadi
    4. Mzazi, fahari, enye, maridadi
  3. Chagua wingi wa sentensi ifuatayo.
    Hakuelewa kuwa ningechelewa.
    1. Hawakuelewa kuwa tungechelewa
    2. Hamkuelewa kuwa tungechelewa.
    3. Hamkuelewa kuwa ningechelewa.
    4. Hawakuelewa kuwa ningechelewa.
  4. Tambua sentensi sanifu inayolinganisha hizi.
    Utubora alifaulu.
    Utubora hakufurahi.
    1. Lau Utubora alifaulu hakufurahi.
    2. Utubora hakufurahi aghalabu alifaulu.
    3. Utubora hakufurahi licha ya kufaulu.
    4. Maadamu Utubora hakufurahi alifaulu.
  5. 3051660 kwa maneno ni
    1. Milioni tatu, laki hamsini na moja mia sita sitini
    2. Milioni tatu elfu hamsini na moja mia sita na sita
    3. Milioni tatu hamsini na moja elfu, mia sita na sitini
    4. Milioni tatu hamsini elfu na moja mia sita na tisini
  6. Ni nini maana ya 'kutia masikio nta"?
    1. Kutojali yasemwayo.
    2. Kujali yasemwayo.
    3. Kuweka masikio vipuli.
    4. Kutia masikio pamba.
  7. Mwasaru alinipigia simu, nami nikampigia simu. Kwa hivyo sote wawili ...............................
    1. tulipigiana pigiana simu
    2. tulipigiwa simu
    3. tulipigana simu
    4. tulipigiana simu
  8. Ni methali gani iliyo na maana sawa na
    "polepole ndio mwendo"?
    1. Chelewa chelewa utapata mwana si wako.
    2. Haraka haraka haina baraka.
    3. Chovya chovya humaliza buyu la asali.
    4. Heri kenda kuliko kumi nenda rudi.
  9. Ni sentensi gani iliyo na kivumishi cha pekee?
    1. Kusafiri kwa gari moshi ni kuzuri
    2. Chakula hiki ni kitamu sana.
    3. Ukucha wangu umekatika.
    4. Nyumba yote iliteketea moto.
  10. Chagua ukubwa wa sentensi hii
    Gari hili zuri, lina dirisha kubwa na mlango wa kupendeza.
    1. Kigari hiki ni kizuri, kina kijidirisha kikubwa na kijilango cha kupendeza.
    2. Jigari hili ni zuri, lina jidirisha kubwa na lango la kupendeza.
    3. Jigari hili ni mzuri, lina dirisha kubwa na lango la kupendeza.
    4. Ligari hili ni zuri, lina dirisha kubwa na lango la kupendeza.
  11. Fuma ni kusuka nyusi. Vile vile fuma ni
    1. kudunga kwa kifaa chenye makali.
    2. kudunga kwa mtutu wa bunduki. 
    3. kushona nguo paliporaruka.
    4. kupachika nguo kiraka kipya.
  12. Umbo lifuatalo ni
    27 asdadada
    1. Mstari sulubu
    2. Pembe butu
    3. Pembe kali
    4. Pembe nyoofu
  13. Chagua sentensi inayoonyesha 'jl' ya nafsi.
    1. Uimbaji wake uliwatumbuiza wageni. 
    2. Jibwa limefungiwa chumbani. 
    3. Msomaji wa taarifa alisikika vizuri.
    4. Nilijisomea Riwaya ya Siku Njema.
  14. Ikiwa mtondogoo itakuwa Jumamosi Machi tarehe mbili 2023, jana ilikuwa lini?
    1. Jumatatu Februari tarehe ishirini na tatu
    2. Jumatatu Februari tarehe ishirini na saba.
    3. Jumatatu Februari tarehe ishirini na sita.
    4. Jumatatu Februari tarehe ishirini na tano.
  15. Mzee Weru ameishi miaka mingi sana. Yaani
    1. amekula siku zake
    2. ameona mambo mengi
    3. amekula tarehe
    4. amekula chumvi nyingi

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31-40

Waswahili husema kuwa safari ya kesho hupangwa leo. Waaidha, msafiri ni aliye bandarini. Mwanadamu anatakiwa awe na mpango madhubuti wakati anapohitaji kufanya jambo lolote; liwe jambo dogo au kubwa. Kimsingi ni kwamba, mtu hawezi akafyeka kichaka akalima, akapanda, akapalilia na kufaidi matunda kwa siku moja. Ni sharti mtu kujua kwamba mambo hutayarishwa hatua kwa hatua na kupatiwa muda ili yatengence.

Mtahiniwa yeyote anafaa kujiandaa barabara wakati ambapo anaungojea mtihani

wowote. Mtu hupata kufahamu wakati wa mtihani mapema zaidi. Kwa hivyo si vyema hata kidogo mtu kungojea hadi siku ya siku kuwa pua karibu na mdomo illi aweze kuanza kujiandaa. Mwanzo kabisa, ni sharti awe na ratiba yake binafsi. Ratiba huwa kama dira na rubani. Rubani anapokosa dira bila shaka atasalia pale hewani na wala hataweza kutua hata kidogo. Hivyo ndivyo ilivyo kwa mwanafunzi pia. Hakuna vile unaweza kuketi tu na kuchomoa kitabu na kuanza kusoma. Mwanafunzi anapofanya hivyo atajipata kuwa amesoma masomo anayoyapenda huku akiyasahau yale ambayo yanampa changamoto.

Mtahiniwa anapodurusu, afanye udadisi wa kutosha. Asichukue vitabu tu bila kufahamu kinachohitajika ili kujiandaa vyema ni lazima asome mwanzo akili ya mtahini. Atafanya hivi kwa kutazama karatasi zilizofanywa awali. Hili litamsaidia kusoma tu yale muhimu kwa mujibu wa kuupasi mtihani huo. Mtu anaposomasoma kila kitu hata kisichomhusu atamalizia kuyajua mambo mengi zaidi ambayo hayamhusu ndewe wala sikio. Huu ndio unaoitwa ukasuku katika kusoma. Hebu nikuulize, je, mwanafunzi anaweza kufaulu kwa kusoma magazeti tokea asubuhi hadi jioni? Hapo nafikiri hatafua dafu mtihanini.

Aidha, mwanafunzi anashauriwa kuwa pahali pake pa kusomea pasiwe karakana. Yaani pasiwe na kelele wala vitu vinavyoweza kumchachawiza msomaji akaacha kusoma. Ijapokuwa wengine hupenda kudurusu huku wakisikiliza muziki, ni bora kuwe kutulivu na shwari kwa uelewa aula. Vile vile, sehemu hiyo iwe na hewa safi; madirisha yafunguliwe, pasiwe baridi sana au joto kupita kiasi. Licha ya hayo, aandae vifaa vyake mapema, mathalan meza, kiti, vitabu, kallamu, karatasi na vingine vingi vinavyohitajika. Fauka ya hayo, awe na saa ili aweze kuyapatia masomo yake wakati maalum.

Kusoma pia kuna mipaka. Mwanafunzi asijilazimishe na kujipagaza bure hasa anapoona kwamba anasinzia. Inafaa ajipumzishe kidogo au atembee kidogo ili kupata hewa safi, halafu arudie kusoma. Ikiwa ni usiku, anaweza hata akaenda kulala ili aamke alfajiri kuendelea na masomo wakati hana chelewa ya usingizi. Ifahamike kwamba binadamu anapaswa angalau kulala muda wa saa sita na saa nane ili akili na mwili viweze kufanya kazi vyema. Pia, anaposoma, ahakikishe kwamba hana njaa wala kushiba sana kupita kiasi.

Wakati wa mtihani, mtahiniwa anafaa kuamka mapema kama kawaida. Afike darasani kabla ya muda rasmi wa kuanza mtihani. Apatiwapo karatasi ya maswali, asome maagizo kwa makini na ayaclewe vizuri kabla ya kuanza kujibu maswali. Kufuata maagizo aliyopewa pia ni sehemu ya mtihani. Asilimia kubwa ya watahiniwa hufeli mtihani kwa kuyapuuza maagizo yaliyotolewa. Kumbuka kuwa mtu hutungiwa mtihani, hajitungii mwenyewe.

  1. Mwandishi anazingatia nini katika aya ya kwanza?
    1. Mtu akifanya maandalizi vyema anaweza kuvuna siku hiyo hiyo
    2. Hakuna haja ya kuyafanya mambo hatua kwa hatua ila kwa mkupuo
    3. Ili jambo lolote kufanikiwa linahitaji kupewa subira
    4. Wakulima ndio watu wanaotakikana kuwa na subira
  2. "...akafyeka kichaka, akalima, akapanda, akapalilia..." 'ka' imetumikaje katika muktadha huu?
    1. Mfululizo wa matukio
    2. Kuradidi kwa matukio
    3. Usisitizo wa matukio
    4. Mkururo wa matukio
  3. Ratiba kwa mwanafunzi imemithilishwa na
    1. ndege kwa rubani
    2. mwanafunzi na bidii
    3. mtahiniwa na mtihani
    4. dira kwa rubani
  4. Mwanafunzi anayesomasoma tu bila kuwa na ratiba hutokewa na nini?
    1. Kufeli katika mitihani yake kila mara
    2. Kuyasoma masomo anayoyahenzi pekee
    3. Kuyadurusu hata yale masomo asiyoyapenda
    4. Hujiandaa barabara dhidi ya mitihani ijayo
  5. 'Ukasuku katika kusoma unamaanisha nini kulingana na mwandishi?
    1. Kusomasoma mambo mengi ambayo hayakuhusu
    2. Kusomasoma kwa kukariri tu bila kuelewa
    3. Kusoma jinsi kasuku anavyosoma
    4. Kusoma na kuropokwa kwa kuiga kasuku
  6. Ni kwa nini mwanafunzi anafaa kusomea mahali patulivu?
    1. Ili aweze kuwa na vitu vinavyohitajika
    2. Kuna wengine wanaopenda kusoma huku muziki ukidunda
    3. Ili yanayosomwa yaweze kueleweka bila shida yoyote
    4. Kwa kuwa muziki hautahiniwi katika mtihani wowote
  7. Mwanafunzi anayesoma tu somo moja kila wakati hatimaye
    1. hupita vizuri mitihani yake
    2. hujiburudisha
    3. huchoka akili
    4. hafaulu mtihani wake
  8. Ni mambo gani mwanafunzi hafai kufanya anapodurusu ili kujiandaa kufanya mtihani? 
    1. Asome mchana na usiku bila kupumzika 
    2. Ale lakini asishibe kupita kiasi
    3. Asisome huku akiwa na chelewa ya usingizi
    4. Asiendelee kusoma iwapo anahisi uchovu
  9. Mwanafunzi anapofanya mtihani bila kusoma na kufuata maagizo ni sawa na
    1. anayefanya mtihani akipanga kufeli
    2. anayejitahini na kuyajibu maswali yake mwenyewe
    3. wanafunzi wale werevu wanaoanguka mtihani
    4. anayechelewa kufika kwenye chumba cha mtihani
  10. Baadhi ya wanafunzi waliojiandaa vyema hufeli mtihani kwa
    1. kufanya mtihani pasi kusoma maagizo
    2. kufanya mtihani palipo na kelele nyingi
    3. kuanza kujibu maswali pasi kusoma na kuelewa maagizo
    4. kufanya asilimia kubwa ya maswali kwa papara 

Soma habari inayofuata kisha ujibu maswali 41-50

Nilikuwa nimeungojea wakati huo kwa hamu na ghamu. Japo niliona kuwa siku hiyo ilikuwa mbali, hauchi hauchi unakucha, hatimaye iliwadia. Mwalimu wetu alikuwa anasisitiza kuwa achanikaye kwenye mpini hafi njaa; waaidha, mchumia juani hulia kivulini. Wahaka usio na kifani ulinivaa kwani nilifahamu kuwa ni vyema kujiandaa mapema ili niende kupokea Hidaya yangu. Furaha mpwitompwito ilinivaa kwelikweli.

Niliondoka kitandani huku nikiimba nyimbo za furaha. Nilijua kuwa safari yangu ingechukua takriban saa tatu unusu. Tayari ilikuwa saa thenashara na sherehe ingeanza mida ya saa nane. Kwa pupa nilivalia sare zangu za shule yangu ya awali. Mwalimu mkuu ambaye angeandamana nami alikuwa amenishauri niweze kuvalia sare hizo. Hafla hiyo yote ingeonekana kwenye televisheni zote nchini. Alikuwa akitaka sare hiyo ipate kunadi shule yake ambayo ilikuwa haijatia fora kwa mwongo mmoja mtawalia. "Shule ya upili ya Busara itatambuliwa leo na dunia nzima," nilijisemea kimoyomoyo. Niliwaza na kuwazua kuhusu maisha ya chuo.

Baada ya kujiandaa, niliharakisha kufika katika kituo cha mabasi. Inshallah, nipate basi bado halijaondoka. Mwalimu mkuu alikuwa tayari amekata nauli ya watu wawili. Basi lenyewe lilikuwa jipya. Mlikuwa na abiria wengi ambao walikuwa wameabiri. Basini mlikuwa na viti vinne ambavyo havikuwa na abiria. Mwalimu aliniambia kuwa twende kutafuta staftahi. Tuliandamana naye kuelekea kwenye mkahawa tukanywa chai kwa mahamri. Japo mwalimu alitaka tunywe kwa haraka, chai ile ilikuwa moto ajabu. Hata hivyo, tulijikaza tukaimaliza. Tulirudi kituoni huku tukihema na kutweta. Tulifahamishwa kuwa basi lilikuwa limeondoka. Kwa hivyo ilitulazimu kusubiri saa moja kabla ya basi jingine kufika. Nilitekwa na hisia za huzuni lakini nikajizuia kulia. Hapo ndipo nilianza kusinzia na kukumbuka maisha yangu yalivyokuwa.

Nilikuwa nimezaliwa katika familia ya ukata. Mazingira niliyokulia yalikuwa yenye matatizo chungu nzima. Haya ndiyo yaliyonifanya kusoma kwa bidii ili niinusuru familia yetu kutokana na uchochole. Nilipopelekwa katika shule ya msingi nilitia fora masomoni nikaweza kujiunga na shule ya sekondari ya kutwa pale karibu na kwetu. Kupitia wadhamini wenye ukarimu si haba niliweza kukamilisha masomo yangu na kupata alama ya A iliyonipa hadhi niliyokuwa nayo.

Mawazo yangu yalikatizwa na milio ya hofu. Mwalimu wangu aliniashiria kitu. Nilipotazama upande wangu wa kulia niliona basi ambalo nilikuwa nikilisubiri likigongana na lori la takataka. Niliharakisha kwenda kuwasaidia watu waliokuwa wamejeruhiwa. Kwa nyota ya jaha, wote walikuwa salama salimini. Lakini tatizo la usafiri likatokea tena. Basi hilo lilihitajika kukarabatiwa tena kabla ya kuendelea na safari. Pasipo budi hubidi.

Punde si punde, simu ya mwalimu ilitoa mlio. Alitazama kidogo kisha akaanza kutetemeka kama aliyetoka kwenye friji. "Wamepiga simu" alisema. Aliichukua, akazungumza nayo kisha nikaona akitabasamu. Baada ya kumaliza, alinifahamisha kuwa sherehe ile ilihairishwa hadi wiki ambayo ingefuata. Nilifurahia sana kwa kuwa nilikuwa nimekata tamaa-muda wetu ulikuwa umekwisha. Tuliamua kurudi nyumbani japo tulikuwa tumechoka hoi bin tiki.

  1.  Ni kwa nini mwandishi wa makala haya alikuwa na furaha?
    1. Siku yenyewe ilikuwa imengojewa kwa hamu na ghamu
    2. Jitihada zake masomoni zingetambuliwa siku hiyo
    3. Alikuwa ametuzwa kwa bidii zake
    4. Maisha yake yangebadilika siku hiyo
  2. Kulingana na aya ya pili ni kweli kusema kuwa
    1. mwandishi alikuwa amefaulu katika mtihani wa shule ya msingi
    2. shule ya Busara ilikuwa na utamaduni wa kung'aa mtihanini
    3. mwandishi hakutarajiwa kuvalia sare ya shule ya awali
    4. hafla hiyo ilitarajiwa kuonyeshwa kwenye televisheni za kitaifa
  3. Msimulizi alivalia sare
    1. kwa kuwa alinuia kuitumia kunadi umaarufu mpya wa shule hiyo
    2. alikuwa amefanya vizuri katika mtihani uliotangulia
    3. kwa kuwa alikuwa na furaha mpwitompwito
    4. kwa kuwa walikuwa waandamane na mwalimu mkuu
  4. Mwandishi wa makala haya alitarajiwa kufika shereheni saa ngapi?
    1. Saa thenashara
    2. Saa nane mchana
    3. Saa saba za asubuhi
    4. Saa kumi na mbili
  5. Lengo la kujitahidi masomoni ilikuwa 
    1. kuinua hali ya jamii aliyoishi
    2. kujipatia shahada na kazi bora 
    3. kuimarisha hali ya jamaa yake
    4. kupata tunu maridhawa
  6. Kuachwa na basi kwa mwandishi
    1. kulimkumbusha shida alizokulia kijijini
    2. kulimfanya akate tamaa kuhusu zawadi yake
    3. kulimfanya aende kutafuta staftahi
    4. kulimfanya afanye bidii masomoni
  7. Taarifa hii inatoa sifa gani kwa mwandishi wa makala haya?
    1. Mkakamavu, mwenye moyo mwepesi
    2. Mkakamavu, mwenye moyo thabiti
    3. Mchochole, mwenye moyo thabiti
    4. Mlegevu, mwenye mori kubwa
  8. Tunajifunza nini kuhusiana na maisha ya mwandishi?
    1. Mafanikio hupatikana tu wadhamini wakijitolea
    2. Wanaojiunga na shule za kutwa hujiunga na vyuo vikuu
    3. Wenye elimu ya juu hupata tunu masomoni
    4. Mafanikio huweza kupatikana hata na walio na uwezo duni wa kifedha
  9. Mwandishi alitabasamu katika aya ya mwisho kwa kuwa
    1. alikuwa na nafasi nyingine ya kuhudhuria sherehe
    2. alimwona mwalimu wake akitabasamu
    3. aliruhusiwa kurudi nyumbani baada ya kuchoka
    4. hakuna mtu aliyejeruhiwa katika ajali iliyotendeka
  10. "... kutetemeka kama aliyetoka kwenye friji." Ni tamathali gani ya lugha iliyotumiwa kwenye kifungu hiki?
    1. Methali
    2. Istiari
    3. Tashbihi
    4. Msemo

INSHA

Andika insha ya kusisimua isiyopungua ukurasa mmoja na nusu huku ukimalizia kwa kifungu kifuatacho:-

....................................................................................... nilifurahishwa na tabia ya utu wema wa rafiki yangu.

MWONGOZO

swa ms 

Tagged under

MASWALI

Soma vifungu vifuatavyo. Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila nafasi umepewa majibu manne hapo. Jaza kila pengo kwa kuchagua Jawabu lifaalo zaidi.

Ni muhimu kwa mtu kujaribu kadri ...............1................kuwa na uhusiano....................2......................na wenzake popote alipo. Hata akipatwa na shida, ajue kuwa  ....................3.....................  ....................4..................... jamaa zake ....................5..................... watakaomfaa ....................6.....................  wale walio karibu naye. Jambo la ajabu ni kuwa watu wengi ....................7..................... na wenzao lakini hujipata wakikimbia kuwalilia hali pindi tu, ....................8..................... na maafa. Jamii yenye watu, ....................9..................... utangamano hupiga hatua kwa urahisi.

  1.                          
    1. awezalo
    2. awezavyo
    3. awezapo
    4. awezayo
  2.                                    
    1. wema
    2. njema
    3. jema
    4. mwema
  3.              
    1. Hamadi ni iliyo kibindoni
    2. Kwa mwoga huenda kicheko kwa shujaa huenda kilio
    3. Mkataa wengi ni mchawi
    4. Imara ya jembe kaingoje shambani
  4.                              
    1. :
    2. ;
    3. ,
    4. -
  5.                      
    1. ndio
    2. siyo
    3. sio
    4. sizo
  6.                          
    1. wala
    2. ingawa
    3. japo
    4. bali
  7.              
    1. hujitenga
    2. huwatenga
    3. hukutenga
    4. humtenga
  8.                
    1. wangefikwa
    2. wamefikwa
    3. wakifikwa
    4. wanafikwa
  9.                  
    1. wanaoudhamini
    2. wanaoithamini
    3. wanaoidhamini
    4. wanaouthamini

Hamu yangu ya kulielewa zaidi somo la kiswahili, .....................10...................  nimwendee mwalimu .....................11................... msaada. Nilimkuta .....................12................... akisahihisha madaftari ya wanafunzi nikamwomba nafasi ya kunena naye. Alianza kwa kunifunza kutenga silabi katika maneno. Kwa mfano, neno iliyojumlishwa lina silabi .....................13................... Pia, mwalimu aliniongoza kutambua vielezi kama vile: .....................14................... Hivi sasa nimeweza kutumia tamathali za usemi kama sitiari ninapoandika insha. Mfano wa sitiari ni .....................15...................

  1.                  
    1. ndilo lililonifanya
    2. ndio ilionifanya
    3. ndicho kilichonifanya
    4. ndiyo iliyonifanya
  2.              
    1. wa
    2. kwa
    3. na
    4. katika
  3.                
    1. maliwatoni
    2. pambajioni
    3. majilisini
    4. handakini
  4.                        
    1. 7
    2. 13
    3. 8
    4. 6
  5.                    
    1. gani, bora, laini
    2. dhidi ya, mithili, lau
    3. kiasi, tena, kwao
    4. yule, kama, kando
  6.                    
    1. Yakobo anatia akitoa
    2. Selemani ni lumbwi
    3. gari lilibingirika bingiribingiri
    4. miguu yangu imegomea safari

Kuanzia nambari 16 mpaka 30, chagua jibu lifaalo zaidi.

  1. Chagua sentensi iliyotumia kiambishi ka kuonyesha kusudi la kufanya jambo
    1. Baba alienda shambani akalima kutwa nzima.
    2. Wavuvi wameenda baharini wakavue samaki.
    3. Alipika chajio akapakua akala akalala.
    4. "Jua limewaka sana msimu huu," akasema.
  2. Ni jozi ipi iliyo tofauti na nyingine?
    1. legeza - kaza
    2. nenda- rudi
    3. tii-kaidi
    4. tulia - nyamaza
  3. Andika ukubwa wa sentensi:
    Ndovu huyo ana mkonga mrefu.
    1. Jidovu hilo lina jikonga refu
    2. Dovu huyo ana mkonga mrefu 
    3. Dovu hilo lina konga refu
    4. Jidovu hilo linakonga lirefu
  4. Kipi ni kivumishi kilichoundwa kutokana na nomino?
    1. angalia - uangalifu
    2. mwangaza - angavu 
    3. aminika mwaminifu
    4. ucheshi kicheko
  5. Mtu akitaka kupishwa njia husemaje?
    1. simile
    2. kunradhi
    3. ashakum
    4. alamsiki
  6. Tambua nomino za ngeli ya U-YA pekee
    1. wimbi, mawele
    2. ugomvi, wasiwasi
    3. ua, ufito
    4. mabele, magonjwa
  7. Nini maana ya sentensi 'Angalijua unakoishi angalikuja kukutembelea.' 
    1. Alikuja kukutembelea lakini hakujua unakoishi
    2. Kutojua unakoishi ndiko kulikomfanya. asikutembelee
    3. Licha ya kujua unakoishi hakuja kukutembelea
    4. Akijua unakoishi atakuja kukutembelea 
  8. Chagua nahau iliyoambatanishwa ipasavyo na maana yake.
    1. Lilia ngoa - onea wivu
    2. Vilka kilemba cha ukoka - sema mtu kwa mafumbo
    3. Tia mrija - kumpa mtu msaada
    4. Mkono birika - kupenda kutoa msaada bila malipo
  9. Tegua kitendawili: Chepesi chavunja hata majengo.
    1. jiwe
    2. upepo
    3. nyundo
    4. kisu
  10. Andika usemi wa taarifa wa sentensi: Zela: Mwanangu, ukisoma kwa bidii utasaidia jamaa yetu kukabiliana na uchochole.
    1. Zela aliagizwa asome kwa bidii ili aisaidie jamaa yao kukabiliana na uchochole.
    2. Zela alimwambia mwanawe kuwa akisoma kwa bidii atasaidia jamaa yao kukabiliana na uchochole.
    3. Zela alimwambia mwanawe kuwa iwapo angesoma kwa bidii angesaidia jamaa yao kukabiliana na uchochole.
    4. Zela aliambiwa kuwa iwapo angesoma kwa bidii angesaidia jamaa yao kukabiliana na uchochole.
  11. Mkungu ni kwa ndizi lakini mkururo ni kwa ..............................................
    1. Watoto
    2. nyota
    3. waasi
    4. maembe
  12. Chagua kielezi katika sentensi ifuatayo. watoto watiifu na wapole aghalabu huwafurahisha wazazi wao.
    1. watiifu
    2. wapole
    3. wao
    4. aghalabu
  13. Ni maelezo yapi yaliyo sahihi?
    1. Mbia ni mshirika wa kibiashara lakini bia ni kinywaji kinacholevya.
    2. Vumba ni wayo wa mnyama lakini fumba ni harufu mbaya
    3. Daka ni kushika kitu kilichorushwa lakini taka ni kutoa yai katika kiloaka.
    4. Dhamana ni ubora wa kitu lakini thamani ni malipo atolewayo mtu ili apokee huduma.
  14. Chagua sentensi changamano kati ya hizi.
    1. Tuliwapelekea.
    2. Kasisi anaongoza ibada kanisani.
    3. Tuliwakaribisha kwetu lakini hawakuja.
    4. Daraja lililojengwa pale limeanza kutumika.
  15. Ni vyema mtu kuridhika na kile ambacho amejaliwa kupata badala ya kuvitamani vya wenzake.
    Chagua methali inayoambatana na kauli hii.
    1. Mwenye shoka hakosi kuni.
    2. Achanikaye kwenye mpini hafi njaa.
    3. Bura yangu sibadili na rehani.
    4. Mtumai cha ndugu hufa maskini. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali 31-40

Bara la Afrika limejaliwa maliasili chungu nzima. Haya ni pamoja na mito, maanguko ya maji, wanyama pori, misitu, milima, madini na kadhalika. Si ajabu kwamba mabara mengi hulihusudu bara hili kutokana na ukwasi huu ambao wenyeji wake hawajaulalia wala kuuamkia. Je, kwa nini bara hili bado linaselelea katika lindi la ufukara licha ya ukwasi huo wote? Au ni yale ya kozi mwanamadada kulala njaa kupenda?

Ukosefu wa uongozi bora katika mengi ya mataifa haya ni kiini kimojawapo cha hali hii. Aghalabu, viongozi wengi huwa wamba ngozi wasiojali maslahi ya wakazi hata kidogo. Viongozi wa aina hii huchumia vibindo vyao tu bila kujali uchochole unaowaguguna wakazi wengine wa mataifa hayo. Viongozi wao hao hukwamilia madarakani huku wakitaka kutawala kwa miaka na dahari. Matokeo yake ni kudorora kwa hali ya kiuchumi katika mataifa husika.

Ukoloni mamboleo aidha umechangia kudhulumiwa kwa mataifa mengi kiuchumi. 'Misaada' hutolewa katika nchi hizi, huku masharti makali yakiwekwa ndiposa 'usaidizi' uweze kupatikana. Kati ya masharti hayo ni kwamba kampuni za kuchimba madini lazima zitoke katika mataifa ya wafadhili. Tujuavyo ni kuwa uso wa kufadhiliwa u chini na tangu hapo, wenyeji wa mataifa haya maskini huwa hawana lao ila tu kufuata maagizo yanayotolewa. Wakati mwingine viongozi hupakwa mafuta viganjani ili wapitishe sera zitakazoleta manufaa kwa wenye nguvu.

Elimu duni wanayopata wenyeji aidha hufanya viwanda viadimike kama wali wa daku. Katika hali hiyo, wenyeji hawana mahali pa kupeleka malighafi ila tu kuuza nje kwa bei ya kutupa. Hili nalo hutomelewa zaidi na wanunuzi wa bidhaa katika mataifa maskini ambao wana kasumba kwamba chochote kiagizwacho kutoka ughaibuni ni bora kuliko kilichoundiwa nchini. Kwa hivyo, wachache wanaodiriki kuanzisha viwanda nchini huambulia patupu kwa kukosa wateja wa bidhaa zao. Lakini tukichunguza kwa kina tutapata kuwa hivyo vilivyotoka katika mataifa ya kigeni ni vya hali ya chini zaidi.

Viwango vya juu vya ushuru ni tatizo jingine sugu kwa wawekezaji wa humu nchini na wale kigeni. Jambo hili hasa ndilo husababisha gharama ya bidhaa zilizoundiwa nchini kuwa juu kuliko zile zinazotolewa nje. Serikali inapaswa kuwapunguzia mzigo huu wawekezaji ikiwa wanatarajiwa kukabiliana na ushindani wa bidhaa kutoka nje.

Ni muhimu wananchi wawachague viongozi waadilifu ambao wana maono ya kuyaokoa mataifa yao. Voingozi kama hawa wataanzisha miradi ya kuzalisha nguvu za umeme, kuchimba na kutumia madini, kulinda mbuga za wanyama na kuepuka misaada na mikopo inayoambatana na masharti kandamizi. Vijana nao wahimizwe kutilia maanani elimu yao ili waje kufaidika wao na mataifa yao kwa jumla.

Huu ni wakati mwafaka wa mwafrika kujistahi Asipumbazwe na imani potovu kwamba ustaarabu hutoka tu uzunguni na kuwa chochote afanyacho mwafrika ni ushenzi. Yafaa sisi wenyewe tubuni na kutumia vyetu; tukishajitosheleza tuwauzie wao hao wageni ili tupate pesa za kigeni.

  1. Kulingana na aya ya kwanza,
    1. Maliasili ni utajiri unaopatikana pasipo na gharama yoyote.
    2. Afrika imezalisha maliasili kwa wingi kuliko mabara mengine.
    3. Maliasili ya kipekee hupatikana barani Afrika
    4. Afrika imeendelea kiasi cha kuonewa gere na mabara mengi.
  2. Viongozi wanalaumiwa katika kifungu kwa;
    1. ukosefu wa maarifa
    2. kutumia mabavu
    3. ubinafsi walio nao
    4. kutawala kwa muda mrefu
  3. Kauli 'uchochole unaowaguguna wakazi' imetumia tamathali gani ya usemi?
    1. Kinaya
    2. tashhisi
    3. sitiari
    4. chuku
  4. Misaada inayotolewa na nchi za kigeni,
    1. haijalisaidia bara Afrika kwa vyovyote vile.
    2. inakashifiwa kwa viwango vya juu vya riba.
    3. yote hutolewa kwa nia ya kulifaidi bara hili.
    4. Mara nyingi huandamana na masharti ya kuwadhulumu wafadhiliwa.
  5. NI kweli kusema kuwa;
    1. mtu hujichagulia mwenyewe msaada atakaopata
    2. Kuwekewa vikwazo huwafanya wengi kukataa msaada
    3. Mtu anapotaka hisani huwa kama mtumwa asiye na uhuru
    4. Msaada hauwezi kumsaidia mtu kuinuka kiuchumi
  6. Hupakwa mafuta viganjani katika kifungu ni sawa na:
    1. kupumbazwa kwa maneno matamu
    2. kuhongwa
    3. kukashifiwa
    4. kutishiwa hali ya maisha
  7. Imani potovu anayozungumzia mwandishi katika kifungu ni kuwa;
    1. viwango vya elimu vinavyotolewa ni vya chini.
    2. bidhaa bora ni zile zinazonunuliwa nje ya nchi.
    3. malighafi yanafaa kutumika katika viwanda vya nchi.
    4. malighafi yanayouzwa nje hayaleti faida ifaayo.
  8. Kwa nini wawekezaji wanatatizika kuendesha shuguli zao nchini?
    1. Ushuru mkali nchini unawazuia kushindana na bidhaa zinazoagizwa kutoka nje.
    2. Bidhaa kutoka nje ya nchi zinatozwa ushuru wa juu zaidi.
    3. Wamekosa maarifa ya kuendesha shuguli zao ipasavyo.
    4. Nchi nyingi hazina nafasi zifaazo za kutumiwa na wawekezaji.
  9. Mwito wa mwandishi wa makala haya kwa mwafrika ni kuwa;
    1. ajiheshimu na kuwajibika ipasavyo
    2. aachane kabisa na ustaarabu wa kigeni 
    3. atumie rasilimali zake kikamilifu chochote kisitoke nje
    4. abadili mtindo wa kufanya mambo ili aige ya kizungu
  10. Neno 'hulihusudu' kulingana na muktadha lina maana ya
    1. kushangazwa na hali yake
    2. kujivunia hali yake
    3. kuvutiwa na hali yake
    4. kutamaushwa na hali yake. 

Soma makala yafuatayo kisha uilbu maswali kuanzia nambari 41 mpaka 50

Mapuya alitembea taratibu, akapiga kisogo makazi yake kuelekea kwenye kituo cha karibu cha kibiashara. Makazi haya aliyoita kwake sasa yalishageuka mahame baada ya mkewe kuwachukua wanawe wawili akarudi kwao kijijini alikotoka. Mapuya mwenyewe alipatikana pale kwa nadra mithili ya kupatwa kwa jua. Kila siku, alikuwa kiguu na njia kusaka ugimbi ambao tangu hapo ulikuwa ada yake. Hata unadhifu na kutafuta lishe bora sasa ni mambo aliyoyatia kapuni kabisa. Ukimsaili kini cha hali hii, jibu ni lile lile maisha hayana huruma kwake, ameenda nguu kabisa.

Siku hiyo, kinyume na ada yake, Mapuya alihisi hofu na ukiwa wa kipekee. Hakusita kujiuliza kiini cha hali hiyo kwani hakuwa mwanagenzi kamwe katika mchezo wa kupiga maji; kubugia kopo baada ya kopo. Alitulia kidogo nje ya banda milimouziwa pombe tumbo likanguruma kumkumbusha kuwa nalo lilikuwa likidai haki yako. Hapo alijiambia kuwa hata kileo chenyewe ni halall ya tumbo kwa hivyo hana haja ya kujali. Mara hiyo akajitoma bandani kwa vishindo.

Mie ndani, Mapuya alijibanza kwenye kona, akawatazama waliokuwemo kana kwamba ndipo anawaona kwa mara ya kwanza. Mwenzake mmoja aliduwezwa na hali ya Mapuya. akapaza sauti akamwuliza, Vipi leo mwenzangu ama huna chochote umekuja kurondea kama ilivyo ada? Wateja wengine mie bandani walivunjika mbavu huku moyo ukimwuma Mapuya kama aliyepigwa mshale wa sumu. Alivuta taswira akaiona hali yake ya kisogoni hadi kufikia hapo. Akajuta na kusikitika. Kwa hakika maisha yalikuwa yamempiga dharuba kali kiasi kisichosemeka.

Aliyakunjua maisha yake akaona siku zile alipokuwa akifanya kazi katika shirika moja la kuuza mitambo ya kielektroniki. Siku hizo, alivalia suti nadhifu zilizopigwa pasi zikanyoka mithili ya mwanzi. Mshahara wake ulikuwa wa kugugumiwa mate. Hili hasa lilitokana na kisomo chake kilichompa wadhifa wa juu katika shirika hilo. Alikuwa na kilakitu. Wanawe walisomea katika shule za kifahari. Mkewe alipaliliwa vyema kwa mavazi na mitindo aali ya nywele. Majirani walimwonea gere nao wanawe wakamwonea fahari.

Magwiji wa lugha waliamba kuwa pavumapo palilie si kazi kudamirika. Maisha yalipozidi kumtononokea Mapuya, alipata starehe mpya ya vileo na disko. Kwake, aliona hii ni njia mwafaka ya kulifuta jasho lake. Polepole, alianza kuzama kwenye kinamasi mzimamzima. Ulevi wake ulipokidhiri, wasimamizi wake walimwonya mara kadhaa. Hatimaye akaambiwa shirika hilo alione paa.

Baada ya kumwaga unga, shida zilimwandama Mapuya akaingilia uraibu wa pombe haramu ili kujipurukusha. Hivi ndivyo alivyojipata katika hali yake hii. Wakati haya yalipokuwa yakimpitia Mapuya akilini, alisikia mayowe makali kutoka kwa walevi mle bandani. Awali alidhani ni utani lakini mayowe yalipoongezeka huku wengine wakianguka na kutokwa povu midomoni ndipo alipokelewa nususi ya mambo. Dakika chache baadaye, wawili walikata roho wachache wakapofuka huku manusura wakibaki katika hali mahututi.

Baada ya kushuhudia hali ile, Mapuya alinyanyuka akachapuka chapuchapu kuelekea manzilini. Akilini alijikumbusha kauli ya wahenga kwamba, Fisi akimla mwele, mzima funga mlango. Aliamua kutupa jongoo na mti wake. Ingebidi atafute kazi angaa ya kijungujiko almradi we halali. Ikiwezekana, angemwendea mkewe amwangukie miguuni angaa ainusuru aila yake kabla mambo hayajaharibika kabisa.

  1. Chagua maelezo yaliyo sahihi.
    1. Mapuya na aila yake waliishi katika mahame
    2. Mapuya alifanya kazi katika kituo cha kibiashara hapo karibu
    3. Mapuya alikuwa akishiriki ulevi wa pombe kila siku
    4. Mapuya aliingilia ulevi pindi tu shida zilipomkabili
  2. Madhara ya pombe kulingana na kifungu hiki ni,
    1. Kukosa kula na ubovu wa mavazi 
    2. kuwa kiguu na njia, kukata tamaa 
    3. kuathirika kiafya, ukosefu wa mavazi 
    4. kukosa kuwajibika,kusambaratika kwa familia
  3. Mnamo siku ya tukio:
    1. Mapuya alikuwa na uhakika kuwa mambo yangeenda mrama
    2. Huzuni ya Mapuya iliongezeka kwa kuachwa na mke
    3. Mapuya alikosa utulivu akashindwa hata kutembea
    4. Hisia za Mapuya zilikuwa kinyume na jinsi alivyozoea
  4. Kwa nini Mapuya aliamua kutokula chakula?
    1. Kwa maoni yake, pombe ingemshibisha kama chakula
    2. Hakuwa na pesa za kununulia chakula chochote
    3. Ulevi aliozoea ulimmalizia hamu ya chakula
    4. Hakuwa na wakati wa kula kwani alikuwa ulevini wakati wote
  5. Ni kweli kuwa Mapuya,
    1. alikuwa afisa wa ngazi ya juu zaidi kazini
    2. awali aliwajibika katika kutunza familia 
    3. alipikiwa majungu na wakubwa wake akafutwa kazi
    4. aliacha kazi kwa hiari ili ashiriki ulevi 
  6. Mambo yafuatayo yanaonyesha jinsi Mapuya alivyokuwa na maisha mazuri ila, 
    1. suti nadhifu zilizopigwa pasi
    2. mshahara wa kugugumiwa mate 
    3. shirika lililouza mitambo ya kielekroniki
    4. wanawe kusomea katika shule za Kifahari
  7. Maana ya shirika hilo alione paa ni kuwa;
    1. alionywa dhidi ya ulevi
    2. alifukuzwa kazini
    3. alikumbushwa majukumu yake
    4. alitazama paa la shirika.
  8. Aya ya sita inadokeza kuwa:
    1. Mapuya alishiriki ulevi haramu ili kujisahaulisha madhila yake
    2. ulevi uliwafanya wenzake Mapuya wapige mayowe
    3. kushuhudia madhara ya wenzao kuliwafanya wengi wachanganyikiwe
    4. kuongezeka kwa mayowe kuliwafanya wengi wakate roho
  9. Methali 'Fisi akimla mwele, mzima funga mlango' inatuhimiza;
    1. wenzetu wakifikwa na shida tujiandae kwa zizo hizo
    2. wengine wanapohasirika tushukuru kwa kunusurika
    3. udhaifu wa wenzetu uwe njia yetu ya kujitetea
    4. wenzetu wakiingia taabani tuweke mikakati bora ya kujilinda
  10. Kulingana na kifungu hiki;
    1. Mapuya aliamua kufanya kazi yoyote hata kama haikubaliki
    2. Mapuya ameamua kuyarekebisha makosa yake kwa vyovyote vile
    3. Mapuya ameshindwa kabisa kukabiliana na hali yake
    4. Mapuya yuko radhi kufanya kazi yoyote inayohitaji nguvu nyingi

INSHA

SEHEMU B: KISWAHILI INSHA

Wewe ni kiranja mkuu katika shule yenu. Umechaguliwa kutoa hotuba kuhusu JINSI YA KUIMARISHA AFYA MAISHANI.

Andika hotuba hiyo.............................................

MWONGOZO

swa da 

Tagged under

MASWALI

Soma vifungu vifuatavyo, Vina nafasi 1 mpaka 15. Kwa kila pengo umepewa majibu manne. Chagua Jawabu lifaalo zaidi.

Binadarau ..................1................ kwa njia nyingi. ...................2............... njia  ................3.................. ni jinsi  ...............4................... mazingira yake kiholela. Hulka hiyo  .................5................. mapema, yeye mwenyewe, ...................6.......................... kwani ..............7................. Shughuli ya kutunza mazingira ni ...............8................... wetu sote ...............9................... hatutaki kuhasirika.

  1.                          
    1. amejipalia makaa
    2. amejitia hamnazo
    3. amekula njama
    4. amejipikia majungu
  2.                  
    1. Mojawapo wa
    2. Mojayapo ya
    3. Mojawapo ya
    4. Mojayapo wa
  3.                
    1. hiyo
    2. hizo
    3. hilo
    4. hayo
  4.              
    1. anayoyachafua
    2. anaoyachafua
    3. anapoyachafua
    4. anavyoyachafua
  5.            
    1. isingekomeshwa
    2. isiyokomeshwa
    3. isipokomeshwa
    4. ikikomeshwa
  6.                  
    1. ndiye atakayeathirika
    2. ndiwe ataathirika
    3. ndio atakayeathirika
    4. ndiyo atakayeathirika
  7.                
    1. mchelea mwana kulia hulia yeye
    2. mchimba kisima huingia mwenyewe
    3. majuto ni mjukuu huja baadaye
    4. mchuma janga hula na wa kwao
  8.                      
    1. mujibu
    2. jukumu
    3. dhima
    4. wajibu
  9.                
    1. ili
    2. japo
    3. iwapo
    4. ilhali

Ukuaji wa lugha ..................10.................... kutumia neno moja kuzalisha  ................11...................... Kwa mfano, kivumishi 'mwaminifu' kinaweza kutupatia nomino  ................12...................... Ukitaka kuwa  ....................13.................. katika lugha, ni .................14.....................  ujifunze kutumia upatanisho ufaao wa kisarufi. Maneno kama  .................15..................... huorodheshwa katika ngeli ya I-I.

  1.                    
    1. inahusu
    2. kunahusu
    3. unahusu
    4. zinahusu
  2.                
    1. nyingine
    2. jingine
    3. kingine
    4. kwingine
  3.                      
    1. uaminifu
    2. waaminifu
    3. kuaminifu
    4. aminika
  4.                
    1. mhodari
    2. jasiri
    3. mjuba
    4. stadi
  5.                
    1. kawaida kama sheria
    2. hakika kama mauti
    3. lazima kama ibada
    4. nadra kama kupatwa kwa jua
  6.              
    1. mikunga, mijusi na mijomba
    2. asali, miwani na amani
    3. mate, maziwa na mazingira
    4. mikoba, mibibo na mifumo

Kutoka swali 16-30, chagua jibu sahihi kulingana na maagizo

  1. Chagua sentensi yenye kiwakilishi cha idadi.
    1. Wanafunzi wote thelathini wamefaulu mtihani huo.
    2. Miji mingine ilikuwa na vurugu bali hii miwili ilikuwa na utulivu.
    3. Vijana wanapenda michezo ingawa wale wanapenda kuchora sana.
    4. Wengi hawakuamini kuwa mwimbaji yule alikuwa binamu yangu.
  2. Ni kifaa kipi anachotumia seremala kushikia vitu imara wakati anapofanya kazi?
    1. Jiriwa
    2. Timazi
    3. Kekee
    4. Mvukuto.
  3. Andika wingi wa sentensi ifuatayo. Waadhi uliopewa na buda huyo ulikufaa sana.
    1. Waadhi mliopewa na buda hao uliwafaa sana.
    2. Nyaadhi mliyopewa na buda hao iliwafaa sana.
    3. Nyaadhi mlizopewa na mabuda hao ziliwafaa sana.
    4. Waadhi mliopewa na mabuda hao uliwafaa sana.
  4. Bainisha matumizi ya kiambishi 'ka' katika sentensi.
    Badi alienda shambani akapanda miche. 
    1. Kuonyesha kufuatana kwa vitendo.
    2. Kuonyesha kuendelea kwa kitendo. 
    3. Kuonyesha kukamilika kwa vitendo.
    4. Kuonyesha kusudi la kitendo.
  5. Nahau ipi imeambatanishwa ipasavyo na maana yake?
    1. Fanya msirimbo-Fanya jambo kwa utaratibu.
    2. Fumba maneno - Weka siri.
    3. Piga vijembe Fanyia mtu ishara ya dharau.
    4. Iva macho-Ona aibu.
  6. Kanusha sentensi ifuatayo.
    Kamanda ametumwa nyumbani akamlete mzazi.
    1. Kamanda hakutumwa nyumbani akamlete mzazi.
    2. Kamanda hajatumwa nyumbani wala kumleta mzazi.
    3. Kamanda hatumwi hajamleta mzazi.
    4. Kamanda hajatumwa nyumbani akamlete mzazi.
  7. Chagua udogo wa senteni ifuatayo.
    Mtoto aliumia mkono alipogongwa na ukuta
    1. Toto liliumia kono lilipogongwa na kuta
    2. Kitoto kiliumia mkono kilipogongwa na kijikuta.
    3. Kitoto aliumia kikono alipogongwa na kijikuta
    4. Kitoto kiliumia kikono kilipogongwa na kijikuta.
  8. Tegua kitendawili kifuatacho. Mchana kutwa yupo ananizomea tu..
    1. Upepo
    2. Nzi 
    3. Jua
    4. Kivuli.
  9. Neno 'waliokosoana' lina silabi ngapi?
    1. 7
    2. 6
    3. 12
    4. 11
  10. Koko ni miti inayomea baharini. Koko pia ni
    1. vuta kirungu ili kuweka risasi ndani ya bunduki
    2. kinywaji kinachotokana na unga wa mbegu za mkakau
    3. mbegu ngumu iliyo ndani ya tunda
    4. kuondoa punje za mahindi kwenye kigunzi.
  11. Chagua sentensi iliyo katika nafsi ya pili wingi.
    1. Mtoto wako ametoroka.
    2. Nyadhifa zenu zimehifadhiwa.
    3. Wajapo kwetu tutawaelekeza. 
    4. Walimu wetu wameenda likizo.
  12. Jibu lipi linaonyesha aina za mashairi?
    1. Ngonjera, kibwagizo
    2. Utao, mloto
    3. Utenzi, takhmisa
    4. Tarbia, urari.
  13. Milima, mabonde, mito na bahari, vyote ni
    1. malighafi
    2. mandhari 
    3. madini
    4. maliasili.
  14. Chagua methali yenye maana sawa na
    'Usiache mbachao kwa mswala upitao
    1. Afadhali dooteni kama ambari kutanda.
    2. Kipya kinyemi kingawa kidonda. 
    3. Mfumai cha ndugu hufa maskini. 
    4. Mwanzo wa ngoma ni lele.
  15. Ikiwa mtondogoo itakuwa Jumanne, juzi ilikuwa siku gani?
    1. Jumatano 
    2. Jumatatu
    3. Jumapili 
    4. Alhamisi.

 Soma ufahamu kwa makini kisha ujibu maswali 31-40

Ama kukuli kuntu, imepita takriban miongo sita tangu taifa letu lilipojinyakulia uhuru mikononi mwa mabeberu. Maisha kabla ya uhuru yalikuwa usiku wa giza totoro. Mwafrika hakuidhinishwa kufaidi rasilimali za nchi wala kusoma elimu ya kumfaidi maishani. Kile kilichoitwa elimu wakati ule ni maneno machache yaliyonuiwa kumwezesha Mwafrika kupokea amri kutoka kwa mzungu. Mambo yalipomfika Mwafrika huyo kooni, aliamua mno ni mno, tangu hapo ikawa amani haiji ila kwa ncha ya upanga.

Mabeberu walipofunganya virago vyao na Mwafrika kutwaa hatamu za uongozi, nuru ya matumaini iliangaza kote nchini. Mwafrika alisadiki kuwa dhiki zake sasa ni mambo yaliyofukiwa katika kaburi la sahau. Wimbo wa amani, umoja na udugu ulitungwa ukaimbwa kwa mahadhi yaliyopokelewa vyema na raia wote. Ahadi nyingi zilitolewa na viongozi wa wakati huo. Hizi ni pamoja na elimu bora, kuangamiza maradhi na kuangamiza umaskini. Hata hivyo, ahadi hizi zimesalia katika vitabu vya kumbukumbu tu. Je, ni nini hasa kilichokwamisha juhudi za kufikia mafanikio hayo?

Tunaweza kusema kwamba aliondoka mkoloni wa kizungu akaja mkoloni wa kiafrika. Tuliodhani kuwa wakombozi wetu waligeuka kuwa wamba ngoma waliovuta ngozi kwao. Badala ya kuleta mwamko mpya, waliendeleza sera zilezile za watangulizi wao. Rasilimali za umma ziliporwa kwa manufaa ya watu binafsi. Wachache waliojaribu kupinga uhalifu huo

walinyamazishwa milele. Uligeuka kuwa ulirnwengu, wa mnyonge kupata haki ni mwenye nguvu kupenda.

Hatua nyingi zimependekezwa kama njia mwafaka ya kukabiliana na hali hii. Hizi ni pamoja na kuzinduliwa kwa katiba mpya, kubuniwa kwa sera mbalimbali na kufanyiwa marekebisho kwa asasi kama vile polisi na mahakama. Harakati za hivi punde zilihusiana na kubadilishwa kwa mfumo wa elimu kwa azma ya kuwawezesha wengi kujitegemea badala ya kutafuta kazi za ajira tu. Hata hivyo, juhudi kama hizi zitabaki ngoma gova iwapo mambo yanayokwamisha maendeleo hayatatafutiwa suluhisho la kudumu.

Kwanza, ni lazima rasilimali za nchi ziondolewe mikononi mwa watu binafsi ili zilifaidi taifa kwa jumla. Iweje madini yamfaidi mtu binafsi huku wazalendo wengine wakiambulia patupu? Halikadhalika, ufisadi ambao umekithiri kote nchini uangamizwe kwa njia inayofaa. Idara ya mahakama isitekwe na watu binafsi kwa lengo la kubadili mkondo wa sheria.

Tumewaona washukiwa wengi wa ufisadi wakikimbilia mahakamani ili wapewe vibali vya kuzuilia kutiwa mbaroni kwao. Iweje asasi inayopaswa kuzuia ufisadi ndiyo inayowasetiri mafisadi?

Ustawi wa jamii yetu utapatikana tu iwapo sote tutaukumbatia uzalendo. Raia mzalendo huwa tayari kuitetea nchi yake kwa hali na mali. Yeye na maovu huwa wamebaidika mithili ya ardhi na mbingu. Hana tamaa wala ubinafsi. Yeye huwajali ndugu zake bila kujali dini, jinsia, kabila wala tabaka. Huo ndio moyo tunaohitaji ili kulijenga taifa thabiti.

  1. Kulingana na aya ya kwanza, ni kweli kuwa
    1. ni zaidi ya miaka sitini tangu taifa lianze kujitawala
    2. ni karibu miaka sitini tangu taifa lianze kujitawala
    3. taifa lilitawaliwa na mabeberu kwa miongo sita
    4. taifa lilitawaliwa na mabeberu kwa takriban miongo sita.
  2. Si kweli kusema kuwa
    1. awali mwafrika hakupata elimu yoyote
    2. wakati wa ukoloni maisha ya mwafrika yaligubikwa na dhiki
    3. mwafrika alipata elimu duni wakati wa ukoloni
    4. wakoloni walitumia rasilimali za bara letu kujifaidi.
  3. Uhuru unaozungumziwa ulipatikana kwa njia ya
    1. maridhiano
    2. bahati nasibu
    3. maafikiano
    4. makabiliano.
  4. Maneno 'ahadi hizi zimesalia katika vitabu vya kumbukumbu tu' yana maana kuwa
    1. Mwafrika hakusomewa ahadi zilizowekwa
    2. ahadi zilizingatiwa muda mrefu uliopita
    3. ahadi zilizowekwa hazikutimizwa kamwe
    4. yaliwekwa malengo makubwa yasiyowezekana.
  5. Kilichozuia ustawi baada ya uhuru hasa ni
    1. ubinafsi wa wale waliotwaa madaraka 
    2. umaskini ambao tuliachiwa na mabeberu
    3. ukosefu wa maarifa wa wananchi wenyewe
    4. uhaba wa rasilimali katika taifa letu.
  6. Mfumo wa elimu ulibadilishwa ili 
    1. nafasi za ajira ziweze kuongezeka 
    2. watu binafsi wabuni njia za kujiimarisha kiuchumi
    3. kupunguza mzigo wa masomo kwa wanafunzi
    4. kuondoa mfumo duni tulioachiwa na wakoloni.
  7. Zitabaki ngoma gova' ndiko kusema
    1. hazitakuwa na manufaa 
    2. zitatufaidi ipasavyo
    3. zitapingwa na wananchi
    4. zitashabikiwa na wengi.
  8. Watu wanaokimbilia mahakamani kwa mujibu wa kifungu huwa na lengo lipi? 
    1. Kuwashtaki mafisadi.
    2. Kuepuka dhuluma za polisi.
    3. Kuepuka kukamatwa kutokana na uhalifu wao.
    4. Kuchukua vibali vya kushiriki njama za ufisadi.
  9. Kifungu yamebaidika mithili ya ardhi na mbingu' kimetumia tamathali gani ya usemi?
    1. Sitiari
    2. Chuku
    3. Kinaya
    4. Tashbihi.
  10. Aya ya mwisho inadokeza kwamba mzalendo
    1. huwajali watu wa taifa lake tu
    2. hana ubaguzi kwa yeyote
    3. hajali lolote kuhusu ufisadi
    4. huwatetea hata wanaolipuja taifa. 

Soma kifungu kifuatacho kisha ujibu maswali kuanzia 41 hadi 50.

Makeke alikuwa mwanamume wa makamo. Hakuna mtu ambaye hakumfahamu kijijini kwa vitimbi vyake. La kushangaza ni kuwa ukimwuliza mwanakijiji yeyote, atakuambia kuwa hakuwahi kumwona Makeke akiwa si mlevi. Alizovaa hazikuwa nguo bali mararu tu. Ukija kwenye usafi wa mwili wake, msalie mtume tu! Uvundo aliotoa ulikithiri. Nzi, chawa, viroboto na mafunza walipata mazingira mwafaka katika mwili wake. Kwa bahati nzuri, alijijengea kijumba cha msonge nje ya makao ya mke na wanawe ili kuepuka kile alichoitwa 'udhia wa watoto na wanawake. Kwa njia hiyo aliwaepusha na wageni hao ambao hawakumbanduka mwilini mwake.

Familia hii ilikuwa na wana kumi na mmoja. Kati yao, hakuna aliyewahi kuliona lango la shule. Walikuwa kama vibarua wa kulihudumia shamba la Makeke. Awali, shamba hilo, ambalo Makeke alirithi kutoka kwa baba yake, lilikuwa kubwa. Hata hivyo, alianza kulipiga bei polepole ili apate darahima za kukinaisha hamu yake ya ugimbi. Mwishowe kilibaki kikataa kidogo tu. Kipato chote hiki kilimiminwa mifukoni mwa wagemaji haramu kijijini.

Kila asubuhi, Makeke aligawa majukumu kwa mkewe na wanawe. Wapo waliohitajika kumtafutia ng'ombe malisho, wa kulima na kupalilia miche shambani au kumwandalia uji wa wimbi ambao aliupenda sana. Meno yake yalidhoofika kiasi cha kutoweza kutafuna chakula kigumu. Macho yake nayo yalidhoofika yakabaki na nuru hafifu kama ya kikongwe aliyechungulia kuzimuni. Ilikuwa wazi kwamba uraibu wake ulimwacha taabani. Juhudi za mkewe za kujaribu kumwasa apunguze ulevi huo zilijibiwa kwa kipigo na matusi makali huku akionywa asimletec Makeke 'upuuzi wa wanawake. Tangu hapo, mkewe lake likawa jicho tu. Wanakijiji waliposhuhudia dhiki za watoto hawa ambao walivalia mavazi duni na kudhoofika kwa kukosa lishe bora, waliamua kuchukua hatua zifaazo. Walishika njia hadi kwa chifu wakamshtakia hali. Chifu naye aliandamana na wanakijiji hadi kwa Bwana Makeke. Walipofika, waliwakuta watoto wakifanya kazi shambani. Wakati huo, Makeke mwenyewe alikuwa ameshayoyomea zake ulevini. Chifu aliwaagiza askari wake wamsake kokote alikokuwa amlete kadamnasi.

Makeke alipofika na kuupata umati kwake, alikuja juu kama moto wa kifuu. Alitaka kujua aliyewapa kibali cha kumwingilia kwake bila idhini. Wananchi walijawa na hamaki wakataka kumtia adabu lakini Bwana chifu akawatahadharisha dhidi ya kuchukua sheria mikononi mwao.

Afisa wa maslahi ya watoto aliyekuwa miongoni mwa wanakijiji wale alimwelimisha Makeke na wale waliokuwepo kuhusu haki za watoto. Aliwaeleza kuwa ni jukumu sio tu la kila mzazi bali wananchi wote kuhakikisha kuwa mtoto anatimiziwa haki hizo. Haki zenyewe ni pamoja na lishe bora, mavazi, makazi, huduma za afya na elimu ya msingi miongoni mwa nyingine. Yeyote aliyepatikana na hatia ya kumdhulumu mtoto haki hizo alipaswa kukabiliwa na mkono mrefu wa sheria. Hayo yalimwacha Makeke akigwaya kwa hofu. Papo hapo, aliomba radhi kwa wote waliokuwepo. Akaahidi kutupa jongoo na mti wake.

Wanakijiji walipendekeza watoto wale wanunuliwe mavazi na nyenzo nyingine kutokana na hazina ya kustawisha kijiji ili waende shuleni. Chifu na Afisa wa maslahi ya watoto waliahidi kufuatilia kwa karibu malezi ya wana hawa. Makeke alionywa kuwa iwapo angeendeleza ukaidi wake asingeepuka mkono wa sheria.

Watoto walienda shuleni wakainukia kuwa wenye vichwa vyepesi. Waliendelea kuwasaidia wazazi baada ya masomo na wakati wa likizo. Hatimaye, walihitimu wakapata kazi katika sekta mbalimbali. Familia hii iliimarika sana kihali na kiuchumi. Ama kweli kuinamako ndiko kuinukako.

  1. Chagua maelezo sahihi kulingana na kifungu
    1. Ulevi ndio uliomfanya Makeke awe maarufu zaidi.
    2. Makeke alijulikana kutokana na vitendo vyake vya hila.
    3. Watu walimjua Makeke kwa umaskini wake.
    4. Wanakijiji walishangaa walipogundua ulevi wa Makeke.
  2. Madhara ya ulevi kwa jumla kulingana na kifungu ni
    1. kupunguza uwajibikaji
    2. kukaribisha vimelea
    3. kudhulumu familia
    4. kudhoofisha afya.
  3. Kwa nini Makeke hakuwapeleka wanawe shuleni?
    1. Elimu haikutiliwa maanani siku hizo.
    2. Yeye na mkewe hawakujua maana ya elimu.
    3. Alitaka wabaki nyumbani ili wafanye kazi.
    4. Umaskini ulimfanya ashindwe kuwapa mahitaji.
  4. Mkewe Makeke ni mwenye busara kwa kuwa
    1. alivumilia licha ya vitimbi vya mumewe
    2. aliwafahamisha wanakijiji hali ilipokithiri
    3. alijitenga ili asiathiriwe na vimelea kama mumewe
    4. alijaribu kumnasihi mumewe dhidi ya ulevi.
  5. Haki za watoto zilizokiukwa katika kifungu ni
    1. elimu na utangamano
    2. afya na makazi
    3. lishe bora na mavazi
    4. upendo na matibabu.
  6. Jambo lililomkera Bwana Makeke alipofika ni
    1. watoto kuacha kazi aliyawapa
    2. watu kufika kwake bila ruhusa
    3. kuitwa ulevini kabla ya kujitosheleza
    4. kutishiwa kuchukuliwa hatua na wanakijiji.
  7. Bwana Chifu aliagiza Makeke asakwe kokote alikokuwa aletwe kadamnasi. Hali hii inaonyesha kuwa
    1. serikali ina mkono mrefu
    2. watu walijua aliko Makeke
    3. chifu hakuwa na huruma
    4. hakutaka kuwaudhi wanakijiji.
  8. Funzo alilotoa Afisa wa maslahi ya watoto ni kwamba
    1. jukumu la kulinda haki za watoto ni la wazazi
    2. siku hizi watu hawakiuki haki za watoto kiholela
    3. watu wengi hawana habari kuhusu haki za watoto
    4. kila mwananchi ana jukumu la kulinda haki za watoto.
  9. Sifa za wanakijiji zinazojitokeza katika kifungu ni
    1. ukali na uwajibikaji
    2. ushirikiano na kujaliana maslahi
    3. uaminifu na maridhiano
    4. upendo na uvumilivu.
  10. Methali 'Kuinamako ndiko kuinukako' ina maana kuwa
    1. mahali kwenye mabonde kunaweza kubadilika na kuwa na mwinuko
    2. mtu mwovu anaweza kubadilika mwenendo akawa mwadilifu
    3. hali ya wanyonge inaweza kubadilika wawe wenye uwezo
    4. watu wanaozozana wanaweza kumaliza tofauti zao wakapatana.

 INSHA

Umepewa dakika 40 kuandika insha yako.

Andika insha isiyopungua ukurasa mmoja na nusu ukifuata maagizo uliyopewa. Andika insha ya kusisimua itakayomalizika kwa maneno yafuatayo.

...................................................................................Alitimiza ahadi yake akayaacha maovu na kuwa mtu wa kutegemewa na jamii yake.

MAJIBU

swa cdadad

Tagged under
Page 4 of 14