Kiswahili paper 3 Questions and Answers - Form 3 End Term 1 Exams 2023

Share via Whatsapp
SEHEMU YA A: USHAIRI
Soma shairi na kisha uyajibu maswali yafuatayo:-
  1. Ni sumu, sumu hatari
    Unahatarisha watoto
    Kwa ndoto zako zako leweshi
    Za kupanda ngazi
    Ndoto motomoto ambazo
    Zimejenga ukuta
    Baina ya watoto
    Na maneno laini
    Ya ulimi wa wazazi
  2. Ni sumu, sumu hasiri
    Unahasiri watoto
    Kwa pupa yako hangaishi
    Ya kuwa tajiri mtajika
    Pupa pumbazi ambayo
    Imezaa jangwa bahili
    Badala ya chemichemi
    Ya mazungumzo na maadili
    Baina ya watoto na mzazi
  3. Ni sumu, sumu legezi
    Unalegeza watoto
    Kwa mazoea yako tenganishi
    Ya daima kunywa ‘moja baridi’
    Mazoea mabaya ambayo yanafunga katika klabu
    Hadi saa nane usiku
    Huku yakijenga kutofahamiana
    Baina ya watoto na mzazi
  4. Ni sumu, sumu jeruhi
    Unajeruhi watoto kwa pesa,
    Kwa mapenzi yako hatari
    Ya kuwaliwaza watoto kwa pesa
    Zinawafikisha kwenye sigara na ulevi
    Na kisha kwenye madawa ya giza baridi
    Barabara inayofikisha kwenye giza baridi la kaburi la asubuhi

Maswali

  1. Pendekeza kichwa kwa shairi hili. (alama 1)
  2. Fafanua maudhui ya shairi hili. (alama 2)
  3. Ni kwa njia gani kinachozungumziwa kinajenga ukuta? . (alama 2)
  4. Dondoa tamathali mbili za usemi zilizotumika katika shairi na uzitolee mfano (alama 4)
  5. Eleza umbo la shairi hili. (alama 3)
  6. Uandike ubeti wa nne kwa lugha nathari. (alama 4)
  7. Eleza maana ya vifungu hivi vilivyotumika katika shairi . (alama 4)
    1. Giza baridi
    2. Yanakufunga katika klabu

SEHEMU B:FASIHI SIMULIZI

  1.  
    1. Taja na ueleze sifa za mtambaji bora katika fasihi simulizi. (alama 10)
    2. Nyimbo zina wajibu gani katika jamii. (alama 4)
    3.  
      1. Eleza maana ya vitendawili. (alama 2)
      2. Onyesha sifa za kitendawili. (alama 4)
  2.  
    1. Taja na ueleze aina nne kuu za hadithi (alama 8)
    2. Eleza mbinu tatu ambazo mtambaji anaweza kutumia kuishirikisha hadhira yake.(alama 6)
    3. Fafanua vipera vifuatavyo vya fasihi simulizi. (alama 6)
      1. Majigambo
      2. Mivigha
      3. Lakabu

MARKING SCHEME

USHAIRI

  1. Kichwa
    • Kielelezo kibaya
    • Tabia mbovu kwa watoto
    • Wazazi wabaya/ walegevu
  2. Maudhui ya shairi
    • Mshairi anasema kuwa wazazi wanahasiri watoto kwa pupa yao ya kulewa kila wakati na kuwa kielelzo kibaya
    • Wazazi kukaa vilabuni mpaka usiku wa manane bila kufahamiana na watoto wao ni vibaya
    • Wazazi kuwapa watoto pesa nyingi ni tabia potovu kwani wanazitumia dawa za kulevya
    • Wazazi wanatafuta utajiri na kukosa wakati wa kuwashauri/ kuwafunza maadili mema
  3. Kinachojenga ukuta
    • Hapana mazungumzo ya kishauri baina ya watoto na wazazi nah ii hujenga ukuta baina ya watoto na wazazi
    • Kulewa kila wakati na kukaa kilabuni kwa mpaka usiku wa manane hujenga ukuta kwa kuwa mzazi huwa hapati wakati wa kuzungumza na mtoto 2x1=2
  4. Tamatahli za usemi
    1. Takriri – ni sumu, sumu
    2. Tashihisi – ndoto zinajenga ukuta/ yanakufunga katika klabu
    3. Istiara – ni sumu                                                                                        Kutaja – 1, Mfano – 1
  5. Umbo la shairi
    1. Lina beti nne
    2. Kila mshororo una mishororo tisa isipokuwa ubeti wa mwisho
    3. Ni shairi huru kwa kuwa halizingatii arudhi
  6. Lugha nathari- ubeti wa nne
    1. Mshairi anasema kuwa wazazi wanaumiza watoto kwa kuwapa pesa
    2. Ni vibaya kuliwaza watoto kwa kuwapa pesa
    3. Kwani huwaingiza katika maovu ya kuvuta sigara na ulevi na mihadarati
    4. Hali hii inaishia upotofu wa watoto/ huwaingiza katika hali mbaya/ kifo
  7. Maana ya vifungu
    1. Giza baridi – hali mbaya/ kifo
    2. Yanakufunga katika klabu – kuwa na mazoea mabaya ya kukaa kilabuni kulewa mpaka usiku wa manane

FASIHI SIMULIZI

  1.  
    1. Sifa za mtambaji bora
      • Awe na uwezo wa kuwasilisha hadithi.
      • Anafaa kutumia njia inayochangamsha hadhira.
      • Awe na ujuzi wa kuifahamu hadhira yake.
      • Awe na ufahamu mpana wa lugha pamoja na utamaduni unaohusika.
      • Awe na uwezo wa ufaraguzi.
      • Aweze kufahamu tabia za binadamu na mikondo mbalimbali ya jamii. 5 x 2 = 10
    2. Wajibu wa nyimbo
      • Hutumbuiza
      • Kuwasifu watu maarufu
      • Kusahihisha maovu ya jamii
      • Huhifahi utamaduni
      • Huelimisha watu
      • Hukuza lugha
      • Huhamasisha watu
      • Kufariji waliofiwa
      • Kuendeleza uhai wa jamii n.k (1 x 4)
    3.  
      1. Kitendawili ni fumbo/msemo wa kinafumbo amabao hufumbua jambo Fulani na hutolewa hadhira au wasikilizaji ili waufumbue. 1 x 2= 2
      2. Hutangulizwa kwa njia maalumu
        1. Ujumbe wake ni wa kimafumbo
        2. Ufananisho wa kihazanda
        3. Ni fupi kwa maelezo
        4. Hutegemea mazingira/sehemu Fulani 4 x 1 =  4
  2.  
    1.  
      1. Visasili - Hadithi zinazosimulia asili ya watu, vitu ama tabia Fulani.
      2. Ngano za mazimwi - Husimulia kuhusu mazimwi
      3. Hurafa - Hadithi ambazo zina wahusika wanyama lakini waliopewa tabia za binadamu.
      4. Hekaya - Ngano fupi zinazosimulia matukio ya kushangaza  yanayoonyesha hila au ujanja wa mwanadamu
      5. Mighani huwa na lengo la kueleza visa na mikasa ya watu ama mashujaa wa jamii fulani.
    2.  
      1. Kutumia viungo vyake vya mwili kuikuza na kuifanya hadithi kusisimua.
      2. Msimuliaji kuchukua nafasi ya wahusika katika hadithi ili kuishirikisha hadhira.
      3. Uwezo wa kuiga matendo na wahusika kwa kuimba na kupiga makofi ili kuvutia hadhira.
      4. Ucheshi na mvuto wa lugha ili kuifanya hadhira kushikika.
    3.  
      1. Majigambo – Mazungumzo yanayotolewa na mtu fulani ili kutapa
      2. Mivigha – sherehe maalum za kitamaduni ambazo hufanywa na jamii katika kipindi maalum.
      3. Lakabu – Majina ya utani au kupanga ambayo watu hujipa au kupewa
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili paper 3 Questions and Answers - Form 3 End Term 1 Exams 2023.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest