Kiswahili P1 Questions and Answers - Form 3 Term 3 Opener Exams 2022

Share via Whatsapp

MAAGIZO

  1. Andika insha mbili.Insha ya kwanza ni ya lazima.
  2. Chagua insha nyingine moja kati ya hizo tatu zilizobakia
  3. Kila insha isipungue maneno 400
  4. Kila insha ina alama 20 


MASWALI

  1. Wewe ni katibu wa kamati iliyoteuliwa na rais kuchunguza madhara ya pombe haramu na mbinu za kuangamiza pombe hiyo. Andika ripoti rasmi.
  2. Vijana wanakumbwa na changamoto si haba.
    Thibitisha
  3. Andika insha itakayothibitisha ukweli wa methali
    ‘’Mwiba wa kujichoma hauambiwi pole.
  4. Andika kisa kitakachokamilika kwa maneno yafuatayo…………… waliwasili saa tatu baadaye.Uharibifu wa mali na maisha ulikuwa umeshatendeka


MWONGOZO WA KUSAHIHISHA

  1. Ni insha vya ripoti.Muundo uzingatie mambo yafuatayo :
    • Kichwa
    • Kitaje mada ya ripoti na tarehe
    • kiandikwe kwa herufi kubwa na kipigiwe mstari
    • utangulizi-uhusishe usuli mfupi au maelezo ya jumla kuhusu mada ya ripoti
    • Orodha ya majina ya wanakamati
    • hadidu za rejea-mambo yaliyohitajika kufanywa wakati wa utafiti
    • utaratibu-mbinu zilizotumiwa kutekeleza utafiti
    • mwili-ueleza maudhui(matokeo)-inaweza kuwa na visehemu vyenye vichwa vidodo vidogo
    • mapendekezo-inapendekeza namna ya kutatua tatizo lililotafitiwa.
    • Hitimisho-ushauri kuhusu mada iliyoshughulikiwa. 
    • Kitambulisho-jina la mtayarishi
    • sahihi
    • tarehe
      Baadhi ya madhara ya pombe haramu
    • magonjwa
    • ukosefu wa maadili
    • kusambaratika kwa familia
    • watoto kukosa elimu (mahitaji ya kimsingi)
    • vifo
    • upofu
    • ubadhirifu
    • huendeleza ufisadi
      Njia za kuangamiza pombe haramu (mapendekezo)
    • kuelimisha wananchi kuhusu madhara ya pombe haramu
    • kufutwa kazi kwa viongozi wanaokubali uuzaji wa pombe haramu kwenye sehemu wanazosimamia
    • kushtakiwa,kuhukumiwa,kutozwa faini kwa wauzaji wa pombe haramu
    • mikakati ya kupunguza umaskini
    • mafunzo ya dini
      Mwalimu akadirie hoja za mwanafunzi
  2. Changamoto zinazowakumba vijana
    • shinikizo la rika
    • athari za utandawazi
    • uigaji wa tamaduni za kigeni
    • ukosefu wa ajira
    • umaskini
    • dawa za kulevya
    • ushababi (ujana)
    • lugha
      Mwalimu akadirie hoja nyingine
  3. Ni insha ya methali
    • insha ishughulikie pande mbili za methali
    • mwanafunzi atunge kisa cha kuthibitisha ukweli wa methali
    • Kisa kihusu mhusika ambaye amefanya jambo/mambo mabaya kwa maksudi kisha likaishia kumletea madhara
  4. Hii ni insha ya mdokezo
    • mtahiniwa lazima amalizie insha yake kwa mdokezo.
    • Insha inaweza kuhusisha uvamizi,mkasa au tukio lingine lenye hatari,ambapo wanaofaa kutoa msaada hawakufika kwa wakati unaofaa
Join our whatsapp group for latest updates

Download Kiswahili P1 Questions and Answers - Form 3 Term 3 Opener Exams 2022.


Tap Here to Download for 50/-




Why download?

  • ✔ To read offline at any time.
  • ✔ To Print at your convenience
  • ✔ Share Easily with Friends / Students


Get on WhatsApp Download as PDF
.
Subscribe now

access all the content at an affordable rate
or
Buy any individual paper or notes as a pdf via MPESA
and get it sent to you via WhatsApp

 

What does our community say about us?

Join our community on:

  • easyelimu app
  • Telegram
  • facebook page
  • twitter page
  • Pinterest